Maombi Ya Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu
(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi.)
1 Moyo wangu hauna kiburi, EeBwana,
macho yangu hayajivuni;
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi
wala mambo ya ajabu mno kwangu.
2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.
3 Ee Israeli, mtumainiBwana
tangu sasa na hata milele.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/131-437d8757822eb8e3099c323a4841105e.mp3?version_id=1627—