Zaburi 70

Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Maombolezo)

1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa,

EeBwana, njoo hima unisaidie.

2 Waaibike na kufedheheshwa

wale wanaotafuta uhai wangu;

wale wanaotamani kuangamizwa kwangu

warudishwe nyuma kwa aibu.

3 Wale waniambiao, “Aha! Aha!”

warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4 Lakini wote wakutafutao

na washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako daima na waseme,

“Mungu na atukuzwe!”

5 Hata sasa mimi ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

EeBwana, usikawie.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/70-098f2b592afdfeb0c290fdafa03c8c88.mp3?version_id=1627—

Zaburi 71

Kuomba Ulinzi Na Msaada Siku Zote Za Maisha

1 EeBwana, nimekukimbilia wewe,

usiniache nikaaibika kamwe.

2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa,

unitegee sikio lako uniokoe.

3 Uwe mwamba wa kimbilio langu,

mahali nitakapokimbilia kila wakati;

toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe

ni mwamba wangu

na ngome yangu.

4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu,

kutoka kwenye makucha

ya watu wabaya na wakatili.

5 EeBwanaMwenyezi, kwa kuwa umekuwa tumaini langu,

tegemeo langu tangu ujana wangu.

6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,

ulinitoa tumboni mwa mama yangu.

Nitakusifu wewe daima.

7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi,

lakini wewe ni kimbilio langu imara.

8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako,

nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.

9 Usinitupe wakati wa uzee,

wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.

10 Kwa maana adui zangu wananisengenya,

wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.

11 Wanasema, “Mungu amemwacha,

mkimbilieni mumkamate,

kwani hakuna wa kumwokoa.”

12 Ee Mungu, usiwe mbali nami,

Ee Mungu wangu njoo haraka kunisaidia.

13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu,

wale wanaotaka kunidhuru

na wafunikwe kwa dharau na fedheha.

14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote,

nitakusifu zaidi na zaidi.

15 Kinywa changu kitasimulia haki yako,

wokovu wako mchana kutwa,

ingawa sifahamu kipimo chake.

16 EeBwanaMwenyezi, nitakuja

na kutangaza matendo yako makuu,

nitatangaza haki yako, yako peke yako.

17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,

hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.

18 Ee Mungu, usiniache,

hata niwapo mzee wa mvi,

mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho,

nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.

19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu,

wewe ambaye umefanya mambo makuu.

Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?

20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu,

utanihuisha tena,

kutoka vilindi vya dunia

utaniinua tena.

21 Utaongeza heshima yangu

na kunifariji tena.

22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi

kwa ajili ya uaminifu wako;

Ee Mtakatifu Pekee wa Israeli,

nitakuimbia sifa kwa zeze.

23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha

ninapokuimbia sifa,

mimi, ambaye umenikomboa.

24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki

mchana kutwa,

kwa maana wale waliotaka kunidhuru,

wameaibishwa na kufadhaishwa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/71-149ba03c6f364dd403de2bd6907a5c88.mp3?version_id=1627—

Zaburi 72

Maombi Kwa Ajili Ya Mfalme

(Zaburi Ya Solomoni)

1 Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako,

mwana wa kifalme kwa haki yako.

2 Atawaamua watu wako kwa haki,

watu wako walioonewa kwa haki.

3 Milima italeta mafanikio kwa watu,

vilima tunda la haki.

4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu

na atawaokoa watoto wa wahitaji,

ataponda mdhalimu.

5 Atadumu kama jua, kama mwezi,

vizazi vyote.

6 Atakuwa kama mvua inyeshayo

juu ya shamba lililofyekwa,

kama manyunyu yanyeshayo ardhi.

7 Katika siku zake wenye haki watastawi;

mafanikio yatakuwepo

mpaka mwezi utakapokoma.

8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari

# na kutoka Mtompaka miisho ya dunia.

9 Makabila ya jangwani watamsujudia,

na adui zake wataramba mavumbi.

