Isaya 47

Anguko La Babeli

1 “Shuka uketi mavumbini,

Ee Bikira Binti Babeli;

keti chini pasipo na kiti cha enzi,

Ee binti wa Wakaldayo.

Hutaitwa tena mwororo wala wa kupendeza.

2 Chukua mawe ya kusagia na usage unga,

vua shela yako.

Pandisha mavazi yako, ondoa viatu vyako,

vuka vijito kwa shida.

3 Uchi wako utafunuliwa

na aibu yako itaonekana.

Nitalipa kisasi;

sitamhurumia hata mmoja.”

4 Mkombozi wetu:BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo jina lake;

ndiye yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

5 “Keti kimya, ingia gizani,

Binti wa Wakaldayo,

hutaitwa tena malkia wa falme.

6 Niliwakasirikia watu wangu

na kuaibisha urithi wangu;

niliwatia mikononi mwako,

nawe hukuwaonea huruma.

Hata juu ya wazee

uliweka nira nzito sana.

7 Ukasema, ‘Nitaendelea

kuwa malkia milele!’

Lakini hukutafakari mambo haya

wala hukuwaza juu ya kile ambacho

kingeweza kutokea.

8 “Sasa basi, sikiliza, ewe kiumbe mpenda anasa,

ukaaye katika mahali pako pa salama

na kujiambia mwenyewe,

‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.

Kamwe sitakuwa mjane

wala sitafiwa na watoto.’

9 Haya yote mawili yatakupata kufumba na kufumbua,

katika siku moja:

kufiwa na watoto na ujane.

Vyote hivyo vitakupata kwa kipimo kikamilifu,

ijapokuwa uchawi wako ni mwingi

na uaguzi wako ni mwingi.

10 Umeutegemea uovu wako,

nawe umesema, ‘Hakuna ye yote anionaye.’

Hekima yako na maarifa yako vinakupoteza

unapojiambia mwenyewe,

‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.’

11 Maafa yatakujia,

nawe hutaweza kuyaondoa kwa uaguzi.

Janga litakuangukia

wala hutaweza kulikinga kwa fidia;

msiba mkuu usioweza kuutabiri

utakujia ghafula.

12 “Endelea basi na uaguzi wako

na wingi wa uchawi wako,

ambao umeutumikia tangu utoto wako.

Labda utafanikiwa,

labda unaweza ukasababisha hofu kuu.

13 Ushauri wote uliopokea umekuchosha bure!

Wanajimu wako na waje mbele,

wale watazamao nyota na watabirio mwezi baada ya mwezi,

wao na wawaokoe na lile linalokuja juu yenu.

14 Hakika wako kama mabua makavu,

moto utawateketeza.

Hawawezi hata kujiokoa wao wenyewe

kutokana na nguvu za mwali wa moto.

Hapa hakuna makaa ya kumtia mtu ye yote joto;

hapa hakuna moto wa kuota.

15 Hayo ndiyo yote wanayoweza kuwatendea ninyi,

hawa ambao umetaabika nao

na kufanya nao biashara tangu utoto.

Kila mmoja atatoroka;

hakuna ye yote awezaye kukuokoa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/47-c3e227e8184bc18015f56aa605c72ec6.mp3?version_id=1627—

Isaya 48

Israeli Mkaidi

1 “Sikilizeni hili, Ee nyumba ya Yakobo,

ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli

na mnaotoka katika ukoo wa Yuda,

ninyi mnaoapa kwa jina laBwana,

mnaomwomba Mungu wa Israeli,

lakini si katika kweli au kwa haki;

2 ninyi mnaojiita raia wa mji mtakatifu,

na kumtegemea Mungu wa Israeli,

BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:

3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani,

kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane;

kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.

4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi;

mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma,

kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.

5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani,

kabla hayajatokea nilikutangazia

ili kwamba usije ukasema,

‘Sanamu zangu zilifanya hayo;

kinyago changu cha mti

na mungu wangu wa chuma ameyaamuru.’

6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote.

Je, hutayakubali?

“Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya,

juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.

7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani;

hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo.

Hivyo huwezi kusema,

‘Naam, niliyajua hayo.’

8 Hujayasikia wala kuyaelewa,

tangu zamani sikio lako halikufunguka.

Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu,

uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.

