Isaya 57

Ibada Ya Sanamu Ya Israeli Iliyo Batili

1 Mwenye haki hupotea,

wala hakuna hata mmoja

awazaye hilo moyoni mwake;

watu wanaomcha Mungu huondolewa,

wala hakuna hata mmoja anayeelewa

kuwa wenye haki wameondolewa

wasipatikane na maovu.

2 Wale waendao kwa unyofu

huwa na amani;

hupata pumziko walalapo mautini.

3 “Lakini ninyi, njoni hapa, ninyi wana wa wachawi,

ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!

4 Mnamdhihaki nani?

Ni nani mnayemcheka kwa dharau

na kumtolea ndimi zenu?

Je, ninyi si watoto wa waasi,

Uzao wa waongo?

5 Mnawaka tamaa katikati ya mialoni

na chini ya kila mti uliotanda matawi;

mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde

na chini ya majabali yenye mianya.

6 “Sanamu zilizoko katikati ya mawe laini ya mabondeni

ndiyo fungu lenu;

hizo ndizo sehemu yenu.

Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji,

na kutoa sadaka za nafaka.

Kwa ajili ya haya yote,

niendelee kuona huruma?

7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka,

huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.

8 Nyuma ya milango yako na miimo yako

umeweka alama zako za kipagani.

Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako,

umepanda juu yake

na kukipanua sana;

ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao,

nawe uliangalia uchi wao.

9 Ulikwenda kwa Molekiukiwa na mafuta ya zeituni

na ukaongeza manukato yako.

Ukawatuma wajumbe wako mbali sana,

# ukashuka kwenye kaburilenyewe!

10 Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote,

lakini usingeliweza kusema,

‘Hakuna tumaini.’

Ulipata uhuisho wa nguvu zako,

kwa sababu hiyo hukuzimia.

11 “Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa

hata ukaniambia uongo,

wala hukunikumbuka

au kutafakari hili moyoni mwako?

Si kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu

kwamba huniogopi?

12 Nitaifunua haki yako na matendo yako,

nayo hayatakufaidia.

13 Utakapolia kwa kuhitaji msaada,

sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe!

Upepo utazipeperusha zote,

pumzi peke yake itazipeperusha,

Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake,

atairithi nchi

na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”

Faraja Kwa Wenye Majuto

14 Tena itasemwa:

“Jengeni, jengeni, itengenezeni njia!

Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”

15 Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu,

yeye aliyeinuliwa sana,

yeye aishiye milele,

ambaye jina lake ni Mtakatifu:

“Ninaishi mimi mahali palipoinuka

tena palipo patakatifu,

tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu

na mwenye roho ya unyenyekevu,

ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu

na kuihuisha mioyo yao waliotubu.

16 Sitaendelea kulaumu milele,

wala sitakasirika siku zote,

kwa kuwa roho ya mwanadamu

ingezimia mbele zangu:

yaani pumzi ya mwanadamu niliyemwumba.

17 Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi;

nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira,

yeye bado aliendelea katika njia zake za tamaa.

18 Nimeziona njia zake, lakini nitamponya,

nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,

19 nikiumba sifa katika midomo ya waombolezaji

katika Israeli.

Amani, amani, kwa wale walio mbali

na kwa wale walio karibu,”

asemaBwana. “Nami nitawaponya.”

20 Bali waovu ni kama bahari ichafukayo,

ambayo haiwezi kutulia,

mawimbi yake hutupa takataka na matope.

21 Mungu wangu asema,

“Hakuna amani kwa waovu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/57-5d612401288fe3f4bde3fa1583fde07c.mp3?version_id=1627—

Isaya 58

Mfungo Wa Kweli

1 “Piga kelele, usizuie.

Paza sauti yako kama tarumbeta.

Watangazieni watu wangu uasi wao

na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.

2 Kwa maana kila siku hunitafuta,

wanaonekana kutaka kujua njia zangu,

kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lile lililo sawa

na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake.

Hutaka kwangu maamuzi ya haki,

nao hutamani Mungu awakaribie.

3 Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona?

Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’

“Lakini katika siku ya kufunga kwenu,

mnafanya mnavyotaka

na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.

4 Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano,

na kupigana ninyi kwa ninyi

kwa ngumi za uovu.

Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo

na kutazamia sauti zenu

kusikiwa huko juu.

5 Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua,

siku moja tu kwa ajili ya mtu kujinyenyekeza?

Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama unyasi

Na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu?

Je, huo ndio mnaouita mfungo,

siku iliyokubalika kwaBwana?

6 “Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua:

kufungua minyororo ya udhalimu

na kufungua kamba za nira,

kuwaweka huru walioonewa

na kuvunja kila nira?

7 Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa

na kuwapatia maskini

wasiokuwa na makao hifadhi,

unapomwona aliye uchi, umvike,

wala si kumkimbia mtu

wa nyama na damu yako mwenyewe?

8 Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko

na uponyaji wako utatokea upesi;

ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako,

na utukufu waBwana

utakuwa mlinzi nyuma yako.

9 Ndipo utaita, nayeBwanaatajibu,

utalia kuomba msaada,

naye atasema: Mimi hapa.

“Kama ukiiondoa nira ya udhalimu,

kutokunyosha kidole na kuzungumza maovu,

10 nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu

na kutosheleza mahitaji ya walioonewa,

ndipo nuru yenu itakapong’aa gizani,

nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.

11 Bwanaatakuongoza siku zote,

atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame,

naye ataitia nguvu mifupa yako.

Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri,

kama chemchemi ambayo maji yake

hayakauki kamwe.

12 Watu wako watajenga tena magofu ya zamani

na kuinua misingi ya kale;

utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka,

Mwenye Kufanya upya Barabara zenye Makazi.

13 “Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato

na kutokufanya kama vile upendavyo

katika siku yangu takatifu,

kama ukiita Sabato siku ya furaha

na siku takatifu yaBwanaya kuheshimiwa,

kama utaiheshimu kwa kutoenenda

katika njia zako mwenyewe

na kutokufanya yakupendezayo

au kusema maneno ya upuzi,

14 ndipo utakapojipatia furaha yako katikaBwana,

nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi

na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.”

Kinywa chaBwanakimenena haya.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/58-c7382a8cff973714fa434a93b7cf7d85.mp3?version_id=1627—

Isaya 59

Dhambi, Toba Na Ukombozi

1 Hakika mkono waBwanasi mfupi hata usiweze kuokoa,

wala sikio lake si zito hata lisiweze kusikia.

2 Lakini maovu yenu yamewatenga ninyi

na Mungu wenu,

dhambi zenu zimewaficha ninyi uso wake,

ili asisikie.

3 Kwa maana mikono yenu imetiwa mawaa kwa damu

na vidole vyenu kwa hatia.

Midomo yenu imenena uongo,

nazo ndimi zenu zimenong’ona mambo maovu.

4 Hakuna hata mmoja anayedai kwa haki;

hakuna hata mmoja

anayetetea shauri lake kwa haki.

Wanategemea mabishano matupu na kusema uongo,

huchukua mimba ya magomvi na kuzaa uovu.

5 Huangua mayai ya nyoka wenye sumu kali

na kutanda wavu wa buibui.

Ye yote alaye mayai yao atakufa,

na wakati moja lianguliwapo,

nyoka mwenye sumu kali hutoka humo.

6 Utando wao wa buibui haufai kwa nguo;

hawawezi kujifunika

kwa kile walichokitengeneza.

Matendo yao ni matendo maovu,

vitendo vya jeuri vipo mikononi mwao.

7 Miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,

ni myepesi kumwaga damu isiyo na hatia.

Mawazo yao ni mawazo mabaya;

uharibifu na maangamizi

huweka alama njia zao.

8 Hawajui njia ya amani,

hakuna haki katika mapito yao.

Wamezigeuza kuwa njia za upotovu,

hakuna ye yote apitaye katika njia hizo

atakayeifahamu amani.

9 Hivyo uadilifu uko mbali nasi,

nayo haki haitufikii.

Tunatazamia nuru, kumbe! yote ni giza,

tunatazamia mwanga,

lakini tunatembea katika giza kuu.

10 Tunapapasa ukuta kama kipofu,

tunapapasa katika njia zetu

kama watu wasio na macho.

Adhuhuri tunajikwaa kama wakati wa gizagiza,

katikati ya wenye nguvu, tuko kama wafu.

