Yeremia 49

Ujumbe Kuhusu Amoni

1 Kuhusu Waamoni:

Hili ndilo asemaloBwana:

“Je, Israeli hana wana?

Je, hana warithi?

Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi?

Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?

2 Lakini siku zinakuja,”

asemaBwana,

“nitakapopiga kelele ya vita

dhidi ya Raba mji wa Waamoni;

utakuwa kilima cha magofu,

navyo vijiji vinavyouzunguka

vitateketezwa kwa moto.

Kisha Israeli atawafukuza

wale waliomfukuza,”

asemaBwana.

3 “Lia kwa huzuni, Ee Heshboni,

kwa kuwa Ai umeangamizwa!

Piga kelele,

Enyi wakazi wa Raba!

Vaeni nguo ya gunia na kuomboleza,

kimbieni hapa na pale ndani ya kuta,

kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni,

yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.

4 Kwa nini unajivunia mabonde yako,

ukijivunia mabonde yako yaliyozaa sana?

Ee binti usiye mwaminifu,

unayeutumainia utajiri wako na kusema,

‘Ni nani atakayenishambulia?’

5 Nitaleta hofu kuu juu yako

kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,”

asema Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote.

“Kila mmoja wenu ataondolewa,

wala hakuna hata mmoja

atakayekusanya wakimbizi.

6 “Lakini hatimaye,

nitarudisha mateka wa Waamoni,”

asemaBwana.

Ujumbe Kuhusu Edomu

7 Kuhusu Edomu:

Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote:

“Je, hakuna tena hekima katika Temani?

Je, shauri limewapotea wenye busara?

Je, hekima yao imechakaa?

8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa,

wewe uishiye Dedani,

kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau

wakati nitakapomwadhibu.

9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako,

wasingebakiza zabibu chache?

Kama wezi wangekuja usiku,

je, si wangeiba kiasi ambacho wangehitaji tu?

10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi,

nitayafunua maficho yake,

ili asiweze kujificha.

Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia,

naye hatakuwepo tena.

11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao.

Wajane wako pia

wanaweza kunitumaini mimi.”

12 Hili ndilo asemaloBwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.

13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asemaBwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”

14 Nimesikia ujumbe kutoka kwaBwana:

Mjumbe ametumwa kwa mataifa kusema,

“Jikusanyeni ili kuushambulia!

Inukeni kwa ajili ya vita!”

15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa,

aliyedharauliwa miongoni mwa watu.

16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako

vimekudanganya,

wewe unayeishi katika majabali ya miamba,

wewe unayemiliki katika miinuko ya kilima.

Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai,

kutoka huko nitakushusha chini,”

asemaBwana.

17 “Edomu atakuwa kitu cha kutisha;

wote wapitao kando yake

watashangaa na kuzomea

kwa sababu ya majeraha yake yote.

18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa,

pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,”

asemaBwana,

“hivyo hakuna ye yote atakayeishi humo;

hakuna mtu atakayeishi ndani yake.

19 “Kama simba anayepanda kutoka katika vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho mengi,

nitamfukuza Edomu kutoka kwenye nchi yake ghafula.

Ni nani mteule nitakayemweka

kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi na ni nani

awezaye kupingana nami?

Na ni mchungaji yupi awezaye

kusimama kinyume nami?”

20 Kwa hiyo, sikia kile ambachoBwana

amepanga dhidi ya Edomu,

kile alichokusudia

dhidi ya wale waishio Temani:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali;

yeye ataangamiza kabisa

malisho yao kwa sababu yao.

21 Kwa sauti ya anguko lao dunia itatetemeka,

# kilio chao kitasikika mpaka Bahari ya Shamu.

22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula,

akitandaza mbawa zake juu ya Bosra.

Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu

itakuwa kama moyo wa mwanamke

aliye katika utungu wa kuzaa.

Ujumbe Kuhusu Dameski

23 Kuhusu Dameski:

“Hamathi na Arpadi imetahayarika,

kwa kuwa wamesikia habari mbaya.

Wamevunjika moyo na wametaabika

kama bahari iliyochafuka.

24 Dameski amedhoofika,

amegeuka na kukimbia,

hofu ya ghafula imemkamata sana;

amepatwa na uchungu na maumivu,

maumivu kama ya mwanamke

aliye katika utungu wa kuzaa.

25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa,

mji ambao ninaupenda?

26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote

watanyamazishwa siku hiyo,”

asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

27 “Nitatia moto kuta za Dameski;

utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”

Ujumbe Kuhusu Kedari Na Hazori

28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia:

Hili ndilo asemaloBwana:

“Inuka, ushambulie Kedari

na kuwaangamiza watu wa mashariki.

29 Hema zao na makundi yao ya kondoo na mbuzi yatachukuliwa;

vibanda vyao vitatwaliwa

pamoja na mali zao zote na ngamia zao.

Watu watawapigia kelele,

‘Hofu kuu iko kila upande!’

30 “Kimbieni haraka!

Kaeni kwenye mapango marefu sana,

ninyi mkaao Hazori,”

asemaBwana.

“Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu;

amebuni hila dhidi yenu.

31 “Inuka na ulishambulie taifa lililostarehe,

linaloishi kwa kujiamini,”

asemaBwana,

“taifa lisilo na malango wala makomeo;

watu wake huishi peke yao.

32 Ngamia wao watakuwa nyara,

nayo makundi yao makubwa ya ng’ombe yatatekwa.

Wale walio maeneo ya mbali

nitawatawanya pande zote

nami nitaleta maafa juu yao

kutoka kila upande,”

asemaBwana.

33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha,

mahali pa ukiwa milele.

Hakuna ye yote atakayeishi humo;

hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”

Ujumbe Kuhusu Elamu

34 Hili ndilo neno laBwanalililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema wakati wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:

35 Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote asemalo:

“Tazama, nitavunja upinde wa Elamu,

ulio tegemeo la nguvu zao.

