Mika 2

Mipango Ya Mwanadamu Na Ya Mungu

1 Ole kwa wale wapangao uovu,

kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao!

Kunapopambazuka wanalitimiza

kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.

2 Wanatamani mashamba na kuyakamata,

pia nyumba na kuzichukua.

Wanamlaghai mwanaume nyumba yake,

mwanadamu mwenzake urithi wake.

3 Kwa hiyo,Bwanaasema:

“Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa,

ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe.

Hamtatembea tena kwa majivuno,

kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.

4 Siku hiyo watu watawadhihaki,

watawafanyia mzaha

kwa wimbo huu wa maombolezo:

‘Tumeangamizwa kabisa;

mali ya watu wangu imegawanywa.

Ameninyang’anya!

Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’ ”

5 Kwa hiyo hutakuwa na ye yote katika kusanyiko laBwana

wa kugawanya mashamba kwa kura.

Manabii Wa Uongo

6 Manabii wao husema, “Usitabiri.

Usitabiri kuhusu vitu hivi;

aibu haitatupata.”

7 Je, ingesemwa, Ee nyumba ya Yakobo:

“Je, Roho waBwanaamekasirika?

Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?”

“Je, maneno yangu hayamfanyii mema

yeye ambaye njia zake ni nyofu?

8 Siku hizi watu wangu wameinuka

kama adui.

Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita

pasipo kujali,

kama watu warudio kutoka vitani.

9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu

kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza.

Unaondoa baraka yangu

kwa watoto wao milele.

10 Inuka, nenda zako!

Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia,

kwa sababu pametiwa unajisi,

pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.

11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema,

‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’

angekuwa ndiye nabii

anayekubalika na watu hawa!

Ahadi Ya Ukombozi

12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, Ee Yakobo,

Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli.

Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi,

kama kundi kwenye malisho yake,

mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.

13 Yeye afunguaye njia atawatangulia;

watapita kwenye lango na kutoka nje.

Mfalme wao atawatangulia,

Bwanaatakuwa kiongozi.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/2-61aa4bb2bd6125b458447424fc120017.mp3?version_id=1627—

Mika 3

Viongozi Na Manabii Wakemewa

1 Kisha nikasema,

“Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo,

enyi watawala wa nyumba ya Israeli.

Je, hampaswi kujua hukumu,

2 ninyi mnaochukia mema

na kupenda maovu;

ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi

na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;

3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu,

mnaowachuna ngozi

na kuvunja mifupa yao vipande vipande;

mnaowakatakata kama nyama

ya kuwekwa kwenye sufuria

na kama nyama

ya kuwekwa kwenye chungu?”

4 Kisha watamliliaBwana,

lakini hatawajibu.

Wakati huo atawaficha uso wake

kwa sababu ya uovu waliotenda.

5 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu,

mtu akiwalisha,

wanatangaza ‘amani’;

kama hakufanya hivyo,

wanaandaa kupigana vita dhidi yake.

6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono,

na giza, msiweze kubashiri.

Jua litawachwea manabii hao,

nao mchana utakuwa giza kwao.

7 Waonaji wataaibika

na waaguzi watafedheheka.

Wote watafunika nyuso zao

kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”

8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu,

nimejazwa Roho waBwana,

haki na uweza,

kumtangazia Yakobo kosa lake,

na Israeli dhambi yake.

9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo,

enyi watawala wa nyumba ya Israeli,

mnaodharau haki

na kupotosha kila lililo sawa;

10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu

na Yerusalemu kwa uovu.

11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa,

na makuhani wake wanafundisha kwa malipo,

nao manabii wake wanatabiri kwa fedha.

Hata hivyo wanamwegemeaBwanana kusema,

“Je,Bwanasi yumo miongoni mwetu?

Hakuna maafa yatakayotupata.”

12 Kwa hiyo kwa sababu yenu,

Sayuni italimwa kama shamba,

Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto

na kilima cha Hekalu

kuwa kama kichuguu

kilichofunikwa na vichaka.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/3-ab13fe7fa79e1ebce9ede403a655dfa0.mp3?version_id=1627—

Mika 4

Mlima Wa Bwana

1 Katika siku za mwisho

mlima wa Hekalu laBwanautaimarishwa

na kuwa mkuu kuliko milima yote;

utainuliwa juu ya vilima

na mataifa yatamiminika humo.

