Yoeli 1

1 Neno laBwanaambalo lilimjia Yoeli mwana wa Pethueli.

Uvamizi Wa Nzige

2 Sikilizeni hili, enyi wazee;

sikilizeni, ninyi nyote mnaoishi katika nchi.

Je, jambo kama hili lilishawahi kutokea

katika siku zenu au katika siku za babu zenu?

3 Waelezeni watoto wenu,

na watoto wenu wawaambie watoto wao,

na watoto wao kwa kizazi kitakachofuata.

4 Kilichosazwa na kundi la tunutu

nzige wakubwa wamekula,

kilichosazwa na nzige wakubwa

parare wamekula,

kilichosazwa na parare

madumadu wamekula.

5 Amkeni, enyi walevi, mlie!

Pigeni yowe enyi wanywaji wote wa mvinyo,

pigeni yowe kwa sababu ya mvinyo mpya,

kwa kuwa mmenyang’anywa

kutoka midomoni mwenu.

6 Taifa limevamia nchi yangu,

lenye nguvu tena lisilo na idadi;

lina meno ya simba,

magego ya simba jike.

7 Limeharibu mizabibu yangu

na kuangamiza mitini yangu.

Limebambua magome yake

na kuyatupilia mbali,

likayaacha matawi yake yakiwa meupe.

8 Omboleza kama bikira aliyevaa nguo ya gunia

anayehuzunika kwa ajili ya mume wa ujana wake.

9 Sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji

zimekatiliwa mbali kutoka nyumba yaBwana.

Makuhani wanaomboleza,

wale wanaohudumu mbele zaBwana.

10 Mashamba yameharibiwa,

ardhi imekauka;

nafaka imeharibiwa,

mvinyo mpya umekauka,

mafuta yamekoma.

11 Kateni tamaa, enyi wakulima,

lieni, enyi mlimao mizabibu;

huzunikeni kwa ajili ya ngano na shayiri,

kwa sababu mavuno ya shambani yameharibiwa.

12 Mzabibu umekauka

na mtini umenyauka;

mkomamanga, mtende na mtofaa,

miti yote ya shambani, imekauka.

Hakika furaha yote ya mwanadamu

imeondoka.

Wito Wa Toba

13 Vaeni nguo ya gunia, Enyi makuhani, muomboleze;

pigeni yowe, enyi mnaohudumu madhabahuni.

Njoni, vaeni nguo ya gunia usiku kucha,

enyi mnaohudumu mbele za Mungu wangu;

kwa kuwa sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji

zimezuiliwa kufika katika nyumba ya Mungu wenu.

14 Tangazeni saumu takatifu;

liiteni kusanyiko takatifu.

Iteni wazee

na wote waishio katika nchi

waende katika nyumba yaBwanaMungu wenu,

wakamlilieBwana.

15 Ole kwa siku hiyo!

Kwa kuwa siku yaBwanaiko karibu;

itakuja kama uharibifu

# kutoka kwa Mwenyezi.

16 Je, chakula hakikukatiliwa mbali

mbele ya macho yetu:

furaha na shangwe

kutoka katika nyumba ya Mungu wetu?

17 Mbegu zinakauka

chini ya mabonge ya udongo.

Ghala zimeachwa katika uharibifu,

ghala za nafaka zimebomolewa,

kwa maana hakuna nafaka.

18 Jinsi gani ng’ombe wanavyolia!

Makundi ya mifugo yanahangaika

kwa sababu hawana malisho;

hata makundi ya kondoo yanateseka.

19 Kwako, EeBwana, naita,

kwa kuwa moto umeteketeza

malisho ya mbugani

na miali ya moto imeunguza

miti yote ya shambani.

20 Hata wanyama wa porini wanakuonea shauku;

vijito vya maji vimekauka,

na moto umeteketeza

malisho yote ya mbugani.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOL/1-c143eaab6d0d73e6f8727b9d2499d297.mp3?version_id=1627—

Yoeli 2

Jeshi La Nzige

1 Pigeni tarumbeta katika Sayuni;

pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu.

Wote waishio katika nchi na watetemeke,

kwa kuwa siku yaBwanainakuja. Iko karibu,

2 siku ya giza na huzuni,

siku ya mawingu na utusitusi.

Kama mapambazuko yasambaavyo

toka upande huu wa milima

hata upande mwingine

jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja.