10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali

watamletea kodi;

wafalme wa Sheba na Seba

watampa zawadi.

11 Wafalme wote watamsujudia

na mataifa yote yatamtumikia.

12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia,

aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.

13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji

na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.

14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili,

kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.

15 Aishi maisha marefu!

Dhahabu ya Sheba na apewe.

Watu na wamwombee daima

na kumbariki mchana kutwa.

16 Nafaka ijae tele katika nchi yote,

juu ya vilele vya vilima na istawi.

Tunda lake na listawi kama Lebanoni,

listawi kama majani ya kondeni.

17 Jina lake na lidumu milele,

na lidumu kama jua.

Mataifa yote yatabarikiwa kupitia yeye,

nao watamwita mbarikiwa.

18 BwanaMungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa,

yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.

19 Jina lake tukufu lisifiwe milele,

ulimwengu wote ujae utukufu wake.

Amen na Amen.

20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/72-abe08fca07014b184f67512ba27e742f.mp3?version_id=1627—

Zaburi 73

Haki Ya Mungu

(Zaburi Ya Asafu)

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli,

kwa wale ambao mioyo yao ni safi.

2 Bali kwangu mimi, miguu yangu

ilikuwa karibu kuteleza;

nilikuwa karibu mguu wangu

kuachia uliposimama.

3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna

nilipoona kufanikiwa kwa waovu.

4 Wao hawana taabu,

miili yao ina afya na nguvu.

5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine,

wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.

6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao,

wamejivika jeuri.

7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi,

ubaya wa majivuno kutoka mioyoni mwao

hauna kikomo.

8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi,

katika majivuno yao wanatishia kutesa.

9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu,

nazo ndimi zao humiliki duniani.

10 Kwa hiyo watu wao huwageukia

# na kunywa maji tele.

11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua?

Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”

12 Hivi ndivyo walivyo waovu:

siku zote hawajali,

wanaongezeka katika utajiri.

13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure,

ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.

14 Mchana kutwa nimetaabika,

nimeadhibiwa kila asubuhi.

15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,”

ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

16 Nilipojaribu kuelewa haya yote,

yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

17 Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu,

ndipo nilipotambua mwisho wao.

18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi,

unawaangusha chini kwa uharibifu.

19 Tazama ni jinsi gani wanavyoangamizwa ghafula,

wanatoweshwa kabisa na vitisho!

20 Kama ndoto mtu aamkapo,

hivyo wakati uinukapo, EeBwana,

utawatowesha kama ndoto.

21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa,

na roho yangu ilipotiwa uchungu,

22 nilikuwa mpumbavu na mjinga,

nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote,

umenishika mkono wangu wa kuume.

24 Unaniongoza kwa shauri lako,

hatimaye utaniingiza katika utukufu.

25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe?

Dunia haina cho chote ninachokitamani ila wewe.

26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa,

bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu

na fungu langu milele.

27 Wale walio mbali nawe wataangamia,

unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

28 Lakini kwangu mimi,

ni vyema kuwa karibu na Mungu.

NimemfanyaBwanaMwenyezi kimbilio langu;

nami nitayasimulia matendo yako yote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/73-ab948d2191334554d6a119482f5bea6c.mp3?version_id=1627—

Zaburi 74

Maombi Kwa Ajili Ya Taifa Kuokolewa

(Utenzi Wa Asafu)

1 Ee Mungu, mbona umetukataa milele?

Mbona hasira yako inawaka na kutoka moshi

juu ya kondoo wa malisho yako?

2 Kumbuka watu uliowanunua zamani,

kabila la urithi wako, ambao uliwakomboa:

Mlima Sayuni, ambamo uliishi.

3 Geuza hatua zako kuelekea magofu haya ya kudumu,

uharibifu wote huu ambao adui ameuleta

katika mahali patakatifu.

4 Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi,

wanaweka bendera zao kama alama.

