Zaburi 30

Maombi Ya Shukrani

Utenzi Wa Kuweka Wakfu Hekalu (Zaburi Ya Daudi)

1 Nitakutukuza wewe, EeBwana,

kwa kuwa umeniinua

na hukuacha adui zangu

washangilie juu yangu.

2 EeBwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie

na wewe umeniponya.

3 EeBwana, umenitoa Kuzimu,

umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti.

4 MwimbieniBwana, enyi watakatifu wake;

lisifuni jina lake takatifu,

kwa kumbukumbu la utakatifu wake.

5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,

bali upendo wake hudumu siku zote;

inawezekana kilio kikawepo usiku kucha,

lakini asubuhi kukawa na furaha.

6 Nilipofanikiwa nilisema,

“Sitatikiswa kamwe.”

7 EeBwana, uliponijalia,

uliuimarisha mlima wangu,

lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.

8 Kwako wewe, EeBwana, niliita,

kwa Bwana niliomba rehema:

9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu?

Katika kushuka kwangu shimoni?

Je, mavumbi yatakusifu?

Je, yatatangaza uaminifu wako?

10 EeBwana, unisikie na kunihurumia,

EeBwana, uwe msaada wangu.”

11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza,

ulinivua nguo za gunia

ukanivika shangwe,

12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya.

EeBwanaMungu wangu,

nitakushukuru milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/30-445301d403cecad780d7e1817451227b.mp3?version_id=1627—

Zaburi 31

Maombi na Sifa Kwa Kuokolewa Kutoka Kwa Adui

(Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, ninakukimbilia wewe,

usiache nikaaibika kamwe,

kwa haki yako uniokoe.

2 Nitegee sikio lako, uje uniokoe haraka,

uwe kwangu mwamba wa kimbilio,

ngome imara ya kuniokoa.

3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu

na ngome yangu, uniongoze na kunilinda

kwa ajili ya jina lako.

4 Uniepushe na mtego niliotegewa,

maana wewe ndiwe kimbilio langu.

5 Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako,

EeBwanaunikomboe,

wewe uliye Mungu wa kweli.

6 Ninawachukia wale wanaong’ang’ania sanamu batili;

mimi ninamtumainiBwana.

7 Nitafurahia na kushangilia upendo wako,

kwa kuwa uliona mateso yangu

na ulijua maumivu ya nafsi yangu.

8 Hukunikabidhi kwa adui yangu

bali umeiweka miguu yangu

mahali penye nafasi.

9 EeBwanaunihurumie, kwa kuwa niko kwenye shida;

macho yangu yanafifia kwa huzuni,

nafsi yangu na mwili wangu kwa sikitiko.

10 Maisha yangu yamedhoofika kwa majonzi,

naam, miaka yangu kwa kulia kwa maumivu makali;

nguvu zangu zinaisha kwa ajili ya mateso,

na mifupa yangu inachakaa.

11 Kwa sababu ya adui zangu wote,

nimedharauliwa kabisa na jirani zangu,

hata rafiki zangu wananiogopa,

wale wanionao barabarani hunikimbia.

12 Nimesahaulika miongoni mwao kama mtu aliyekufa,

nimekuwa kama chombo cha mfinyanzi kilichovunjika.

13 Kwa maana nimesikia maneno

niliyosingiziwa na watu wengi;

vitisho viko pande zote;

kwa kuwa wamefanya mashauri ya pamoja dhidi yangu

na kula njama kuniua.

14 Lakini mimi ninakutumaini wewe peke yako, EeBwana;

nimesema, “Wewe ndiwe Mungu wangu.”

15 Siku za maisha yangu ziko mikononi mwako,

uniokoe mikononi mwa adui zangu

na wale wanifuatiao.

16 Mwangazie mtumishi wako uso wako,

uniokoe kwa ajili ya upendo wako usiokoma.

17 Usiniache niaibike, EeBwana,

kwa maana nimekulilia wewe,

bali waovu waaibishwe

na kunyamazishwa Kuzimu.