Jambo kama hili halijakuwapo tangu zamani

wala halitakuwapo tena kamwe

kwa vizazi vijavyo.

3 Mbele yao moto unateketeza,

nyuma yao miali ya moto

inawaka kwa nguvu.

Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni,

nyuma yao ni jangwa lisilofaa:

hakuna kitu kinachowaepuka.

4 Wanaonekana kama farasi;

wanakwenda mbio

kama askari wapanda farasi.

5 Wanatoa sauti kama magari ya vita,

wanaporukaruka juu ya vilele vya milima,

kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua,

kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.

6 Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu;

kila uso unabadilika rangi.

7 Wanashambulia kama wapiganaji wa vita;

wanapanda kuta kama askari.

Wote wanatembea katika safu,

hawapotoshi safu zao.

8 Hakuna anayemsukuma mwenzake;

kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja.

Wanapita katika vizuizi

bila kuharibu safu zao.

9 Wanaenda kasi kuingia mjini;

wanakimbia ukutani.

Wanaingia ndani ya nyumba;

kwa kuingilia madirishani kama wevi.

10 Mbele yao dunia inatikisika,

anga linatetemeka,

jua na mwezi vinatiwa giza,

na nyota hazitoi mwanga wake tena.

11 Bwanaanatoa mshindo wa ngurumo

mbele ya jeshi lake;

majeshi yake hayana idadi,

ni wenye nguvu nyingi

wale ambao hutii agizo lake.

Siku yaBwanani kuu,

ni ya kutisha.

Ni nani anayeweza kuistahimili?

Rarueni Mioyo Yenu

12 “Hata sasa,” asemaBwana,

“nirudieni kwa mioyo yenu yote,

kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”

13 Rarueni mioyo yenu

na siyo mavazi yenu.

MrudieniBwana, Mungu wenu,

kwa maana yeye ndiye mwenye neema

na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo,

huona huruma, hujizuia kuleta maafa.

14 Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma

na kuacha baraka nyuma yake:

sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji

kwa ajili yaBwanaMungu wenu.

15 Pigeni tarumbeta katika Sayuni,

tangazeni saumu takatifu,

liiteni kusanyiko takatifu.

16 Wakusanyeni watu,

wekeni wakfu kusanyiko;

waleteni pamoja wazee,

wakusanyeni watoto,

wale wanyonyao maziwa.

Bwana arusi na atoke chumbani mwake

na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.

17 Makuhani, ambao wanahudumu mbele zaBwana,

na walie katikati ya ukumbi

wa Hekalu na madhabahu.

Waseme, “Wahurumie watu wako, EeBwana.

Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa,

neno la dhihaka kati ya mataifa.

Kwa nini wasemezane miongoni mwao,

‘Yuko wapi Mungu wao?’ ”

Jibu La Bwana

18 KishaBwanaatakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake

na kuwa na huruma juu ya watu wake.

19 Bwanaatawajibu:

“Ninawapelekea nafaka,

mvinyo mpya na mafuta,

vya kuwatosha ninyi

hadi mridhike kabisa;

kamwe sitawafanya tena

kitu cha kudharauliwa na mataifa.

20 “Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi,

nikilisukuma ndani ya jangwa,

askari wa safu za mbele wakienda

ndani ya bahari ya mashariki

na wale wa safu za nyuma

katika bahari ya magharibi.

Uvundo wake utapaa juu;

harufu yake itapanda juu.”

Hakika ametenda mambo makubwa.

21 Usiogope, Ee nchi;

furahi na kushangilia.

HakikaBwanaametenda mambo makubwa.

22 Msiogope, Enyi wanyama pori,

kwa kuwa mbuga za malisho yenu

zinarudia ubichi.

Miti nayo inazaa matunda,

mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.

23 Furahini, Enyi watu wa Sayuni,

shangilieni katikaBwanaMungu wenu,

kwa kuwa amewapa mvua za vuli

kwa kipimo cha haki.

Anawapelekea mvua nyingi,

mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.

24 Sakafu za kupuria zitajaa nafaka,

mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.

25 “Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige:

parare, madumadu na tunutu,

jeshi langu kubwa ambalo

nililituma katikati yenu.

26 Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe,

na mtalisifu jina laBwanaMungu wenu,

ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu;

kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.