11 Wote tunanguruma kama dubu;

tunalia kwa uchungu

kwa maombolezo kama hua.

Tunatafuta haki, kumbe hakuna kabisa;

tunatafuta wokovu, lakini uko mbali.

12 Kwa sababu makosa yetu ni mengi machoni pako,

na dhambi zetu zinashuhudia dhidi yetu.

Makosa yetu yako pamoja nasi daima,

nasi tunayatambua maovu yetu:

13 Uasi na udanganyifu dhidi yaBwana,

kumgeuzia Mungu wetu kisogo,

tukichochea udhalimu na maasi,

tukinena uongo ambao mioyo yetu imeuhifadhi.

14 Hivyo uadilifu umerudishwa nyuma,

nayo haki inasimama mbali,

kweli imejikwaa njiani,

uaminifu hauwezi kuingia.

15 Kweli haipatikani po pote,

na ye yote aepukaye uovu huwa mawindo.

Bwanaalitazama naye akachukizwa

kwamba hapakuwepo haki.

16 Aliona kuwa hakuwepo hata mtu mmoja,

akashangaa kwamba hakuwepo

hata mmoja wa kuingilia kati;

hivyo mkono wake mwenyewe

ndio uliomfanyia wokovu,

nayo haki yake mwenyewe

ndiyo iliyomtegemeza.

17 Alivaa haki kama dirii kifuani mwake,

na chapeo ya wokovu kichwani mwake,

alivaa mavazi ya kisasi

naye akajifunga wivu kama joho.

18 Kulingana na kile walichokuwa wametenda,

ndivyo atakavyolipa

ghadhabu kwa watesi wake

na kisasi kwa adui zake,

atavilipa tena visiwa sawa na wanavyostahili.

19 Kuanzia magharibi, watu wataliogopa jina laBwana

na kuanzia maawio ya jua,

watauheshimu utukufu wake.

Wakati adui atakapokuja kama mafuriko,

Roho waBwanaatainua kiwango dhidi yake

na kumshinda kumfukuza.

20 “Mkombozi atakuja Sayuni,

kwa wale wa uzao wa Yakobo

wanaozitubia dhambi zao,”

asemaBwana.

21 “Kwa habari yangu mimi, hili ni Agano langu nao,” asemaBwana. “Roho wangu, aliyeko juu yenu na maneno yangu ambayo nimeyaweka katika vinywa vyenu hayataondoka vinywani mwenu, wala kutoka vinywani mwa watoto wenu, wala kutoka vinywani mwa wazao wao kuanzia sasa na hata milele,” asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/59-ecfce4b395d865a4f791bddcefdd149a.mp3?version_id=1627—

Isaya 60

Utukufu Wa Sayuni

1 “Ondoka, angaza, kwa kuwa nuru yako imekuja

na utukufu waBwanaumezuka juu yako.

2 Tazama, giza litaifunika dunia

na giza kuu litayafunika mataifa,

lakiniBwanaatazuka juu yako

na utukufu wake utaonekana juu yako.

3 Mataifa wataijia nuru yako

na wafalme kuujia mwanga

wa mapambazuko yako.

4 “Inua macho yako na utazame pande zote:

Wote wanakusanyika na kukujia,

wana wako wanakuja toka mbali,

nao binti zako wanabebwa mikononi.

5 Ndipo utatazama na kutiwa nuru,

moyo wako utasisimka na kujaa furaha,

mali zilizo baharini zitaletwa kwako,

utajiri wa mataifa utakujilia.

6 Makundi ya ngamia yatajaa katika nchi yako,

ngamia vijana wa Midiani na Efa.

Nao wote watokao Sheba watakuja,

wakichukua dhahabu na uvumba

na kutangaza sifa zaBwana.

7 Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako,

kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia,

watakubalika kama sadaka juu ya madhabahu yangu,

nami nitalipamba Hekalu langu tukufu.

8 “Ni nani hawa warukao kama mawingu

kama hua kuelekea kwenye viota vyao?

9 Hakika visiwa vinanitazama,

# merikebu za Tarshishindizo zinazotangulia,

zikiwaleta wana wenu kutoka mbali,

wakiwa na fedha na dhahabu zao,

kwa heshima yaBwana, Mungu wenu,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,

kwa maana amekujalia utukufu.