18 Midomo yao isemayo uongo na inyamazishwe,

kwa maana kwa kiburi na dharau husema

kwa majivuno dhidi ya wenye haki.

19 Tazama jinsi ulivyo mkuu wema wako,

uliowawekea akiba wakuchao,

ambao huwapa wale wakukimbiliao

machoni pa watu.

20 Unawahifadhi katika uvuli wa uwepo wako

kutokana na hila za wanadamu;

katika makao yako huwaweka salama

kutokana na ndimi za mashtaka.

21 AtukuzweBwana,

kwa kuwa amenionyesha upendo wake wa ajabu

nilipokuwa katika mji uliozingirwa.

22 Kwa haraka yangu nilisema,

“Nimekatiliwa mbali na macho yako!”

Hata hivyo ulisikia kilio changu

ukanihurumia nilipokuita unisaidie.

23 MpendeniBwananinyi watakatifu wake wote!

Bwanahuwahifadhi waaminifu,

lakini wenye kiburi huwalipiza kikamilifu.

24 Iweni hodari na mjipe moyo,

ninyi nyote mnaomtumainiBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/31-5c2a77da4be1198712267b5c53c1fb47.mp3?version_id=1627—

Zaburi 32

Furaha Ya Msamaha

(Utenzi: Zaburi Ya Daudi. Funzo)

1 Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,

ambaye dhambi zake zimefunikwa.

2 Heri mtu yule ambayeBwana

hamhesabii dhambi,

na ambaye rohoni mwake

hamna udanganyifu.

3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa

kwa kulia kwa maumivu makali

mchana kutwa.

4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea,

nguvu zangu zilinyonywa

kama vile katika joto la kiangazi.

5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu

wala sikuficha uovu wangu.

Nikasema, “Nitaungama

makosa yangu kwaBwana,”

ndipo uliponisamehe

hatia ya dhambi yangu.

6 Kwa hiyo kila mtu mtauwa na akuombe

maadamu unapatikana,

hakika maji makuu yatakapofurika

hayatamfikia yeye.

7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha,

utaniepusha na taabu

na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.

8 Nitakufundisha na kukuonyesha

njia utakayoiendea;

nitakushauri na kukuangalia.

9 Usiwe kama farasi au nyumbu

wasio na akili,

ambao ni lazima waongozwe

kwa lijamu na hatamu

la sivyo hawatakukaribia.

10 Mtu mwovu ana taabu nyingi,

bali upendo usio na kikomo waBwana

unamzunguka mtu anayemtumaini.

11 Shangilieni katikaBwanana mfurahi,

enyi wenye haki!

Imbeni, ninyi nyote mlio wanyofu wa moyo!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/32-6087b1c971c45e990043259d2e9cb7ac.mp3?version_id=1627—

Zaburi 33

Ukuu Na Wema Wa Mungu

1 MwimbieniBwanakwa furaha, enyi wenye haki;

kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

2 MsifuniBwanakwa kinubi,

mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.

3 Mwimbieni wimbo mpya;

pigeni kwa ustadi,

pigeni kelele za furaha.

4 Maana neno laBwanani haki na kweli,

ni mwaminifu kwa yote atendayo.

5 Hupenda uadilifu na haki;

dunia imejaa upendo wake usiokoma.

6 Kwa neno laBwanambingu ziliumbwa,

jeshi lao la angani

kwa pumzi ya kinywa chake.

7 Ameyakusanya maji ya bahari

kama kwenye mtungi;

vilindi vya bahari

ameviweka katika ghala.

8 Dunia yote na imwogopeBwana,

watu wote wa dunia wamche.

9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa,

aliamuru na ikasimama imara.

10 Bwanahuzuia mipango ya mataifa,

hupinga makusudi ya mataifa.

11 Lakini mipango yaBwana

inasimama imara milele,

makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.

12 Heri taifa ambaloBwanani Mungu wao,

watu ambao aliwachagua

kuwa urithi wake.

13 Kutoka mbinguniBwanahutazama chini

na kuwaona wanadamu wote;

14 kutoka maskani mwake huwaangalia

wote wakaao duniani,

15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote,

ambaye huangalia

kila kitu wanachokitenda.