27 Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli

kwamba mimi ndimiBwanaMungu wenu,

na kwamba hakuna mwingine;

kamwe watu wangu hawataaibika tena.

Siku Ya Bwana

28 “Hata itakuwa, baada ya hayo,

nitamimina Roho yangu juu ya wote wenye mwili.

Wana wenu, waume kwa wake, watatabiri,

wazee wenu wataota ndoto,

na vijana wenu wataona maono.

29 Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake,

katika siku zile nitamimina Roho yangu.

30 Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu

na juu ya nchi,

damu, moto na wimbi la moshi.

31 Jua litageuzwa kuwa giza

na mwezi kuwa damu

kabla ya kuja siku yaBwana

iliyo kuu na ya kutisha.

32 Na kila mmoja atakayeliitia

jina laBwanaataokolewa.

Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu

kutakuwako wokovu,

kamaBwanaalivyosema,

miongoni mwa walionusurika

ambaoBwanaawaita.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOL/2-834e1ac8d2542f5b1a07a9f9571d5538.mp3?version_id=1627—

Yoeli 3

Mataifa Yahukumiwa

1 “Katika siku hizo na wakati huo,

nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,

2 nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta

# katika Bonde la Yehoshafati.

Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao

kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli,

kwa kuwa waliwatawanya watu wangu

miongoni mwa mataifa

na kuigawa nchi yangu.

3 Wanawapigia kura watu wangu

na kuwauza wavulana ili kupata makahaba;

waliwauza wasichana

ili wapate kunywa mvinyo.

4 “Sasa una nini dhidi yangu, Ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.

5 Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.

6 Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.

7 “Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.

8 Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Washeba, taifa lililo mbali.”Bwanaamesema.

9 Tangazeni hili miongoni mwa mataifa:

Jiandaeni kwa vita!

Amsha askari!

Wanaume wote wapiganaji

wasogee karibu na kushambulia.

10 Majembe yenu yafueni yawe panga

na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki.

Aliye dhaifu na aseme,

“Mimi nina nguvu!”

11 Njoni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote,

kusanyikeni huko.

Shusha wapiganaji wako, EeBwana!

12 “Mataifa na yaamshwe;

na yasonge mbele kuelekea katika Bonde la Yehoshafati,

kwa kuwa nitaketi mahali pale

kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.

13 Tia mundu,

kwa kuwa mavuno yamekomaa.

Njoni, mkanyage zabibu,

kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa

na mapipa yanafurika:

kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”

14 Umati mkubwa, umati mkubwa

katika bonde la uamuzi!

Kwa kuwa siku yaBwanani karibu

katika bonde la uamuzi.

15 Jua na mwezi vitatiwa giza,

na nyota hazitatoa mwanga wake tena.

16 Bwanaatanguruma kutoka Sayuni

na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu;

dunia na mbingu vitatikisika.

LakiniBwanaatakuwa kimbilio la watu wake,

ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.

Baraka Kwa Watu Wa Mungu

17 “Ndipo mtakapojua kwamba Mimi,BwanaMungu wenu,

nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.

Yerusalemu utakuwa mtakatifu;

kamwe wageni hawataivamia tena.

18 “Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya,

na vilima vitatiririka maziwa;

mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji.

Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba yaBwana

# na kunywesha Bonde la Shitimu.

19 Lakini Misri itakuwa ukiwa,

Edomu itakuwa jangwa tupu,

kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda,

ambao katika nchi yao

walimwaga damu isiyo na hatia.

20 Yuda itakaliwa na watu milele

na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.

21 Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe,

nitasamehe.”

Bwanaanakaa Sayuni!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOL/3-8663e10b8d72a40fd5193aeae4bf422a.mp3?version_id=1627—

Hosea 1

1 Neno laBwanalililomjia Hosea mwana wa Beeri wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na wakati wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Yekoashi mfalme wa Israeli:

Mke Wa Hosea Na Watoto

2 WakatiBwanaalipoanza kuzungumza kupitia Hosea,Bwanaalimwambia, “Nenda ukajitwalie mwanamke wa uzinzi na watoto wa uzinzi, kwa sababu nchi ina hatia ya uzinzi wa kupindukia kwa kumwachaBwana.”