2 Mataifa mengi yatakuja na kusema,

“Njoni, twendeni mlimani kwaBwana,

kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.

Atatufundisha njia zake,

ili tutembee katika mapito yake.”

Sheria itatoka Sayuni,

neno laBwanalitatoka Yerusalemu.

3 Atahukumu kati ya mataifa mengi

na ataamua migogoro ya mataifa

yenye nguvu na yaliyo mbali.

Watafua panga zao ziwe majembe ya kulimia

na mikuki yao kuwa miundu ya kukatia matawi.

Taifa halitachukua upanga dhidi ya taifa,

wala hawatajifunza vita tena.

4 Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake

na chini ya mtini wake,

wala hakuna mtu atakayewaogopesha,

kwa kuwaBwanaMwenye Nguvu Zote amesema.

5 Mataifa yote yanaweza kutembea

katika jina la miungu yao;

sisi tutatembea katika jina laBwana

Mungu wetu milele na milele.

Mpango Wa Bwana

6 “Katika siku hiyo,” asemaBwana,

“nitawakusanya walemavu;

nitawakusanya walio uhamishoni

na wale niliowahuzunisha.

7 Nitawafanya walemavu kuwa mabaki,

wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu.

Bwanaatatawala juu yao katika Mlima Sayuni

kuanzia siku hiyo na hata milele.

8 Lakini kuhusu wewe, Ee mnara wa ulinzi wa kundi,

Ee ngome ya Binti Sayuni,

milki ya awali itarudishwa kwako,

ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”

9 Kwa nini sasa unalia kwa nguvu:

kwani huna mfalme?

Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate

kama ya mwanamke

aliye na utungu wa kuzaa?

10 Gaagaa kwa utungu, Ee Binti Sayuni,

kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa,

kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji

ukapige kambi uwanjani.

Utakwenda Babeli;

huko utaokolewa.

HukoBwanaatakukomboa

kutoka mikononi mwa adui zako.

11 Lakini sasa mataifa mengi

yamekusanyika dhidi yako.

Wanasema, “Mwache anajisiwe,

macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”

12 Lakini hawayajui

mawazo yaBwana;

hawauelewi mpango wake,

yeye awakusanyaye kama miganda

kwenye sakafu ya kupuria.

13 “Inuka upure, Ee Binti Sayuni,

kwa kuwa nitakupa pembe za chuma;

nitakupa kwato za shaba

na utavunja vipande vipande mataifa mengi.”

Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwaBwana,

utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/4-afe6010954f60b8538d4c7d5d9bcb9dc.mp3?version_id=1627—

Mika 5

Mtawala Aliyeahidiwa Kutoka Bethlehemu

1 Panga majeshi yako, Ee mji wa majeshi,

kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu.

Watampiga mtawala wa Israeli

shavuni kwa fimbo.

2 “Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi,

ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda,

kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu

yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,

ambaye asili yake ni kutoka zamani,

kutoka milele.”

3 Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati

mwanamke aliye na utungu atakapozaa

na ndugu zake wengine warudi

kujiunga na Waisraeli.

4 Atasimama na kulichunga kundi lake

katika nguvu yaBwana,

katika utukufu wa jina laBwanaMungu wake.

Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo

ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.

5 Naye atakuwa amani yao.

Ukombozi Na Uharibifu

Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu

na kupita katika ngome zetu,

tutawainua wachungaji saba dhidi yake,

hata viongozi wanane wa watu.

6 Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga,

nchi ya Nimrodi kwa upanga.

Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru

atakapoivamia nchi yetu

na kuingia katika mipaka yetu.

7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa

katikati ya mataifa mengi

kama umande kutoka kwaBwana,

kama manyunyu juu ya majani,

ambayo hayamngoji mtu

wala kukawia kwa mwanadamu.

