Zaburi 40

Wimbo Wa Sifa

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 NilimngojaBwanakwa saburi,

naye akaniinamia akasikia kilio changu.

2 Akanipandisha kutoka shimo la uharibifu,

kutoka katika matope na utelezi;

akaiweka miguu yangu juu ya mwamba

na kunipa mahali imara pa kusimama.

3 Akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,

wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.

Wengi wataona na kuogopa

na kuweka tumaini lao kwaBwana.

4 Heri mtu yule amfanyayeBwanakuwa tumaini lake,

asiyewategemea wenye kiburi,

wale wenye kugeukia miungu ya uongo.

5 EeBwanaMungu wangu,

umefanya mambo mengi ya ajabu.

Mambo uliyopanga kwa ajili yetu

hakuna awezaye kukuhesabia;

kama ningesema na kuyaelezea,

yangekuwa mengi mno kuyaelezea.

6 Dhabihu na sadaka hukuvitaka,

# lakini umefungua masikio yangu,

sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi

hukuzihitaji.

7 Ndipo niliposema, “Mimi hapa, nimekuja:

imeandikwa kuhusu mimi katika gombo.

8 Ee Mungu wangu,

natamani kufanya mapenzi yako;

sheria yako iko ndani ya moyo wangu.”

9 Nimehubiri haki katika kusanyiko kubwa,

sikufunga mdomo wangu,

EeBwana, kama ujuavyo.

10 Sikuficha haki yako moyoni mwangu;

ninasema juu ya uaminifu wako na wokovu wako.

Sikuficha upendo wako na kweli yako

mbele ya kusanyiko kubwa.

11 EeBwana, usizuilie huruma zako,

upendo wako na kweli yako daima vinilinde.

12 Kwa maana taabu zisizo na hesabu zimenizunguka,

dhambi zangu zimenikamata, hata nisiweze kuona.

Zimekuwa nyingi kuliko nywele za kichwa changu,

nao moyo unazimia ndani yangu.

13 EeBwana, uwe radhi kuniokoa,

EeBwana, njoo hima unisaidie.

14 Wote wanaotafuta kuuondoa uhai wangu

na waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu

na warudishwe nyuma kwa aibu.

15 Wale waniambiao, “Aha!”

wafadhaishwe na iwe aibu yao.

16 Bali wote wakutafutao

washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,

“Bwanaatukuzwe!”

17 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;

Bwana na anifikirie.

Wewe ni msaada wangu na Mwokozi wangu;

Ee Mungu wangu, usikawie.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/40-6e5c826ea55f00171622d693cfba7ef5.mp3?version_id=1627—

Zaburi 41

Maombi Ya Mtu Mgonjwa

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Heri mtu yule anayemjali mnyonge,

Bwanaatamwokoa wakati wa shida.

2 Bwanaatamlinda na kuyahifadhi maisha yake,

atambariki katika nchi

na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.

3 Bwanaatamtegemeza awapo mgonjwa kitandani,

atamwinua kutoka kitandani mwake.

4 Nilisema, “EeBwananihurumie,

niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”

5 Adui zangu wanasema kwa hila,

“Lini atakufa na jina lake litokomee kabisa.”

6 Kila anapokuja mtu kunitazama,

huzungumza uongo,

huku moyo wake hukusanya masingizio;

kisha huondoka na kuyasambaza huko na huko.

7 Adui zangu wote hunong’onezana dhidi yangu,

hao huniwazia mabaya sana, wakisema,

8 “Ugonjwa mbaya sana umempata,

kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”

9 Hata rafiki yangu wa karibu, niliyemwamini,

yule aliyekula chakula changu

ameniinulia kisigino chake.

10 Lakini wewe, EeBwana, unihurumie,

ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.

11 Najua kwamba wapendezwa nami,

kwa kuwa adui yangu hanishindi.

12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza

na kuniweka kwenye uwepo wako milele.