9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe

ninaichelewesha ghadhabu yangu,

kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate,

ili nisije nikakukatilia mbali.

10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha,

nimekujaribu katika tanuru ya mateso.

11 Kwa ajili yangu mwenyewe,

kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili.

Kwa jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe?

Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.

Israeli Anawekwa Huru

12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi,

Israeli, ambaye nimekuita:

Mimi ndiye;

mimi ndimi mwanzo na mwisho.

13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia,

nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu;

niziitapo, zote husimama pamoja.

14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize:

Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu

ambayo imetabiri vitu hivi?

Watu waBwanawaliochaguliwa na kuungana

watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli;

mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.

15 Mimi, yaani Mimi, nimenena;

naam, nimemwita yeye.

Nitamleta,

naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.

16 “Nikaribieni na msikilize hili:

“Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri;

wakati litokeapo, nitakuwako hapo.”

SasaBwanaMwenyezi amenituma,

kwa Roho wake.

17 Hili ndilo asemaloBwana,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli:

“Mimi niBwana, Mungu wako,

nikufundishaye ili upate faida,

nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.

18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu,

amani yako ingekuwa kama mto,

haki yako kama mawimbi ya bahari.

19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga,

watoto wako kama chembe zake zisizohesabika;

kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali,

wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”

20 Tokeni Babeli,

kimbieni kutoka kwa Wakaldayo!

Tangazeni hili kwa kelele za shangwe

na kulihubiri.

Lipelekeni mpaka miisho ya dunia;

semeni, “Bwanaamemkomboa

mtumishi wake Yakobo.”

21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita katika majangwa;

alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao;

akapasua mwamba

na maji yakatoka kwa nguvu.

22 “Hakuna amani kwa waovu,” asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/48-ef9faba49d1e960ff4a6402c1f9b7397.mp3?version_id=1627—

Isaya 49

Mtumishi Wa Bwana

1 Nisikilizeni, Enyi visiwa, sikieni hili,

ninyi mataifa mlio mbali:

Kabla sijazaliwaBwanaaliniita,

tangu kuzaliwa kwangu amelitaja jina langu.

2 Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa,

katika uvuli wa mkono wake akanificha;

akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa

na kunificha katika podo lake.

3 Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu,

Israeli, ambaye katika yeye

nitaonyesha utukufu wangu.”

4 Lakini nilisema, “Nimetumika bure,

nimetumia nguvu zangu bure bila faida.

Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwaBwana,

nayo ijara yangu iko kwa Mungu wangu.”

5 SasaBwanaasema,

yeye aliyeniumba tumboni

kuwa mtumishi wake

kumrudisha tena Yakobo kwake

na kumkusanyia Israeli,

kwa maana nimepata heshima machoni paBwana,

naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;

6 anasema:

“Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu

ili kurejeza upya makabila ya Yakobo,

na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi?

Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu Mataifa,

ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”

7 Hili ndilo asemaloBwana,

yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli,

kwake yeye ambaye alidharauliwa na

kuchukiwa na taifa,

kwa mtumishi wa watawala:

“Wafalme watakuona na kusimama,

wakuu wataona na kuanguka kifudifudi,

kwa sababu yaBwana, aliye mwaminifu,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,

ambaye amekuchagua wewe.”

Kurejezwa Kwa Israeli

8 Hili ndilo asemaloBwana:

“Wakati wangu uliokubalika nitakujibu,

nami katika siku ya wokovu nitakusaidia;

nitakuhifadhi nami nitakufanya

kuwa Agano kwa ajili ya watu,

ili kurudisha nchi na kugawanyia tena

urithi waliokuwa ukiwa,

9 kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’

nao wale walio gizani, ‘Iweni huru!’

“Watajilisha kando ya barabara

na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.

10 Hawataona njaa wala kuona kiu,

wala hari ya jangwani au jua halitawapiga.

Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia

na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.

11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara

na njia kuu zangu zitainuliwa.

12 Tazama, watakuja kutoka mbali:

wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi,

# wengine kutoka nchi ya Sinimu.”

13 Pigeni kelele kwa furaha, Enyi mbingu;

furahi, Ee dunia;

pazeni sauti kwa kuimba, Enyi milima!

Kwa maanaBwanaanawafariji watu wake,

naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.