8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa,

katikati ya mataifa mengi,

kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni,

kama mwana simba miongoni

mwa makundi ya kondoo,

ambaye anaumiza vibaya na kuwararua

kila anapopita katikati yao,

wala hakuna awezaye kuokoa.

9 Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako,

nao adui zako wote wataangamizwa.

10 “Katika siku ile,” asemaBwana,

“nitaangamiza farasi zenu katikati yenu

na kubomoa magari yenu ya vita.

11 Nitaiangamiza miji ya nchi yenu

na kuziangusha chini ngome zenu zote.

12 Nitaangamiza uchawi wenu

na hamtapiga tena ramli.

13 Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga

na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu;

hamtasujudia tena

kazi ya mikono yenu.

14 Nitang’oa nguzo za Ashera katikati yenu

na kubomoa miji yenu.

15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu

juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/5-89f2f5314d9cbc53b197da6836b87709.mp3?version_id=1627—

Mika 6

Shauri La Bwana Dhidi Ya Israeli

1 Sikiliza asemaloBwana:

“Simama, tetea shauri lako mbele ya milima;

vilima na visikie lile unalotaka kusema.

2 Sikilizeni, Ee milima, mashtaka yaBwana,

sikilizeni, enyi misingi ya milele ya dunia.

Kwa kuwaBwanaana shauri dhidi ya watu wake;

anatoa mashtaka dhidi ya Israeli.

3 “Watu wangu, nimewatendea nini?

Nimewalemea kwa jinsi gani? Mnijibu.

4 Nimewatoa kutoka Misri na kuwakomboa

kutoka nchi ya utumwa.

Nilimtuma Mose awaongoze,

pia Aroni na Miriamu.

5 Watu wangu, kumbukeni jinsi Balaki mfalme wa Moabu

alivyofanya shauri

na kile Balamu mwana wa Beori alichojibu.

Kumbukeni safari yenu kutoka Shitimu mpaka Gilgali,

ili mfahamu matendo ya haki yaBwana.”

6 NimjieBwanana kitu gani na kusujudu

mbele za Mungu aliyetukuka?

Je, nije mbele zake na sadaka za kuteketezwa,

nije na ndama za mwaka mmoja?

7 Je,Bwanaatafurahishwa na kondoo dume elfu,

au mito elfu kumi ya mafuta?

Je, nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu,

mtoto wangu mwenyewe

kwa ajili ya dhambi ya nafsi yangu?

8 Amekuonyesha yaliyo mema, ee mwanadamu.

Bwanaanataka nini kwako?

Ila kutenda kwa haki na kupenda rehema,

na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako.

Hatia Na Adhabu Ya Israeli

9 Sikiliza!Bwanaanauita mji:

kulicha jina lako ni hekima:

“Tii hiyo fimbo na yeye aliyeiamuru.

10 Je, bado nisahau, Ee nyumba ya uovu,

hazina yako uliyopata kwa udanganyifu

na vipimo vilivyopunguka,

ambavyo vimelaaniwa?

11 Je, naweza kuhukumu kuwa

mtu mwenye mizani ya udanganyifu hana hatia,

aliye na mfuko wa mawe ya kupimia ya uongo?

12 Matajiri wake ni wajeuri;

watu wake ni waongo

na ndimi zao zinazungumza

kwa udanganyifu.

13 Kwa hiyo, nimeanza kukuharibu,

kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.

14 Mtakula lakini hamtashiba;

matumbo yenu bado yatakuwa matupu.

Mtaweka akiba lakini hamtaokoa cho chote,

kwa sababu mtakachoweka akiba

nitatoa kwa upanga.

15 Mtapanda lakini hamtavuna;

mtakamua zeituni lakini

hamtatumia mafuta yake.

Mtakamua zabibu

lakini hamtakunywa hiyo divai.

16 Mmezishika sheria za Omri

na matendo yote ya nyumba ya Ahabu,

tena umefuata desturi zao.

