Mithali 31

Mithali Za Mfalme Lemueli

1 Mithali za Mfalme Lamueli, mausia ya mama yake aliyomfundisha:

2 “Ee mwanangu, Ee mwana wa tumbo langu,

# Ee mwana wa nadhiri zangu,

3 Usitumie nguvu zako kwa wanawake,

uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.

4 “Ee Lemueli, haifai wafalme,

haifai wafalme kunywa mvinyo,

haifai watawala kutamani sana kileo,

5 wasije wakanywa na kusahau ile sheria inayoamuru

na kuwanyima haki zao wote walioonewa.

6 Wape kileo wale wanaoangamia,

mvinyo wale walio na uchungu,

7 Wanywe na kusahau umaskini wao

na wasikumbuke taabu yao tena.

8 “Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea,

kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.

9 Sema na uamue kwa haki,

tetea haki za maskini na wahitaji.”

Maneno Ya Mwisho: Mke Mwenye Sifa Nzuri #

10 Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata?

Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.

11 Mume wake anamwamini kikamilifu

wala hakosi kitu cho chote cha thamani.

12 Humtendea mumewe mema, wala si mabaya,

siku zote za maisha yake.

13 Huchagua sufu na kitani

naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.

14 Yeye ni kama meli za biashara

akileta chakula chake kutoka mbali.

15 Yeye huamka kungali bado giza

huwapa jamaa yake chakula

na mafungu kwa watumishi wake wa kike.

16 Huangalia shamba na kulinunua,

kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.

17 Hufanya kazi zake kwa nguvu,

mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.

18 Huona kwamba biashara yake ina faida,

wala taa yake haizimiki usiku.

19 Huweka mikono yake kwenye pia,

navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.

20 Huwanyoshea maskini mikono yake

na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.

21 Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake,

kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.

22 Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake,

yeye huvaa kitani safi na urujuani.

23 Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji,

aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.

24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza,

naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.

25 Amevikwa nguvu na heshima,

anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.

26 Huzungumza kwa hekima

na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.

27 Huangalia mambo ya nyumbani mwake

wala hali chakula cha uvivu.

28 Watoto wake huamka na kumwita mbarikiwa

na mumewe pia, naye humsifu:

29 “Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri,

lakini wewe umewapita wote.”

30 Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu, uzuri unapita upesi,

bali mwanamke anayemchaBwanaatasifiwa.

31 Mpe thawabu anayostahili,

nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PRO/31-ecf3346235bffee3325871f0fdf858ff.mp3?version_id=1627—

Zaburi 1

Furaha Ya Kweli

1 Heri mtu yule ambaye

haendi katika shauri la watu waovu,

wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi

au kuketi katika baraza la wenye mizaha.

2 Bali huifurahia sheria yaBwana,

naye huitafakari hiyo sheria mchana na usiku.

3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa

kando ya vijito vya maji,

ambao huzaa matunda kwa majira yake

na majani yake hayanyauki.

Lo lote afanyalo hufanikiwa.

Huzuni Ya Waovu

4 Sivyo walivyo waovu!

Wao ni kama makapi

yapeperushwayo na upepo.

5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,

wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.

6 Kwa maanaBwanahuziangalia njia za mwenye haki,

bali njia ya waovu itaangamia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/1-461588185b7df957126ca69dd341074d.mp3?version_id=1627—

Zaburi 2

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,

na mataifa kula njama bure?

2 Wafalme wa dunia wanajipanga

na watawala wanajikusanya pamoja

dhidi yaBwana

na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao

na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka,

Bwana huwadharau.

5 Kisha huwakemea katika hasira yake

na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

6 “Nimemtawaza mfalme wangu

juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

Ushindi Wa Mfalme

7 Nitatangaza amri yaBwana:

Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu,

leo mimi nimekuzaa.

8 Niombe, nami nitayafanya mataifa

kuwa urithi wako,

miisho ya dunia kuwa milki yako.

9 Utawatawala kwa fimbo ya kifalme ya chuma

na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, iweni na hekima;

mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

11 MtumikieniBwanakwa hofu

na mshangilieni kwa kutetemeka.

12 Mbusu Mwana, asije akakasirika

nawe ukaangamizwa katika njia yako,

kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula.

Heri wote wanaomkimbilia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/2-a11c6bc14963afae6c73d8884c7251e0.mp3?version_id=1627—

Zaburi 3

Sala Ya Asubuhi Ya Kuomba Msaada

(Zaburi Ya Daudi Alipomkimbia Absalomu)

1 EeBwana, tazama adui zangu walivyo wengi!

Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

2 Wengi wanasema juu yangu,

“Mungu hatamwokoa.”

3 Lakini wewe, EeBwana, ni ngao pande zote;

umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

4 NinamliliaBwanakwa sauti kuu,

naye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.