36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu

toka pande nne za mbingu,

nitawatawanya katika hizo pande nne,

wala hapatakuwa na taifa

ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.

37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao,

mbele yao wale wanaotafuta uhai wao;

nitaleta maafa juu yao,

pia hasira yangu kali,”

asemaBwana.

“Nitawafuatia kwa upanga

mpaka nitakapowamaliza.

38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu

na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,”

asemaBwana.

39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu

katika siku zijazo,”

asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/49-b499d4b1d5b8ec8b7770b9dfae75750a.mp3?version_id=1627—

Yeremia 50

Ujumbe Kuhusu Babeli

1 Hili ndilo neno alilosemaBwanakupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:

2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa,

twekeni bendera na mkahubiri;

msiache kitu cho chote, bali semeni,

‘Babeli utatekwa;

Beli ataaibishwa,

Merodaki atajazwa na hofu kuu.

Sanamu zake zitaaibishwa

na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’

3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia

na kuifanya nchi yake ukiwa.

Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,

watu na wanyama wataikimbia.

4 “Katika siku hizo, wakati huo,”

asemaBwana,

“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda

wataenda wakilia

ili kumtafutaBwanaMungu wao.

5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni

na kuelekeza nyuso zao huko.

Watakuja na kuambatana naBwana

katika Agano la milele

ambalo halitasahaulika.

6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;

wachungaji wao wamewapotosha

na kuwasababisha kuzungukazunguka

juu ya milima.

Walitangatanga juu ya mlima na kilima

na kusahau mahali pao wenyewe

pa kupumzikia.

7 Ye yote aliyewakuta aliwala;

adui zao walisema,

‘Sisi hatuna hatia,

kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi yaBwana,

malisho yao halisi,

Bwana, aliye tumaini la baba zao.’

8 “Kimbieni kutoka Babeli;

ondokeni katika nchi ya Wakaldayo

tena iweni kama mbuzi wale waongozao kundi.

9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli

muungano wa mataifa makubwa

kutoka nchi ya kaskazini.

Watashika nafasi zao dhidi yake,

naye kwa kutokea kaskazini atatekwa.

Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari

ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.

10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara;

wote wamtekao nyara watapata za kutosha,”

asemaBwana.

11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi,

wewe utekaye urithi wangu,

kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka

na kulia kama farasi dume asiyehasiwa,

12 mama yako ataaibika mno,

yeye aliyekuzaa atatahayari.

Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote,

atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.

13 Kwa sababu ya hasira yaBwanahatakaliwa na mtu,

lakini ataachwa ukiwa kabisa.

Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki

kwa sababu ya majeraha yake yote.

14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli,

enyi nyote mvutao upinde.

Mpigeni! Msibakize mshale wo wote,

kwa kuwa ametenda dhambi dhidi yaBwana.

15 Piga kelele dhidi yake kila upande!

Anajisalimisha, minara yake inaanguka,

kuta zake zimebomoka.

Kwa kuwa hiki ni kisasi chaBwana,

mlipizeni kisasi;

mtendeeni kama alivyowatendea wengine.

16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli,

naye mvunaji pamoja na mundu wake akivuna.

Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu

kila mmoja na arejee

kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja na akimbilie

kwenye nchi yake mwenyewe.

17 “Israeli ni kundi lililotawanyika

ambalo simba wamelifukuzia mbali.

Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru,

wa mwisho kuponda mifupa yake

alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”

18 Kwa hiyo hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake

kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.

19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe

naye atalisha huko Karmeli na Bashani;

njaa yake itashibishwa

juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.

20 Katika siku hizo, wakati huo,”

asemaBwana,

“uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli,

lakini halitakuwepo,

kwa ajili ya dhambi za Yuda,

lakini haitapatikana hata moja,

kwa kuwa nitawasamehe

mabaki nitakaowaacha.

21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu

na wale waishio huko Pekodi.

Wafuatieni, waueni

na kuwaangamiza kabisa,”

asemaBwana.

“Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.

22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi,

kelele ya maangamizi makuu!

23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote

ilivyovunjika na kuharibika!

Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa

miongoni mwa mataifa!

24 Nimetega mtego kwa ajili yako, Ee Babeli,

nawe ukakamatwa kabla haujafahamu;

ulipatikana na ukakamatwa

kwa sababu ulimpingaBwana.

25 Bwanaamefungua ghala lake la silaha

na kuzitoa silaha za ghadhabu yake,

kwa kuwaBwanaMwenyezi Mwenye Nguvu Zote

anayo kazi ya kufanya

katika nchi ya Wakaldayo.

26 Njoni dhidi yake kutoka mbali.

Zifungueni ghala zake za nafaka;

mlundikeni kama lundo la nafaka.

Mwangamizeni kabisa

na msimwachie mabaki yo yote.

27 Waueni mafahali wake wachanga wote;

waacheni washuke machinjoni!

Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia,

wakati wao wa kuadhibiwa.

28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli

wakitangaza katika Sayuni

jinsiBwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli,

wote wale wavutao upinde.

Pigeni kambi kumzunguka kabisa,

asitoroke mtu ye yote.

Mlipizeni kwa matendo yake;

mtendeeni kama alivyotenda.

Kwa kuwa alimdharauBwana,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote watanyamazishwa siku ile,”

asemaBwana.

31 “Tazama, niko kinyume nawe, Ewe mwenye majivuno,”

asema Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote,

“kwa kuwa siku yako imewadia,

yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.

32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka,

wala hakuna ye yote atakayemuinua;

nitawasha moto katika miji yake,

utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

33 Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote:

“Watu wa Israeli wameonewa,

nao watu wa Yuda pia.