Kwa hiyo nitakutoa kwa maangamizi

na watu wako kuwa dhihaka;

mtachukua dharau za mataifa.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/6-ff861ca39e31ef65682dde44fedc0dd1.mp3?version_id=1627—

Mika 7

Taabu Ya Israeli

1 Taabu gani hii niliyo nayo!

Nimefanana na yule akusanyaye

matunda ya kiangazi,

aokotaye masazo baada ya kuvunwa

shamba la mizabibu;

hakuna kishada chenye matunda ya kula,

hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.

2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka katika nchi;

hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki.

Watu wote wanavizia kumwaga damu,

kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.

3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya,

mtawala anadai zawadi,

hakimu anapokea rushwa,

wenye nguvu wanaamuru wanachotaka:

wote wanafanya shauri baya pamoja.

4 Aliye mwema kupita wote kati yao

ni kama mchongoma,

anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao

ni mbaya kuliko uzio wa miiba.

Siku ya walinzi wako imewadia,

siku atakayokutembelea Mungu.

Sasa ni wakati wao

wa kuchanganyikiwa.

5 Usimtumaini jirani;

usiweke matumaini kwa rafiki.

Hata kwa yule alalaye kifuani mwako

uwe mwangalifu kwa maneno yako.

6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake,

naye binti huinuka dhidi ya mama yake,

mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake:

adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.

7 Lakini mimi, namtazamaBwanakwa matumaini,

namngoja Mungu Mwokozi wangu;

Mungu wangu atanisikia mimi.

Israeli Atainuka

8 Usifurahie msiba wangu, Ee adui yangu!

Ingawa nimeanguka, nitainuka.

Japo ninaketi gizani,

Bwanaatakuwa nuru yangu.

9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake,

nitabeba ghadhabu yaBwana,

mpaka atakaponitetea shauri langu

na kuithibitisha haki yangu.

Atanileta nje kwenye mwanga,

nami nitaiona haki yake.

10 Kisha adui yangu ataliona

naye atafunikwa na aibu,

yule aliyeniambia,

“Yu wapiBwanaMungu wako?”

Macho yangu yataona kuanguka kwake,

hata sasa atakanyagwa chini ya mguu

kama tope barabarani.

11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia,

siku ya kupanua mipaka yako.

12 Siku hiyo watu watakuja kwako

kutoka Ashuru na miji ya Misri,

hata kutoka Misri hadi Eufrati

na kutoka bahari hadi bahari

na kutoka mlima hadi mlima.

13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake,

kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Sala Na Sifa

14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako,

kundi la urithi wako,

ambalo linaishi peke yake msituni,

katika nchi ya malisho yenye rutuba.

Waache walishe katika Bashani na Gileadi

kama ilivyokuwa siku za kale.

15 “Kama siku zile mlipotoka Misri,

nitawaonyesha maajabu yangu.”

16 Mataifa yataona na kuaibika,

waliondolewa nguvu zao zote.

Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao

na masikio yao yatakuwa na uziwi.

17 Wataramba mavumbi kama nyoka,

kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi.

Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka;

watamgeukiaBwanaMungu wetu kwa hofu

nao watakuogopa.

18 Ni nani Mungu kama wewe,

ambaye anaachilia dhambi

na kusamehe makosa

ya mabaki ya urithi wake?

Wewe huwi na hasira milele,

bali unafurahia kuonyesha rehema.

19 Utatuhurumia tena,

utazikanyaga dhambi zetu

chini ya nyayo zako,

na kutupa maovu yetu yote

katika vilindi vya bahari.

20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo,

nawe utamwonyesha Abrahamu rehema,

kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu

siku za kale.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/7-ca45d233b469bf8ef7c59311f5f4c08e.mp3?version_id=1627—

Yona 1

Yona Anamkimbia Bwana

1 Neno laBwanalilimjia Yona mwana wa Amitai:

2 “Nenda katika mji mkubwa wa Ninawi ukahubiri juu yake, kwa sababu uovu wake umekuja juu mbele zangu.”

3 Lakini Yona alimkimbiaBwanana kuelekea Tarshishi. Alishuka mpaka Yafa, ambapo alikuta meli iliyokuwa imepangwa kuelekea bandari ile. Baada ya kulipa nauli, akapanda melini na kuelekea Tarshishi ili kumkimbiaBwana.

