Zaburi 100

Dunia Yote Yaitwa Kumsifu Mungu

(Zaburi Ya Shukrani)

1 MpigieniBwanakelele za shangwe,

dunia yote.

2 MwabuduniBwanakwa furaha;

njoni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.

3 Jueni kwambaBwanandiye Mungu.

Yeye ndiye aliyetuumba,

sisi tu mali yake;

sisi tu watu wake,

kondoo wa malisho yake.

4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani

na katika nyua zake kwa kusifu,

mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.

5 Kwa maanaBwanani mwema

na upendo wake wadumu milele;

uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/100-eff14a40452cabadf74ec057d9d8d961.mp3?version_id=1627—

Zaburi 101

Ahadi Ya Kuishi Kwa Uadilifu Na Kwa Haki

(Zaburi Ya Daudi)

1 Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako;

kwako wewe, EeBwana,

nitaimba sifa.

2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama:

utakuja kwangu lini?

Nitatembea nyumbani mwangu

kwa moyo usio na lawama.

3 Sitaweka mbele ya macho yangu

kitu kiovu.

Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani;

hawatashikamana nami.

4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami;

nitajitenga na kila ubaya.

5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri,

huyo nitamnyamazisha;

mwenye macho ya dharau

na moyo wa kiburi sitamvumilia.

6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,

ili waweze kuishi pamoja nami;

yeye ambaye moyo wake

hauna lawama atanitumikia.

7 Mdanganyifu hatakaa

nyumbani mwangu,

yeye asemaye kwa uongo

hatasimama mbele yangu.

8 Kila asubuhi nitawanyamazisha

waovu wote katika nchi;

nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya

kutoka katika mji waBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/101-94c837dab923fee4400aad2840d4c3c4.mp3?version_id=1627—

Zaburi 102

Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu

(Maombi Ya Mtu Aliyechoka, Anayeteseka, Anayemimina Malalamiko Kwa

Bwana

)

1 EeBwana, usikie maombi yangu,

kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.

2 Usinifiche uso wako

ninapokuwa katika shida.

Unitegee sikio lako,

ninapoita, unijibu kwa upesi.

3 Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,

mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.

4 Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,

ninasahau kula chakula changu.

5 Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,

nimebakia ngozi na mifupa.

6 Nimekuwa kama bundi wa jangwani,

kama bundi kwenye magofu.

7 Nilalapo sipati usingizi,

nimekuwa kama ndege mpweke

kwenye paa la nyumba.

8 Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki,

wale wanaonizunguka

hutumia jina langu kama laana.

9 Ninakula majivu kama chakula changu

na nimechanganya kinywaji changu na machozi

10 kwa sababu ya ghadhabu yako kuu,

kwa maana umeniinua na kunitupa kando.

11 Siku zangu ni kama kivuli cha jioni,

ninanyauka kama jani.

12 Lakini wewe, EeBwana,

umeketi katika kiti chako cha enzi milele,

sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.

13 Utainuka na kuihurumia Sayuni,

kwa maana ni wakati

wa kumwonyesha wema;

wakati uliokubalika umewadia.

14 Kwa maana mawe yake ni ya thamani

kwa watumishi wako,

vumbi lake lenyewe hulionea huruma.

15 Mataifa wataogopa jina laBwana,

wafalme wote wa dunia

watauheshimu utukufu wako.

16 Kwa maanaBwanaataijenga tena Sayuni

na kutokea katika utukufu wake.

17 Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,

wala hatadharau hoja yao.

18 Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho,

ili taifa litakaloumbwa baadaye

waweze kumsifuBwana:

19 “Bwanaalitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu,

kutoka mbinguni alitazama dunia,

20 kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa

na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”

21 Kwa hiyo jina laBwanalatangazwa huko Sayuni

na sifa zake katika Yerusalemu,

22 wakati mataifa na falme zitakapokusanyika

kumwabuduBwana.

23 Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu,

akafupisha siku zangu.

24 Ndipo niliposema:

“Ee Mungu wangu,

usinichukue katikati ya siku zangu;

miaka yako inaendelea vizazi vyote.

25 Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia,

na mbingu ni kazi ya mikono yako.

26 Hivi vitatoweka, lakini wewe utadumu,

vyote vitachakaa kama vazi.

Utavibadilisha kama nguo

navyo vitaondoshwa.

27 Lakini wewe, U yeye yule,

nayo miaka yako haikomi kamwe.

28 Watoto wa watumishi wako

wataishi mbele zako;

wazao wao wataimarishwa

mbele zako.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/102-dc2ab09e05dc7cba3ad9c246c7c4d214.mp3?version_id=1627—

Zaburi 103

Upendo Wa Mungu

(Zaburi Ya Daudi)

1 Ee nafsi yangu, umhimidiBwana,

vyote vilivyomo ndani yangu

vilihimidi jina lake takatifu.

2 Ee nafsi yangu, umhimidiBwana,

wala usisahau wema wake wote,

3 akusamehe dhambi zako zote,

akuponya magonjwa yako yote,

4 aukomboa uhai wako na kaburi,

akuvika taji ya upendo na huruma,

5 atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema,

ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.