13 MsifuniBwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Amen na Amen.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/41-e49091db6bebff4e9f22e709b3efe730.mp3?version_id=1627—

Zaburi 42

Maombi Ya Mtu Aliye Uhamishoni

(Kwa Mwimbishaji: Utenzi Wa Wana Wa Kora)

1 Kama vile paa aoneavyo shauku vijito vya maji,

ndivyo nafsi yangu ikuoneavyo shauku, Ee Mungu.

2 Nafsi yangu inamwonea Mungu kiu, Mungu aliye hai.

Ni lini nitaweza kwenda kukutana na Mungu?

3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu

mchana na usiku,

huku watu wakiniambia mchana kutwa,

“Yuko wapi Mungu wako?”

4 Vitu hivi ninavikumbuka

ninapoimimina nafsi yangu:

Jinsi nilivyokuwa nikienda na umati wa watu,

nikiongoza maandamano

kuelekea kwenye nyumba ya Mungu,

kwa kelele za shangwe na za shukrani

katikati ya umati wa watu

wanaoadhimisha sikukuu.

5 Ee nafsi yangu kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu,

aliye afya ya uso wangu

Mwokozi wangu na

6 Mungu wangu.

Nafsi yangu inasononeka ndani yangu;

kwa hiyo nitakukumbuka

kutoka nchi ya Yordani,

katika vilele vya Hermoni,

kutoka Mlima Mizari.

7 Kilindi huita kilindi,

katika ngurumo za maporomoko ya maji yako;

mawimbi yako yote pamoja na viwimbi

vimepita juu yangu.

8 MchanaBwanahuelekeza upendo wake,

usiku wimbo wake uko nami:

maombi kwa Mungu wa uzima wangu.

9 Ninamwambia Mungu Mwamba wangu,

“Kwa nini umenisahau?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?”

10 Mifupa yangu inateseka kwa maumivu makali

adui zangu wanaponidhihaki,

wakiniambia mchana kutwa,

“Yuko wapi Mungu wako?”

11 Ee nafsi yangu kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu,

aliye afya ya uso wangu,

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/42-b22cac1a8003a7912ce1f01e13fe83ca.mp3?version_id=1627—

Zaburi 43

Maombi Ya Mtu Aliyeko Uhamishoni Yanaendelea

1 Ee Mungu unihukumu,

nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,

niokoe na watu wadanganyifu na waovu.

2 Wewe ni Mungu ngome yangu.

Kwa nini umenikataa?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?

3 Tuma hima nuru yako na kweli yako

na viniongoze;

vinilete mpaka mlima wako mtakatifu,

mpaka mahali unapoishi.

4 Ndipo nitakwenda madhabahuni pa Mungu,

kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.

Nitakusifu kwa kinubi,

Ee Mungu, Mungu wangu.

5 Ee nafsi yangu kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu

aliye afya ya uso wangu,

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/43-73dc30c516be7542f8dd7374742d54b2.mp3?version_id=1627—

Zaburi 44

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Utenzi Wa Wana Wa Kora)

1 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,

baba zetu wametueleza

yale uliyotenda katika siku zao,

siku za kale.

2 Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa katika nchi hii

na ukawapanda baba zetu,

uliangamiza mataifa

na kuwastawisha baba zetu.

3 Sio kwa upanga wao waliipata nchi,

wala si mkono wao uliwapatia ushindi;

ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume,

na nuru ya uso wako,

kwa kuwa uliwapenda.

4 Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu,

unayeamuru ushindi kwa Yakobo.

5 Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu;

kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.

6 Siutumaini upinde wangu,

upanga wangu hauniletei ushindi;

7 bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu,

unawaaibisha watesi wetu.

8 Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa,

nasi tutalisifu jina lako milele.

9 Lakini sasa umetukataa na kutudhili,

wala huendi tena na jeshi letu.

10 Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui,

nao watesi wetu wametuteka nyara.

11 Umetuacha tutafunwe kama kondoo

na umetutawanya katika mataifa.

12 Umewauza watu wako kwa fedha kidogo,

wala hukupata faida yo yote kwa mauzo yao.

13 Umetufanya lawama kwa jirani zetu,

dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.

14 Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa,

mataifa hutikisa vichwa vyao.

15 Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa,

na uso wangu umejaa aibu tele,

16 kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana,

kwa sababu ya adui,

ambaye anatamani kulipiza kisasi.

