Zaburi 138

Maombi Ya Shukrani

(Zaburi Ya Daudi)

1 Nitakusifu wewe, EeBwana,

kwa moyo wangu wote,

mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.

2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,

nami nitalisifu jina lako

kwa ajili ya upendo wako

na uaminifu,

kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako

juu ya vitu vyote.

3 Nilipoita, ulinijibu;

ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4 Wafalme wote wa dunia,

na wakusifu wewe EeBwana,

wakati wanaposikia

maneno ya kinywa chako.

5 Wao na waimbe kuhusu njia zaBwana,

kwa maana utukufu waBwanani mkuu.

6 IngawaBwanayuko juu,

humwangalia mnyonge,

bali mwenye kiburi

yeye anamjua kutokea mbali.

7 Nijapopita katikati ya shida,

wewe unayahifadhi maisha yangu,

unanyosha mkono wako

dhidi ya hasira ya adui zangu,

kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

8 Bwanaatatimiza kusudi lake kwangu,

EeBwana, upendo wako wadumu milele:

usiziache kazi za mikono yako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/138-d40040723c8c708f47c1cf84d80d04cd.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nine + 2 =