10 “Wageni watazijenga upya kuta zako,

na wafalme wao watakutumikia.

Ingawa katika hasira nilikupiga,

lakini katika upendeleo wangu

nitakuonyesha huruma.

11 Malango yako yatakuwa wazi siku zote,

kamwe hayatafungwa, mchana wala usiku,

ili kwamba watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa:

wafalme wao wakiongoza

maandamano ya ushindi.

12 Kwa maana taifa au ufalme ule ambao hautakutumikia utaangamia;

utaharibiwa kabisa.

13 “Utukufu wa Lebanoni utakujilia,

msunobari, mvinje pamoja na mteashuri,

ili kupapamba mahali pangu patakatifu,

nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.

14 Wana wa wale waliokuonea

watakuja wakisujudu mbele yako,

wote wanaokudharau

watasujudu kwenye miguu yako

nao watakuita Mji waBwana,

Sayuni wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

15 “Ingawa umeachwa na kuchukiwa,

bila kuwapo na ye yote anayesafiri ndani yako,

nitakufanya kuwa fahari ya milele

na furaha ya vizazi vyote.

16 Utanyonya maziwa ya mataifa

na kunyonyeshwa matiti ya wafalme.

Ndipo utakapojua kwamba Mimi,Bwana, ni Mwokozi wako,

Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.

17 Badala ya shaba nitakuletea dhahabu

na fedha badala ya chuma.

Badala ya mti nitakuletea shaba,

na chuma badala ya mawe.

Nitafanya amani kuwa mtawala wako

na haki kuwa mfalme wako.

18 Jeuri hazitasikika tena katika nchi yako,

wala maangamizi

au uharibifu ndani ya mipaka yako,

lakini utaita kuta zako Wokovu

na malango yako Sifa.

19 Jua halitakuwa tena nuru yako mchana,

wala mwangaza wa mwezi hautakuangazia,

kwa maanaBwanaatakuwa nuru yako ya milele,

naye Mungu wako atakuwa utukufu wako.

20 Jua lako halitazama tena,

nao mwezi wako hautafifia tena;

Bwanaatakuwa nuru yako milele,

nazo siku zako za huzuni zitakoma.

21 Ndipo watu wako wote watakuwa waadilifu

nao wataimiliki nchi milele.

Wao ni chipukizi nililolipanda,

kazi ya mikono yangu,

kwa ajili ya kuonyesha utukufu wangu.

22 Aliye mdogo kwenu atakuwa elfu,

mdogo kuliko wote

atakuwa taifa lenye nguvu.

Mimi ndimiBwana;

katika wakati wake

nitayatimiza haya upesi.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/60-adb772b686a020b5ab89ef6afd31c9f6.mp3?version_id=1627—

Isaya 61

Mwaka Wa Upendeleo Wa Bwana

1 Roho waBwanaMwenyezi yu juu yangu,

kwa sababuBwanaamenitia mafuta

kuwahubiri maskini habari njema.

Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo,

kuwatangazia mateka uhuru wao

na hao waliofungwa

habari za kufunguliwa kwao,

2 kutangaza mwaka waBwanauliokubaliwa

na siku ya kisasi ya Mungu wetu,

kuwafariji wote waombolezao,

3 na kuwapa mahitaji

wale wanaohuzunika katika Sayuni,

ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu,

mafuta ya furaha badala ya maombolezo,

vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa.

Nao wataitwa mialoni ya haki,

pando laBwana

kwa ajili ya kuonyesha utukufu wake.

4 Watajenga upya magofu ya zamani na

kupatengeneza mahali

palipoachwa ukiwa zamani;

watafanya upya miji iliyoharibiwa

iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.

5 Wageni watayachunga makundi yenu,

wageni watafanya kazi katika mashamba yenu

na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.

6 Nanyi mtaitwa makuhani waBwana,

mtaitwa watumishi wa Mungu wetu.

Mtakula utajiri wa mataifa,

nanyi katika utajiri wao mtajisifu.

7 Badala ya aibu yao

watu wangu watapokea sehemu maradufu,

na badala ya fedheha

watafurahia katika urithi wao;

hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao,

nayo furaha ya milele itakuwa yao.

8 “Kwa maana Mimi,Bwana, napenda haki,

ninachukia unyang’anyi na uovu.

Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao

ya haki na kufanya Agano la milele nao.

9 Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa

na uzao wao miongoni mwa kabila za watu.

Wale wote watakaowaona watatambua

kuwa ni taifa ambaloBwanaamelibariki.”

10 Ninafurahia sana katikaBwana,

nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu.

Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu

na kunipamba kwa joho la haki,

kama vile bwana arusi apambavyo

kichwa chake kama kuhani,

na kama bibi arusi ajipambavyo

kwa vito vyake vya thamani.

11 Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota

na bustani isababishavyo mbegu kuota,

hivyo hivyoBwanaMwenyezi atafanya haki na sifa

zichipuke mbele ya mataifa yote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/61-97beb3b5258f8abd70a3e59639a345a3.mp3?version_id=1627—

Isaya 62

Jina Jipya La Sayuni

1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza kimya,

kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,

mpaka haki yake itakapoangaza kama mapambazuko,

wokovu wake kama mwanga wa moto.

2 Mataifa wataona haki yako,

nao wafalme wote wataona utukufu wako;

wewe utaitwa kwa jina jipya

lile ambalo kinywa chaBwanakitatamka.

3 Utakuwa taji ya fahari mkononi mwaBwana,

taji ya kifalme mkononi mwa Mungu wako.

4 Hawatakuita tena Aliyeachwa,

wala nchi yako kuiita Ukiwa.

# Bali utaitwa Hefsiba,

# nayo nchi yako itaitwa Beula,

kwa maanaBwanaatakufurahia,

nayo nchi yako itaolewa.

5 Kama vile mwanaume kijana aoavyo mwanamwali,

# ndivyo wanaowatakavyokuoa wewe;

kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake,

ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu,

hawatanyamaza mchana wala usiku.

Ninyi wenye kumwitaBwana,

msitulie,

7 msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu

na kuufanya uwe sifa ya dunia.

8 Bwanaameapa kwa mkono wake wa kuume

na kwa mkono wake wenye nguvu:

“Kamwe sitawapa tena adui zenu

nafaka zenu kama chakula chao;

kamwe wageni hawatakunywa tena

divai mpya ambayo hiyo mmeitaabikia,

9 lakini wale waivunao nafaka wataila

na kumsifuBwana,

nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake

katika nyua za patakatifu pangu.”

10 Piteni, piteni katika malango!

Tengenezeni njia kwa ajili ya watu.

Jengeni, jengeni njia kuu!

Ondoeni mawe.

Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.

11 Bwanaametoa tangazo

mpaka miisho ya dunia:

“Mwambie Binti Sayuni,

‘Tazama, mwokozi wako anakuja!

Tazama ujira wake ukiwa pamoja naye,

na malipo yake yanafuatana naye!’ ”

12 Wataitwa Watu Watakatifu,

Waliokombolewa naBwana;

nawe utaitwa Aliyetafutwa,

Mji Usioachwa Tena.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/62-7cb6a6fcfd003392984c732ae7925927.mp3?version_id=1627—

Isaya 63

Siku Ya Mungu Ya Kisasi Na Ukombozi

1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu,

kutoka Bosra, mwenye mavazi

yaliyotiwa madoa mekundu?

Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari,

anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake?

“Mimi ndimi, nisemaye katika haki,

mwenye nguvu wa kuokoa.”

2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu,

kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?

3 “Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu;

kutoka katika mataifa

hakuna mtu awaye yote

aliyekuwa pamoja nami.

Nimewaponda mataifa kwa miguu katika hasira yangu

na kuwakanyaga chini

katika ghadhabu yangu;

damu yao ilitia matone matone kwenye mavazi yangu

na kutia madoa nguo zangu zote.

4 Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu,

mwaka wa ukombozi wangu umefika.

5 Nilitazama, lakini hakuwepo ye yote wa kunisaidia,

nilishangaa kwa kuwa hakuwepo

ye yote aliyetoa msaada;

hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu,

na ghadhabu yangu mwenyewe

ndiyo iliyonitegemeza.

6 Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu,

katika ghadhabu yangu niliwalewesha

na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”

Kusifu Na Kuomba

7 Nitasimulia juu ya wema waBwana,

kwa ajili ya matendo ambayo

kwayo apaswa kusifiwa,

sawasawa na yote ambayoBwana

ametenda kwa ajili yetu:

naam, mambo mengi mema aliyoyatenda

kwa ajili ya nyumba ya Israeli,

sawasawa na huruma zake

na wema wake mwingi.