14 Lakini Sayuni alisema, “Bwanaameniacha,

Bwana amenisahau.”

15 “Je, mama aweza kumsahau mtoto

aliyeko matitini mwake akinyonya,

wala asiwe na huruma

juu ya mtoto aliyemzaa?

Ingawa anaweza kusahau,

mimi sitakusahau wewe!

16 Tazama, nimekuchora kama muhuri

katika vitanga vya mikono yangu,

kuta zako zi mbele yangu daima.

17 Wana wako wanaharakisha kurudi,

nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.

18 Inua macho yako ukatazame pande zote,

wana wako wote wanakusanyika na kukujia.

Kwa hakika kama vile niishivyo,

utawavaa wote kama mapambo,

na kujifunga nao kama bibi arusi,”

asemaBwana.

19 “Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa

na nchi yako ikaharibiwa,

sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako,

nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.

20 Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako

bado watakuambia,

‘Mahali hapa ni finyu sana kwa ajili yetu,

tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’

21 Ndipo utasema moyoni mwako,

‘Ni nani aliyenizalia hawa?

Nilikuwa nimefiwa tena ni tasa;

nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa.

Ni nani aliyewalea hawa?

Niliachwa peke yangu,

lakini hawa, wametoka wapi?’ ”

22 Hili ndilo asemaloBwanaMwenyezi:

“Tazama, nitawaashiria watu Mataifa,

nitainua bendera yangu kwa mataifa;

watawaleta wana wako kwenye mikono yao

na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.

23 Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea

na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea.

Watasujudu mbele yako na nyuso zao zikigusa ardhi;

watalamba mavumbi yaliyo miguuni mwako.

Ndipo utajua yakuwa Mimi ndimiBwana;

wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”

24 Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita,

au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?

25 Lakini hili ndilo asemaloBwana:

“Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa,

na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali.

Nitashindana na wale wanaoshindana nawe,

nami nitawaokoa watoto wako.

26 Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe,

watalewa kwa damu yao wenyewe,

kama vile kwa mvinyo.

Ndipo wanadamu wote watajua

ya kuwa Mimi,Bwana, ni Mwokozi wako,

Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/49-3756dc0655b9545f1a78eec34c6ba2cd.mp3?version_id=1627—

Isaya 50

Dhambi Ya Israeli Na Utii Wa Mtumishi

1 Hili ndilo asemaloBwana:

“Iko wapi hati ya talaka ya mama yako

ambayo kwayo niliachana naye?

Au nimewauza ninyi kwa nani

miongoni mwa watu wanaonidai?

Kwa ajili ya dhambi zenu mliuzwa,

kwa sababu ya makosa mama yenu aliachwa.

2 Nilipokuja, kwa nini hakuwepo hata mmoja?

Nilipoita, kwa nini hakuwepo hata mmoja wa kujibu?

Je, mkono wangu ni mfupi mno hata nisiweze kuwakomboa?

Je, mimi sina nguvu za kukuokoa?

Kwa kukemea tu naikausha bahari,

naigeuza mito ya maji kuwa jangwa;

samaki wake wanaoza kwa kukosa maji

na kufa kwa ajili ya kiu.

3 Ninalivika anga weusi na kufanya nguo ya gunia

kuwa kifuniko chake.”

4 BwanaMwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa,

ili kujua neno lile limtegemezalo aliyechoka.

Huniamsha asubuhi kwa asubuhi,

huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.

5 BwanaMwenyezi amezibua masikio yangu,

nami sikuwa mwasi,

wala sikurudi nyuma.

6 Niliwapa mgongo wangu wale wanipigao,

mashavu yangu wale wang’oao ndevu zangu;

sikuuficha uso wangu kutokana na fedheha

na kutemewa mate.

7 Kwa sababuBwanaMwenyezi ananisaidia,

sitatahayarika.

Kwa hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe la gumegume,

nami ninajua sitaaibika.

8 Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu.

Ni nani basi atakayeleta mashtaka dhidi yangu?

Tukabiliane uso kwa uso!

Mshitaki wangu ni nani?

Ni nani aliye mshitaki wangu?

9 NiBwanaMwenyezi ndiye anisaidiaye mimi.

Ni nani huyo atakayenihukumu?

Wote watachakaa kama vazi,

nondo atawala awamalize.