Wote waliowateka wamewashikilia sana,

wanakataa kuwaachia waende.

34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu;

BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

Atatetea kwa nguvu shauri lao

ili kwamba alete raha katika nchi yao,

lakini ataleta msukosuko

kwa wale waishio Babeli.

35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!”

asemaBwana,

“dhidi ya wale waishio Babeli

na dhidi ya maafisa wake

na watu wenye busara!

36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo!

Watakuwa wapumbavu.

Upanga dhidi ya mashujaa wake!

Watajazwa na hofu kuu

37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita

pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake!

Wao watakuwa kama wanawake.

Upanga dhidi ya hazina zake!

Hizo zitatekwa nyara.

38 Ukame juu ya maji yake!

Nayo yatakauka.

Kwa kuwa ni nchi ya sanamu,

wao wanapenda sana sanamu.

39 “Hivyo viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo,

nao bundi watakaa humo.

Kamwe haitakaliwa tena

wala watu hawataishi humo

kutoka kizazi hadi kizazi.

40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora

pamoja na miji iliyo jirani nayo,”

asemaBwana,

“vivyo hivyo hapatakuwa na mtu ye yote

atakayeishi humo.

Naam, hakuna mtu ye yote

atakayekaa humo.

41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini;

taifa kubwa na wafalme wengi

wameamshwa kutoka miisho ya dunia.

42 Wamejifunga pinde na mikuki;

ni wakatili na wasio na huruma.

Wanasikika kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao;

wanakuja kama watu waliojipanga kwa vita

ili kukushambulia, Ee Binti Babeli.

43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu hao,

nayo mikono yake imelegea.

Uchungu umemshika,

maumivu kama yale ya mwanamke

aliye katika utungu wa kuzaa.

44 Kama simba anayepanda kutoka kwenye vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho manono,

nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula.

Ni nani aliye mteule,

nimweke kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi

na ni nani awezaye kunipinga?

Tena ni mchungaji yupi

awezaye kusimama dhidi yangu?”

45 Kwa hiyo, sikia kileBwanaalichokipanga dhidi ya Babeli,

kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali,

ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.

46 Kwa kusikika kutekwa kwa Babeli,

dunia itatetemeka;

kilio chake kitaenea pote

miongoni mwa mataifa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/50-5b601e05cff5714c3c5f4e4f3abb1384.mp3?version_id=1627—

Yeremia 51

1 Hili ndilo asemaloBwana:

“Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi

# dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.

2 Nitawatuma wageni Babeli

kumpepeta na kuiharibu nchi yake;

watampinga kila upande

katika siku ya maafa yake.

3 Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake,

wala usimwache avae silaha zake.

Usiwaonee huruma vijana wake;

angamiza jeshi lake kabisa.

4 Wataanguka waliouawa katika Babeli,

wakiwa na majeraha ya kutisha

katika barabara zake.

5 Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa

na Mungu wao,BwanaMwenye Nguvu Zote,

ingawa nchi yao imejaa uovu

mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

6 “Kimbieni kutoka Babeli!

Okoeni maisha yenu!

Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake.

Ni wakati wa kisasi chaBwana,

atamlipa kile anachostahili.

7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono waBwana;

aliufanya ulimwengu wote ulewe.

Mataifa walikunywa mvinyo wake;

kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.

8 Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika.

Mwombolezeeni!

Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake,

labda anaweza kupona.

9 “ ‘Tungemponya Babeli,

lakini hawezi kuponyeka;

tumwache na kila mmoja aende kwenye nchi yake mwenyewe,

kwa kuwa hukumu yake inafika angani,

inapanda juu mpaka mawinguni.’

10 “ ‘Bwanaamethibitisha haki yetu;

njoni, tutangaze katika Sayuni

kitu ambachoBwanaMungu wetu amefanya.’

11 “Noeni mishale,

chukueni ngao!

Bwanaamewaamsha wafalme wa Wamedi,

kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli.

Bwanaatalipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli!

Imarisheni ulinzi,

wekeni walinzi,

andaeni waviziao!

Bwanaatatimiza kusudi lake,

amri yake juu ya watu wa Babeli.

13 Wewe uishiye kando ya maji mengi

na uliye na wingi wa hazina,

mwisho wako umekuja,

wakati wako wa kukatiliwa mbali.

14 BwanaMwenye Nguvu Zote

ameapa kwa nafsi yake mwenyewe:

‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige,

nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’

15 “Aliifanya dunia kwa uweza wake;

ameweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake

na kuzitandaza mbingu kwa ufahamu wake.

16 Apigapo radi, maji katika mbingu hunguruma,

huyafanya mawingu yainuke

kutoka miisho ya dunia.

Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua

Na huuleta upepo kutoka kwenye ghala zake.

17 “Kila mtu hana ufahamu na hana maarifa;

kila sonara ameaibika kwa sanamu zake.

Vinyago vyake ni vya udanganyifu,

havina pumzi ndani yake.

18 Hazifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha,

hukumu yao itawadia, zitaangamia.

19 Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo,

kwa maana yeye ni Muumba wa vitu vyote,

pamoja na kabila la urithi wake:

BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo ni jina lake.

20 “Wewe ndiwe rungu langu la vita,

silaha yangu ya vita

kwa wewe navunjavunja mataifa,

kwa wewe naangamiza falme,

21 kwa wewe navunjavunja

farasi na mpanda farasi,

kwa wewe navunjavunja

gari la vita na mwendeshaji wake,

22 kwa wewe napondaponda

mwanaume na mwanamke,

kwa wewe napondaponda

mzee na kijana,

kwa wewe napondaponda

kijana wa kiume na mwanamwali,

23 kwa wewe nampondaponda

mchungaji na kundi,

kwa wewe nampondaponda

mkulima na maksai,

kwa wewe nawapondaponda

watawala na maafisa.