8 Alisema, “Hakika wao ni watu wangu,

wana ambao hawatanidanganya”;

kisha akawa Mwokozi wao.

9 Katika taabu zao zote naye alitaabika

na malaika wa uso wake akawaokoa.

Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa,

akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.

10 Lakini waliasi

na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake.

Hivyo aligeuka na kuwa adui yao

na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.

11 Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita,

siku za Mose na watu wake:

yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari,

pamoja na wachungaji wa kundi lake?

Yuko wapi yule aliyeweka

Roho wake Mtakatifu katikati yao,

12 aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu

kuwa katika mkono wa kuume wa Mose,

aliyegawa maji ya bahari mbele yao,

ili kujipatia jina milele,

13 aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi?

Kama farasi katika nchi iliyo wazi,

wao hawakujikwaa,

14 kama ng’ombe washukao bondeni kwenye malisho,

walipewa pumziko na Roho waBwana.

Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako

ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.

15 Tazama chini kutoka mbinguni ukaone

kutoka katika kiti chako cha enzi

kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu.

Uko wapi wivu wako na uweza wako?

Umetuzuilia wema wako na huruma zako.

16 Lakini wewe ni Baba yetu,

ingawa Abrahamu hatufahamu sisi

wala Israeli hatutambui;

wewe, EeBwana, ni Baba yetu,

Mkombozi wetu tangu zamani za kale

ndilo jina lako.

17 EeBwana, kwa nini unatuacha tuende mbali na njia zako

na kuifanya mioyo yetu migumu

hata hatukukuheshimu?

Rudi kwa ajili ya watumishi wako,

yale makabila ambayo ni urithi wako.

18 Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki

mahali pako patakatifu,

lakini sasa adui zetu wamepakanyaga

mahali patakatifu pako.

19 Sisi ni watu wako tangu zamani;

lakini tumekuwa kama wale ambao

hujawatawala kamwe,

kama wale ambao

hawajaitwa kwa jina lako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/63-f03a29f94e7239bcc6f2674f5b9a1265.mp3?version_id=1627—

Isaya 64

1 Laiti ungelipasua mbingu na kushuka chini,

kwamba milima ingelitetemeka mbele zako!

2 Kama vile moto uteketezavyo vijiti

na kusababisha maji kuchemka,

shuka ukafanye jina lako lijulikane kwa adui zako

na kusababisha mataifa yatetemeke mbele zako!

3 Kwa maana ulipofanya mambo ya kutisha

ambayo hatukuyatazamia,

ulishuka nayo milima ikatetemeka mbele zako.

4 Tangu nyakati za zamani hakuna ye yote aliyesikia,

hakuna sikio lililotambua,

hakuna jicho lililomwona Mungu mwingine ila wewe,

anayetenda mambo kwa ajili ya wale wamngojeao.

5 Uliwasaidia watu wale watendao yaliyo haki kwa furaha,

wale wazikumbukao njia zako.

Lakini wakati tulipoendelea kutenda dhambi kinyume na njia zako,

ulikasirika.

Tutawezaje basi kuokolewa?

6 Sisi sote tumekuwa kama mtu aliye najisi,

nayo matendo yetu yote ya uadilifu

ni kama matambaa machafu;

sisi sote tunasinyaa kama jani

na kama upepo maovu yetu hutupeperusha.

7 Hakuna ye yote anayeliitia jina lako

wala anayejitahidi kukushika,

kwa kuwa umetuficha uso wako

na kutuacha tudhoofike

kwa sababu ya dhambi zetu.

8 Lakini, EeBwana, wewe ndiwe Baba yetu.

Sisi ni udongo wa mfinyanzi

wewe ndiye mfinyanzi;

sisi sote tu kazi ya mkono wako.

9 EeBwana, usikasirike kupita kiasi,

usizikumbuke dhambi zetu milele.

Ee Bwana, utuangalie, twakuomba,

kwa kuwa sisi sote tu watu wako.

10 Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa;

hata Sayuni ni jangwa,

Yerusalemu imekuwa ukiwa.

