Zaburi 10

Sala Kwa Ajili Ya Haki

1 Kwa nini, EeBwana, unasimama mbali?

Kwa nini unajificha wakati wa shida?

2 Katika kiburi chake mtu mwovu humtesa mtu aliye maskini,

waovu na wanaswe katika hila wanazozitunga.

3 Hujivunia tamaa za moyo wake;

humbariki mlafi na kumtukanaBwana.

4 Katika kiburi chake mtu mwovu hamtafuti Mungu,

katika mawazo yake yote

hakuna nafasi ya Mungu.

5 Njia zake daima hufanikiwa;

hujivuna na amri zako ziko mbali naye,

huwacheka kwa dharau adui zake wote.

6 Anajisemea mwenyewe, “Hakuna kitakachonitikisa,

daima nitakuwa na furaha,

kamwe sitakuwa na shida.”

7 Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho,

shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.

8 Huvizia karibu na vijiji;

kutoka mafichoni huwanasa wasio na hatia,

akivizia wapitaji.

9 Huvizia kama simba aliye mawindoni;

huvizia kumkamata mnyonge,

huwakamata wanyonge na kuwaburuza

katika wavu wake.

10 Mateka wake hupondwa, huzimia;

wanaanguka katika nguvu zake.

11 Anajisemea mwenyewe, “Mungu amesahau,

huficha uso wake na haoni kabisa.”

12 InukaBwana! Inua mkono wako, Ee Mungu.

Usiwasahau wanyonge.

13 Kwa nini mtu mwovu anamtukana Mungu?

Kwa nini anajiambia mwenyewe,

“Hataniita nitoe hesabu?”

14 Lakini wewe, Ee Mungu, unaona shida na huzuni,

umekubali kuyapokea mkononi mwako.

Mhanga anajisalimisha kwako,

wewe ni msaada wa yatima.

15 Vunja mkono wa mtu mwovu na mbaya,

mwite atoe hesabu ya maovu yake

ambayo yasingejulikana.

16 Bwanani Mfalme milele na milele,

mataifa wataangamia watoke nchini mwake.

17 Unasikia, EeBwana, shauku ya wanaoonewa,

watie moyo nawe usikilize kilio chao,

18 ukiwatetea yatima na walioonewa,

ili kwamba mwanadamu,

ambaye ni udongo,

asiogopeshe tena.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/10-754824ce0d2c446f4f9a8c6e83c222fa.mp3?version_id=1627—

Zaburi 11

Kumtumaini Bwana

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 KwaBwananinakimbilia,

unawezaje basi kuniambia:

“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.

2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,

huweka mishale kwenye uzi wake,

wakiwa gizani ili kuwapiga

wanyofu wa moyo.

3 Wakati misingi imeharibiwa,

mwenye haki anaweza kufanya nini?”

4 Bwanayuko ndani ya Hekalu lake takatifu;

Bwanayuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.

Huwaangalia wana wa watu,

macho yake yanawajaribu.

5 Bwanahuwajaribu wenye haki,

lakini waovu na wale wanaopenda jeuri

nafsi yake huwachukia.

6 Juu ya waovu atawanyeshea makaa ya moto mkali

na kiberiti kinachowaka,

upepo wenye joto kali ndio fungu lao.

7 Kwa kuwaBwanani mwenye haki,

hupenda haki;

watu wanyofu watauona uso wake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/11-5c07d8f7f91202ea2f0e5f2cfada8510.mp3?version_id=1627—

Zaburi 12

Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Sheminithi: Zaburi Ya Daudi)

1 Bwanatusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;

waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.

2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;

midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

3 Bwanana akatilie mbali midomo yote ya hila

na kila ulimi uliojaa majivuno

4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;

midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”

5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge

na kulia kwa uchungu kwa wahitaji,

nitainuka sasa,” asemaBwana.

“Nitawalinda kutokana na wale

wenye nia mbaya juu yao.”

6 Maneno yaBwanani safi,

kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,

iliyosafishwa mara saba.

