Zaburi 137

Maombolezo Ya Israeli Uhamishoni

1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza

tulipokumbuka Sayuni.

2 Kwenye miti ya huko

tulitundika vinubi vyetu,

3 kwa maana huko hao waliotuteka

walitaka tuwaimbie nyimbo,

watesi wetu walidai nyimbo za furaha;

walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja

kati ya nyimbo za Sayuni!”

4 Tutaimbaje nyimbo zaBwana,

tukiwa katika nchi ya kigeni?

5 Nikikusahau wewe, Ee Yerusalemu,

basi mkono wangu wa kuume

na usahau ujuzi wake.

6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu

kama sitakukumbuka wewe,

kama nisipokufikiri Yerusalemu

kuwa furaha yangu kubwa.

7 Kumbuka, EeBwana,

walichokifanya Waedomu,

siku ile Yerusalemu ilipoanguka.

Walisema, “Bomoa, Bomoa

mpaka kwenye misingi yake!”

8 Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,

ana furaha yeye ambaye atakulipiza wewe

kwa yale uliyotutenda sisi:

9 yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga

na kuwaponda juu ya miamba.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/137-aa0e5e3e6f830102379a716d0b434f81.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

16 − one =