Sefania 1

1 Neno laBwanaambalo lilimjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:

Onyo La Maangamizi Yanayokuja

2 Bwanaasema,

“Nitafagia kila kitu

kutoka kwenye uso wa dunia.”

3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama;

nitafagilia mbali ndege wa angani

na samaki wa baharini.

Wafanyao maovu wajikwae, pamoja na hao waovu,

nami nitamkatilia mbali mwanadamu

atoke katika dunia,”

asemaBwana.

Dhidi Ya Yuda

4 “Nitaiadhibu Yuda

na wote wakaao Yerusalemu.

Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali

kila mabaki ya Baali,

majina ya wapagani na makuhani

waabuduo sanamu:

5 wale ambao husujudu juu ya mapaa

kuabudu jeshi la vitu vya angani,

wale ambao husujudu na kuapa kwaBwana

na ambao pia huapa kwa Malkamu,

6 wale ambao wanaacha kumfuataBwana,

wala hawamtafutiBwana

wala kutaka shauri lake.

7 Nyamazeni mbele zaBwanaMwenyezi,

kwa maana siku yaBwanaiko karibu.

Bwanaameandaa dhabihu,

amewaweka wakfu wale aliowaalika.

8 Katika siku ya dhabihu yaBwana

nitawaadhibu wakuu

na wana wa mfalme

na wale wote wanaovaa

nguo za kigeni.

9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao

hukwepa kukanyaga kizingiti,

ambao hujaza hekalu la miungu yao

kwa jeuri na udanganyifu.”

10 Bwanaasema, “Katika siku hiyo

kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki,

maombolezo kutoka mtaa wa pili,

na mshindo mkubwa kutoka vilimani.

11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni;

wafanyabiashara wenu

wote wameangamizwa,

wote ambao wanafanya

biashara ya fedha

wameangamizwa.

12 Wakati huo nitasaka katika mji wa Yerusalemu kwa taa

na kuwaadhibu wale ambao

wanakaa katika hali ya kuridhika,

ambao ni kama divai

iliyobaki kwenye machicha,

ambao hudhani, ‘Bwanahatafanya lo lote,

jema au baya.’

13 Utajiri wao utatekwa nyara,

nyumba zao zitabomolewa.

Watajenga nyumba,

lakini hawataishi ndani yake;

watapanda mizabibu

lakini hawatakunywa divai yake.

Siku Kubwa Ya Bwana

14 “Siku kubwa yaBwanaiko karibu:

iko karibu na inakuja haraka.

Sikilizeni! Kilio katika siku yaBwana

kitakuwa kichungu,

hata shujaa atapiga kelele.

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu,

siku ya fadhaa na dhiki,

siku ya uharibifu na ukiwa,

siku ya giza na utusitusi,

siku ya mawingu na giza nene,

16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita

dhidi ya miji yenye ngome

na dhidi ya minara mirefu.

17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea

kama wasio na macho,

kwa sababu wametenda dhambi

dhidi yaBwana.

Damu yao itamwagwa kama vumbi

na matumbo yao kama taka.

18 Fedha yao wala dhahabu yao

haitaweza kuwaokoa

katika siku hiyo ya ghadhabu yaBwana.

Katika moto wa wivu wake

dunia yote itateketezwa,

kwa maana ataleta mwisho

wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEP/1-7b0933800ffffe34ebb9fa5dcbd54cdb.mp3?version_id=1627—

Sefania 2

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja,

enyi taifa lisilo na aibu,

2 kabla ya wakati ulioamuriwa haujafika

na siku ile inayopeperusha kama makapi,

kabla hasira kali yaBwanahaijaja juu yenu,

kabla siku ya ghadhabu yaBwana

haijaja juu yenu.

3 MtafuteniBwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi,

ninyi ambao hufanya lile analoamuru.

Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu;

labda mtahifadhiwa

siku ya hasira yaBwana.

Dhidi Ya Ufilisti

4 Gaza utaachwa

na Ashkeloni utaachwa magofu.

Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu

na Ekroni utang’olewa.

5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari,

Enyi Wakerethi;

neno laBwanaliko dhidi yenu,

Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti.

“Mimi nitawaangamiza,

wala hakuna atakayebaki.”

6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi,

patakuwa mahali pa wachungaji

na mazizi ya kondoo.

7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda,

hapo watapata malisho.

Wakati wa jioni watajilaza chini

katika nyumba za Ashkeloni.

BwanaMungu wao atawatunza,

naye atawarudishia wafungwa wao.

Dhidi Ya Moabu Na Amoni

8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu

nazo dhihaka za Waamoni,

ambao waliwatukana watu wangu

na kufanya vitisho dhidi ya nchi yao.

9 Hakika, kama niishivyo,”

asemaBwanaMwenye Nguvu Zote,

Mungu wa Israeli,

“hakika Moabu itakuwa kama Sodoma,

Waamori kama Wagomora:

mahali pa magugu na mashimo ya chumvi,

nchi ya ukiwa milele.

Mabaki ya watu wangu watawateka nyara;

mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”

10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao,

kwa kutukana na kudhihaki

watu waBwanaMwenye Nguvu Zote.

11 Bwanaatakuwa wa kutisha kwao

wakati atakapoangamiza

miungu yote ya nchi.

Mataifa katika kila pwani yatamwabudu,

kila moja katika nchi yake.

Dhidi Ya Kushi

12 “Ninyi pia, Ee Wakushi,

mtauawa kwa upanga wangu.”

Dhidi Ya Ashuru

13 Mungu atanyosha mkono wake dhidi ya kaskazini

na kuangamiza Waashuru,

akiiacha Ninawi ukiwa

na pakame kama jangwa.

14 Makundi ya kondoo na ng’ombe yatajilaza pale,

viumbe vya kila aina.

Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba

wataishi juu ya nguzo zake.

Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani,

kifusi kitakuwa milangoni,

boriti za mierezi zitaachwa wazi.

15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha

wakijisikia salama.

Ulisema moyoni mwako,

“Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.”

Jinsi gani umekuwa gofu,

mahali pa kulala wanyama pori!

Wote wanaopita kando yake wanauzomea

na kutikisa mkono kwa dharau.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEP/2-1b18ca38d2ccf242c0429323ed47e58d.mp3?version_id=1627—

Sefania 3

Hatima Ya Yerusalemu

1 Ole wa mji wa wadhalimu,

waasi na waliotiwa unajisi!

2 Hautii mtu ye yote,

haukubali maonyo.

HaumtumainiBwana,

haukaribii karibu na Mungu wake.

3 Maafisa wake ni simba wangurumao,

watawala wake ni mbwa mwitu wa jioni,

ambao hawabakizi cho chote

kwa ajili ya asubuhi.

4 Manabii wake ni wenye kiburi,

ni wadanganyifu.

Makuhani wake hunajisi patakatifu

na kuihalifu sheria.

5 Bwanaaliye ndani yake ni mwenye haki,

hafanyi kosa.

Asubuhi kwa asubuhi hutoa haki yake,

kila kukipambazuka huitimiza,

bali mtu dhalimu hana aibu.

6 “Nimeyafutilia mbali mataifa,

ngome zao zimebomolewa.

Nimeziacha barabara ukiwa,

hakuna anayepita humo.

Miji yao imeharibiwa;

hakuna mmoja atakayeachwa:

hakuna hata mmoja.

7 Niliuambia huo mji,

‘Hakika utaniogopa na kukubali maonyo!’

Ndipo makao yake hayatafutiliwa mbali,

wala adhabu zangu zote hazitakuja juu yake.

Lakini walikuwa bado na shauku

kutenda kwa upotovu katika yote waliyofanya.”

8 Bwanaanasema,

“Kwa hiyo ningojee mimi,

siku nitakayosimama kuteka nyara.

Nimeamua kukusanya mataifa,

kukusanya falme

na kumimina ghadhabu yangu juu yao,

hasira yangu kali yote.