16 Hakuna mfalme aokokaye

kwa ukubwa wa jeshi lake;

hakuna shujaa aokokaye

kwa wingi wa nguvu zake.

17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,

licha ya nguvu zake nyingi hawezi kuokoa.

18 Lakini macho yaBwanayako kwa wale wamchao,

kwa wale ambao tumaini lao

ni katika upendo wake usio na kikomo,

19 ili awaokoe na mauti,

na kuwahifadhi wakati wa njaa.

20 Sisi tunamngojeaBwanakwa matumaini,

yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

21 Katika yeye mioyo yetu hushangilia,

kwa maana tunalitumainia

jina lake takatifu.

22 Upendo wako usio na mwisho

ukae juu yetu, EeBwana,

kama vile tunavyoweka

tumaini letu kwako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/33-1fce9b791359e502eb1f99b6a9c33f07.mp3?version_id=1627—

Zaburi 34

Sifa Na Wema Wa Mungu

(Zaburi Ya Daudi, Alipojifanya Mwendawazimu Mbele Ya Abimeleki, Ambaye Alimfukuza, Naye Akaondoka)

1 NitamtukuzaBwananyakati zote,

sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.

2 Nafsi yangu itajisifu katikaBwana

walioonewa wasikie na wafurahi.

3 MtukuzeniBwanapamoja nami,

naam, na tulitukuze jina lake pamoja.

4 NilimtafutaBwananaye akanijibu,

akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

5 Wale wamtazamao hutiwa nuru,

nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

6 Maskini huyu alimwitaBwanaakamsikia,

akamwokoa katika taabu zake zote.

7 Malaika waBwanahufanya kituo

akiwazunguka wale wamchao,

naye huwaokoa.

8 Onjeni mwone kwambaBwanani mwema,

heri mtu yule anayemkimbilia.

9 McheniBwanaenyi watakatifu wake,

kwa maana wale wamchao

hawapungukiwi na kitu cho chote.

10 Wana simba wenye nguvu

hutindikiwa na kuona njaa,

bali wale wamtafutaoBwana

hawatakosa kitu cho chote kilicho chema.

11 Njoni, watoto wangu, mnisikilize,

nitawafundisha kumchaBwana.

12 Ye yote kati yenu anayependa maisha

na kutamani kuziona siku nyingi njema,

13 auzuie ulimi wake na mabaya

na midomo yake kutokana

na kusema uongo.

14 Aache uovu na atende mema,

aitafute amani na kuifuatia.

15 Macho yaBwanayako kwa wenye haki

na masikio yake yako makini

kusikia kilio chao;

16 uso waBwanauko kinyume na watenda mabaya,

kufuta kumbukumbu lao duniani.

17 Wenye haki hulia, nayeBwanahuwasikia,

huwaokoa katika taabu zao zote.

18 Bwanayu karibu nao waliovunjika moyo

na huwaokoa waliopondeka roho.

19 Mwenye haki ana mateso mengi,

lakiniBwanahumwokoa nayo yote,

20 huhifadhi mifupa yake yote,

hata mmoja hautavunjika.

21 Ubaya utamwua mtu mwovu,

adui za mwenye haki watahukumiwa.

22 Bwanahuwakomboa watumishi wake,

wale wanaomkimbilia yeye

hawatahukumiwa hata mmoja wao.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/34-ccb420443dc43577cc3db3894086b01d.mp3?version_id=1627—

Zaburi 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

(Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, pingana na wale wanaopingana nami,

upigane na hao wanaopigana nami.

2 Uchukue ngao na kigao,

inuka unisaidie.

3 Inua mkuki wako na fumolako

dhidi ya hao wanaonifuatia.

Uiambie nafsi yangu,

“Mimi ni wokovu wako.”

4 Wafedheheshwe na waaibishwe

wale wanaotafuta uhai wangu,

wanaofanya shauri kuniangamiza

warudishwe nyuma kwa hofu.

5 Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,

malaika waBwanaakiwafukuza;

6 njia yao na iwe giza na ya utelezi,

malaika waBwanaakiwafuatilia.