4 NdipoBwanaakatuma upepo mkali baharini, nayo dhoruba kali sana ikavuma hata meli ikawa hatarini kuvunjika.

5 Mabaharia wote waliogopa na kila mmoja akamlilia mungu wake mwenyewe. Nao wakatupa mizigo baharini ili meli ipungue uzito.

Lakini Yona alikuwa ametelemkia chumba cha ndani ya meli, mahali ambapo alilala na kupatwa na usingizi mzito.

6 Nahodha akamwendea na kusema, “Wewe unawezaje kulala? Amka ukamwite mungu wako! Huenda akatuangalia, tusiangamie.”

7 Kisha mabaharia wakasemezana wao kwa wao, “Njoni, tupige kura tumtafute anayehusika na maafa haya.” Wakapiga kura, kura ikamwangukia Yona.

8 Kwa hiyo walimuuliza, “Tuambie, ni nani anayehusika kwa kutuletea tatizo hili lote? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Nchi yako ni ipi? Wewe ni kutoka taifa lipi?”

9 Akajibu, “Mimi ni Mwebrania, nami namwabuduBwana, Mungu wa Mbinguni, aliyeumba bahari na nchi kavu.”

10 Hili liliwaogopesha nao wakamuuliza,

“Umefanya nini?” (Walijua alikuwa anamkimbiaBwana, kwa sababu alishawaambia hivyo.)

11 Bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Kwa hiyo walimuuliza, “Tukutendee nini ili kufanya bahari itulie kwa ajili yetu?”

12 Akawajibu, “Niinueni mnitupe baharini, nayo itakuwa shwari. Ninajua mawimbi haya makubwa yamewatokea kwa ajili ya kosa langu.”

13 Badala yake, wale watu walijitahidi kupiga makasia wawezavyo ili wapate kurudi pwani. Lakini hawakuweza, kwa kuwa bahari ilizidi kuchafuka kuliko mwanzo.

14 Ndipo wakamliliaBwana, “EeBwana, tafadhali usituue kwa kuondoa uhai wa mtu huyu. Usituhesabie hatia kwa kuutoa uhai wa mtu asiyekuwa na hatia, kwa kuwa wewe EeBwana, umefanya kama ilivyokupendeza.”

15 Kisha walimchukua Yona, wakamtupa baharini nayo bahari iliyokuwa imechafuka ikatulia.

16 Katika jambo hili watu wakamwogopaBwanasana, wakamtoleaBwanadhabihu na kumwekea nadhiri.

17 LakiniBwanaakamwandaa nyangumikummeza Yona, naye Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu mchana na usiku.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JON/1-88d9c5090d23b0666bf1c2f3f721558c.mp3?version_id=1627—

Yona 2

Maombi ya Yona Katika Tumbo la Nyangumi

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwombaBwanaMungu wake.

2 Akasema:

“Katika shida yangu nalimwitaBwana,

naye akanijibu.

# Kutoka kina cha kaburiniliomba msaada,

nawe ukasikiliza kilio changu.

3 Ulinitupa kwenye kilindi,

ndani kabisa ya moyo wa bahari,

mikondo ya maji ilinizunguka,

mawimbi yako yote na viwimbi

vilipita juu yangu.

4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa

mbali na uso wako,

hata hivyo nitatazama tena

kuelekea Hekalu lako takatifu.’

5 Maji yaliyonimeza yalinitisha,

kilindi kilinizunguka;

# mwaniulijisokota kichwani pangu.

6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima,

makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele.

Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni,

EeBwanaMungu wangu.

7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka,

nilikukumbuka wewe,Bwana,

nayo maombi yangu yalikufikia wewe,

katika Hekalu lako takatifu.

8 “Wale watu wanaong’ang’ana na sanamu zisizofaa

hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.

9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,

nitakutolea dhabihu.

Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza.

Wokovu watoka kwaBwana.”

10 BasiBwanaakamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JON/2-1ef80839c1ff5f108dbc49b6c823801f.mp3?version_id=1627—

Yona 3

Yona Aenda Ninawi

1 Ndipo neno laBwanalikamjia Yona mara ya pili:

2 “Ondoka uende katika mji mkubwa wa Ninawi, ukautangazie ujumbe ninaokupa.”