5 Ninajilaza na kupata usingizi;

naamka tena, kwa maanaBwanahunitegemeza.

6 Sitaogopa makumi elfu ya adui,

wanaojipanga dhidi yangu kila upande.

7 EeBwana, amka!

Uniokoe, Ee Mungu wangu!

Wapige adui zangu wote kwenye taya,

vunja meno ya waovu.

8 Kwa maana wokovu watoka kwaBwana.

Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/3-02ebf1108eb4cf43d48b6134dc9a3fcb.mp3?version_id=1627—

Zaburi 4

Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Zaburi Ya Daudi)

1 Unijibu nikuitapo,

Ee Mungu wangu mwenye haki!

Unipumzishe katika shida zangu,

nirehemu, usikie ombi langu.

2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu

kuwa aibu mpaka lini?

Mtapenda udanganyifu

na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?

3 Fahamuni hakika kwambaBwanaamewatenga

wale wamchao kwa ajili yake;

Bwanaatanisikia nimwitapo.

4 Katika hasira yako usitende dhambi,

mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya

mkiichunguza mioyo yenu.

5 Toeni dhabihu iliyo sahihi

na mumtegemeeBwana.

6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye

kutuonyesha jema lo lote?”

EeBwana, utuangazie nuru ya uso wako.

7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata ngano na divai kwa wingi.

8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,

kwa kuwa wewe peke yako, EeBwana,

waniwezesha kukaa kwa salama.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/4-d29771b2637e4953932c84584e8c7c0e.mp3?version_id=1627—

Zaburi 5

Sala Kwa Ajili Ya Ulinzi Wakati Wa Hatari

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Filimbi. Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, tegea sikio maneno yangu,

uangalie kupiga kite kwangu.

2 Sikiliza kilio changu ili unisaidie,

Mfalme wangu na Mungu wangu,

kwa maana kwako ninaomba.

3 Asubuhi, unasikia sauti yangu, EeBwana;

asubuhi naleta haja zangu mbele zako,

na kusubiri kwa matumaini.

4 Wewe si Mungu unayefurahia uovu,

kwako mtu mwovu hataishi.

5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako,

unawachukia wote watendao mabaya.

6 Unawaangamiza wasemao uongo,

wamwagao damu

na wadanganyifuBwanahuwachukia.

7 Lakini mimi, kwa rehema zako kuu,

nitakuja katika nyumba yako,

kwa unyenyekevu, nitasujudu

kuelekea Hekalu lako takatifu.

8 Niongoze katika haki yako, EeBwana,

kwa sababu ya adui zangu,

nyosha njia yako mbele yangu.

9 Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika,

mioyo yao imejaa maangamizi.

Koo zao ni kaburi lililo wazi,

kwa ndimi zao hunena udanganyifu.

10 Uwatangaze kwamba wana hatia, Ee Mungu!

Hila zao ziwe anguko lao wenyewe.

Wafukuzie mbali kwa sababu ya dhambi zao nyingi,

kwa kuwa wamekuasi wewe.

11 Lakini wote wakimbiliao kwako na wafurahi,

waimbe kwa shangwe daima.

Ueneze ulinzi wako juu yao,

ili wale wapendao jina lako

wapate kukushangilia.

12 Kwa hakika, EeBwana, unawabariki wenye haki,

unawazunguka kwa wema wako kama ngao.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/5-2a517cdb34986fc621a99e3f7cba50d4.mp3?version_id=1627—

Zaburi 6

Sala Kwa Ajili Ya Msaada Wakati Wa Taabu

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Mtindo Wa Sheminithi

#

. Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, usinikemee katika hasira yako,

wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.

2 UnirehemuBwana,

kwa maana nimedhoofika;

EeBwana, uniponye,

kwa maana mifupa yangu

ina maumivu makali.

3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi.

Mpaka lini, EeBwana, mpaka lini?

4 Geuka EeBwana, unikomboe,

uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.

5 Hakuna mtu anayekukumbuka

akiwa amekufa.

Ni nani awezaye kukusifu

akiwa kuzimu?

6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;

usiku kucha nafurikisha

kitanda changu kwa machozi;

nimelowesha viti vyangu vya fahari

kwa machozi.

7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,

yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.

8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,

kwa maanaBwanaamesikia kulia kwangu.

9 Bwanaamesikia kilio changu kwa huruma,

Bwanaamekubali sala yangu.

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,

watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/6-a9a79421fa300ef0aa37e5024d36f37d.mp3?version_id=1627—

Zaburi 7

Sala Ya Mtu Anayedhulumiwa

(Ombolezo La Daudi Kwa Mungu Kwa Sababu Ya Kushi, Mbenyamini)

1 EeBwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe,

uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,

2 la sivyo watanirarua kama simba

na kunichana vipande vipande asiwepo wa kuniokoa.

