Isaya 56

Wokovu Kwa Ajili Ya Wengine

1 Hili ndilo asemaloBwana:

“Dumisheni haki

na mkatende lile lililo sawa,

kwa maana wokovu wangu u karibu

na haki yangu itafunuliwa upesi.

2 Amebarikiwa mtu yule atendaye hili,

mtu yule alishikaye kwa uthabiti,

yeye ashikaye Sabato bila kuinajisi,

auzuiaye mkono wake

usifanye uovu wo wote.”

3 Usimwache mgeni aambatanaye naBwanaaseme,

“HakikaBwanaatanitenga na watu wake.”

Usimwache towashi ye yote alalamike akisema,

“Mimi ni mti mkavu tu.”

4 Kwa kuwa hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa matowashi washikao Sabato zangu,

ambao huchagua kile kinachonipendeza

na kulishika sana Agano langu,

5 hao nitawapa ndani ya Hekalu langu na kuta zake

kumbukumbu na jina bora kuliko kuwa

na watoto wa kiume na wa kike:

Nitawapa jina lidumulo milele

ambalo halitakatiliwa mbali.

6 Wageni wanaoambatana naBwana

kumtumikia,

kulipenda jina laBwana,

na kumwabudu yeye,

wote washikao Sabato bila kuinajisi

na ambao hushika sana Agano langu

7 hawa nitawaleta kwenye mlima wangu mtakatifu

na kuwapa furaha

ndani ya nyumba yangu ya sala.

Sadaka zao za kuteketeza na dhabihu zao

zitakubalika juu ya madhabahu yangu,

kwa maana nyumba yangu itaitwa

nyumba ya sala kwa mataifa yote.”

8 BwanaMwenyezi asema, yeye awakusanyaye

Waisraeli waliohamishwa:

“Bado nitawakusanya na wengine kwao zaidi ya hao

ambao wameshakusanywa tayari.”

Mashtaka Ya Mungu Dhidi Ya Waovu

9 Njoni, enyi wanyama wote wa kondeni,

njoni mle, ninyi wanyama wote wa mwituni!

10 Walinzi wa Israeli ni vipofu,

wote wamepungukiwa na maarifa;

wote ni mbwa walio bubu

hawawezi kubweka;

hulala na kuota ndoto,

hupenda kulala.

11 Ni mbwa wenye tamaa kubwa,

kamwe hawatosheki.

Wao ni wachungaji waliopungukiwa na ufahamu;

wote wamegeukia njia yao wenyewe,

kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.

12 Kila mmoja hulia, “Njoni, tupate mvinyo!

Tunywe kileo sana!

Kesho itakuwa kama leo,

au hata bora zaidi.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/56-27fcdddbb4db5bf23fb1c37da12ab46c.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

18 − eight =