7 Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,

na bila sababu wamenichimbia shimo,

8 maafa na yawapate ghafula:

wavu walionifichia na uwatege wenyewe,

na waanguke katika shimo hilo,

kwa maangamizo yao.

9 Ndipo nafsi yangu itashangilia katikaBwana

na kuufurahia wokovu wake.

10 Nitapaza sauti yangu nikisema,

“Ni nani aliye kama wewe, EeBwana?

Huwaokoa maskini kutokana na watu

walio na nguvu kuliko wao,

maskini na mhitaji kutokana

na wanaowanyang’anya!”

11 Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza kwa mambo nisiyoyajua.

12 Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

13 Lakini walipokuwa wagonjwa,

nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

14 niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama vile ninayemwombolezea mama yangu.

15 Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

16 Kama watu wasiomcha Mungu wamedhihaki,

wamenisagia meno.

17 EeBwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

18 Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

19 Usiwaache wale wanaonisimanga,

wale ambao ni adui zangu bila sababu;

usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu

wakonyeze jicho kwa hila.

20 Hawazungumzi kwa amani,

bali wanatunga mashtaka ya uongo

dhidi ya wale wanaoishi kwa utulivu katika nchi.

21 Hunifumbulia vinywa vyao wakisema,

“Aha! Aha! Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

22 EeBwana, umeona hili, usiwe kimya.

Usiwe mbali nami, EeBwana.

23 Amka, inuka unitetee!

Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

24 Nihukumu kwa haki yako, EeBwanaMungu wangu,

sawasawa na haki yako;

usiwaache wakusimange.

25 Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”

Au waseme, “Tumemmeza.”

26 Wote wanaofurahia dhiki yangu

na waaibishwe na wachanganyikiwe;

hao wanaojiinua dhidi yangu

na wavikwe aibu na dharau.

27 Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki

na wapige kelele za shangwe na furaha;

hebu waseme siku zote,

“Bwanaatukuzwe,

ambaye amefurahia

mafanikio ya mtumishi wake.”

28 Ulimi wangu utanena haki yako

na sifa zako mchana kutwa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/35-55cb7add9158b71d13574b9940749697.mp3?version_id=1627—

Zaburi 36

Uovu Wa Mwanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi Mtumishi Wa Mungu)

1 Kuna neno moyoni mwangu

kuhusu hali ya dhambi ya mwovu.

Hakuna hofu ya Mungu

mbele ya macho yake.

2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno

kiasi kwamba hawezi kugundua

au kuichukia dhambi yake.

3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu,

ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.

4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya,

hujitia katika njia ya dhambi

na hakatai lililo baya.

5 Upendo wako, EeBwana,

unafika hadi katika mbingu,

uaminifu wako hadi kwenye anga.

6 Haki yako ni kama milima mikubwa,

hukumu zako ni kama kilindi kirefu sana.

EeBwana, wewe huwahifadhi

mwanadamu na mnyama.

7 Upendo wako usiokoma

ni wa thamani mno!

Wale wa daraja ya juu na ya chini

miongoni mwa wanadamu

hupata kimbilio katika uvuli wa mbawa zako.

8 Watajifurahisha katika wingi wa vitu vya nyumbani mwako,

nawe utawanywesha

katika mto wa furaha zako.

9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,

katika nuru yako twaona nuru.

10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe,

haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.

11 Mguu wa mwenye kiburi na usije dhidi yangu,

wala mkono wa mwovu usinifukuze.

12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka:

wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/36-1a88171c243532a801b4f48713566e12.mp3?version_id=1627—

Zaburi 37

Mwisho Wa Mtu Mwovu

(Zaburi Ya Daudi)

1 Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu wala usiwaonee wivu watu watendao maovu,

2 kwa maana kama majani watanyauka mara,

kama mimea ya kijani watakufa mara.

3 MtumainiBwanana utende yaliyo mema,

ukae katika nchi ukafurahie malisho salama.

4 Jifurahishe katikaBwananaye atakupa

haja za moyo wako.