3 Yona akalitii neno laBwananaye akaenda Ninawi. Basi Ninawi ulikuwa mji maarufu sana, ilichukua siku tatu kuuzunguka.

4 Siku ya kwanza, Yona aliingia mjini. Akatangaza: “Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.”

5 Watu wa Ninawi wakamwamini Mungu, wakatangaza kufunga, watu wote kuanzia mkubwa sana hadi yule mdogo kabisa, wakavaa nguo za gunia.

6 Habari zilipomfikia mfalme wa Ninawi, aliondoka kwenye kiti chake cha enzi, akavua majoho yake ya kifalme, akajifunika nguo ya gunia kisha akaketi chini mavumbini.

7 Ndipo akatoa tangazo katika Ninawi yote:

“Kwa amri ya mfalme na wakuu wake:

“Msiruhusu mtu ye yote au mnyama, makundi ya ng’ombe au wanyama wengine wafugwao, kuonja kitu cho chote, msiwaruhusu kula wala kunywa.

8 Bali wanadamu na wanyama wafunikwe kwa nguo za gunia. Kila mmoja afanye hima kumwomba Mungu. Waziache njia zao mbaya na udhalimu ulio mikononi mwao.

9 Ni nani ajuaye? Huenda Mungu akaghairi kwa huruma yake akaacha hasira yake kali ili tusiangamie.”

10 Mungu alipoona walivyofanya na jinsi walivyogeuka kutoka katika njia zao mbaya, akawa na huruma wala hakuleta maangamizi juu yao kama alivyokuwa ameonya.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JON/3-dab15e2b36e80b076aaf45c9f9cf3e67.mp3?version_id=1627—

Yona 4

Hasira ya Yona Kwa Ajili ya Huruma ya Bwana.

1 Lakini Yona alichukizwa sana akakasirika.

2 AkamwombaBwana, “EeBwana, hili si lile nililolisema nilipokuwa ningali nyumbani? Hii ndiyo sababu niliharikisha kukimbilia Tarshishi. Nikifahamu kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na huruma, si mwepesi wa hasira na umejaa upendo, ni Mungu ambaye hughairi katika kupeleka maafa.

3 Sasa, EeBwana, niondolee uhai wangu, kwa kuwa ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”

4 LakiniBwanaakamjibu, “Je unayo haki yo yote kukasirika?”

5 Yona akatoka nje akaketi mahali upande wa mashariki wa mji. Hapo akajitengenezea kibanda, akaketi kwenye kivuli chake na kungojea ni nini kitakachotokea katika mji.

6 NdipoBwana, Mungu akaweka tayari mzabibu na kuufanya uote, kumpatia Yona kivuli kilichomfunika kichwa ili kuondoa taabu yake, naye Yona akafurahi sana kwa ajili ya ule mzabibu.

7 Lakini kesho yake asubuhi na mapema Mungu akaamuru buu, autafune mzabibu huo nao ukanyauka.

8 Wakati jua lilipochomoza, Mungu akautuma upepo wa hari wa mashariki, nalo jua likawaka juu ya kichwa cha Yona mpaka akazimia. Akatamani kufa, naye akasema, “Ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”

9 Lakini Mungu alimwambia Yona, “Je, unayo haki kukasirika kuhusu mzabibu huo?”

Akasema, “Ndiyo, ninayo haki. Nimekasirika kiasi cha kufa.”

10 LakiniBwanaakamwambia, “Wewe waona vibaya kwa ajili ya mzabibu huu, nawe hukuusababisha kuota wala kuutunza. Uliota usiku mmoja nao ukafa usiku mmoja.

11 Lakini Ninawi ina zaidi ya watu 120,000 ambao hawawezi kupambanua kulia au kushoto pamoja na ng’ombe wengi. Je, hainipasi kufikiri juu ya mji ule mkubwa?”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JON/4-da616231ce885d25d27bec5b3a1c64da.mp3?version_id=1627—