Dunia yote itateketezwa

kwa moto wa wivu wa hasira yangu.

9 “Ndipo nitatakasa midomo ya mataifa,

kwamba wote waweze kuliitia jina laBwana

na kumtumikia kwa pamoja.

10 Kutoka ng’ambo ya mito ya Kushi

watu wangu wanaoniabudu,

watu wangu waliotawanyika,

wataniletea sadaka.

11 Siku hiyo hutaaibishwa

kwa ajili ya makosa yote ulionitendea,

kwa sababu nitawaondoa kutoka mji huu

wale wote wanaoshangilia

katika kiburi chao.

Kamwe hutajivuna tena

katika kilima changu kitakatifu.

12 Lakini nitakuachia ndani yako

wapole na wanyenyekevu,

ambao wanatumaini jina laBwana.

13 Mabaki ya Israeli hayatafanya kosa;

hawatasema uongo,

wala udanganyifu hautakuwa

katika vinywa vyao.

Watakula na kulala

wala hakuna ye yote

atakayewaogopesha.”

14 Imba, Ee Binti Sayuni;

paza sauti, Ee Israeli!

Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote,

Ee Binti Yerusalemu!

15 Bwanaamekuondolea adhabu yako,

amewarudisha nyuma adui zako.

Bwana, Mfalme wa Israeli, yu pamoja nawe;

kamwe hutaogopa tena madhara yo yote.

16 Katika siku hiyo watauambia Yerusalemu,

“Usiogope, Ee Sayuni;

usiiache mikono yako ilegee.

17 BwanaMungu wako yu pamoja nawe,

yeye ni mwenye nguvu kuokoa.

Atakufurahia kwa furaha kubwa,

atakutuliza kwa pendo lake,

atakufurahia kwa kuimba.”

18 “Huzuni katika sikukuu zilizoamriwa

nitaziondoa kwenu;

hizo ni mzigo wa fedheha kwenu.

19 Katika wakati huo nitawashughulikia

wote waliokudhulumu;

nitaokoa kilema na kukusanya

wale ambao wametawanywa.

Nitawapa sifa na heshima

katika kila nchi ambamo waliaibishwa.

20 Wakati huo nitawakusanya;

wakati huo nitawaleta nyumbani.

Nitawapa sifa na heshima

miongoni mwa mataifa yote ya dunia

wakati nitakapowarudishia mateka yenu

mbele ya macho yenu hasa,”

asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEP/3-f093c4ce0bcf69b438670c034e31a7bd.mp3?version_id=1627—

Habakuki 1

1 Neno alilopokea nabii Habakuki.

Lalamiko La Habakuki

2 EeBwana, hata lini nitakuomba msaada,

lakini wewe husikilizi?

Au kukulilia, “Udhalimu!”

Lakini hutaki kuokoa?

3 Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma?

Kwa nini unavumilia makosa?

Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu;

kuna mabishano na mapambano kwa wingi.

4 Kwa hiyo sheria imepotoshwa,

nayo haki haipo kabisa.

Waovu wanawazunguka wenye haki,

kwa hiyo haki imepotoshwa.

Jibu La Bwana

5 “Yatazame mataifa,

uangalie na ushangae kabisa.

Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu

ambacho hungeamini,

hata kama ungeambiwa.

6 Nitawainua Wababeli,

watu hao wakatili na wenye haraka,

ambao hupita dunia yote

kuteka mahali pa kuishi

pasipo pao wenyewe.

7 Ni watu wanoogopwa na wanaotisha;

wenyewe ndio sheria yao

na huinua heshima yao wenyewe.

8 Farasi wao ni wepesi kuliko chui,

na wakali kuliko mbwa mwitu

wakati wa machweo.

Askari wapanda farasi wao huenda mbio;

waendesha farasi wao wanatoka mbali.

Wanaruka kasi kama tai ili kunyafua;

9 wote wanakuja tayari kwa fujo.

Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele

kama upepo wa jangwani

na kukusanya wafungwa

kama mchanga.