5 MkabidhiBwananjia yako,

mtumaini yeye naye atatenda hili:

6 yeye atafanya haki yako ing’ae

kama mapambazuko,

hukumu kama jua la adhuhuri.

7 Tulia mbele zaBwana

na umngojee kwa uvumilivu;

usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao,

wanapotekeleza mipango yao miovu.

8 Epuka hasira na uache ghadhabu,

usihangaike, itakuongoza tu kwenye ubaya.

9 Kwa maana waovu watakatiliwa mbali,

bali wale wanaomtumainiBwanawatairithi nchi.

10 Bado kitambo kidogo, waovu hawataonekana,

ingawa utawatafuta, hawataonekana.

11 Bali wanyenyekevu watairithi nchi

na watafurahia amani tele.

12 Waovu hula njama dhidi ya wenye haki

na kuwasagia meno,

13 bali Bwana huwacheka waovu,

kwa sababu anajua siku yao inakuja.

14 Waovu huchomoa upanga na kupinda upinde,

ili wawaangushe maskini na wahitaji,

kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.

15 Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe,

na pinde zao zitavunjwa.

16 Bora kidogo walichonacho wenye haki

kuliko wingi wa mali

walizo nazo waovu wengi;

17 kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa,

lakiniBwanahumtegemeza mwenye haki.

18 Bwanaanazifahamu siku za wanyofu,

na urithi wao utadumu milele.

19 Siku za maafa hawatanyauka,

siku za njaa watafurahia kuwa na wingi wa vitu.

20 Lakini waovu wataangamia:

Adui zaBwanawatatoweka

kama uzuri wa mashamba,

watatoweka,

watatoweka kama moshi.

21 Waovu hukopa na hawalipi,

bali wenye haki hutoa kwa ukarimu,

22 wale wanaobarikiwa naBwanawatairithi nchi,

bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali.

23 KamaBwanaakipendezwa na njia ya mtu,

huimarisha hatua zake,

24 ajapojikwaa, hataanguka,

kwa maanaBwana

humtegemeza kwa mkono wake.

25 Nilikuwa kijana na sasa ni mzee,

lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa

au watoto wao wakiomba omba chakula.

26 Wakati wote ni wakarimu hukopesha bila masharti,

watoto wao watabarikiwa.

27 Acha ubaya na utende wema,

nawe utaishi katika nchi milele.

28 Kwa kuwaBwanahuwapenda

wenye haki naye hatawaacha waaminifu wake.

Watalindwa milele,

lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali;

29 wenye haki watairithi nchi,

na kuishi humo milele.

30 Kinywa cha mwenye haki hutamka hekima,

nao ulimi wake huzungumza lililo haki.

31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake;

nyayo zake hazitelezi.

32 Watu waovu huvizia wenye haki,

wakitafuta kuwaua;

33 lakiniBwanahatawaacha mikononi mwao

wala hatawaacha wahukumiwe

kuwa wakosa wanaposhtakiwa.

34 UmngojeeBwana,

na uishike njia yake.

Naye atakutukuza uirithi nchi,

waovu watakapokatiliwa mbali,

utaliona hilo.

35 Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi

kama mwerezi wa Lebanoni,

36 lakini alitoweka mara na hakuonekana,

ingawa nilimtafuta,

hakupatikana.

37 Watafakari watu wasio na hatia,

wachunguze watu wakamilifu,

kuna mafanikio kwa mtu apendaye amani.

38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa,

mafanikio yao yatakatiliwa mbali.

39 Wokovu wa wenye haki hutoka kwaBwana,

yeye ni ngome yao wakati wa shida.

40 Bwanahuwasaidia na kuwaokoa,

huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi,

kwa maana wanamkimbilia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/37-e0d9208b6fe305ab72a7084c51613c73.mp3?version_id=1627—

Zaburi 38

Maombi Ya Mtu Anayeteseka

(Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, usinikemee katika hasira yako

wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.

2 Kwa kuwa mishale yako imenichoma,

na mkono wako umenishukia.

3 Hakuna afya mwilini mwangu

kwa sababu ya ghadhabu yako,

mifupa yangu haina uzima

kwa sababu ya dhambi zangu.