17 Hayo yote yametutokea,

ingawa tulikuwa hatujakusahau

wala hatujaenda kinyume na Agano lako.

18 Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma;

lakini nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.

19 Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha

na ukatufunika kwa giza nene.

20 Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu

au kunyoshea mikono yetu kwa mungu mgeni,

21 je, Mungu hangaligundua hili,

kwa kuwa anazijua siri za moyo?

22 Hata hivyo kwa ajili yako tunakabiliwa na kifo mchana kutwa;

tunahesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.

23 Amka, EeBwana! Kwa nini unalala?

Zinduka! Usitukatae milele.

24 Kwa nini unauficha uso wako

na kusahau taabu na mateso yetu?

25 Tumeshushwa hadi mavumbini,

miili yetu imegandamana na ardhi.

26 Inuka na utusaidie,

utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/44-54b75441df84580e0380dbf22b6a37c2.mp3?version_id=1627—

Zaburi 45

Wimbo Wa Arusi Ya Kifalme

(Kwa Mwimbishaji: Utenzi Wa Wana Wa Kora)

1 Moyo wangu umesisimuliwa na jambo

jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu,

ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.

2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote

na midomo yako imepakwa neema,

kwa kuwa Mungu amekubariki milele.

3 Jifunge upanga wako pajani mwako, Ee mwenye nguvu,

jivike fahari na utukufu.

4 Katika fahari yako songa mbele kwa ushindi,

kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki,

mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.

5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme,

mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.

6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi

kitadumu milele na milele,

fimbo ya utawala wa haki

itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.

7 Unaipenda haki na kuchukia uovu;

kwa hiyo Mungu, Mungu wako,

amekuweka juu ya rafiki zako,

kwa kukupaka mafuta ya furaha.

8 Mavazi yako yote ni yenye harufu nzuri

ya manemane, udi na mdalasini;

kutoka kwenye majumba ya kifalme

yaliyopambwa kwa pembe za ndovu,

sauti za vinanda vya nyuzi

zinakufanya ufurahi.

9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa;

kuume kwako yupo bibi arusi wa kifalme

aliyevaa dhahabu ya Ofiri.

10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio:

Sahau watu wako na wa nyumbani mwa baba yako.

11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako;

mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.

12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi,

watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.

13 Utukufu wote ni binti mfalme katika chumba chake;

vazi lake limefumwa kwa kuchanganya nyuzi za dhahabu.

14 Akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa anaongozwa kwa mfalme,

mabikira wenzake wanamfuata

na wanaletwa kwako.

15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha,

na kuingia katika jumba la mfalme.

16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu,

mtawafanya wana wa kifalme katika nchi yote.

17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote,

kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/45-1dff6e6f94c36fcf53e0a799560014ec.mp3?version_id=1627—

Zaburi 46

Mungu Yuko Pamoja Nasi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora. Mtindo Wa Alamothi)

1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,

msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa

nayo milima ikiangukia moyoni wa bahari.

3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka,

milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.

4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu,

mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.

5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka,

Mungu atausaidia asubuhi na mapema.

6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka,

Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.

7 BwanaMwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

8 Njoni mkaone kazi zaBwana

jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.

9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia,

anakata upinde na kuvunjavunja mkuki,

anateketeza ngao kwa moto.

10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu;

nitatukuzwa katikati ya mataifa,

nitatukuzwa katika dunia.”

11 BwanaMwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi;

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/46-2f02b0237beb5a914cb3b0cb7ee4c0f0.mp3?version_id=1627—

Zaburi 47

Mtawala Mwenye Enzi Yote

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora)

1 Pigeni makofi, enyi mataifa yote,

mpigieni Mungu kelele za shangwe!

2 Jinsi gani alivyo wa kutisha,BwanaAliye Juu Sana,

Mfalme mkuu juu ya dunia yote.

3 Ametiisha mataifa chini yetu

na mataifa chini ya miguu yetu.

4 Alituchagulia urithi wetu kwa ajili yetu

fahari ya Yakobo, aliyempenda.

