Zaburi 90

Umilele Wa Mungu Na Udhaifu Wa Mwanadamu

(Maombi Ya Mose, Mtu Wa Mungu)

1 Bwana, wewe umekuwa makao yetu

katika vizazi vyote.

2 Kabla ya kuzaliwa milima

au hujaumba dunia na ulimwengu,

wewe ni Mungu tangu milele hata milele.

3 Huwarudisha watu mavumbini,

ukisema, “Rudini mavumbini,

enyi wanadamu.”

4 Kwa maana kwako miaka elfu

ni kama siku moja iliyokwisha pita,

au kama kesha la usiku.

5 Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo,

nao ni kama majani machanga ya asubuhi,

6 ingawa asubuhi yanachipua,

ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.

7 Tumeangamizwa kwa hasira yako

na tumetishwa kwa ghadhabu yako.

8 Umeyaweka maovu yetu mbele yako,

dhambi zetu za sirini katika nuru ya uwepo wako.

9 Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako,

tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza.

10 Siku zetu za kuishi ni miaka sabini,

ikiwa tuna nguvu ni miaka themanini,

lakini yote ni ya shida na taabu,

nazo zapita haraka, nasi twatoweka.

11 Ni nani ajuaye nguvu za hasira yako?

Kwa maana ghadhabu yako ni kubwa

kama hofu tunayopaswa kuwa nayo kwako.

12 Tufundishe kuzihesabu siku zetu vizuri,

ili tujipatie moyo wa hekima.

13 EeBwana, uwe na huruma! Utakawia hata lini?

Wahurumie watumishi wako.

14 Asubuhi tushibishe upendo wako usiokoma,

ili tuweze kuimba kwa shangwe

na kufurahi siku zetu zote.

15 Utufurahishe kulingana na siku ulizotuadhibu,

kulingana na miaka tuliyotaabika.

16 Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako,

utukufu wako kwa watoto wao.

17 Wema waBwanaMungu wetu, uwe juu yetu;

uzithibitishe kazi za mikono yetu:

naam, uzithibitishe kazi za mikono yetu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/90-150d8cdc999650290c1142b4dce37179.mp3?version_id=1627—

Zaburi 91

Mungu Mlinzi Wetu

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,

# atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.

2 Nitasema kuhusuBwana, “Yeye ndiye

kimbilio langu na ngome yangu,

Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”

3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji

na maradhi ya kuambukiza ya kuua.

4 Atakufunika kwa manyoya yake,

chini ya mbawa zake utapata kimbilio,

uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.

5 Hutaogopa vitisho vya usiku,

wala mshale urukao mchana,

6 wala maradhi ya kuambukiza

yanayonyemelea gizani,

wala tauni iharibuyo adhuhuri.

7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako,

kumi elfu mkono wako wa kuume,

lakini haitakukaribia wewe.

8 Utatazama tu kwa macho yako

na kuona adhabu ya waovu.

9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako:

naam,Bwanaambaye ni kimbilio langu;

10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe,

wala maafa hayataikaribia hema yako.

11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako,

wakulinde katika njia zako zote.

12 Mikononi mwao watakuinua,

ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.

13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali,

simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.

14 Bwanaasema, “Kwa kuwa ananipenda

nitamwokoa;

nitamlinda kwa kuwa amelikubali Jina langu.

15 Ataniita, nami nitamjibu;

nitakuwa pamoja naye katika taabu,

nitamwokoa na kumheshimu.

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha

na kumwonyesha wokovu wangu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/91-1e8eb4d06957f2222bb9adcc5be6fad7.mp3?version_id=1627—

Zaburi 92

Wimbo Wa Kumsifu Mungu

(Zaburi: Wimbo Wa Sabato)

1 Ni vyema kumshukuruBwana

na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,

2 kuutangaza upendo wako asubuhi,

uaminifu wako wakati wa usiku,

3 kwa zeze yenye nyuzi kumi

na kwa sauti ya kinubi.

4 EeBwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha,

nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.

5 EeBwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako,

tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!

6 Mjinga hafahamu,

mpumbavu haelewi,

7 ingawa waovu huchipua kama majani

na wote watendao mabaya wanastawi,

wataangamizwa milele.

8 Bali wewe, EeBwana,

utatukuzwa milele.

9 EeBwana, hakika adui zako,

hakika adui zako wataangamia,

wote watendao mabaya watatawanyika.

10 Umeitukuza pembeyangu kama ile ya nyati dume,

mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.

11 Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa,

masikio yangu yamesikia

maangamizi ya adui zangu waovu.

