Isaya 35

Furaha Ya Waliokombolewa

1 Jangwa na nchi kame vitafurahi;

nyika itashangilia na kuchanua maua.

Kama waridi,

2 litachanua maua,

litashangilia sana na kupaza sauti kwa furaha.

Litapewa utukufu wa Lebanoni.

Fahari ya Karmeli na Sharoni;

wataona utukufu waBwana,

fahari ya Mungu wetu.

3 Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu,

yafanyeni imara magoti yaliyolegea,

4 waambieni wale wenye mioyo ya hofu,

“Iweni hodari, msiogope;

tazama, Mungu wenu atakuja,

pamoja na malipo ya Mungu,

atakuja na kuwaokoa ninyi.”

5 Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa

na masikio ya viziwi yatazibuliwa.

6 Ndipo kilema atarukaruka kama kulungu,

nao ulimi wa aliye bubu utapaza sauti kwa shangwe.

Maji yatatiririka kwa kasi katika nyika

na vijito katika jangwa.

7 Mchanga wa moto utakuwa bwawa la maji,

ardhi yenye kiu itabubujika chemchemi.

Maskani ya mbweha walikolala hapo awali

# patamea majani, matete na mafunjo.

8 Nako kutakuwa na njia kuu,

nayo itaitwa Njia ya Utakatifu.

Wasio safi hawatapita juu yake;

itakuwa kwa ajili ya wale

watembeao katika Njia ile;

yeye asafiriye juu yake,

ajapokuwa mjinga, hatapotea.

9 Huko hakutakuwepo na simba,

wala mnyama mkali hatapita njia hiyo,

wala hawatapatikana humo.

Ila waliokombolewa tu ndio watakaopita huko,

10 waliokombolewa naBwanawatarudi.

Wataingia Sayuni wakiimba;

furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao.

Watapata furaha na shangwe;

huzuni na majonzi vitakimbia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/35-96b8b13a1ac9d2d57620cc3bb28ea101.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five + ten =