5 Mungu amepaa katikati ya kelele za shangwe,

Bwanakatikati ya sauti za tarumbeta.

6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa,

mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.

7 Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote,

mwimbieni zaburi za sifa.

8 Mungu anatawala juu ya mataifa,

Mungu ameketi juu ya kiti chake cha enzi kitakatifu.

9 Wakuu wa mataifa wanakusanyika kama watu wa Mungu wa Abrahamu,

kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu;

yeye ametukuka sana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/47-e21b9683f9512765cfa2895d3ed9ceab.mp3?version_id=1627—

Zaburi 48

Sayuni, Mji Wa Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora)

1 Bwanani mkuu na anayestahili kusifiwa sana,

katika mji wa Mungu wetu,

mlima wake mtakatifu.

2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana,

furaha ya dunia yote.

# Kama vilele vya juu sana vya Safonini Mlima Sayuni,

mji wa Mfalme Mkuu.

3 Mungu yuko katika ngome zake;

amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.

4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu,

waliposonga mbele pamoja,

5 Danwalimwona nao wakashangaa,

wakakimbia kwa hofu.

6 Kutetemeka kuliwashika huko,

maumivu kama ya mwanamke

mwenye utungu wa kuzaa.

7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi

zilizovunjwa na upepo wa mashariki.

8 Kama tulivyokuwa tumesikia,

ndivyo tulivyoona

katika mji waBwanaMwenye Nguvu Zote,

katika mji wa Mungu wetu:

Mungu ataufanya uwe salama milele.

9 Ee Mungu, hekaluni mwako

tunatafakari upendo wako usiokoma.

10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo,

sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia,

Mkono wako wa kuume umejazwa na haki.

11 Mlima Sayuni unashangilia,

vijiji vya Yuda vinafurahi

kwa sababu ya hukumu zako.

12 Tembeeni katika Sayuni,

uzungukeni mji,

hesabuni minara yake.

13 Yatafakarini vyema maboma yake,

angalieni ngome zake,

ili mpate kusimulia habari zake

kwa kizazi kijacho.

14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu

milele na milele;

atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/48-e221b6e7706605fa6c85745014786c40.mp3?version_id=1627—

Zaburi 49

Upumbavu Wa Kutegemea Mali

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora)

1 Sikieni haya, enyi mataifa yote,

sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.

2 Wakubwa kwa wadogo,

matajiri na maskini pamoja:

3 Kinywa changu kitasema maneno ya hekima,

usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.

4 Nitatega sikio langu nisikilize mithali,

nitafafanua kitendawili kwa zeze:

5 Kwa nini niogope siku mbaya zinapokuja,

wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,

6 wale wanaotegemea mali zao

na kujivunia utajiri wao mwingi?

7 Hakuna mwanadamu awaye yote

awezaye kuukomboa uhai wa mwingine,

au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.

8 Fidia ya uhai ni gharama kubwa,

hakuna malipo yo yote yanayotosha,

9 ili kwamba aishi milele

na asione uharibifu.

10 Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa;

wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia

na kuwaachia wengine mali zao.

11 Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele,

makao yao vizazi vyote;

ingawa walikuwa na mashamba

na kuyaita kwa majina yao.

12 Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu;

anafanana na mnyama aangamiaye.

13 Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe,

pia wa wafuasi wao,

waliothibitisha misemo yao.

14 Kama kondoo wamewekewa kwenda kaburini

na kifo kitawala.

Wanyofu watawatawala asubuhi,

maumbile yao yataozea kaburini,

mbali na majumba yao makubwa ya fahari.

15 Lakini Mungu atakomboa uhaiwangu na kaburi,

hakika atanichukua kwake.

16 Usitishwe mtu anapotajirika,

fahari ya nyumba yake inapoongezeka,

17 kwa maana hatachukua cho chote atakapokufa,

fahari yake haitashuka pamoja naye.

18 Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri,

na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa,

19 atajiunga na kizazi cha baba zake,

ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.

20 Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu

ni kama wanyama waangamiao.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/49-4c002caae8dd81754a149ad4bb43413d.mp3?version_id=1627—