5 Walifanya kama watu wanaotumia mashoka

kukata kichaka chote cha miti.

6 Walivunjavunja milango yote iliyonakishiwa

kwa mashoka na vishoka vyao.

7 Waliteketeza kabisa mahali patakatifu,

wakayanajisi makao ya Jina lako.

8 Walisema mioyoni mwao,

“Tutawaponda kabisa!”

Walichoma kila mahali ambapo Mungu

aliabudiwa katika nchi.

9 Hatukupewa ishara za miujiza;

hakuna manabii waliobaki,

hakuna ye yote kati yetu ajuaye

kwamba hali hii itachukua muda gani.

10 Ee Mungu, mtesi atakudhihaki mpaka lini?

Je, adui watalitukana jina lako milele?

11 Kwa nini unazuia mkono wako,

mkono wako wa kuume?

Uutoe kutoka katika makunjo ya vazi lako

na uwaangamize!

12 Lakini wewe, Ee Mungu,

ni mfalme wangu tangu zamani,

unaleta wokovu duniani.

13 Ni wewe uliyeigawanya bahari kwa uweza wako;

ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa kutisha katika maji.

14 Ni wewe uliyeponda vichwa vya Lewiathani

nawe ukamtoa kama chakula

cha viumbe vya jangwani.

15 Ni wewe uliyefungua chemchemi na vijito,

ulikausha mito ambayo ilikuwa ikitiririka daima.

16 Mchana ni wako, nao usiku ni wako pia,

uliweka jua na mwezi.

17 Ni wewe uliyeiweka mipaka yote ya dunia,

ulifanya kiangazi na masika.

18 EeBwana, kumbuka jinsi mtesi alivyokudhihaki,

jinsi watu wapumbavu walivyolitukana jina lako.

19 Usiukabidhi uhai wa njiwa wako

kwa wanyama wakali wa mwitu;

usisahau kabisa uhai wa watu wako

wanaoteseka milele.

20 Likumbuke agano lako,

maana mara kwa mara mambo ya jeuri

yamejaa katika sehemu za giza katika nchi.

21 Usiruhusu walioonewa warudi nyuma kwa aibu;

maskini na wahitaji na walisifu jina lako.

22 Inuka, Ee Mungu, ujitetee;

kumbuka jinsi wapumbavu

wanavyokudhihaki mchana kutwa.

23 Usipuuze makelele ya watesi wako,

ghasia za adui zako,

zinazoinuka mfululizo.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/74-ecd31c4f04e9b5de7d636b79495e0199.mp3?version_id=1627—

Zaburi 75

Mungu Ni Mwamuzi

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Uimbaji Za Nyuzi. Zaburi Ya Asafu. Wimbo)

1 Ee Mungu, tunakushukuru,

tunakushukuru wewe,

kwa kuwa jina lako li karibu;

watu husimulia matendo yako ya ajabu.

2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum;

ni mimi nihukumuye kwa haki.

3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka,

ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.

4 Kwa wale wenye majivuno ninasema,

‘Msijisifu tena’,

kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.

5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu;

msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’ ”

6 Hakuna ye yote atokaye mashariki wala magharibi

au kutoka jangwani

awezaye kumkweza mwanadamu.

7 Bali Mungu ndiye ahukumuye:

Humshusha huyu na kumkweza mwingine.

8 Mkononi mwaBwanakuna kikombe

kilichojaa mvinyo unaotoka povu

uliochanganywa na vikolezo;

huumimina, nao waovu wote wa dunia

hunywa mpaka tone la mwisho.

9 Bali mimi, nitatangaza hili milele;

nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.

10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote,

bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/75-7aff16755558c333f90a5afc2d18b118.mp3?version_id=1627—

Zaburi 76

Mungu Wa Israeli Ni Mhukumu Wa Dunia Yote

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Zaburi Ya Asafu. Wimbo)

1 Katika Yuda Mungu anajulikana,

jina lake ni kuu katika Israeli.