12 Wenye haki watastawi kama mtende,

watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,

13 waliopandwa katika nyumba yaBwana,

watastawi katika nyua za Mungu wetu.

14 Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda,

watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,

15 wakitangaza, “Bwanani mkamilifu;

yeye ni Mwamba wangu,

na ndani yake hamna uovu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/92-abcb2c0bcc4264747d396a7aa8baa9d6.mp3?version_id=1627—

Zaburi 93

Mungu Mfalme

1 Bwanaanatawala, amejivika utukufu;

Bwanaamejivika utukufu

tena amejivika nguvu.

Dunia imewekwa imara,

haitaondoshwa.

2 Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani;

wewe umekuwako tangu milele.

3 Bahari zimeinua, EeBwana,

bahari zimeinua sauti zake;

bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.

4 Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu,

ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari:

Bwanaaishiye juu sana ni mkuu.

5 EeBwana, sheria zako ni imara;

utakatifu umepamba nyumba yako

pasipo mwisho.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/93-cf07080b63ce6141768c12b426ba7404.mp3?version_id=1627—

Zaburi 94

Mungu Mlipiza Kisasi Kwa Ajili Ya Wenye Haki

1 EeBwana, ulipizaye kisasi,

Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.

2 Ee mhukumu wa dunia, inuka,

uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.

3 Hata lini, waovu, EeBwana,

hata lini waovu watashangilia?

4 Wanamimina maneno ya kiburi,

watenda mabaya wote wamejaa majivuno.

5 EeBwana, wanawaponda watu wako,

wanawaonea urithi wako.

6 Wanamchinja mjane na mgeni,

na kuwaua yatima.

7 Nao husema, “Bwanahaoni,

Mungu wa Yakobo hafahamu.”

8 Sikia, enyi wajinga miongoni mwa watu,

enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?

9 Je, aliyeweka sikio asisikie?

Aliyeumba jicho asione?

10 Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu?

Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?

11 Bwanaanajua mawazo ya mwanadamu,

anajua ya kwamba hayafai.

12 EeBwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe,

mtu unayemfundisha kwa sheria yako,

13 unampa utulivu siku za shida,

mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa

kwa ajili ya mwovu.

14 Kwa kuwaBwanahatawakataa watu wake,

hatauacha urithi wake.

15 Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki,

wote walio na mioyo minyofu wataifuata.

16 Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu?

Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu?

17 KamaBwanaasingelinisaidia upesi,

ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.

18 Niliposema, “Mguu wangu unateleza,”

EeBwana, upendo wako ulinishikilia.

19 Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu,

faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.

20 Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe,

ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake?

21 Huungana kuwashambulia wenye haki,

kuwahukumu kufa wasio na hatia.

22 LakiniBwanaamekuwa ngome yangu,

na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia.

23 Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao

na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao;

BwanaMungu wetu atawaangamiza.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/94-46bff0cdadad6fa6cc848420a248fdf9.mp3?version_id=1627—

Zaburi 95

Wimbo Wa Kumsifu Mungu

1 Njoni, tumwimbieBwanakwa furaha;

tumfanyie kelele za shangwe

Mwamba wa wokovu wetu.

2 Tuje mbele zake kwa shukrani,

tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.

3 Kwa kuwaBwanani Mungu mkuu,

mfalme mkuu juu ya miungu yote.

4 Mkononi mwake mna vilindi vya dunia

na vilele vya milima ni mali yake.

5 Bahari ni yake, kwani ndiye aliyeifanya,

na mikono yake iliumba nchi kavu.

6 Njoni, tusujudu tumwabudu,

tupige magoti mbele zaBwanaMuumba wetu,

7 kwa maana yeye ndiye Mungu wetu

na sisi ni watu wa malisho yake,

kondoo chini ya utunzaji wake.

Kama mkiisikia sauti yake, leo,

8 msiifanye migumu mioyo yenu

# kama mlivyofanya kule Meriba,

kama mlivyofanya siku ile

# kule Masajangwani,

9 ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima,

ingawa walikuwa wameyaona niliyoyafanya.

10 Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile,

nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka,

nao hawajazifahamu njia zangu.”

11 Kwa hiyo nikaapa katika hasira yangu,

“Kamwe hawataingia rahani mwangu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/95-8b88b1c01eacb1139a02594f1d7bf3b8.mp3?version_id=1627—

Zaburi 96

Mungu Mfalme Mkuu

1 MwimbieniBwanawimbo mpya;

mwimbieniBwanadunia yote.

2 MwimbieniBwana, lisifuni jina lake;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu

miongoni mwa mataifa yote.