10 Ni nani miongoni mwenu amchayeBwana

na kulitii neno la mtumishi wake?

Yeye atembeaye gizani,

yeye asiye na nuru,

na alitumainie jina laBwana

na amtegemee Mungu wake.

11 Lakini sasa, ninyi nyote mnaowasha mioto

na kupeana ninyi kwa ninyi mienge iwakayo,

nendeni, tembeeni katika nuru ya moto wenu

na ya mienge mliyoiwasha.

Hili ndilo mtakalolipokea kutoka mkononi mwangu:

Mtalala chini kwa mateso makali.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/50-ebb04f50960cdafa3d3403a8043fd55d.mp3?version_id=1627—

Isaya 51

Wokovu Wa Milele Kwa Sayuni

1 “Nisikilizeni, ninyi mnaofuatia haki

na mnaomtafutaBwana:

Tazameni katika mwamba ambako ndiko mlikokatwa

na mahali pa kuvunjia mawe ambako ndiko mlikochongwa;

2 mwangalieni Abrahamu, baba yenu,

na Sara, ambaye ndiye aliyewazaa.

Wakati nilipomwita alikuwa mmoja tu,

nami nikambariki na kumfanya kuwa wengi.

3 HakikaBwanaataifariji Sayuni

naye atayaangalia kwa huruma magofu yake yote;

atayafanya majangwa yake kama Edeni,

nazo sehemu zake zisizolimika wala zisizofaa

kukaliwa na watu kama bustani yaBwana.

Shangwe na furaha zitakuwako ndani yake,

shukrani na sauti za kuimba.

4 “Nisikilizeni, watu wangu;

nisikieni, taifa langu:

Sheria itatoka kwangu;

haki yangu itakuwa nuru kwa mataifa.

5 Haki yangu inakaribia inakuja mbio,

wokovu wangu unakuja,

nao mkono wangu utaleta hukumu kwa mataifa.

Visiwa vitanitegemea

na kungojea kwa matumaini mkono wangu.

6 Inueni macho yenu mbinguni,

mkaitazame dunia chini;

mbingu zitatoweka kama moshi,

dunia itachakaa kama vazi

na wakazi wake kufa kama mainzi.

Bali wokovu wangu utadumu milele,

haki yangu haitakoma kamwe.

7 “Nisikieni, ninyi mnaojua lile lililo sawa,

ninyi watu ambao mna sheria yangu mioyoni mwenu:

Msiogope mashutumu ya wanadamu

wala msitiwe hofu na matukano yao.

8 Kwa maana nondo atawala kama vazi,

nao funza atawatafuna kama sufu.

Lakini haki yangu itadumu milele,

wokovu wangu kwa vizazi vyote.”

9 Amka, Amka! Jivike nguvu,

Ewe mkono waBwana,

Amka, kama vile siku zilizopita,

kama vile katika vizazi vya zamani.

Si ni wewe uliyemkata Rahabu vipande vipande,

uliyemchoma yule joka?

10 Si ni wewe uliyekausha bahari,

maji ya kilindi kikuu,

uliyefanya barabara katika vilindi vya bahari

ili waliokombolewa wapate kuvuka?

11 Wale waliolipiwa fidia naBwanawatarudi.

Wataingia Sayuni wakiimba;

furaha ya milele itakuwa taji juu ya vichwa vyao.

Furaha na shangwe zitawapata,

huzuni na kulia kwa uchungu kutatoweka.

12 “Mimi, naam mimi,

ndimi niwafarijie ninyi.

Ninyi ni nani hata kuwaogopa

wanadamu wanaokufa,

wana wa wanadamu ambao ni majani tu,

13 kwamba mnamsahauBwanaMuumba wenu,

aliyezitanda mbingu

na kuiweka misingi ya dunia,

kwamba mnaishi katika hofu siku zote

kwa sababu ya ghadhabu ya mdhalimu,

ambaye nia yake ni kuangamiza?

Iko wapi basi ghadhabu ya mdhalimu?

14 Wafungwa waliojikunyata kwa hofu

watawekwa huru karibuni;

hawatafia kwenye gereza lao,

wala hawatakosa chakula.

