Yeremia 33

Ahadi Ya Kurudishwa

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno laBwanalilimjia mara ya pili kusema:

2 “Hili ndiloBwanaasemalo, yeye aliyeumba dunia,Bwanaaliyeifanya na kuithibitisha,Bwanandilo jina lake:

3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika usiyoyajua.’

4 Kwa maana hili ndiloBwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga

5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.

6 “ ‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.

7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka katika nchi ya kutekwa kwao na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.

8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.

9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia juu ya mambo yote mazuri ninayoufanyia, nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’

10 “Hili ndilo asemaloBwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine

11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba yaBwana, wakisema,

“ ‘ “MshukuruniBwanaMwenye Nguvu Zote,

kwa maanaBwanani mwema;

upendo wake wadumu milele.”

Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asemaBwana.

12 “Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa pasipo na wanadamu wala wanyama, katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo na mbuzi.

13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo na mbuzi yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asemaBwana.

14 “ ‘Siku zinakuja,’ asemaBwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.

15 “ ‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki

lichipuke kutoka ukoo wa Daudi,

naye atafanya lile lililo haki na sawa

katika nchi.

16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa

na Yerusalemu ataishi salama.

Hili ndilo jina atakaloitwa:

BwanaNdiye Haki Yetu.’

17 Kwa maana hili ndilo asemaloBwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,

18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’ ”

19 Neno laBwanalikamjia Yeremia kusema:

20 “Hili ndilo asemaloBwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja Agano langu kuhusu mchana na usiku, ili mchana na usiku visiwepo kwa nyakati zake,

21 basi Agano langu na Daudi mtumishi wangu na Agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.

22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’ ”

23 Neno laBwanalikamjia Yeremia kusema:

24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwanaamezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu na hawawaoni tena kama taifa.

25 Hili ndilo asemaloBwana: ‘Kama sijathibitisha Agano langu na mchana na usiku na kuzisimika sheria za mbingu na nchi,

26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka kwenye nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/33-2a1aedabc8ed086cc555318a1a07e42a.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 × 3 =