4 Kwa kuwaBwanani mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakiniBwanaaliziumba mbingu.

6 Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

7 MpeniBwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeniBwanautukufu na nguvu.

8 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;

leteni sadaka na mje katika nyua zake.

9 MwabuduniBwanakatika uzuri wa utakatifu wake;

dunia yote na itetemeke mbele zake.

10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwanaanatawala.”

Ulimwengu ameuweka imara

hauwezi kusogezwa,

atawahukumu mataifa kwa uadilifu.

11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

bahari na ivume,

na vyote vilivyomo ndani yake;

12 mashamba na yashangilie,

pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.

Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha,

13 vitaimba mbele zaBwana

kwa maana anakuja,

anakuja kuhukumu dunia.

Ataihukumu dunia kwa haki

na mataifa katika kweli yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/96-a54c28136746e51ea86d1c4f8707af2d.mp3?version_id=1627—

Zaburi 97

Mungu Mtawala Mkuu

1 Bwanaanatawala, nchi na ifurahi,

visiwa vyote vishangilie.

2 Mawingu na giza nene vinamzunguka,

haki na hukumu ndio msingi

wa kiti chake cha enzi.

3 Moto hutangulia mbele zake

na huteketeza adui zake pande zote.

4 Umeme wake wa radi humulika dunia,

nchi huona na kutetemeka.

5 Milima huyeyuka kama nta mbele zaBwana,

mbele za Bwana wa dunia yote.

6 Mbingu zinatangaza haki yake,

na mataifa yote huona utukufu wake.

7 Wote waabuduo sanamu waaibishwe,

wale wajisifiao sanamu:

mwabuduni yeye, enyi miungu yote!

8 Sayuni husikia na kushangilia,

vijiji vya Yuda vinafurahi

kwa sababu ya hukumu zako, EeBwana.

9 Kwa kuwa wewe, EeBwana,

ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote;

umetukuka sana juu ya miungu yote.

10 Wale wanaompendaBwanana wauchukie uovu,

kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake

na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu.

11 Nuru huangaza wenye haki

na furaha kwa watu wanyofu wa moyo.

12 Furahini katikaBwana, ninyi mlio wenye haki,

lisifuni jina lake takatifu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/97-31c80bbda1a8cd4bd7bfb2719c9c1c1c.mp3?version_id=1627—

Zaburi 98

Mungu Mtawala Wa Dunia

1 MwimbieniBwanawimbo mpya,

kwa maana ametenda mambo ya ajabu;

kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu

umemfanyia wokovu.

2 Bwanaameufanya wokovu wake ujulikane

na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.

3 Ameukumbuka upendo wake

na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli;

miisho yote ya dunia imeuona

wokovu wa Mungu wetu.

4 Mpigieni kelele za shangwe, dunia yote,

ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;

5 mwimbieniBwanakwa kinubi,

kwa kinubi na sauti za kuimba,

6 kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu

za pembe za kondoo dume:

shangilieni kwa furaha mbele zaBwana,

aliye Mfalme.

7 Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake,

dunia na wote wakaao ndani yake.

8 Mito na ipige makofi,

milima na iimbe pamoja kwa furaha,

9 vyote na viimbe mbele zaBwana,

kwa maana yuaja kuhukumu dunia.

Atahukumu dunia kwa haki

na mataifa kwa haki.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/98-7163a39f7828c4519ba46a2a4ee3a38a.mp3?version_id=1627—

Zaburi 99

Mungu Mfalme Mkuu

1 Bwanaanatawala,

mataifa na yatetemeke;

anaketi kwenye kiti cha enzi katikati ya makerubi,

dunia na itikisike.

2 Bwanani mkuu katika Sayuni;

ametukuzwa juu ya mataifa yote.

3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:

yeye ni mtakatifu!

4 Mfalme mwenye nguvu hupenda haki,

wewe umethibitisha adili;

katika Yakobo umefanya

yaliyo haki na sawa.

5 MtukuzeniBwanaMungu wetu,

na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;

yeye ni mtakatifu.

6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,

Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;

walimwita naye aliwajibu.

7 Alizungumza nao kutoka katika nguzo ya wingu;

walizishika sheria zake na amri alizowapa.

8 EeBwana, wetu,

ndiwe uliyewajibu,

kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

9 MtukuzeniBwanaMungu wetu

na mwabudu kwenye mlima wake mtakatifu,

kwa maanaBwanaMungu wetu ni mtakatifu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/99-11d9d4ae955a940aed5492da831339ad.mp3?version_id=1627—