7 EeBwana, utatuweka salama

na kutulinda na kizazi hiki milele.

8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali

wakati ambapo yule aliye mbaya sana

ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/12-78f49a641ddd6c81699450d676c86446.mp3?version_id=1627—

Zaburi 13

Sala Ya Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Mpaka lini, EeBwana? Je, utanisahau milele?

Utanificha uso wako mpaka lini?

2 Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini

na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?

Adui zangu watanishinda mpaka lini?

3 Nitazame unijibu, EeBwanaMungu wangu.

Uyatie nuru macho yangu,

ama sivyo nitalala usingizi wa mauti;

4 adui yangu atasema, “Nimemshinda,”

nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.

5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;

moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.

6 NitamwimbiaBwana,

kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/13-e4324ab50d31ef0ba6d185a93f9159ae.mp3?version_id=1627—

Zaburi 14

Uovu Wa Wanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Mahalathi. Zaburi Ya Daudi)

1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;

hakuna atendaye mema.

2 Toka mbinguniBwanaanawachungulia

wanadamu chini

aone kama wako wenye akili,

wo wote wanaomtafuta Mungu.

3 Wote wamepotoka,

wameoza wote pamoja;

hakuna atendaye mema,

naam! Hata mmoja.

4 Je, watendao mabaya hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwitiBwana?

5 Hapo ndipo walipo, wameingiwa na hofu nyingi,

maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,

baliBwanani kimbilio lao.

7 Laiti wokovu wa Israeli

ungalikuja kutoka Sayuni!

WakatiBwanaarejeshapo

wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie,

Israeli na afurahi!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/14-dc78f06060b2adf0d54a4e409f70b76f.mp3?version_id=1627—

Zaburi 15

Kitu Mungu Anachotaka

(Zaburi Ya Daudi)

1 Bwana, ni nani awezaye kukaa

katika Hekalu lako?

Nani awezaye kuishi

katika mlima wako mtakatifu?

2 Ni yule aendaye pasipo mawaa,

anayetenda yaliyo haki,

asemaye kweli toka moyoni mwake

3 na hana masingizio ulimini mwake,

asiyemtenda jirani yake vibaya

na asiyemsingizia mwenzake,

4 ambaye humdharau mtu mbaya sana,

lakini huwaheshimu wale

ambao humwogopaBwana,

yule atunzaye kiapo chake

hata kama anaumia.

5 Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,

na hapokei rushwa

dhidi ya mtu asiye na hatia.

Mtu afanyaye haya

kamwe hatatikisika.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/15-12ac0bb687ff8678dd16cf5435ddfab1.mp3?version_id=1627—

Zaburi 16

Sala ya Matumaini

(Utenzi wa Daudi)

1 Ee Mungu, uniweke salama,

kwa maana kwako nimekimbilia.

2 NilimwambiaBwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;

pasipo wewe sina jambo jema.”

3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani,

ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.

4 Huzuni itaongezeka kwa wale

wanaokimbilia miungu mingine.

Sitazimimina sadaka zao za damu

au kutaja majina yao midomoni mwangu.

5 Bwanaumeniwekea fungu langu na kikombe changu;

umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,

hakika nimepata urithi mzuri.

7 NitamsifuBwanaambaye hunishauri,

hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.

8 NimemwekaBwanambele yangu daima.

Kwa kuwa yupo mkono wangu wa kuume,

sitatikiswa.

9 Kwa hiyo moyo wangu una furaha na ulimi wangu unashangilia;

pia mwili wangu utapumzika salama,

10 kwa sababu hutanitelekeza kuzimu,

wala hutaacha Mtakatifu Wako aone uharibifu.

11 Umenijulisha njia ya uzima;

utanijaza na shangwe katika uwepo wako,

pamoja na furaha za milele

katika mkono wako wa kuume.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/16-4ccaddf1574a9e1359b06bd28e2a0236.mp3?version_id=1627—

Zaburi 17

Sala Ya Mtu Asiye Na Hatia

(Sala Ya Daudi)

1 Sikia, EeBwana, kusihi kwangu kwa haki,

sikiliza kilio changu.