10 Wanawabeza wafalme

na kuwadhihaki watawala.

Wanaicheka miji yote,

iliyozungushiwa maboma;

wanafanya malundo ya udongo

na kuiteka hiyo miji.

11 Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele:

watu wenye hatia,

ambao nguvu zao ndio mungu wao.”

Lalamiko La Pili La Habakuki

12 EeBwana, je, wewe sio wa tangu milele?

Mungu wangu, Mtakatifu wangu, hatutakufa.

EeBwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu;

Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.

13 Macho yako ni safi mno hata yasiweze kutazama uovu,

wala huwezi kuvumilia makosa.

Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu?

Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu

wakiwameza wale wenye haki

kuliko wao wenyewe?

14 Umewafanya watu kama samaki baharini,

kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.

15 Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana,

anawakamata katika wavu wake,

anawakusanya katika juya lake,

kwa hiyo anashangilia na anafurahi.

16 Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake

na kuchoma uvumba kwa juya lake,

kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe

na anafurahia chakula kizuri.

17 Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake,

akiangamiza mataifa bila huruma?

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HAB/1-2499ca2309f069f88b812cf56b5f222e.mp3?version_id=1627—

Habakuki 2

1 Nitasimama katika zamu yangu

na kujiweka mwenyewe juu ya maboma;

nitatazama nione atakaloniambia,

na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.

Jibu La Bwana

2 KishaBwanaakajibu:

“Andika ufunuo huu

na ukaufanye wazi juu ya vibao

ili mpiga mbiu akimbie nao.

3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika;

unazungumzia mambo ya mwisho

na kamwe hautakosea.

Iwapo utakawia, wewe usubiri;

kwa hakika utakuja na hautachelewa.

4 “Tazama, amejaa majivuno,

anavyovitamani si vya unyofu.

Lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:

5 hakika mvinyo humsaliti;

ni mwenye kiburi na hana amani.

Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu

na kama kifo kamwe hatosheki;

anajikusanyia mataifa yote

na kuchukua watu wote mateka.

6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema,

“ ‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa

na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu!

Ataendelea hivi kwa muda gani?’

7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula?

Je, hawataamka na kukufanya utetemeke?

Kisha utakuwa mhanga kwao.

8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi,

watu waliobaki watakuteka nyara wewe.

Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji

na kila mmoja ndani yake.

9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu,

awekaye kiota chake juu,

ili kukimbia makucha ya uharibifu!

10 Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi,

ukiaibisha nyumba yako mwenyewe

na kupotewa na maisha yako.

11 Mawe ya kuta yatapiga kelele,

na mihimili ya kazi ya mbao

itarudisha mwangwi wake.

12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga

damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!

13 Je,BwanaMwenye Nguvu Zote hakuonyesha

kwamba kazi ya wanadamu

ni mafuta tu kwa ajili ya moto,

na kwamba mataifa

yanajichosha bure?

14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu waBwana,

kama maji yaifunikavyo bahari.

15 “Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo,

akiimimina kutoka kwenye kiriba

cha mvinyo mpaka wamelewa,

ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.

16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu.

Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue!

Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume waBwanakinakujia,

na aibu itafunika utukufu wako.

17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika,

na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha.

Kwa sababu umemwaga damu ya mtu,

umeharibu nchi na miji

na kila mmoja aliyeko ndani yake.

18 “Sanamu ina thamani gani,

kwani mwanadamu ndiye aliyechonga?

Ama kinyago kinachofundisha uongo?

Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza

hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe;

hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.

19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’

Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’

Je, linaweza kuongoza?

Limefunikwa kwa dhahabu na fedha,

hakuna pumzi ndani yake.

20 LakiniBwanayuko katika Hekalu lake takatifu;

dunia yote na inyamaze mbele yake.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HAB/2-04979c73066568b41ab1d6b764839675.mp3?version_id=1627—

Habakuki 3

Maombi Ya Habakuki

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.

2 Bwana, nimezisikia sifa zako,

nami naogopa, EeBwana.

