Maombolezo Ya Israeli Uhamishoni
1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza
tulipokumbuka Sayuni.
2 Kwenye miti ya huko
tulitundika vinubi vyetu,
3 kwa maana huko hao waliotuteka
walitaka tuwaimbie nyimbo,
watesi wetu walidai nyimbo za furaha;
walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja
kati ya nyimbo za Sayuni!”
4 Tutaimbaje nyimbo zaBwana,
tukiwa katika nchi ya kigeni?
5 Nikikusahau wewe, Ee Yerusalemu,
basi mkono wangu wa kuume
na usahau ujuzi wake.
6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu
kama sitakukumbuka wewe,
kama nisipokufikiri Yerusalemu
kuwa furaha yangu kubwa.
7 Kumbuka, EeBwana,
walichokifanya Waedomu,
siku ile Yerusalemu ilipoanguka.
Walisema, “Bomoa, Bomoa
mpaka kwenye misingi yake!”
8 Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,
ana furaha yeye ambaye atakulipiza wewe
kwa yale uliyotutenda sisi:
9 yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga
na kuwaponda juu ya miamba.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/137-aa0e5e3e6f830102379a716d0b434f81.mp3?version_id=1627—