Tega sikio kwa ombi langu,

halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.

2 Hukumu yangu na itoke kwako,

macho yako na yaone yale yaliyo haki.

3 Ingawa unauchunguza moyo wangu

na kunikagua usiku,

ingawa umenijaribu,

hutaona cho chote,

nimeamua kwamba kinywa changu

hakitatenda dhambi.

4 Kutokana na matendo ya wanadamu,

kwa neno la midomo yako,

nimejiepusha na njia

za wenye jeuri.

5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako;

nyayo zangu hazikuteleza.

6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu,

unitegee sikio lako na usikie ombi langu.

7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu,

wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume

wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.

8 Nilinde kama mboni ya jicho lako,

unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako

9 kutokana na waovu wanaonishambulia,

kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.

10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu,

vinywa vyao hunena kwa majivuno.

11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira,

wakiwa macho, waniangushe chini.

12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye,

kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.

13 Inuka, EeBwana, pambana nao, uwaangushe,

niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.

14 EeBwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii,

kutokana na watu wa ulimwengu huu

ambao fungu lao liko katika maisha haya.

Na wapate adhabu ya kuwatosha.

Watoto wao na wapate zaidi ya hayo,

hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.

15 Na mimi katika haki nitauona uso wako,

niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/17-27adb72ba79fd5e18265fd8a5f1a0844.mp3?version_id=1627—

Zaburi 18

Wimbo Wa Daudi Wa Ushindi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi Mtumishi Wa Mungu Aliyomwimbia Mungu Wakati Mungu Alipomwokoa Mkononi Mwa Sauli Na Adui Wengine)

1 Nakupenda wewe, EeBwana,

nguvu yangu.

2 Bwanani mwamba wangu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

Mungu wangu ni mwamba,

ambaye kwake ninakimbilia.

Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu,

ngome yangu.

3 NinamwitaBwanaanayestahili kusifiwa,

nami nimeokoka kutoka kwa adui zangu.

4 Kamba za mauti zilinizunguka,

mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

5 Kamba za kuzimu zilinizunguka,

mitego ya mauti ilinikabili.

6 Katika shida yangu nalimwitaBwana,

nilimlilia Mungu wangu anisaidie.

Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu,

kilio changu kikafika mbele zake,

masikioni mwake.

7 Dunia ikatetemeka na kutikisika,

misingi ya milima ikayumbayumba,

ilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.

8 Pua zake zilitoa moshi,

moto uteketezao ulitoka kinywani mwake,

makaa ya moto yawakayo

yakatoka ndani mwake.

9 Alizipasua mbingu akashuka chini,

mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

10 Alipanda kerubi akaruka,

akapaa juu kwa mbawa za upepo.

11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika,

chandarua chake kumzunguka,

mawingu meusi ya mvua angani.

12 Kutokana na mwanga mkali wa uwepo wake

mawingu yalisogea,

ikanyesha mvua ya mawe

na umeme wa radi.

13 Bwanaalinguruma kutoka mbinguni,

sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui,

naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.

15 EeBwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako,

sakafu ya bahari ikaonekana,

misingi ya dunia ikawa wazi.

16 Akanyosha mkono wake kutoka juu, akanishika,

akanitoa kutoka katika maji mengi.

17 Akaniokoa kutoka adui yangu mwenye nguvu nyingi,

kutoka adui zangu,

waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.

18 Walinishambulia siku ya taabu yangu,

lakiniBwanaalikuwa msaada wangu.

19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele,

akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.

20 Bwanaalinitendea sawa sawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.

21 Kwa maana nimezishika njia zaBwana,

sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

22 Sheria zake zote zi mbele yangu,

wala sijayaacha maagizo yake.

23 Nimekuwa sina hatia mbele zake,

nami nimejilinda nisitende dhambi.

