Dhambi Ya Israeli Na Utii Wa Mtumishi
1 Hili ndilo asemaloBwana:
“Iko wapi hati ya talaka ya mama yako
ambayo kwayo niliachana naye?
Au nimewauza ninyi kwa nani
miongoni mwa watu wanaonidai?
Kwa ajili ya dhambi zenu mliuzwa,
kwa sababu ya makosa mama yenu aliachwa.
2 Nilipokuja, kwa nini hakuwepo hata mmoja?
Nilipoita, kwa nini hakuwepo hata mmoja wa kujibu?
Je, mkono wangu ni mfupi mno hata nisiweze kuwakomboa?
Je, mimi sina nguvu za kukuokoa?
Kwa kukemea tu naikausha bahari,
naigeuza mito ya maji kuwa jangwa;
samaki wake wanaoza kwa kukosa maji
na kufa kwa ajili ya kiu.
3 Ninalivika anga weusi na kufanya nguo ya gunia
kuwa kifuniko chake.”
4 BwanaMwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa,
ili kujua neno lile limtegemezalo aliyechoka.
Huniamsha asubuhi kwa asubuhi,
huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.
5 BwanaMwenyezi amezibua masikio yangu,
nami sikuwa mwasi,
wala sikurudi nyuma.
6 Niliwapa mgongo wangu wale wanipigao,
mashavu yangu wale wang’oao ndevu zangu;
sikuuficha uso wangu kutokana na fedheha
na kutemewa mate.
7 Kwa sababuBwanaMwenyezi ananisaidia,
sitatahayarika.
Kwa hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe la gumegume,
nami ninajua sitaaibika.
8 Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu.
Ni nani basi atakayeleta mashtaka dhidi yangu?
Tukabiliane uso kwa uso!
Mshitaki wangu ni nani?
Ni nani aliye mshitaki wangu?
9 NiBwanaMwenyezi ndiye anisaidiaye mimi.
Ni nani huyo atakayenihukumu?
Wote watachakaa kama vazi,
nondo atawala awamalize.
10 Ni nani miongoni mwenu amchayeBwana
na kulitii neno la mtumishi wake?
Yeye atembeaye gizani,
yeye asiye na nuru,
na alitumainie jina laBwana
na amtegemee Mungu wake.
11 Lakini sasa, ninyi nyote mnaowasha mioto
na kupeana ninyi kwa ninyi mienge iwakayo,
nendeni, tembeeni katika nuru ya moto wenu
na ya mienge mliyoiwasha.
Hili ndilo mtakalolipokea kutoka mkononi mwangu:
Mtalala chini kwa mateso makali.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/50-ebb04f50960cdafa3d3403a8043fd55d.mp3?version_id=1627—