2 Hema lake liko Salemu,

makao yake katika Sayuni.

3 Huko alivunja mishale imetametayo,

ngao na panga, silaha za vita.

4 Wewe unang’aa kwa mwanga,

mwenye fahari zaidi ya milima

yenye utajiri wa wanyama pori.

5 Mashujaa hulala wametekwa nyara,

hulala usingizi wao wa mwisho;

hakuna hata mmoja wa watu wa vita

anayeweza kuinua mikono yake.

6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo,

farasi na gari la vita vilikaa kimya.

7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa.

Ni nani awezaye kusimama mbele yako

wakati umekasirika?

8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu,

nayo nchi ikaogopa ikawa kimya,

9 wakati wewe, Ee Mungu,

ulipoinuka kuhukumu,

kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.

10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu

inakuletea sifa,

na masalia ya ghadhabu yako

utajifunga mshipi.

11 Wekeni nadhiri kwaBwanaMungu wenu na kuzitimiza;

nchi zote za jirani na walete zawadi

kwa yeye astahiliye kuogopwa.

12 Huvunja roho za watawala;

anaogopwa na wafalme wa dunia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/76-0310f348750f1c41b2c81d2903b2e953.mp3?version_id=1627—

Zaburi 77

Matendo Makuu Ya Mungu Yanakumbukwa

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Yeduthuni. Zaburi Ya Asafu)

1 Nilimlilia Mungu ili anisaidie,

nilimlilia Mungu ili anisikie.

2 Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana,

usiku nilinyosha mikono bila kuchoka

na nafsi yangu ilikataa kufarijiwa.

3 Ee Mungu, nilikukumbuka wewe, nililia kwa huzuni;

nikatafakari, roho yangu ikadhoofika.

4 Ulizuia macho yangu kufumba;

nilikuwa nasumbuka

kiasi cha kushindwa kusema.

5 Nilitafakari juu ya siku zilizopita,

miaka mingi iliyopita,

6 Usiku nilizikumbuka nyimbo zangu.

Moyo wangu ulitafakari

na roho yangu ikauliza:

7 “Je, Bwana atakataa milele?

Je, hatatenda mema tena?

8 Je, upendo wake usio na mwisho umetoweka milele?

Je, ahadi yake imekoma nyakati zote?

9 Je, Mungu amesahau kuwa na huruma?

Je, yeye katika hasira yake

amezuia huruma yake?”

10 Ndipo nikawaza, “Huu ndio udhaifu wangu:

lakini nitakumbuka

miaka ya mkono wa kuume

wa Aliye Juu Sana.”

11 Nitayakumbuka matendo yaBwana;

naam, nitaikumbuka miujiza yako ya zamani.

12 Nitazitafakari kazi zako zote

na kuyawaza matendo yako makuu.

13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu.

Ni mungu yupi aliye mkuu kama Mungu wetu?

14 Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza,

umeonyesha uwezo wako katikati ya mataifa.

15 Kwa mkono wako wenye nguvu

umewakomboa watu wako,

uzao wa Yakobo na Yosefu.

16 Maji yalikuona, Ee Mungu,

maji yalikuona yakakimbia,

vilindi vilitetemeka.

17 Mawingu yalimwaga maji,

mbingu zikatoa ngurumo kwa radi,

mishale yako ikametameta huku na huko.

18 Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli,

umeme wako wa radi ukaangaza dunia,

dunia ikatetemeka na kutikisika.

19 Njia yako ilipita baharini,

mapito yako kwenye maji makuu,

ingawa nyayo zako hazikuonekana.

20 Uliongoza watu wako kama kundi

kwa mkono wa Mose na Aroni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/77-92567aad6c2595bb9449a6d396229bf2.mp3?version_id=1627—

Zaburi 78

Mungu Na Watu Wake

(Utenzi Wa Asafu)

1 Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,

sikilizeni maneno ya kinywa changu.

