Zaburi 131

Maombi Ya Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi.)

1 Moyo wangu hauna kiburi, EeBwana,

macho yangu hayajivuni;

sijishughulishi na mambo makuu kunizidi

wala mambo ya ajabu mno kwangu.

2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.

3 Ee Israeli, mtumainiBwana

tangu sasa na hata milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/131-437d8757822eb8e3099c323a4841105e.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

5 × 2 =