Fufua kazi yako katikati ya miaka,

katikati ya miaka tangaza habari yako;

katika ghadhabu kumbuka rehema.

3 Mungu alitoka Temani,

yeye aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani.

Utukufu wake ulifunika mbingu

na sifa zake zikaifunika dunia.

4 Mng’ao wake ulikuwa kama jua lichomozalo,

mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake,

ambako nguvu zake zilifichwa.

5 Tauni ilimtangulia;

maradhi ya kuambukiza

yalifuata nyayo zake.

6 Alisimama, akaitikisa dunia;

alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke.

Milima ya zamani iligeuka mavumbi

na vilima vilivyozeeka vikaanguka.

Njia zake ni za milele.

7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki,

na makazi ya Midiani katika maumivu makali.

8 EeBwana, uliikasirikia mito?

Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito?

Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi

wako na magari yako ya ushindi?

9 Uliufunua upindi wako

na kuita mishale mingi.

Uliigawa dunia kwa mito;

10 milima ilikuona ikatetemeka.

Mafuriko ya maji yakapita huko;

vilindi vilinguruma

na kuinua mawimbi yake juu.

11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni

katika mng’ao wa mishale yako inayoruka,

na katika mng’ao wa mkuki wako umeremetao.

12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia

na katika hasira ulikanyaga mataifa.

13 Ulikuja kuwaokoa watu wako,

kumwokoa masiya wako.

Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu,

ukamvua toka kichwani hadi wayo.

14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake

wakati mashujaa wake

walipofurika nje kwa kishindo kututawanya,

wakifurahi kama waliokaribu kutafuna

wale wanyonge waliokuwa mafichoni.

15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako,

ukisukasuka maji makuu.

16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu,

midomo yangu ikatetemeka kwa hofu

niliposikia sauti;

uchakavu ukanyemelea mifupa yangu,

na miguu yangu ikatetemeka.

Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa

kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.

17 Ingawa mtini hauchanui maua

na hakuna zabibu juu ya mizabibu,

ingawaje mzeituni hauzai,

na hata mashamba hayatoi chakula,

iwapo hakuna kondoo katika banda

wala ng’ombe katika zizi,

18 hata hivyo nitashangilia katikaBwana,

nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.

19 BwanaMwenyezi ni nguvu yangu;

huifanya miguu yangu kama miguu ya paa,

huniwezesha kupita juu ya vilima.

(Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.)

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HAB/3-bec1d4175c363e1dfe8d2d3391793194.mp3?version_id=1627—

Nahumu 1

1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

2 Bwanani mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwanahulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwanahulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

3 Bwanasi mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwanahataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

4 Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

5 Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

7 Bwanani Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

8 lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

9 Shauri baya lo lote wapangalo dhidi yaBwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

10 Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi yaBwana

na kushauri uovu.

12 Hili ndilo asemaloBwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, Ee Yuda,

sitakutesa tena.

13 Sasa nitavunja nira zao kutoka katika shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

14 Hii ndiyo amriBwanaaliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

15 Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sheherekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NAM/1-e7b3a0bd3e138a8d3423ddb036387da5.mp3?version_id=1627—

Nahumu 2

Ninawi Kuanguka

1 Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi.

Linda ngome,

chunga barabara,

jitieni nguvu wenyewe,

kusanya nguvu zako zote!

2 Bwanaatarudisha fahari ya Yakobo,

kama fahari ya Israeli,

ingawa waangamizi wamewaacha ukiwa

na wameharibu mizabibu yao.

3 Ngao za askari wake ni nyekundu,

mashujaa wamevaa nguo nyekundu.

Chuma kwenye magari ya vita chametameta,

katika siku aliyoyaweka tayari,

mikuki ya mierezi inametameta.

4 Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani,

yakikimbia nyuma na mbele uwanjani.

Yanaonekana kama mienge ya moto;

yanakwenda kasi kama umeme.

5 Anaita vikosi vilivyochaguliwa,

lakini bado wanajikwaa njiani.

Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wa mji,

ile ngao ya kuwakinga imetayarishwa.

6 Malango ya mto yamefunguliwa wazi,

na jumba la kifalme limeanguka.

7 Imeagizwa kwamba mji uchukuliwe

na upelekwe uhamishoni.

Vijakazi wake wanaomboleza kama hua

na kupigapiga vifua vyao.

8 Ninawi ni kama dimbwi,

nayo maji yake yanakauka.

Wanalia, “Simama! Simama!”

Lakini hakuna anayegeuka nyuma.

9 Chukueni nyara za fedha!

Chukueni nyara za dhahabu!

Wingi wake hauna mwisho,

utajiri kutoka hazina zake zote!

10 Ameharibiwa, ametekwa nyara, ameachwa uchi!

Mioyo inayeyuka, magoti yanalegea,

miili inatetemeka,

na kila uso umebadilika rangi.

11 Liko wapi sasa pango la simba,

mahali ambapo waliwalisha watoto wao,

ambapo simba dume na simba jike walikwenda

na ambapo wana simba walikwenda

bila kuogopa cho chote?

12 Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake,

alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake,

akijaza makao yake kwa alivyoua

na mapango yake kwa mawindo.

13 BwanaMwenye Nguvu Zote anatangaza,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Magari yenu ya vita nitayateketeza kwa moto,

na upanga utakula wana simba wako.

Sitawaachia mawindo juu ya nchi.

Sauti za wajumbe wako

hazitasikika tena.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NAM/2-a38be8b5316b20df831b93932f1e5efe.mp3?version_id=1627—

Nahumu 3

Ole Wa Ninawi

1 Ole wa mji umwagao damu,

uliojaa uongo,

umejaa nyara,

usiokosa kuwa na vitu vya kuteka nyara.

2 Kelele za mijeledi,

vishindo vya magurudumu,

farasi waendao mbio

na mshtuo wa magari ya vita!

3 Wapanda farasi wanaenda mbio,

panga zinameremeta,

na mikuki inang’aa!

Majeruhi wengi,

marundo ya maiti,

idadi kubwa ya miili isiyohesabika,

watu wanajikwaa juu ya mizoga:

4 yote haya kwa sababu ya wingi wa tamaa za kahaba,

anayeshawishi, bibi wa mambo ya uchawi,

anayewatia utumwani mataifa kwa ukahaba wake

na pia jamaa za watu kwa ulozi wake.

5 BwanaMwenye Nguvu Zote anasema,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Nitafunika uso wako kwa gauni lako.

Nitaonyesha mataifa uchi wako

na falme aibu yako.

6 Nitakutupia uchafu,

nitakufanyia dharau

na kukufanya kioja.

7 Wote wanaokuona watakukimbia na kusema,

‘Ninawi ipo katika kuangamia:

ni nani atakayeomboleza kwa ajili yake?’

Nitampata wapi ye yote wa kukufariji?”

8 Je, wewe ni bora kuliko No-Amoni,

uliopo katika Mto Nile,

uliozungukwa na maji?

Mto ulikuwa kinga yake,

nayo maji yalikuwa ukuta wake.

9 Kushina Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka;

Putu na Libya walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.

10 Hata hivyo alichukuliwa mateka

na kwenda uhamishoni.

Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande

kwenye mwanzo wa kila barabara.

Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima,

na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.

11 Wewe pia utalewa;

utakwenda mafichoni

na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.

12 Ngome zako zote ni kama mitini

yenye matunda yake ya kwanza yaliyoiva;

wakati inapotikiswa,

tini huanguka kwenye kinywa chake alaye.

13 Tazama vikosi vyako:

wote ni wanawake!

Malango ya nchi yako

yamekuwa wazi kwa adui zako;

moto umeteketeza mapingo yake.

14 Teka maji kwa ajili ya kuzingirwa kwako,

imarisha ulinzi wako,

Ufanyie udongo wa mfinyanzi kazi,

yakanyage matope,

karabati tanuru ya kuchomea matofali!