2 Nitafumbua kinywa changu kwa mafumbo,

nitazungumza mambo yaliyofichika,

mambo ya kale:

3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,

yale ambayo baba zetu walituambia.

4 Hatutayaficha kwa watoto wao;

tutakiambia kizazi kijacho

matendo yastahiliyo sifa yaBwana,

uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.

5 Aliagiza amri kwa Yakobo

na akaweka sheria katika Israeli,

ambazo aliwaamuru baba zetu

wawafundishe watoto wao,

6 ili kizazi kijacho kizijue,

pamoja na watoto ambao watazaliwa,

nao pia kwa wakati wao wapate kuwaeleza watoto wao.

7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,

nao wasingesahau matendo yake,

bali wangalizishika amri zake.

8 Ili kwamba wasifanane na baba zao,

waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,

ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,

ambao roho zao hazikumwamini yeye.

9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde,

walikimbia siku ya vita,

10 Hawakulishika Agano la Mungu

na walikataa kuishi kwa sheria yake.

11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda,

maajabu aliyokuwa amewaonyesha.

12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao,

huko Soani, katika nchi ya Misri.

13 Aliigawanya bahari akawaongoza wakapita,

alifanya maji yasimame imara kama ukuta.

14 Aliwaongoza kwa wingu mchana

na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.

15 Alipasua miamba jangwani

na akawapa maji tele kama bahari,

16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka,

akayafanya maji yatiririke kama mito.

17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake,

wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.

18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu,

wakidai vyakula walivyovitamani.

19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema,

“Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?

20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu,

vijito vikatiririka maji mengi.

Lakini je, aweza kutupa chakula pia?

Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”

21 Bwanaalipowasikia,

alikasirika sana,

moto wake ukawa dhidi ya Yakobo,

na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,

22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu,

wala kuutumainia ukombozi wake.

23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu

na kufungua milango ya mbingu,

24 akawanyeshea mana ili watu wale,

aliwapa nafaka ya mbinguni.

25 Watu walikula mkate wa malaika,

aliwatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.

26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu

na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.

27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi,

ndege warukao kama mchanga wa pwani.

28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao,

kuzunguka mahema yao yote.

29 Walikula na kusaza,

kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.

30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani,

hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,

31 hasira ya Mungu iliwaka juu yao,

akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao,

akiwaangusha vijana wa Israeli.

32 Licha ya haya yote,

waliendelea kutenda dhambi,

licha ya maajabu yake,

hawakuamini.

33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili

na miaka yao katika vitisho.

34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao,

waliosalia walimtafuta,

walimgeukia tena kwa shauku.

35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,

kwamba Mungu Aliye Juu Sana

alikuwa Mkombozi wao.

36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao,

wakisema uongo kwa ndimi zao,

37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake,

wala hawakuwa waaminifu katika Agano lake.

38 Hata hivyo alikuwa na huruma,

alisamehe maovu yao

na hakuwaangamiza.

Mara kwa mara alizuia hasira yake

wala hakuchochea ghadhabu yake yote.

39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu,

upepo upitao ambao haurudi.

40 Mara ngapi walimwasi jangwani

na kumhuzunisha nyikani!

41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara,

walimkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

42 Hawakukumbuka uwezo wake,

siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,

43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri,

maajabu yake huko Soani.

44 Aligeuza mito yao kuwa damu,

hawakuweza kunywa maji

kutoka kwenye vijito vyao.

45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala,

na vyura wakawaharibu.

46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao,

mazao yao kwa nzige.

47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe

na mikuyu yao kwa mvua

iliyochangamana na theluji.

48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe,

akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.

49 Aliwafungulia hasira yake kali,

ghadhabu yake, hasira na uadui,

na kundi la malaika wa kuharibu.

50 Aliitengenezea njia hasira yake,

hakuwaepusha na kifo bali aliwaachia tauni.

51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,

matunda ya kwanza ya ujana

katika mahema ya Hamu.