3 EeBwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya

na kuna hatia mikononi mwangu,

4 au ikiwa nimetenda uovu kwake yeye aliye na amani nami,

au pasipo sababu nimemnyang’anya adui yangu,

5 basi adui anifuatie na kunipata,

auponde uhai wangu ardhini

na kunilaza mavumbini.

6 Amka kwa hasira yako, EeBwana,

inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu.

Uamke, Mungu wangu, uamue haki.

7 Kusanyiko la watu na likuzunguke.

Uwatawale kutoka juu;

8 Bwanana awahukumu kabila za watu.

Unihukumu EeBwana,

kwa kadiri ya haki yangu,

kwa kadiri ya uadilifu wangu,

Ewe Uliye Juu Sana.

9 Ee Mungu mwenye haki,

uchunguzaye mawazo na mioyo,

komesha ghasia za waovu

na ufanye wenye haki waishi kwa amani.

10 Ngao yangu, ni Mungu Aliye Juu Sana,

awaokoaye wanyofu wa moyo.

11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki,

Mungu aghadhibikaye kila siku.

12 Kama hakutuhurumia,

atanoa upanga wake,

atainama na kufyatua upinde wake.

13 Ameandaa silaha kali,

ameweka tayari mishale yake ya moto.

14 Yeye aliye na mimba ya ubaya

na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.

15 Yeye achimbaye shimo na kulifukua

hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.

16 Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe,

ukatili wake humrudia kichwani.

17 NitamshukuruBwanakwa ajili ya haki yake,

na nitaliimbia sifa jina laBwanaAliye Juu Sana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/7-9e53f9c428c3200c087bbe4527cde841.mp3?version_id=1627—

Zaburi 8

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako

juu ya mbingu.

2 Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao

umeweka sifa,

kwa sababu ya watesi wako,

kuwanyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 Nikiziangalia mbingu zako,

kazi ya vidole vyako,

mwezi na nyota,

ulizoziratibisha,

4 mwanadamu ni kitu gani hata umkumbuke,

binadamu hata umwangalie?

5 Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu,

umemvika taji ya utukufu na heshima.

6 Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;

umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.

7 Kondoo, mbuzi na ng’ombe wote pia,

naam, na wanyama wa kondeni,

8 ndege wa angani na samaki wa baharini,

naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

9 EeBwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/8-9b9688e20a06c6dd7f5a4839406532c4.mp3?version_id=1627—

Zaburi 9

Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Haki Yake

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Muth-Labeni

#

. Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,

nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.

2 Nitafurahi na kushangilia katika wewe,

nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.

3 Adui zangu wamerudi nyuma,

wamejikwaa na kuangamia mbele zako.

4 Kwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu;

umeketi kwenye kiti chako cha enzi,

ukihukumu kwa haki.

5 Umekemea mataifa na kuwaangamiza waovu;

umeyafuta majina yao milele na milele.

6 Uharibifu usiokoma umempata adui,

umeing’oa miji yao,

hata kumbukumbu lao limetoweka.

7 Bwanaanatawala milele,

ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.

8 Mungu atahukumu ulimwengu kwa haki,

atatawala mataifa kwa haki.

9 Bwanani kimbilio la watu wanaoonewa,

ni ngome imara wakati wa shida.

10 Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe,

kwa maana weweBwana,

hujawaacha kamwe wakutafutao.

11 MwimbieniBwanasifa, amefanywa mtawala Sayuni,

tangazeni miongoni mwa mataifa, yale aliyoyatenda.

12 Kwa maana yeye alipizaye kisasi cha damu hukumbuka,

hapuuzi kilio cha wanaoonewa.

13 EeBwana, tazama jinsi walivyo wengi adui zangu wanaonitesa!

Unihurumie, uniinue kutoka malango ya mauti,

14 ili niweze kutangaza sifa zako

katika malango ya Binti Sayuni

na huko niushangilie wokovu wako.

15 Mataifa wameanguka kwenye shimo walilolichimba,

miguu yao imenaswa kwenye wavu waliouficha.

16 Bwanaanajulikana kwa haki yake,

waovu wamenaswa katika kazi za mikono yao.

17 Waovu wataishia kuzimu,

naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.

18 Lakini mhitaji hatasahaulika siku zote,

wala matumaini ya walioonewa hayatapotea.

19 EeBwana, inuka, usimwache binadamu ashinde,

mataifa na yahukumiwe mbele zako.

20 EeBwana, wapige kwa hofu,

mataifa na yajue kuwa wao ni watu tu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/9-0f5efef9c3685c2abd60fe6eb0bef333.mp3?version_id=1627—