15 Kwa maana Mimi ndimiBwana, Mungu wako,

ambaye huisukasuka bahari ili mawimbi yake yangurume,

BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

16 Nimeweka maneno yangu kinywani mwako

na kukufunika kwa uvuli wa mkono wangu:

Mimi niliyeweka mbingu katika nafasi,

niliyeweka misingi ya dunia,

niwaambiaye Sayuni,

‘Ninyi ni watu wangu.’ ”

Kikombe Cha Ghadhabu Ya Bwana

17 Amka, amka!

Simama, Ee Yerusalemu,

wewe uliyekunywa kutoka katika mkono waBwana

kikombe cha ghadhabu yake,

wewe uliyekunywa mpaka kufikia machujo yake,

kikombe kile cha kunywea

kiwafanyacho watu kuyumbayumba.

18 Kati ya wana wote aliowazaa

hakuwepo hata mmoja wa kumwongoza,

kati ya wana wote aliowalea

hakuwepo hata mmoja wa kumshika mkono.

19 Majanga haya mawili yamekuja juu yako:

ni nani awezaye kukufariji?

Maangamizi, uharibifu, njaa na upanga:

ni nani awezaye kukutuliza?

20 Wana wako wamezimia,

wamelala kwenye mwanzo wa kila barabara,

kama swala aliyenaswa kwenye wavu.

Wamejazwa na ghadhabu yaBwana

na makaripio ya Mungu wako.

21 Kwa hiyo sikiliza hili, wewe uliyeteswa,

uliyelewa, lakini si kwa mvinyo.

22 Hili ndilo asemaloBwanaMwenyezi wako,

Mungu wako, yeye ambaye huwatetea watu wake:

“Tazama, nimeondoa mkononi mwako

kikombe kilichokufanya uyumbeyumbe;

kutoka katika kikombe hicho,

kikombe cha kunywa cha ghadhabu yangu,

kamwe hutakunywa tena.

23 Nitakiweka mikononi mwa watesi wako,

wale waliokuambia,

‘Anguka kifudifudi

ili tuweze kutembea juu yako.’

Ukaufanya mgongo wako kama ardhi,

kama njia yao ya kupita.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/51-f745b61a926dc7b2dcdcd68d4df3598b.mp3?version_id=1627—

Isaya 52

1 Amka, amka, Ee Sayuni,

jivike nguvu.

Vaa mavazi yako ya fahari,

Ee Yerusalemu, mji mtakatifu.

Asiyetahiriwa na aliye najisi

hataingia kwako tena.

2 Jikung’ute mavumbi yako,

inuka, uketi kwenye kiti cha enzi, Ee Yerusalemu.

Jifungue minyororo iliyo shingoni mwako.

Ee Binti Sayuni uliye mateka.

3 Kwa kuwa hili ndilo asemaloBwana:

“Mliuzwa pasipo malipo,

nanyi mtakombolewa bila fedha.”

4 Kwa maana hili ndilo asemaloBwanaMwenyezi:

“Hapo kwanza watu wangu walishuka Misri kuishi,

hatimaye, Ashuru wakawaonea.

5 “Basi sasa nina nini hapa?” asemaBwana.

“Kwa kuwa watu wangu wamechukuliwa pasipo malipo,

nao wale wanaowatawala wanawadhihaki,”

asemaBwana.

“Mchana kutwa

jina langu limetukanwa bila kikomo.

6 Kwa hiyo watu wangu watalijua Jina langu;

kwa hiyo katika siku ile watajua

kwamba ndimi niliyetangulia kulisema.

Naam, ni mimi.”

7 Tazama jinsi ilivyo mizuri juu ya milima

miguu yao wale waletao habari njema,

wale wanaotangaza amani,

wanaoleta habari njema,

wanaotangaza wokovu,

wauambiao Sayuni,

“Mungu wako anatawala!”

8 Sikiliza! Walinzi wako wanapaza sauti zao,

kwa pamoja wanapaza sauti zao kwa furaha.

WakatiBwanaatakaporejea Sayuni,

wataliona kwa macho yao wenyewe.

9 Pazeni sauti ya nyimbo za furaha kwa pamoja,

enyi magofu ya Yerusalemu,

kwa maanaBwanaamewafariji watu wake,

ameikomboa Yerusalemu.

10 Mkono mtakatifu waBwanaumefunuliwa

machoni pa mataifa yote,

nayo miisho yote ya dunia itaona

wokovu wa Mungu wetu.