24 “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asemaBwana.

25 “Mimi niko kinyume nawe, Ee mlima unaoharibu,

wewe uangamizaye dunia yote,”

asemaBwana.

“Nitanyosha mkono wangu dhidi yako,

nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba,

na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.

26 Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako

kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni,

wala jiwe lo lote kwa ajili ya msingi,

kwa maana utakuwa ukiwa milele,”

asemaBwana.

27 “Twekeni bendera katika nchi!

Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa!

Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

iteni falme hizi dhidi yake:

Ararati, Mini na Ashkenazi.

Wekeni jemadari dhidi yake,

pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.

28 Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

wafalme wa Wamedi,

watawala wao na maafisa wao wote,

pamoja na nchi zote wanazotawala.

29 Nchi inatetemeka na kugagaa,

kwa kuwa makusudi yaBwana

dhidi ya Babeli yanasimama:

yaani, kuangamiza nchi ya Babeli

ili kwamba pasiwe na ye yote atakayeishi humo.

30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana,

wamebaki katika ngome zao.

Nguvu zao zimekwisha,

wamekuwa kama wanawake.

Makazi yake yameteketezwa kwa moto,

makomeo ya malango yake yamevunjika.

31 Tarishi mmoja humfuata mwingine

na mjumbe humfuata mjumbe

kumtangazia mfalme wa Babeli

kwamba mji wake wote umetekwa,

32 Vivuko vya mito vimekamatwa,

# mabwawa yenye mafunjoyametiwa moto,

nao askari wameingiwa na hofu kuu.”

33 Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria

wakati inapokanyagwa;

wakati wa kumvuna utakuja upesi.”

34 “Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula,

ametufanya tuchangayikiwe,

ametufanya tuwe gudulia tupu.

Kama nyoka ametumeza

na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri,

kisha akatutapika.

35 Jeuri iliyofanyiwa miili yetuna iwe juu ya Babeli,”

ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni.

“Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,”

asema Yerusalemu.

36 Kwa hiyo, hili ndiloBwanaasemalo:

“Tazama, nitatetea shauri lako

na kulipiza kisasi kwa ajili yako;

nitaikausha bahari yake

na kuzikausha chemchemi zake.

37 Babeli utakuwa lundo la magofu

na makao ya mbweha,

kitu cha kutisha na kudharauliwa,

mahali asipoishi mtu.

38 Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo,

wanakoroma kama wana simba.

39 Lakini wakati wakiwa wameamshwa,

nitawaandalia karamu

na kuwafanya walewe,

ili wapige kelele kwa kicheko,

kisha walale milele na wasiamke,”

asemaBwana.

40 “Nitawatelemsha kama wana-kondoo

waendao machinjoni,

kama kondoo dume na mbuzi.

41 “Tazama Sheshakiatakamatwa,

majivuno ya dunia yote

yatakuwa yamefikia mwisho.

Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani

kati ya mataifa!

42 Bahari itainuka juu ya Babeli;

mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.

43 Miji yake itakuwa ukiwa,

kame na jangwa,

nchi ambayo hakuna ye yote anayeishi ndani yake,

ambayo hakuna mtu anayepita humo.

44 Nitamwadhibu Beli katika Babeli

na kumfanya atapike kile alichokimeza.

Mataifa hayatamiminika tena kwake.

Nao ukuta wa Babeli utaanguka.

45 “Tokeni ndani yake, enyi watu wangu!

Okoeni maisha yenu!

Ikimbieni hasira kali yaBwana.

46 Msikate tamaa wala msiogope tetesi

zitakaposikika katika nchi;

tetesi moja inasikika mwaka huu,

nyingine mwaka unaofuata;

tetesi juu ya jeuri katika nchi

na ya mtawala dhidi ya mtawala.

47 Kwa kuwa hakika wakati utawadia

nitakapoziadhibu sanamu za Babeli;

nchi yake yote itatiwa aibu

na watu wake wote waliouawa

wataangukia ndani yake.

48 Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake

vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli,

kwa kuwa kutoka kaskazini

waharabu watamshambulia,”

asemaBwana.

49 “Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli,

kama vile waliouawa duniani kote

walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.

50 Wewe uliyepona upanga,

ondoka wala usikawie!

MkumbukeBwanaukiwa katika nchi ya mbali,

na utafakari juu ya Yerusalemu.”

51 “Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa

na aibu imefunika nyuso zetu,

kwa sababu wageni wameingia

mahali patakatifu pa nyumba yaBwana.”

52 “Lakini siku zinakuja,” asemaBwana,

“nitakapoadhibu sanamu zake,

na katika nchi yake yote

waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.

53 Hata kama Babeli ikifika angani

na kuziimarisha ngome zake ndefu,

nitatuma waharabu dhidi yake,”

asemaBwana.

54 “Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli,

sauti ya uharibifu mkuu

kutoka nchi ya Wakaldayo.

55 Bwanaataiangamiza Babeli,

atanyamazisha makelele ya kishindo chake.

Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu,

ngurumo ya sauti zao itavuma.

56 Mharabu atakuja dhidi ya Babeli,

mashujaa wake watakamatwa,

nazo pinde zao zitavunjwa.

Kwa kuwaBwanani Mungu wa kisasi,

yeye atalipiza kikamilifu.

57 Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe,

watawala wao, maafisa,

pamoja na wapiganaji wao;

watalala milele na hawataamka,”

asema Mfalme, ambaye jina lake

niBwanaMwenye Nguvu Zote.

58 Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote asemalo:

“Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa,

na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto;

mataifa yanajichosha bure,

taabu ya mataifa ni nishati tu

kwa ajili ya miali ya moto.”

59 Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake.

60 Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli.

61 Akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa.

62 Kisha sema, ‘EeBwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili kwamba mtu wala mnyama asiishi ndani yake, itakuwa ukiwa milele.’