3 Kwa hiyo alimwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba na kumzalia Hosea mwana.

4 KishaBwanaakamwambia Hosea, “Mwite Yezreeli, kwa kuwa kitambo kidogo nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa ajili ya mauaji ya kule Yezreeli, nami nitaukomesha ufalme wa Israeli.

5 Katika siku ile nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la Yezreeli.”

6 Gomeri akachukua tena mimba akamzaa binti. KishaBwanaakamwambia Hosea, “Mwite Lo-Ruhama, kwa maana sitaonyesha tena upendo kwa nyumba ya Israeli, kwamba nisije kabisa nikawasamehe.

7 Hata hivyo nitaonyesha upendo kwa nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa si kwa upinde, upanga au vita, wala kwa farasi na wapanda farasi, bali kwa njia yaBwanaMungu wao.”

8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo-Ruhama kunyonya, Gomeri alipata mwana mwingine.

9 KishaBwanaakasema, “Mwite Lo-Amikwa maana ninyi si watu wangu, nami si Mungu wenu.

10 “Hata hivyo Waisraeli watakuwa kama mchanga kando ya bahari, ambao hauwezi kupimika wala kuhesabiwa. Mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’

11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli wataunganishwa tena, nao watamchagua kiongozi mmoja nao watakwea watoke katika nchi, kwa kuwa siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/1-3c0b99c1b9b82448541b0fa16862dcd1.mp3?version_id=1627—

Hosea 2

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’

Israeli Aadhibiwa Na Kurudishwa

2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni,

kwa maana yeye si mke wangu,

nami si mume wake.

Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake

na uzinzi kati ya matiti yake.

3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi

na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa.

Nitamfanya kama jangwa,

nitamgeuza awe nchi ya kiu,

nami nitamwua kwa kiu.

4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake,

kwa sababu ni watoto wa uzinzi.

5 Mama yao amekosa uaminifu

na amewachukua mimba katika aibu.

Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu,

ambao hunipa chakula changu

na maji yangu,

sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu

na kinywaji changu.’

6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake

kwa vichaka vya miiba,

nitamjengea ukuta ili kwamba

asiweze kutoka.

7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata;

atawatafuta lakini hatawapata.

Kisha atasema,

‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza,

kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi

kuliko sasa.’

8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye

niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta,

niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia

kwa kumtumikia Baali.

9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa

na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari.

Nitamnyang’anya sufu yangu na kitani yangu

iliyokusudiwa kufunika uchi wake.

10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake

mbele ya wapenzi wake;

hakuna ye yote atakayemtoa

mikononi mwangu.

11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote:

sikukuu zake za mwaka,

sikukuu za Miandamo ya Mwezi,

siku zake za Sabato,

sikukuu zake zote zilizoamuriwa.

12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake,

ambayo alisema yalikuwa malipo yake

kutoka kwa wapenzi wake;

nitaifanya kuwa kichaka,

nao wanyama pori wataila.

13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku

alizowafukizia uvumba Mabaali;

alipojipamba kwa pete

na kwa vito vya thamani,

na kuwaendea wapenzi wake,

lakini mimi alinisahau,”

asemaBwana.

14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi;

nitamwongoza hadi jangwani

na kuzungumza naye kwa upole.

15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu,

# nami nitalifanya Bonde la Akori

mlango wa matumaini.

Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake,

kama siku zile alizotoka Misri.

16 “Katika siku ile,” asemaBwana,

“utaniita mimi ‘Mume wangu’;

hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’

17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake,

wala hataomba tena kwa majina yao.

18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao

na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani,

na viumbe vile vitambaavyo ardhini.

Upinde, upanga na vita,

nitaondolea mbali katika nchi,

ili kwamba wote waweze kukaa salama.

19 Nitakuposa uwe wangu milele;

nitakuposa kwa uadilifu na haki,

kwa upendo na huruma.

20 Nitakuposa kwa uaminifu,

nawe utamkubaliBwana.

21 “Katika siku ile nitajibu,”

asemaBwana,

“nitajibu kwa anga,

nazo anga zitajibu kwa nchi;

22 nayo nchi itajibu kwa nafaka,

divai mpya na mafuta,

navyo vitajibu kwa Yezreeli.