11 Ondokeni, ondokeni, tokeni huko!

Msiguse kitu kilicho najisi!

Tokeni kati yake mwe safi,

ninyi mchukuao vyombo vyaBwana.

12 Lakini hamtaondoka kwa haraka,

wala hamtakwenda kwa kukimbia;

kwa maanaBwanaatatangulia mbele yenu,

Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi nyuma yenu.

Mateso Na Utukufu Wa Mtumishi

13 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa hekima;

atatukuzwa na kuinuliwa juu na kukwezwa sana.

14 Kama ambavyo walikuweko wengi

walioshangazwa naye,

uso wake ulikuwa umeharibiwa sana

zaidi ya mtu ye yote

na umbo lake kuharibiwa

zaidi ya mfano wa mwanadamu:

15 hivyo atashangaza mataifa mengi,

nao wafalme watafunga vinywa vyao

kwa sababu yake.

Kwa kuwa yale ambayo hawakuambiwa, watayaona,

nayo yale wasiyoyasikia,

watayafahamu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/52-60ccd17162f8f971ccf3535f61e23995.mp3?version_id=1627—

Isaya 53

1 Ni nani aliyeamini ujumbe wetu

na mkono waBwana

umefunuliwa kwa nani?

2 Alikua mbele yake kama mche mwororo

na kama mzizi katika nchi kavu.

Hakuwa na uzuri wala utukufu wa kutuvuta kwake,

hakuwa na cho chote katika kuonekana kwake

cha kutufanya tumtamani.

3 Alidharauliwa na kukataliwa na wanadamu,

mtu wa huzuni nyingi, ajuaye mateso.

Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao,

alidharauliwa,

wala hatukumhesabu kuwa kitu.

4 Hakika alichukua udhaifu wetu

na akajitwika huzuni zetu,

hata hivyo tulifikiri amepigwa na Mungu,

amepigwa sana naye na kuteswa.

5 Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu,

alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu;

adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake,

na kwa majeraha yake sisi tumepona.

6 Sisi sote, kama kondoo, tumepotea,

kila mmoja wetu amegeukia

njia yake mwenyewe,

nayeBwanaaliweka juu yake

maovu yetu sisi sote.

7 Alionewa na kuteswa,

hata hivyo hakufungua kinywa chake;

aliongozwa kama mwana-kondoo

apelekwaye machinjoni,

kama vile kondoo anyamazavyo mbele yake

yeye amkataye manyoya,

hivyo hakufungua kinywa chake.

8 Kwa kukamatwa na kuhukumiwa aliondolewa.

Ni nani atakayeweza kueleza

kuhusu kizazi chake?

Kwa maana alikatiliwa mbali na nchi ya walio hai,

alipigwa kwa ajili ya makosa ya watu wangu.

9 Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu,

pamoja na matajiri katika kifo chake,

ingawa hakutenda jeuri,

wala hapakuwa na hila kinywani mwake.

10 Lakini yalikuwa ni mapenzi yaBwana

kumchubua na kumsababisha ateseke,

ingawaBwanaamefanya maisha yake

kuwa sadaka ya hatia,

ataona uzao wake na kuishi siku nyingi,

nayo mapenzi yaBwana

yatafanikiwa mkononi mwake.

11 Baada ya maumivu ya nafsi yake,

ataona nuru ya uzima na kuridhika;

kwa maarifa yake, mtumishi wangu mwenye haki

atawafanya wengi kuwa wenye haki,

naye atayachukua maovu yao.

12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu

miongoni mwa wakuu,

naye atagawana nyara

pamoja na wenye nguvu,

kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti,

naye alihesabiwa pamoja na wakosaji.

Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi,

na kuwaombea wakosaji.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/53-ace0856423d7685405dade8d355f362b.mp3?version_id=1627—

Isaya 54

Utukufu Wa Baadaye Wa Sayuni

1 “Imba, Ewe mwanamke tasa,

wewe ambaye kamwe hukuzaa mtoto;

paza sauti kwa kuimba, piga kelele kwa furaha,

ninyi ambao kamwe

hamkupata utungu wa kuzaa;

kwa sababu watoto wa mwanamke

aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume,”

asemaBwana.