15 Huko moto utakuteketeza,

huko upanga utakuangusha chini

na kama vile panzi, watakumaliza.

Ongezeka kama panzi,

ongezeka kama nzige!

16 Umeongeza idadi ya wafanyabiashara wako

mpaka wamekuwa wengi kuliko nyota za angani,

lakini kama nzige wanaacha nchi tupu

kisha huruka na kwenda zake.

17 Walinzi wako ni kama nzige,

maafisa wako ni kama makundi ya nzige

watuao kwenye kuta wakati wa siku ya baridi:

lakini wakati jua linapotokea wanaruka kwenda zao,

na hakuna ajuaye waendako.

18 Ee mfalme wa Ashuru, wachungajia wako wanasinzia;

wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika.

Watu wako wametawanyika juu ya milima

bila kuwa na mtu ye yote wa kuwakusanya.

19 Hakuna kitu kinachoweza kuponya jeraha lako;

jeraha lako ni la kukuua.

Kila anayesikia habari zako,

hupiga makofi kwa kuanguka kwako,

kwa kuwa ni nani ambaye hajaguswa

na ukatili wako usio na mwisho?

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NAM/3-042fb57d52bd9f9110981ba6bbb7d98c.mp3?version_id=1627—

Mika 1

1 Neno laBwanalilimjia Mika, Mmorashti, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.

2 Sikia, Ee mataifa, enyi nyote,

sikilizeni, Ee dunia na wote mliomo ndani yake,

iliBwanaMwenyezi ashuhudie dhidi yenu,

Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.

Hukumu Dhidi Ya Samaria Na Yerusalemu

3 Tazama!Bwanaanakuja kutoka makao yake;

anashuka na kukanyaga

mahali palipoinuka juu pa dunia.

4 Milima inayeyuka chini yake

na mabonde yanagawanyika

kama nta mbele ya moto,

kama maji yatiririkayo kasi

kwenye mtelemko.

5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo,

ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli.

Kosa la Yakobo ni lipi?

Je, sio Samaria?

Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini?

Je, sio Yerusalemu?

6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto,

mahali pa kuotesha mizabibu.

Nitayamwaga mawe yake katika bonde

na kuacha wazi misingi yake.

7 Sanamu zake zote

zitavunjwa vipande vipande;

zawadi zake zote za Hekalu

zitachomwa kwa moto;

nitaharibu vinyago vyake vyote.

Kwa kuwa alikusanya zawadi zake

kutokana na ujira wa kahaba,

nazo zitatumika tena

kulipa mishahara ya kahaba.”

Kulia Na Kuomboleza

8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza;

nitatembea bila viatu na tena uchi.

Nitabweka kama mbweha

na kuomboleza kama bundi.

9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki;

limekuja Yuda.

Limefika hasa kwenye lango la watu wangu,

hata Yerusalemu kwenyewe.

10 Usiliseme hili huko Gathi;

usilie hata kidogo.

Huko Beth-le-Afra

ugaegae mavumbini.

11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu,

ninyi mkaao Shafiri.

Wale waishio Saanani

hawatatoka nje.

Beth-Eseli iko katika maombolezo;

kinga yake imeondolewa kwako.

12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu

wakingoja msaada,

kwa sababu maangamizi yamekuja

kutoka kwaBwana,

hata katika lango la Yerusalemu.

13 Enyi mkaao Lakishi,

fungeni farasi kwenye magari ya vita.

Mlikuwa chanzo cha dhambi

kwa Binti Sayuni,

kwa kuwa makosa ya Israeli

yalikutwa kwako.

14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi

zawadi za kuagana.

Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu

kwa wafalme wa Israeli.

15 Nitawaleteeni atakayewashinda

ninyi mnaoishi Maresha.

Yeye aliye utukufu wa Israeli

atakuja Adulamu.

16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza

kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia;

jifanyieni upara kama tai,

kwa kuwa watawaacha

na kwenda uhamishoni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/1-c497a0b0b0e802008686ab0250d6b152.mp3?version_id=1627—