63 Utakapomaliza kusoma hiki kitabu lifungie jiwe kisha ulitupe ndani ya Mto Eufrati.

64 Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’ ”

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/51-4d833f0116381e8ad748c9778b3ebe9b.mp3?version_id=1627—

Yeremia 52

Anguko La Yerusalemu

1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.

2 Alifanya maovu machoni paBwana, kama vile alivyokuwa amefanya Yehoyakimu.

3 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira yaBwanakwamba haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake.

Basi Sedekia aliasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

4 Kwa hiyo katika mwaka wa tisa wa kutawala kwake Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na jeshi lake lote. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.

5 Mji ulizungukwa kwa jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa kutawala kwake Mfalme Sedekia.

6 Ilipowadia siku ya tisa katika mwezi wa nne njaa ilikuwa kali sana ndani ya mji kiasi kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.

7 Kisha ukuta wa mji ulivunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia mlango ulioko kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Walikimbia kuelekea Araba,

8 lakini jeshi la Wakaldayo lilimfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika tambarare za Yeriko. Askari wake wote walitengwa naye na kutawanyika,

9 naye akakamatwa.

Alipelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.

10 Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, pia akawaua maafisa wote wa Yuda.

11 Kisha akayang’oa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.

12 Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa kutawala kwake Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.

13 Alichoma moto Hekalu laBwana, jumba la kifalme na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.

14 Jeshi lote la Wakaldayo chini ya uongozi wa jemadari wa askari walinzi wa mfalme lilivunja kuta zote kuzunguka Yerusalemu.

15 Nebuzaradani jemadari wa walinzi akawachukua uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa hivi hivi na wale waliokuwa wamemwendea mfalme wa Babeli.

16 Lakini Nebuzaradani akaacha yale mabaki ya wale watu maskini sana wa nchi ili kufanya kazi katika mashamba ya mzabibu na mashamba mengine.

17 Wakaldayo walivunja nguzo za shaba, vile vibanio vinavyohamishika na ile Bahari ya Shaba ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu laBwana, wakachukua shaba yote na kuipeleka Babeli.

18 Walichukua pia zile sufuria, yale masepetu, ile mikasi ya kusawazishia tambi, yale mabakuli ya kunyunyizia, sahani pamoja na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika ndani ya Hekalu.

19 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yanayotumika kwa sadaka za kinywaji, vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

20 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vibanio vinavyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu laBwana, vilikuwa na uzito usioweza kupimika.

21 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili zikiwa na unene wa nyanda nne na zote zilikuwa wazi ndani.

22 Sehemu ya juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano na ilipambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Nguzo nyingine, pamoja na makomamanga yake vyote vilifanana na hiyo ya kwanza.

23 Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni, jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.

24 Waliochukuliwa na jemadari wa askari walinzi ni Seraya Kuhani Mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo na mabawabu watatu.

25 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji na washauri saba wa kifalme. Akamchukua pia mwandishi aliyekuwa afisa mkuu wa kuandika watu wa nchi na watu wake sitini waliokutwa katika mji.

26 Nebuzaradani jemadari akawachukua wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.

27 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme akaamuru wote wanyongwe.

Hivyo Yuda alitekwa, akaenda mbali na nchi yake.

28 Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni:

katika mwaka wa saba Wayahudi 3,023;

29 katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake Nebukadneza,

watu 832 kutoka Yerusalemu;

30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa kutawala kwake,

Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi wa mfalme.

Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.

Yehoyakini Anaachiwa Huru

31 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, mwaka ambao Evil-Merodakialifanyika mfalme wa Babeli, akamwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda na kumfungua kutoka gerezani katika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.

32 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima kilicho juu kuliko vya wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.

33 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya gerezani na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula katika meza ya mfalme.

34 Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho wakati wote wa uhai wake, mpaka siku ya kifo chake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/52-c2b86b923a92dc454bdb791d63c04e8c.mp3?version_id=1627—

Isaya 1

1 Maono kuhusu Yuda na Yerusalemu ambayo Isaya mwana wa Amozi aliyaona wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.

Taifa Asi

2 Sikieni, enyi mbingu! Sikilizeni, enyi dunia!

Kwa maanaBwanaamesema:

“Nimewalisha watoto na kuwalea,

lakini wameniasi mimi.

3 Ng’ombe anamjua bwana wake,

naye punda anajua hori la mmiliki wake,

lakini Israeli hajui,

watu wangu hawaelewi.”

4 Lo! Taifa lenye dhambi,

watu waliolemewa na uovu,

uzao wa watenda mabaya,

watoto waliozoelea upotovu!

WamemwachaBwana,

Wamemkataa kwa dharau

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli

na kumgeuzia kisogo.

5 Kwa nini mzidi kupigwa?

Kwa nini kudumu katika uasi?

Kichwa chako chote kimejeruhiwa,

moyo wako wote ni mgonjwa.

6 Kutoka wayo wako wa mguu

hadi kwenye utosi wa kichwa chako

hakuna uzima:

ni majeraha matupu na makovu

na vidonda vitokavyo damu,

havikusafishwa au kufungwa

wala kulainishwa kwa mafuta.

7 Nchi yenu imekuwa ukiwa,

miji yenu imeteketezwa kwa moto;

nchi yenu imeachwa tupu na wageni

mbele ya macho yenu,

imeharibiwa kama vile imepinduliwa na wageni.

8 Binti Sayuni ameachwa kama kipenu

katika shamba la mizabibu,

kama kibanda katika shamba la matikitimaji,

kama mji uliohusuriwa.

9 KamaBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote

asingelituachia walionusurika,

tungelikuwa kama Sodoma,

tungelifanana na Gomora.

10 Sikieni neno laBwana,

ninyi watawala wa Sodoma;

sikilizeni sheria ya Mungu wetu,

enyi watu wa Gomora!