23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe;

nami nitaonyesha pendo langu kwake

# yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu,’

# Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’

‘Ninyi ni watu wangu’

nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/2-e489fbb9dba03145b6b6ec8a3998dd22.mp3?version_id=1627—

Hosea 3

Upatanisho Wa Hosea Na Mkewe

1 Bwanaakaniambia, “Nenda, ukaonyeshe upendo wako kwa mke wako tena, ingawa amependwa na mwingine naye ni mzinzi. Mpende kamaBwanaapendavyo Waisraeli, ingawa wanageukia miungu mingine na kupenda mikate mitamu ya zabibu kavu iliyowekwa wakfu.”

2 Basi nilimnunua huyo mwanamke kwa shekeli kumi na tanoza fedha, pia kwa kiasi kama cha homeri moja na nusuya shayiri.

3 Kisha nilimwambia, “Utaishi nami kwa siku nyingi, hupaswi kuwa kahaba au kuwa na uhusiano wa karibu na mtu ye yote, nami nitaishi na wewe.”

4 Kwa maana Waisraeli wataishi siku nyingi bila kuwa na mfalme wala mkuu, bila kuwa na dhabihu wala mawe matakatifu, bila kisibau wala sanamu.

5 Baadaye Waisraeli watarudi na kumtafutaBwanaMungu wao na Daudi mfalme wao. Watakuja wakitetemeka kwaBwanana kwa baraka zake katika siku za mwisho.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/3-cc76f9180eaa010cd7d5e3abe3bbc37a.mp3?version_id=1627—

Hosea 4

Shtaka Dhidi Ya Israeli

1 Sikieni neno laBwana, enyi Waisraeli,

kwa sababuBwanaanalo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

3 Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu ye yote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

5 Unajikwaa mchana na usiku,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

6 watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

7 Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

8 Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

10 “Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwachaBwana

na kujiingiza wenyewe

11 katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

12 wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

15 “Ingawa umefanya uzinzi, Ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

# usipande kwenda Beth-Aveni.

Wala usiape,

‘Hakika kamaBwanaaishivyo!’

16 Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ng’ombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basiBwanaanaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

17 Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

19 Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/4-23797682a4891b06886ad1291db73701.mp3?version_id=1627—

Hosea 5

Hukumu Dhidi Ya Israeli

1 “Sikieni hili, enyi makuhani!

Iweni wasikivu, enyi Waisraeli!

Sikieni, Ee nyumba ya kifalme!

Hukumu hii ni dhidi yenu:

Mmekuwa mtego huko Mizpa,

wavu uliotandwa juu ya Tabori.

2 Waasi wamezidisha sana mauaji.

Mimi nitawatiisha wote.

3 Ninajua yote kuhusu Efraimu,

Israeli hukufichika kwangu.

Efraimu, sasa umegeukia ukahaba,

Israeli amenajisika.

4 “Matendo yao hayawaachii

kurudi kwa Mungu wao.

Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao,

hawamkubaliBwana.

5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao;

Waisraeli, hata Efraimu,

wanajikwaa katika dhambi zao;

pia Yuda atajikwaa pamoja nao.

6 Wakati wanapokwenda na makundi yao

ya kondoo na ng’ombe

kumtafutaBwana,

hawatampata;

yeye amejiondoa kutoka kwao.

7 Wao si waaminifu kwaBwana;

wamezaa watoto haramu.

Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi

zitawaangamiza wao

pamoja na mashamba yao.

8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea,

baragumu huko Rama.

# Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni,

ongoza, Ee Benyamini.

9 Efraimu ataachwa ukiwa

katika siku ya kuadhibiwa.

Miongoni mwa makabila ya Israeli

ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.

10 Viongozi wa Yuda ni kama wale

wanaosogeza mawe ya mpaka.

Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao

kama mafuriko ya maji.

11 Efraimu ameonewa,

amekanyagwa katika hukumu

kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.

12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu,

na kama uozo kwa watu wa Yuda.

13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake,

naye Yuda vidonda vyake,

ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru,

na kuomba msaada kwa mfalme mkuu.

Lakini hawezi kukuponya,

wala hawezi kukuponya vidonda vyako.

14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu,

kama simba mkubwa kwa Yuda.

Nitawararua vipande vipande na kuondoka;

nitawachukua mbali,

na hakuna wa kuwaokoa.

15 Kisha nitarudi mahali pangu

mpaka watakapokubali kosa lao.