4 Maovu yangu yamenifunika

kama mzigo usiochukulika.

5 Majeraha yangu yameoza na yananuka,

kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.

6 Nimeinamishwa chini na kushushwa sana,

mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.

7 Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo,

hakuna afya mwilini mwangu.

8 Nimedhoofika na kupondwa kabisa,

nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.

9 EeBwana, yote ninayoyaonea shauku

yako wazi mbele zako,

kutamani kwangu sana

hakufichiki mbele zako.

10 Moyo wangu unapigapiga,

nguvu zangu zimeniishia;

hata macho yangu yametiwa giza.

11 Rafiki na wenzangu wananikwepa

kwa sababu ya majeraha yangu;

majirani zangu wanakaa mbali nami.

12 Wale wanaotafuta uhai wangu

wanatega mitego yao,

wale ambao wangetaka kunidhuru

huongea juu ya maangamizi yangu;

hufanya shauri la hila mchana kutwa.

13 Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia,

ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,

14 nimekuwa kama mtu asiyesikia,

ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.

15 EeBwana, ninakungojea wewe,

Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.

16 Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie,

wala wasijitukuze juu yangu

mguu wangu unapoteleza.”

17 Kwa maana ninakaribia kuanguka,

na maumivu yangu yananiandama siku zote.

18 Naungama uovu wangu,

ninataabishwa na dhambi yangu.

19 Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari,

wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.

20 Wanaolipa maovu kwa wema wangu

hunisingizia ninapofuata lililo jema.

21 EeBwana, usiniache,

usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.

22 Ee Bwana Mwokozi wangu,

uje upesi kunisaidia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/38-a4e5602d287546c89aef7971609df7bf.mp3?version_id=1627—

Zaburi 39

Maombi Ya Mtu Anayeteseka

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Yeduthuni. Zaburi Ya Daudi)

1 Nilisema, “Nitaziangalia njia zangu

na kuuzuia ulimi wangu usije ukatenda dhambi;

nitaweka lijamu kinywani mwangu

wakati wote waovu wanapokuwa karibu nami.”

2 Lakini niliponyamaza kimya na kutulia,

hata pasipo kusema lo lote jema,

uchungu wangu uliongezeka.

3 Moyo wangu ulipata moto ndani yangu,

nilipotafakari, moto uliwaka,

ndipo nikasema kwa ulimi wangu:

4 “EeBwana, nijulishe mwisho wa maisha yangu

na hesabu ya siku zangu;

nijalie kujua jinsi maisha yangu

yanavyopita upesi.

5 Umefanya maisha yangu mafupi kama pumzi;

muda wangu wa kuishi ni kama

hauna thamani kwako.

Maisha ya kila mwanadamu

ni kama pumzi.

6 Hakika kila binadamu ni kama njozi

aendapo huku na huko:

hujishughulisha na mengi lakini ni ubatili;

anakusanya mali nyingi,

wala hajui ni nani atakayeifaidi.

7 “Lakini sasa Bwana, nitafute nini?

Tumaini langu ni kwako.

8 Niokoe kutoka kwenye makosa yangu yote,

usinifanye kuwa dhihaka ya wapumbavu.

9 Nilinyamaza kimya,

sikufumbua kinywa changu,

kwa sababu wewe ndiwe uliyetenda hili.

10 Niondolee mjeledi wako,

nimeshindwa kwa mapigo ya mkono wako.

11 Unakemea na kuadhibu wanadamu

kwa ajili ya dhambi zao;

unaharibu utajiri wao kama nondo aharibuvyo:

kila mwanadamu ni kama pumzi tu.

12 “EeBwana, usikie maombi yangu,

usikie kilio changu unisaidie,

usiwe kiziwi kwa kulia kwangu.

Kwani mimi ninaishi na wewe kama mgeni,

kama walivyokuwa baba zangu wote,

13 Tazama mbali nami, ili niweze kufurahi tena

kabla sijaondoka na nisiwepo tena.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/39-cf5301ce3fac771eada1f8c6a16dcd0c.mp3?version_id=1627—