52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi,

aliwaongoza kama kondoo kupitia jangwani.

53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa,

bali bahari iliwameza adui zao.

54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka

wa nchi yake takatifu,

hadi kwenye nchi ya vilima

ambayo mkono wake wa kuume

ulikuwa umeitwaa.

55 Aliyafukuza mataifa mbele yao,

na kuwagawia nchi zao kama urithi,

aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.

56 Lakini wao walimjaribu Mungu

na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana,

wala hawakuzishika sheria zake.

57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu,

wakawa wasioweza kutegemewa

kama upinde wenye kasoro.

58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu,

walichochea wivu wake kwa sanamu zao.

59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana,

akamkataa Israeli kabisa.

60 Akaiacha hema ya Shilo,

hema aliyokuwa ameiweka

katikati ya wanadamu.

61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani,

utukufu wake mikononi mwa adui.

62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga,

akaukasirikia sana urithi wake.

63 Moto uliwaangamiza vijana wao,

na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

64 makuhani wao waliuawa kwa upanga,

wala wajane wao hawakuweza kulia.

65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini,

kama vile mtu aamkavyo

kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.

66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake,

akawatia katika aibu ya milele.

67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu,

hakulichagua kabila la Efraimu,

68 lakini alilichagua kabila la Yuda,

Mlima Sayuni, ambao aliupenda.

69 Alijenga mahali patakatifu pake kama vilele,

kama dunia ambayo aliimarisha milele.

70 Akamchagua Daudi mtumishi wake

na kumtoa kutoka kwenye mazizi ya kondoo,

71 kutoka kuchunga kondoo alimleta

kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo,

na Israeli urithi wake.

72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo,

kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/78-1189d6dae5fa0f6dc31378469c577047.mp3?version_id=1627—

Zaburi 79

Maombi Kwa Ajili Ya Wokovu Wa Taifa

(Zaburi Ya Asafu)

1 Ee Mungu, mataifa yameuvamia urithi wako,

wamelinajisi Hekalu lako takatifu,

wameifanya Yerusalemu kuwa magofu.

2 Wametoa maiti za watumishi

kuwa chakula cha ndege wa angani

na nyama ya watakatifu wako

kwa wanyama wa nchi.

3 Wamemwaga damu kama maji

kuzunguka Yerusalemu yote,

wala hakuna ye yote wa kuwazika.

4 Tumekuwa kitu cha aibu kwa jirani zetu,

cha dharau na mzaha

kwa wale wanaotuzunguka.

5 Hata lini, EeBwana?

Je, wewe utakasirika milele?

Wivu wako utawaka kama moto hadi lini?

6 Mwaga ghadhabu yako kwa mataifa yasiyokukubali,

juu ya falme za hao wasioliitia jina lako,

7 kwa maana wamemrarua Yakobo

na kuharibu nchi ya makao yake.

8 Usituhesabie dhambi za baba zetu,

huruma yako na itujie hima,

kwa maana tu wahitaji mno.

9 Ee Mungu Mwokozi wetu, utusaidie,

kwa ajili ya utukufu wa jina lako;

tuokoe na kutusamehe dhambi zetu

kwa ajili ya jina lako.

10 Kwa nini mataifa waseme,

“Yuko wapi Mungu wenu?”

Mbele ya macho yetu,

dhihirisha kati ya mataifa

kwamba unalipiza kisasi

cha damu iliyomwagwa

ya watumishi wako.

11 Kilio cha huzuni cha wafungwa kifike mbele zako;

kwa nguvu za mkono wako

hifadhi wale waliohukumiwa kufa.

12 Walipize jirani zetu mara saba vifuani mwao

aibu walizovurumisha juu yako, EeBwana.

13 Ndipo sisi watu wako, kondoo wa malisho yako,

tutakusifu milele;

toka kizazi hadi kizazi

tutasimulia sifa zako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/79-be3042ef5e97803f3fb6e99253d7d312.mp3?version_id=1627—