11 Hekalu letu takatifu na tukufu, mahali ambapo baba zetu walikusifu wewe,

limechomwa kwa moto,

navyo vitu vyote tulivyovithamini vimeharibika.

12 EeBwana, baada ya haya yote, utajizuia?

Je, utanyamaza kimya na kutuadhibu kupita kiasi?

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/64-c505bafdc93ede5028d0667993427f8b.mp3?version_id=1627—

Isaya 65

Hukumu Na Wokovu

1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia,

nimeonekana kwa watu wale

ambao hawakunitafuta.

Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu,

nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’

2 Mchana kutwa nimeinyosha mikono yangu

kwa watu wakaidi,

wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri,

wafuatao mawazo yao wenyewe,

3 taifa ambalo daima hunikasirisha

machoni pangu,

wakitoa dhabihu katika bustani

na kufukiza uvumba juu

ya madhabahu za matofali;

4 watu waketio katikati ya makaburi

na kukesha mahali pa siri,

ili kuabudu mizimu,

walao nyama za nguruwe,

nazo sufuria zao zina mchuzi

wa nyama na mboga zilizonajisi,

5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie,

kwa maana mimi

ni mtakatifu mno kwako!’

Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu,

ni moto uwakao mchana kutwa.

6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu:

sitanyamaza kimya

bali nitalipiza kwa ukamilifu;

nitalipiza mapajani mwao:

7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,”

asemaBwana.

“Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima

na kunichokoza mimi juu ya vilima,

nitawapimia mapajani mwao

malipo makamilifu

kwa ajili ya matendo yao ya zamani.”

8 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana

katika kishada cha zabibu,

nao watu husema, ‘Usikiharibu,

kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’

hivyo ndivyo nitakavyofanya

kwa ajili ya watumishi wangu;

sitawaangamiza wote.

9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo,

na kutoka kwa Yuda wale

watakaomiliki milima yangu,

watu wangu wateule watairithi,

nako huko wataishi watumishi wangu.

10 Sharoni itakuwa malisho

kwa ajili ya makundi ya kondoo na mbuzi,

na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia

kwa makundi ya ng’ombe,

kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.

11 “Bali kwenu ninyi mnaomwachaBwana

na kuusahau mlima wangu mtakatifu,

# ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati

na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa

# kwa ajili ya Ajali,

12 nitawaagiza mfe kwa upanga,

nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa;

kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika,

nilisema lakini hamkusikiliza.

Mlitenda maovu machoni pangu,

nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”

13 Kwa hiyo hili ndilo asemaloBwanaMwenyezi:

“Watumishi wangu watakula,

lakini ninyi mtaona njaa;

watumishi wangu watakunywa

lakini ninyi mtaona kiu;

watumishi wangu watafurahi,

lakini ninyi mtaona haya.

14 Watumishi wangu wataimba

kwa furaha ya mioyo yao,

lakini ninyi mtalia

kutokana na uchungu wa moyoni

na kupiga yowe kwa sababu

ya uchungu wa roho zenu.

15 Mtaliacha jina lenu

kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa;

BwanaMwenyezi atawaua ninyi,

lakini watumishi wake atawapa jina jingine.

16 Yeye aombaye baraka katika nchi

atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli;

yeye aapaye katika nchi

ataapa kwa Mungu wa kweli.

Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika

na kufichwa kutoka machoni pangu.

Mbingu Mpya Na Dunia Mpya

17 “Tazama, nitaumba

mbingu mpya na dunia mpya.

Mambo ya zamani hayatakumbukwa,

wala hayatakuja akilini.

18 Lakini furahini na kushangilia daima

katika hivi nitakavyoumba,

kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza,

nao watu wake wawe furaha.

19 Nami nitaifurahia Yerusalemu

na kuwafurahia watu wangu;

sauti ya maombolezo na ya kilio

haitasikika humo tena.

20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake

mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu,

au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake.

Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja

atahesabiwa kwamba ni kijana tu,

yeye ambaye hatafika miaka mia moja,

atahesabiwa kuwa amelaaniwa.

21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake;

watapanda mashamba ya mizabibu

na kula matunda yake.

22 Hawatajenga nyumba

na watu wengine waishi ndani yake,

au kupanda mazao na wengine wale.

Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti,

ndivyo zitakavyokuwa

siku za watu wangu,

wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi

kazi za mikono yao.

23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure

wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga,

kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa naBwana,

wao na wazao wao pamoja nao.

24 Kabla hawajaita nitajibu,

nao wakiwa katika kunena nitasikia.

25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja,

naye simba atakula nyasi kama maksai,

lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka.

Hawatadhuru wala kuharibu

katika mlima wangu mtakatifu wote,”

asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/65-b96d6a2c779da3ede40e458f972ec0be.mp3?version_id=1627—

Isaya 66

Hukumu Na Matumaini

1 Hili ndilo asemaloBwana,

“Mbingu ni kiti changu cha enzi,

nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu.

Iko wapi nyumba mtakayojenga kwa ajili yangu?

Mahali pangu pa kupumzika patakuwa wapi?

2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote,

hivyo vikapata kuwepo?”

asemaBwana.

“Mtu huyu ndiye ninayemthamini:

yeye ambaye ni mnyenyekevu

na mwenye roho yenye toba,

atetemekaye asikiapo neno langu.

3 Lakini ye yote atoaye dhabihu ya fahali

ni kama yeye auaye mtu,

na ye yote atoaye sadaka ya mwana-kondoo,

ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa;

ye yote atoaye sadaka ya nafaka,

ni kama yule aletaye damu ya nguruwe,

na ye yote afukizaye uvumba wa kumbukumbu,

ni kama yule aabuduye sanamu.

Wamejichagulia njia zao wenyewe,

nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao,

4 hivyo, mimi pia nitachagua mapigo makali kwa ajili yao,

nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa.

Kwa maana nilipoita, hakuna ye yote aliyejibu,

niliposema, hakuna ye yote aliyesikiliza.

Walifanya maovu machoni pangu

na kuchagua lile linalonichukiza.”

5 Sikieni neno laBwana,

ninyi mtetemekao kwa neno lake,

“Ndugu zenu wanaowachukia ninyi

na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema,

‘Bwanana atukuzwe,

ili tupate kuona furaha yenu!’

Hata sasa wataaibika.

6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini,

sikieni hizo kelele kutoka hekaluni!

Ni sauti yaBwanaikiwalipa adui zake

yote wanayostahili.

7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa;

kabla hajapata maumivu,

alizaa mtoto mwanaume.

8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili?

Ni nani amepata kuona mambo kama haya?

Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja

au taifa laweza kutokea mara?

Mara Sayuni alipoona utungu,

alizaa watoto wake.

9 Je, nilete hadi wakati wa kuzaliwa

na nisizalishe?” asemaBwana.

“Je, nifunge tumbo la uzazi

wakati mimi ndiye nizalishaye?”

asema Mungu wako.

10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu

na mfurahi kwa ajili yake,

ninyi nyote mnaompenda,

shangilieni kwa nguvu pamoja naye,

ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.

11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka

katika faraja ya matiti yake;

mtakunywa sana,

na kuufurahia wingi wa mafuriko

ya ustawi wake.”

12 Kwa kuwa hili ndilo asemaloBwana:

“Nitamwongezea amani kama mto,

nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho,

utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake

na kubembelezwa magotini pake.

13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake,

ndivyo nitakavyokufariji wewe,

nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”

14 Wakati mtakapoona jambo hili,

mioyo yenu itashangilia,

nanyi mtastawi kama majani;

mkono waBwanautajulikana kwa watumishi wake,

bali ghadhabu yake kali

itaonyeshwa kwa adui zake.

15 Tazama,Bwanaanakuja na moto,

magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli,

atatelemsha hasira yake kwa ghadhabu kali

na karipio lake pamoja na miali ya moto.

16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake

Bwanaatatekeleza hukumu juu ya watu wote,

nao wengi watakuwa ni wale

waliouawa naBwana.

17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asemaBwana.

18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.

19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Putuna Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.

20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka katika mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwaBwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asemaBwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu laBwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.

21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asemaBwana.

22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asemaBwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.

23 Kutoka Mwezi Mpya hata Mwezi Mpya mwingine na kutoka Sabato hadi Sabato nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asemaBwana.

24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi, funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/66-d36be496ce49a45a4cc727d8e05ba436.mp3?version_id=1627—