Isaya 55

Mwaliko Kwa Wenye Kiu

1 “Njoni, ninyi nyote wenye kiu,

njoni kwenye maji;

nanyi ambao hamna fedha,

njoni, nunueni na mle!

Njoni, nunueni divai na maziwa

bila fedha na bila gharama.

2 Kwa nini kutumia fedha kwa kitu ambacho si chakula,

na kutaabikia kitu kisichoshibisha?

Sikilizeni, nisikilizeni mimi na mle kilicho kizuri,

nazo nafsi zenu zitafurahia utajiri wa unono.

3 Tegeni sikio mje kwangu,

nisikieni mimi, ili nafsi zenu zipate kuishi.

Nitafanya Agano la milele nanyi,

pendo la uaminifu nililomwahidi Daudi.

4 Tazama, nimemfanya kuwa shahidi wa mataifa,

kiongozi na jemadari wa mataifa.

5 Hakika utaita mataifa usiyoyajua,

nayo mataifa yale yasiyokujua yataharakisha kukujia,

kwa sababu yaBwanaMungu wako,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,

kwa maana amekutukuza.”

6 MtafuteniBwanamaadamu anapatikana;

mwiteni maadamu yu karibu.

7 Mtu mwovu na aiache njia yake

na mtu mbaya na ayaache mawazo yake.

Yeye na amrudieBwana, naye atamrehemu,

arudi kwa Mungu wetu,

kwa kuwa atamsamehe bure kabisa.

8 “Kwa kuwa mawazo yangu si mawazo yenu,

wala njia zenu si njia zangu,”

asemaBwana.

9 “Kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia,

ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu

na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.

10 Kama vile mvua na theluji

ishukavyo kutoka mbinguni,

nayo hairudi tena huko

bila kunywesha dunia

na kuichipusha na kuistawisha,

hivyo hutoa mbegu kwa mpanzi

na mkate kwa mlaji,

11 ndivyo lilivyo neno langu lile litokalo kinywani mwangu:

Halitanirudia tupu,

bali litatimiliza lile nililokusudia

na litafanikiwa katika kusudi

lile nililolituma.

12 Mtatoka nje kwa furaha

na kuongozwa kwa amani;

milima na vilima

vitapaza sauti kwa nyimbo mbele yenu,

nayo miti yote ya shambani

itapiga makofi.

13 Badala ya kichaka cha miiba

itaota miti ya misunobari,

na badala ya michongoma

# utaota mhadasi.

Hili litakuwa jambo la kumpatiaBwanajina,

kwa ajili ya ishara ya milele,

ambayo haitaharibiwa.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/55-979465adb21391b486fb7a9609b44d28.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

three × 2 =