11 Bwanaanasema, “Wingi wa sadaka zenu,

ni kitu gani kwangu?

Ninazo sadaka za kuteketezwa nyingi kupita kiasi,

za kondoo waume

na mafuta ya wanyama walionona,

Sipendezwi na damu za mafahali

wala za wana-kondoo na mbuzi.

12 Mnapokuja kujihudhurisha mbele zangu,

ni nani aliyewataka ninyi mfanye hivyo,

huku kuzikanyaga nyua zangu?

13 Acheni kuniletea sadaka zisizokuwa na maana!

Uvumba wenu ni chukizo kwangu.

Miandamo ya Mwezi, Sabato na makusanyiko ya ibada:

siwezi kuvumilia makusanyiko yenu maovu.

14 Sikukuu zenu za Miandamo ya Mwezi

na sikukuu zenu zilizoamriwa

moyo wangu unazichukia.

Zimekuwa mzigo kwangu,

nimechoka kuzivumilia.

15 Mnaponyosha mikono yenu katika kuomba,

nitaficha macho yangu nisiwaone;

hata mkiomba maombi mengi

sitasikiliza.

Mikono yenu imejaa damu;

16 jiosheni na mkajitakase.

Yaondoeni matendo yenu maovu

mbele zangu!

Acheni kutenda mabaya,

17 jifunzeni kutenda mema!

Tafuteni haki,

watieni moyo walioonewa.

Teteeni shauri la yatima,

wateteeni wajane.

18 “Njoni basi na tuhojiane,”

asemaBwana.

“Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu,

zitakuwa nyeupe kama theluji;

ingawa ni nyekundu sana kama damu,

zitakuwa nyeupe kama sufu.

19 Kama mkikubali na kutii,

mtakula mema ya nchi,

20 lakini kama mkikataa na kuasi,

mtaangamizwa kwa upanga.”

Kwa kuwa kinywa chaBwanakimenena.

21 Tazama jinsi ambavyo mji uliokuwa mwaminifu

umekuwa kahaba!

Mwanzoni ulikuwa umejaa unyofu,

haki ilikuwa inakaa ndani yake,

lakini sasa ni wauaji!

22 Fedha yenu imekuwa takataka,

divai yenu nzuri imechanganywa na maji.

23 Watawala wenu ni waasi,

rafiki wa wevi,

wote wanapenda rushwa

na kukimbilia hongo.

Hawatetei yatima,

shauri la mjane haliletwi mbele yao likasikilizwa.

24 Kwa hiyo Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote,

Mwenye Nguvu wa Israeli, asema hivi:

“Lo, nitapata faraja kutoka kwa adui zangu

na kujilipizia kisasi juu ya watesi wangu.

25 Nitauelekeza mkono wangu dhidi yenu,

nitawasafisha takataka yenu yote

na kuwaondolea unajisi wenu wote.

26 Nitawarudishieni waamuzi wenu

kama ilivyokuwa siku za zamani,

nao washauri wenu kama ilivyokuwa mwanzoni.

Baadaye utaitwa,

Mji wa Haki,

Mji Mwaminifu.”

27 Sayuni itakombolewa kwa haki,

wale waliomo ndani yake waliotubu kwa uaminifu.

28 Lakini waasi na wenye dhambi wote wataangamizwa,

nao wanaomwachaBwanawataangamia.

29 “Mtaaibika kwa sababu ya hiyo mialoni mliyoipenda

mkaifanya mahali pa kuabudia sanamu,

mtafadhaika kwa sababu ya bustani

mlizozichagua.

30 Mtakuwa kama mwaloni wenye majani yanayonyauka,

kama bustani isiyokuwa na maji.

31 Mtu mwenye nguvu atatoweka

kama majani makavu yawakayo moto

na kazi yake kama cheche ya moto;

vyote vitaungua pamoja,

wala hakuna wa kuuzima huo moto.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/1-7f652a74bdea1a198249732ecbbf8fbe.mp3?version_id=1627—

Isaya 2

Mlima Wa Bwana

1 Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:

2 Katika siku za mwisho

mlima wa Hekalu laBwanautaimarishwa

kama mlima mkuu miongoni mwa milima,

utainuliwa juu kupita vilima

na mataifa yote yatamiminika huko.

3 Mataifa mengi yatakuja na kusema,

“Njoni na tuupande mlima waBwana,

kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.

Atatufundisha njia zake,

ili tuweze kuenenda katika mapito yake.”

Sheria itatoka Sayuni,

neno laBwanakutoka Yerusalemu.

4 Atahukumu kati ya mataifa

na ataamua magomvi ya mataifa mengi.

Watafua panga zao kuwa majembe

na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi.

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine,

wala hayatafanya mazoezi ya vita tena.

5 Njoni, Enyi nyumba ya Yakobo,

sisi na tutembee katika nuru yaBwana

Siku Ya Bwana

6 Umewatelekeza watu wako,

nyumba ya Yakobo.

Wamejaa ushirikina utokao Mashariki,

wanapiga ramli kama Wafilisti

na wanashikana mikono na wapagani.

7 Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,

hakuna mwisho wa hazina zao.

Nchi yao imejaa farasi,

hakuna mwisho wa magari yao.

8 Nchi yao imejaa sanamu,

wanasujudia kazi za mikono yao,

vitu vile ambavyo vidole vyao vimevitengeneza.

9 Kwa hiyo mwanadamu atashushwa

na binadamu atanyenyekezwa,

usiwasamehe.

10 Ingieni kwenye miamba,

jificheni ardhini

kutokana na utisho waBwana

na utukufu wa enzi yake!

11 Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa

na kiburi cha wanadamu kitashushwa,

Bwanapeke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.