2 “Panua mahali pa hema lako,

tandaza mapazia ya hema lako uyaeneze mbali,

wala usiyazuie;

ongeza urefu wa kamba zako,

imarisha vigingi vyako.

3 Kwa maana utaenea upande wa kuume

na upande wa kushoto;

wazao wako watayamiliki mataifa

na kukaa katika miji yao iliyoachwa ukiwa.

4 “Usiogope, wewe hutaaibika.

Usiogope aibu, wewe hutaaibishwa.

Wewe utasahau aibu ya ujana wako,

wala hutakumbuka tena

mashutumu ya ujane wako.

5 Kwa maana Muumba wako ndiye mume wako,

BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo jina lake,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako,

yeye anaitwa Mungu wa dunia yote.

6 Bwanaatakuita urudi

kana kwamba ulikuwa mke aliyeachwa

na kuhuzunishwa rohoni;

kama mke aliyeolewa bado angali kijana

na kukataliwa,” asema Mungu wako.

7 “Kwa kitambo kidogo nilikuacha,

lakini kwa huruma nyingi nitakurudisha.

8 Katika ukali wa hasira

nilikuficha uso wangu kwa kitambo,

lakini kwa fadhili za milele

nitakuwa na huruma juu yako,”

asemaBwanaMkombozi wako.

9 “Kwangu mimi hili ni kama siku za Noa,

nilipoapa kuwa maji ya Noa

kamwe hayatafunika tena dunia.

Hivyo sasa nimeapa sitawakasirikia ninyi,

kamwe sitawakemea tena.

10 Ijapotikisika milima na vilima viondolewe,

hata hivyo upendo wangu

usiokoma kwenu hautatikisika,

wala Agano langu la amani halitaondolewa,”

asemaBwana, mwenye huruma juu yenu.

11 “Ewe mji uliyeteswa, uliyepigwa kwa dhoruba

na usiyetulizwa,

nitakujenga kwa almasi,

nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.

12 Nitafanya minara yako ya akiki,

malango yako kwa vito ving’aavyo,

nazo kuta zako zote za mawe ya thamani.

13 Watoto wako wote watafundishwa naBwana,

nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

14 Kwa haki utathibitika:

Kuonewa kutakuwa mbali nawe;

hutaogopa cho chote.

Hofu itakuwa mbali nawe;

haitakukaribia wewe.

15 Kama mtu ye yote akikushambulia,

haitakuwa kwa ruhusa yangu;

ye yote akushambuliaye

atajisalimisha kwako.

16 “Tazama, ni mimi niliyemwumba mhunzi

yeye afukutaye makaa kuwa moto,

na kutengeneza silaha inayofaa kwa kazi yake.

Tena ni mimi niliyemwambia mharabu

kufanya uharibifu mwingi;

17 hakuna silaha itakayofanyizwa dhidi yako

itakayofanikiwa,

nawe utauthibitisha kuwa mwongo

kila ulimi utakaokushitaki.

Huu ndio urithi wa watumishi waBwana

na hii ndiyo haki yao itokayo kwangu,”

asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/54-8a15f0a458827af4e4b879f5f7f872ed.mp3?version_id=1627—

Isaya 55

Mwaliko Kwa Wenye Kiu

1 “Njoni, ninyi nyote wenye kiu,

njoni kwenye maji;

nanyi ambao hamna fedha,

njoni, nunueni na mle!

Njoni, nunueni divai na maziwa

bila fedha na bila gharama.

2 Kwa nini kutumia fedha kwa kitu ambacho si chakula,

na kutaabikia kitu kisichoshibisha?

Sikilizeni, nisikilizeni mimi na mle kilicho kizuri,

nazo nafsi zenu zitafurahia utajiri wa unono.

3 Tegeni sikio mje kwangu,

nisikieni mimi, ili nafsi zenu zipate kuishi.

Nitafanya Agano la milele nanyi,

pendo la uaminifu nililomwahidi Daudi.

4 Tazama, nimemfanya kuwa shahidi wa mataifa,

kiongozi na jemadari wa mataifa.

5 Hakika utaita mataifa usiyoyajua,

nayo mataifa yale yasiyokujua yataharakisha kukujia,

kwa sababu yaBwanaMungu wako,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,

kwa maana amekutukuza.”

6 MtafuteniBwanamaadamu anapatikana;

mwiteni maadamu yu karibu.