Nao watautafuta uso wangu;

katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/5-d57a757ea2b641d3a776cb16c5cfda6b.mp3?version_id=1627—

Hosea 6

Israeli Asiye Na Toba

1 “Njoni, tumrudieBwana.

Ameturarua vipande vipande

lakini atatuponya;

ametujeruhi lakini

atatufunga majeraha yetu.

2 Baada ya siku mbili atatufufua;

katika siku ya tatu atatuinua,

ili tuweze kuishi mbele zake.

3 TumkubaliBwana,

tukaze kumkubali yeye.

Kutokea kwake ni hakika kama vile

kuchomoza kwa jua;

atatujia kama mvua za masika,

kama vile mvua za vuli

ziinyweshavyo nchi.”

4 “Nifanye nini nawe, Efraimu?

Nifanye nini nawe, Yuda?

Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao.

5 Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande

kwa kutumia manabii wangu;

nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu,

hukumu zangu zinawaka

kama umeme juu yenu.

6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu,

kumkubali Mungu zaidi

kuliko sadaka za kuteketezwa.

7 Wamevunja Agano kama Adamu:

huko hawakuwa waaminifu kwangu.

8 Gileadi ni mji wenye watu waovu,

umetiwa madoa kwa nyayo za damu.

9 Kama wanyang’anyi wamviziavyo mtu,

ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo;

wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu,

wakifanya uhalifu wa aibu.

10 Nimeona jambo la kutisha

katika nyumba ya Israeli.

Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba

na Israeli amenajisika.

11 “Pia kwa ajili yako, Yuda,

mavuno yameamuriwa.

“Wakati wo wote ningerejesha neema ya watu wangu,

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/6-e4752a038858b2342f51514b281dc81f.mp3?version_id=1627—

Hosea 7

1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli,

dhambi za Efraimu zinafichuliwa

na maovu ya Samaria yanafunuliwa.

Wanafanya udanganyifu,

wevi huvunja nyumba,

maharamia hunyang’anya barabarani,

2 lakini hawafahamu kwamba

ninakumbuka matendo yao yote mabaya.

Dhambi zao zimewameza,

ziko mbele zangu siku zote.

3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao,

wakuu wao kwa uongo wao.

4 Wote ni wazinzi,

wanawaka kama tanuru

ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea

kuanzia kukanda unga

hadi umekwisha kuumuka.

5 Katika sikukuu ya mfalme wetu

wakuu wanawaka kwa mvinyo,

naye anawaunga mkono wenye mizaha.

6 Mioyo yao ni kama tanuru,

wanamwendea kwa hila.

Hasira yao inafoka moshi usiku kucha,

wakati wa asubuhi inalipuka

kama miali ya moto.

7 Wote ni moto kama tanuru;

wanawaangamiza watawala wao.

Wafalme wake wote wanaanguka,

wala hakuna ye yote kati yao aniitaye mimi.

8 “Efraimu anajichanganya na mataifa;

Efraimu ni mkate ambao haukuiva.

9 Wageni wananyonya nguvu zake,

lakini hafahamu hilo.

Nywele zake zina mvi hapa na pale,

lakini hana habari.

10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake,

lakini pamoja na haya yote

harudi kwaBwanaMungu wake

wala kumtafuta.

11 “Efraimu ni kama hua,

hudanganywa kwa urahisi na hana akili:

mara anaita Misri,

mara anageukia Ashuru.

12 Wakati watakapokwenda,

nitatupa wavu wangu juu yao;

nitawavuta chini waanguke

kama ndege wa angani.

Nitakaposikia wakikusanyika pamoja,

nitawanasa.

13 Ole wao, kwa sababu

wamepotoka kutoka kwangu!

Maangamizi ni yao

kwa sababu wameniasi!

Ninatamani kuwakomboa,

lakini wanasema uongo dhidi yangu.

14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao,

bali wanaomboleza vitandani mwao.

Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya,

lakini hugeukia mbali nami.

15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu,

lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.

16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana,

wako kama upinde wenye kasoro.

Viongozi wao wataanguka kwa upanga

kwa sababu ya maneno yao ya jeuri.

Kwa ajili ya hili watadhihakiwa

katika nchi ya Misri.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/7-1347b2c0019372d404eccd33f43faa3f.mp3?version_id=1627—