12 BwanaMwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba

kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi,

kwa wote wanaojikweza

(nao watanyenyekezwa),

13 kwa mierezi yote ya Lebanoni,

iliyo mirefu sana,

nayo mialoni yote ya Bashani,

14 kwa milima yote mirefu

na vilima vyote vilivyoinuka,

15 kwa kila mnara ulio mrefu sana

na kila ukuta wenye ngome,

16 kwa kila meli ya biashara ya Tarshishi

na kila chombo cha baharini cha fahari.

17 Majivuno ya mwanadamu yatashushwa

na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa,

Bwanapeke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,

18 nazo sanamu zitatoweka kabisa.

19 Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba

na kwenye mahandaki ardhini

kutokana na utisho waBwana

na utukufu wa enzi yake,

ainukapo kuitikisa dunia.

20 Katika siku ile watu watawatupia

panya na popo

vinyago vyao vya fedha na vya dhahabu,

walivyovitengeneza ili waviabudu.

21 Watakimbilia kwenye mapango miambani

na kwenye nyufa za miamba

kutokana na utisho waBwana

na utukufu wa enzi yake,

ainukapo kuitikisa dunia.

22 Acheni kumtumainia mwanadamu,

ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake.

Yeye ana thamani gani?

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/2-fe1cc94206caa8ad1921991cf7dd89f7.mp3?version_id=1627—

Isaya 3

Hukumu Juu Ya Yerusalemu Na Yuda.

1 Tazama sasa, Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote,

yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda

upatikanaji wa mahitaji na misaada,

upatikanaji wote wa chakula na maji,

2 shujaa na mtu wa vita,

mwamuzi na nabii,

mwaguzi na mzee,

3 jemadari wa kikosi cha watu hamsini

na mtu mwenye cheo, mshauri,

fundi stadi na mlozi mjanja.

4 Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao,

watoto ndio watakaowatawala.

5 Watu wataoneana wao kwa wao

mtu dhidi ya mtu,

jirani dhidi ya jirani yake.

Kijana atainuka dhidi ya mzee,

mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.

6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake

katika nyumba ya baba yake na kusema,

“Unalo joho, wewe uwe kiongozi wetu,

tawala lundo hili la magofu!”

7 Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema,

“Sina uponyaji.

Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu,

msinifanye niwe kiongozi wa watu.”

8 Yerusalemu inapepesuka,

Yuda inaanguka;

maneno yao na matendo yao ni kinyume naBwana,

wakiudharau uwepo wake uliotukuka.

9 Nyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao,

hujivunia dhambi yao kama Sodoma,

wala hawaifichi.

Ole wao!

Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.

10 Waambie wanyofu itakuwa heri kwao,

kwa kuwa watafurahia tunda la matendo yao.

11 Ole wa watu waovu! Maafa yapo juu yao!

Watalipwa kwa ajili ya yale mikono yao iliyotenda.

12 Vijana wanawatesa watu wangu,

wanawake wanawatawala.

Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha,

wanawapoteza njia.

13 Bwanaanachukua nafasi yake mahakamani,

anasimama kuhukumu watu.

14 Bwanaanaingia katika hukumu

dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake:

“Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu,

mali zilizonyang’anywa kutoka kwa maskini

zimo nyumbani mwenu.

15 Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu

na kuzisaga nyuso za maskini?”

asema Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote.

16 Bwanaasema,

“Wanawake wa Sayuni wana kiburi,

wanatembea na shingo ndefu,

wakikonyeza kwa macho yao,

wakitembea kwa hatua fupi fupi za madaha,

wakiwa na mapambo yanayotoa mlio kwenye vifundo vya miguu yao.

17 Kwa hiyo Bwana ataleta majipu kwenye vichwa vya wanawake wa Sayuni;

Bwanaatazifanya ngozi za vichwa vyao kuwa vipara.”

18 Katika siku ile Bwana atawanyang’anya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,

19 vipuli, vikuku, shela,

20 vilemba, mikufu ya kwenye vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,

21 pete zenye muhuri, pete za puani,

22 majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha,

23 vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.

24 Badala ya harufu ya manukato kutakuwa na uvundo;

badala ya mishipi, kamba;

badala ya nywele zilizotengenezwa vizuri, upara;

badala ya mavazi mazuri, nguo za magunia;

badala ya uzuri, alama ya aibu kwa chuma cha moto.

25 Wanaume wako watauawa kwa upanga,

mashujaa wako watauawa vitani.

26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia,

akiwa maskini, ataketi mavumbini.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/3-97337bf7bbab98858f9a6194f2663a83.mp3?version_id=1627—

Isaya 4

1 Katika siku ile wanawake saba

watamshika mwanaume mmoja

wakisema, “Tutakula chakula chetu wenyewe

na kuvaa nguo zetu wenyewe,

ila wewe uturuhusu tu tuitwe kwa jina lako.

Utuondolee aibu yetu!”

Tawi La Bwana

2 Katika siku ile Tawi laBwanalitakuwa zuri na lenye utukufu, nalo tunda la nchi litakuwa fahari na utukufu wa wale Waisraeli watakaonusurika.

3 Wale watakaoachwa Sayuni, watakaobaki Yerusalemu, wataitwa watakatifu, wale wote ambao wameorodheshwa miongoni mwa walio hai huko Yerusalemu.

4 Bwana atausafisha uchafu wa wanawake wa Sayuni, atatakasa madoa ya damu kutoka Yerusalemu kwa Roho ya hukumu na Roho ya moto.

5 KishaBwanaataumba juu ya Mlima wote wa Sayuni na juu ya wale wote wanaokusanyika hapo, wingu la moshi wakati wa mchana na kung’aa kwa miali ya moto wakati wa usiku, juu ya huo utukufu wote kutatanda kifuniko cha ulinzi.

