Zaburi 132

Maskani Ya Mungu Ya Milele Katika Sayuni

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 EeBwana, mkumbuke Daudi

na taabu zote alizozistahimili.

2 Aliapa kiapo kwaBwana

na akaweka nadhiri kwa yeye

Mwenye Nguvu wa Yakobo:

3 “Sitaingia nyumbani mwangu

au kwenda kitandani mwangu:

4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu,

wala kope zangu kusinzia,

5 mpaka nitakapompatiaBwanamahali,

makao kwa ajili ya yeye

Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

6 Tulisikia habari hii huko Efrathi,

# tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara

7 “Twendeni kwenye makao yake,

na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;

8 inuka, EeBwana, uje mahali pako pa kupumzikia,

wewe na Sanduku la nguvu zako.

9 Makuhani wako na wavikwe haki,

watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”

10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,

usimkatae masiya wako.

11 Bwanaalimwapia Daudi kiapo,

kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua:

“Mmoja wa wazao wako mwenyewe

nitamweka katika kiti chako cha enzi,

12 kama wanao watashika Agano langu

na sheria ninazowafundisha,

ndipo wana wao watarithi

kiti chako cha enzi milele na milele.”

13 Kwa maanaBwanaameichagua Sayuni,

amepaonea shauku pawe maskani yake:

14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele;

hapa ndipo nitakapoketi nikitawala,

kwa sababu nimepaonea shauku:

15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele:

nitashibisha maskini wake kwa chakula.

16 Nitawavika makuhani wake wokovu,

nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.

17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe,

# na kuweka taa kwa ajili ya masiyawangu.

18 Adui zake nitawavika aibu,

bali taji kichwani pake itang’aa sana.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/132-f29cd9d9b7dc1d8d234191c8996384b2.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fifteen − 8 =