7 Mtu mwovu na aiache njia yake

na mtu mbaya na ayaache mawazo yake.

Yeye na amrudieBwana, naye atamrehemu,

arudi kwa Mungu wetu,

kwa kuwa atamsamehe bure kabisa.

8 “Kwa kuwa mawazo yangu si mawazo yenu,

wala njia zenu si njia zangu,”

asemaBwana.

9 “Kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia,

ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu

na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.

10 Kama vile mvua na theluji

ishukavyo kutoka mbinguni,

nayo hairudi tena huko

bila kunywesha dunia

na kuichipusha na kuistawisha,

hivyo hutoa mbegu kwa mpanzi

na mkate kwa mlaji,

11 ndivyo lilivyo neno langu lile litokalo kinywani mwangu:

Halitanirudia tupu,

bali litatimiliza lile nililokusudia

na litafanikiwa katika kusudi

lile nililolituma.

12 Mtatoka nje kwa furaha

na kuongozwa kwa amani;

milima na vilima

vitapaza sauti kwa nyimbo mbele yenu,

nayo miti yote ya shambani

itapiga makofi.

13 Badala ya kichaka cha miiba

itaota miti ya misunobari,

na badala ya michongoma

# utaota mhadasi.

Hili litakuwa jambo la kumpatiaBwanajina,

kwa ajili ya ishara ya milele,

ambayo haitaharibiwa.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/55-979465adb21391b486fb7a9609b44d28.mp3?version_id=1627—

Isaya 56

Wokovu Kwa Ajili Ya Wengine

1 Hili ndilo asemaloBwana:

“Dumisheni haki

na mkatende lile lililo sawa,

kwa maana wokovu wangu u karibu

na haki yangu itafunuliwa upesi.

2 Amebarikiwa mtu yule atendaye hili,

mtu yule alishikaye kwa uthabiti,

yeye ashikaye Sabato bila kuinajisi,

auzuiaye mkono wake

usifanye uovu wo wote.”

3 Usimwache mgeni aambatanaye naBwanaaseme,

“HakikaBwanaatanitenga na watu wake.”

Usimwache towashi ye yote alalamike akisema,

“Mimi ni mti mkavu tu.”

4 Kwa kuwa hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa matowashi washikao Sabato zangu,

ambao huchagua kile kinachonipendeza

na kulishika sana Agano langu,

5 hao nitawapa ndani ya Hekalu langu na kuta zake

kumbukumbu na jina bora kuliko kuwa

na watoto wa kiume na wa kike:

Nitawapa jina lidumulo milele

ambalo halitakatiliwa mbali.

6 Wageni wanaoambatana naBwana

kumtumikia,

kulipenda jina laBwana,

na kumwabudu yeye,

wote washikao Sabato bila kuinajisi

na ambao hushika sana Agano langu

7 hawa nitawaleta kwenye mlima wangu mtakatifu

na kuwapa furaha

ndani ya nyumba yangu ya sala.

Sadaka zao za kuteketeza na dhabihu zao

zitakubalika juu ya madhabahu yangu,

kwa maana nyumba yangu itaitwa

nyumba ya sala kwa mataifa yote.”

8 BwanaMwenyezi asema, yeye awakusanyaye

Waisraeli waliohamishwa:

“Bado nitawakusanya na wengine kwao zaidi ya hao

ambao wameshakusanywa tayari.”

Mashtaka Ya Mungu Dhidi Ya Waovu

9 Njoni, enyi wanyama wote wa kondeni,

njoni mle, ninyi wanyama wote wa mwituni!

10 Walinzi wa Israeli ni vipofu,

wote wamepungukiwa na maarifa;

wote ni mbwa walio bubu

hawawezi kubweka;

hulala na kuota ndoto,

hupenda kulala.

11 Ni mbwa wenye tamaa kubwa,

kamwe hawatosheki.

Wao ni wachungaji waliopungukiwa na ufahamu;

wote wamegeukia njia yao wenyewe,

kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.

12 Kila mmoja hulia, “Njoni, tupate mvinyo!

Tunywe kileo sana!

Kesho itakuwa kama leo,

au hata bora zaidi.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/56-27fcdddbb4db5bf23fb1c37da12ab46c.mp3?version_id=1627—