6 Utakuwa sitara na kivuli kutokana na joto la mchana na kuwa mahali pa kujificha kutokana na dhoruba na mvua.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/4-29a0f8ff5e4f3c8fcfb5d73edd660c18.mp3?version_id=1627—

Isaya 5

Wimbo Wa Shamba La Mizabibu

1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye

kuhusu shamba lake la mizabibu:

Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu

kwenye kilima chenye rutuba.

2 Alililima na kuondoa mawe

na akaliotesha mizabibu bora sana.

Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake

na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia.

Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri,

lakini lilizaa matunda mabaya tu.

3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda,

hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.

4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika

kwa ajili ya shamba langu la mizabibu

kuliko yale niliyofanya?

Nilipotazamia kupata zabibu nzuri,

kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?

5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea

shamba langu la mizabibu:

Nitaondoa uzio wake,

nalo litaharibiwa,

nitabomoa ukuta wake,

nalo litakanyagwa.

6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu,

halitakatiwa matawi wala kulimwa,

nayo michongoma na miiba itamea huko,

nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”

7 Shamba la mzabibu laBwanaMwenye Nguvu Zote

ni nyumba ya Israeli,

na watu wa Yuda

ni bustani yake ya kumpendeza.

Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu,

alitazamia uadilifu,

lakini akasikia vilio vya taabu.

8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba

na kuunganisha mashamba baada ya mashamba

hadi hakuna nafasi iliyobaki

nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.

9 BwanaMwenye Nguvu Zote amesema nikisikia:

“Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa,

nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.

10 Shamba la mizabibu la eka kumi

# litatoa bathimoja ya divai,

# na homeriya mbegu zilizopandwa

# itatoa efamoja tu ya nafaka.”

11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema

wakikimbilia kunywa vileo,

wale wakawiao sana mpaka usiku,

mpaka wamewaka kwa mvinyo.

12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao,

matari, filimbi na mvinyo,

lakini hawayajali matendo yaBwana,

wala hawana heshima

kwa ajili ya kazi ya mikono yake.

13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni

kwa sababu ya kukosa ufahamu,

watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa

na watu wao wengi watakauka kwa kiu.

14 Kwa hiyo kaburilimeongeza hamu yake

na kupanua mdomo wake bila kikomo,

ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu

pamoja na wagomvi wao

na wafanyao sherehe wote.

15 Hivyo mwanadamu atashushwa

na binadamu atanyenyekezwa,

macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.

16 LakiniBwanaMwenye Nguvu Zote atatukuzwa

kwa ajili ya haki yake,

naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe

kuwa mtakatifu kwa haki yake.

17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe,

wana-kondoo na wageni watajilisha

katika magofu ya matajiri.

18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu

na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,

19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka,

aharakishe kazi yake

ili tupate kuiona.

Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike,

tena udhihirike ili tupate kuujua.”

20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema

na wema ni ubaya,

wawekao giza badala ya nuru

na nuru badala ya giza,

wawekao uchungu badala ya utamu

na utamu badala ya uchungu.

21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe

na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.

22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo

nao walio hodari katika kuchanganya vileo,

23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo,

lakini huwanyima haki wasio na hatia.

24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi

na kama vile majani makavu

yazamavyo katika miali ya moto,

ndivyo mizizi yao itakavyooza

na maua yao yatakavyopeperushwa

kama mavumbi;

kwa kuwa wameikataa sheria yaBwanaMwenye Nguvu Zote

na kulisukumia mbali

neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.

25 Kwa hiyo hasira yaBwanainawaka dhidi ya watu wake,

mkono wake umeinuliwa na anawapiga.

Milima inatetemeka,

maiti ni kama takataka kwenye barabara.

Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali,

mkono wake bado umeinuliwa juu.

26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali,

anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia.

Tazama wamekuja,

kwa kasi na kwa haraka!

27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa,

hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala,

hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni,

hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.

28 Mishale yao ni mikali,

pinde zao zote zimevutwa,

kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume,

magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.

29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba,

wananguruma kama wana simba,

wanakoroma wanapokamata mawindo yao

na kuondoka nayo pasipo ye yote wa kuokoa.

30 Katika siku ile watanguruma juu yake

kama ngurumo za bahari.

Kama mtu akiitazama nchi,

ataona giza na dhiki;

hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/5-9bfcdfb609100a4924e8bba32be4ad0b.mp3?version_id=1627—

Isaya 6

Agizo Kwa Isaya

1 Katika mwaka ule Mfalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu.

2 Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao na kwa mawili walikuwa wakiruka.

3 Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake:

“Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu

niBwanaMwenye Nguvu Zote;

dunia yote imejaa utukufu wake.”

4 Kwa kutoa kwao sauti miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.

5 Ndipo nikalia, “Ole wangu mimi! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme,BwanaMwenye Nguvu Zote.”

6 Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni.

7 Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa nayo dhambi yako imesamehewa.”

8 Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?”

Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”

9 Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa:

“ ‘Mtaendelea daima kusikia,

lakini kamwe hamtafahamu;

mtaendelea daima kuona,

lakini kamwe hamtatambua.’

10 Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu,

fanya masikio yao yasisikie

na upofushe macho yao.

Ama sivyo wanaweza kuona kwa macho yao,

wakasikia kwa masikio yao,

wakatambua kwa mioyo yao,

nao wakageuka na kuponywa.”

11 Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?”

Naye akanijibu:

“Hadi miji iwe imeachwa magofu

na bila wakazi,

hadi nyumba zitakapobaki bila watu,

na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,

12 hadiBwanaatakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana,

na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.

13 Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi,

itaharibiwa tena.

Lakini kama vile mvinje na mwaloni

ibakizavyo visiki inapokatwa,

ndivyo mbegu takatifu

itakavyokuwa kisiki katika nchi.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/6-477c55de37f264094758a353be047415.mp3?version_id=1627—