24 Bwanaamenilipa sawasawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.

25 Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu,

kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia.

26 Kwa aliye safi unajionyesha kuwa safi,

lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.

27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu

lakini huwashusha wenye kiburi.

28 Wewe, EeBwana, unaifanya taa yangu

iendelee kuwaka,

Mungu wangu hulifanya giza langu

kuwa mwanga.

29 Kwa msaada wako nitashinda jeshi,

nikiwa pamoja na Mungu wangu

nitaweza kuruka ukuta.

30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu,

neno laBwanani kamili.

Yeye ni ngao kwa wote

wanaokimbilia kwake.

31 Kwa maana ni nani aliye Mungu

zaidi yaBwana?

Ni nani aliye Mwamba

isipokuwa Mungu wetu?

32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na

kufanya njia yangu kuwa kamilifu.

33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,

huniwezesha kusimama mahali palipo juu.

34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita,

mikono yangu inaweza

kupinda upinde wa shaba.

35 Hunipa ngao yako ya ushindi,

mkono wako wa kuume hunitegemeza,

huinama chini ili kuniinua.

36 Hupanua mapito yangu,

ili miguu yangu isiteleze.

37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata,

sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.

38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena,

walianguka chini ya miguu yangu.

39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita,

adui zangu uliwafanya wasujudu miguuni pangu.

40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,

nami nikawaangamiza adui zangu.

41 Walipiga yowe kuomba msaada,

lakini hapakuwepo na ye yote wa kuwaokoa;

walimliliaBwana, lakini hakuwajibu.

42 Niliwaponda wakawa kama mavumbi

yanayopeperushwa na upepo,

nikawamwaga nje kama tope barabarani.

43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu;

umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa,

watu ambao sikuwajua wananitumikia.

44 Mara wanisikiapo hunitii,

wageni hunyenyekea mbele yangu.

45 Wote wanalegea,

wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.

46 Bwanayu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!

Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!

47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,

awatiishaye mataifa chini yangu,

48 aniokoaye na adui zangu.

Uliniinua juu ya adui zangu;

uliniokoa toka watu wajeuri.

49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, EeBwana;

nitaliimbia sifa jina lako.

50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu,

huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake,

kwa Daudi na uzao wake milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/18-0f64b340122b4c9189b542d8db0ea1a7.mp3?version_id=1627—

Zaburi 19

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,

anga zahubiri kazi ya mikono yake.

2 Siku baada ya siku zinatoa habari,

usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.

3 Hakuna msemo wala lugha,

ambapo sauti zao hazisikiki.

4 Sauti yao imeenea duniani pote,

maneno yao yameenea

mpaka miisho ya dunia.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,

5 linafanana na bwana arusi

akitoka chumbani mwake,

kama shujaa afurahiavyo

kukamilisha kushindana kwake.

6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu,

na kufanya mzunguko wake

hadi upande mwingine,

hakuna kilichojificha joto lake.

7 Sheria yaBwanani kamilifu,

ikihuisha nafsi.

Shuhuda zaBwanani za kuaminika,

zikimpa mjinga hekima.

8 Maagizo yaBwanani kamili,

nayo hufurahisha moyo.

Amri zaBwanahuangaza,

zatia nuru machoni.

9 KumchaBwanani utakatifu,

nako kwadumu milele.

Amri zaBwanani za hakika,

nazo zina haki.

10 Ni za thamani kuliko dhahabu,

kuliko dhahabu iliyo safi sana,

ni tamu kuliko asali,

kuliko asali kutoka kwenye sega.

11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa,

katika kuzishika kuna thawabu kubwa.

12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake?

Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.

13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi,

nazo zisinitawale.

Ndipo nitakapokuwa sina lawama,

wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.

14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu,

yapate kibali mbele zako,

EeBwana, Mwamba wangu

na Mkombozi wangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/19-9f11ab7437be115ca6c824090f37be77.mp3?version_id=1627—