6 Bwanahutenda haki,

naye huwapa hukumu ya haki

wote wanaoonewa.

7 Alimjulisha Mose njia zake,

matendo yake kwa wana wa Israeli.

8 Bwanani mwenye huruma na rehema,

si mwepesi wa hasira,

amejaa upendo.

9 Yeye hatalaumu siku zote,

wala haweki hasira yake milele,

10 yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu

wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.

11 Kama vile mbingu zilivyo juu sana juu ya dunia,

ndivyo wema wake ulivyo mwingi

kwa wanaomcha;

12 kama mashariki ilivyo mbali na magharibi,

ndivyo Mungu alivyoziweka

dhambi zetu mbali nasi.

13 Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake,

ndivyoBwanaanavyowahurumia

wale wanaomcha;

14 kwa kuwa anajua tulivyoumbwa,

anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.

15 Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani,

anachanua kama ua la shambani;

16 upepo huvuma juu yake nalo hutoweka,

mahali pake hapalikumbuki tena.

17 Lakini kutoka milele hata milele

upendo waBwanauko kwa wale wamchao,

nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao:

18 kwa wale walishikao Agano lake

na kukumbuka kuyatii mausia yake.

19 Bwanaameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni,

ufalme wake unatawala juu ya vyote.

20 MhimidiniBwana, enyi malaika zake,

ninyi mlio mashujaa mnaozitii amri zake,

ninyi mnaotii neno lake.

21 MhimidiniBwana, ninyi jeshi lake lote la mbinguni,

ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake.

22 MhimidiniBwana, kazi zake zote

kila mahali katika milki yake.

Ee nafsi yangu, umhimidiBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/103-27ce97ceb3011e92f6a21ca1ee3d567b.mp3?version_id=1627—

Zaburi 104

Katika Kumsifu Muumba

1 Ee nafsi yangu, umhimidiBwana.

EeBwanaMungu wangu, wewe ni mkuu sana,

umejivika utukufu na enzi.

2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi,

amezitandaza mbingu kama hema

3 na kuziweka nguzo za orofa yake

juu ya maji.

Huyafanya mawingu kuwa gari lake kubwa zuri,

na hupanda kwenye mbawa za upepo.

4 Hufanya pepo kuwa wajumbewake,

miali ya moto watumishi wake.

5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake,

hawezi kamwe kuondoshwa.

6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi,

maji yalisimama juu ya milima.

7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia,

kwa sauti ya radi yako yalikimbia,

8 yakapanda milima, yakatelemka mabondeni,

mpaka mahali pale ulipoyakusudia.

9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka,

kamwe hayataifunika dunia tena.

10 Hufanya chemchemi zimwage maji mabondeni,

hutiririka kati ya milima.

11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni,

punda mwitu huzima kiu yao.

12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji,

huimba katikati ya matawi.

13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake,

dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.

14 Huyafanya majani ya mifugo yaote,

na mimea kwa ajili ya watu kupanda,

wajipatie chakula kutoka ardhini:

15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu,

mafuta kwa ajili ya kung’arisha uso wake

na mkate wa kutia mwili nguvu.

16 Miti yaBwanainanyeshewa vizuri,

mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.

17 Humo ndege hufanya viota vyao,

korongo ana nyumba yake

kwenye msunobari.

18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu,

majabali ni kimbilio la pelele.

19 Mwezi hugawanya majira,

na jua hutambua wakati wake wa kutua.

20 Unaleta giza, kunakuwa usiku,

wanyama wote wa mwituni

huzungukazunguka.

21 Simba hunguruma kwa mawindo yao,

na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.

22 Jua huchomoza, nao huondoka kwa kunyata,

hurudi na kulala katika mapango yao.

23 Kisha mwanadamu hutoka nje

na kwenda kazini kwake,

katika kazi yake mpaka jioni.

24 EeBwana, jinsi gani zilivyo nyingi kazi zako!

Kwa hekima ulizifanya zote,

dunia imejaa viumbe vyako.

25 Pale iko bahari, kubwa na yenye nafasi tele,

imejaa viumbe visivyo na idadi,

vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.

26 Huko meli huenda na kurudi,

# pia Lewiathani, uliyemwumba

acheze ndani yake.

27 Hawa wote wanakutazama wewe,

uwape chakula chao kwa wakati wake.

28 Wakati unapowapa,

wanakikusanya,

unapofumbua mkono wako,

wao wanashibishwa mema.

29 Unapoficha uso wako,

wanapata hofu,

unapoondoa pumzi yao,

wanakufa na kurudi mavumbini.

30 Unapopeleka Roho wako,

wanaumbwa,

nawe huufanya upya uso wa dunia.

31 Utukufu waBwanana udumu milele,

Bwanana azifurahie kazi zake,

32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka,

aigusaye milima nayo ikatoa moshi.

33 NitamwimbiaBwanamaisha yangu yote;

nitaimba sifa kwa Mungu wangu

muda wote ninaoishi.

34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye,

ninapofurahi katikaBwana.

35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia

na waovu wasiwepo tena.

# Ee nafsi yangu, MsifuBwana.

MhimidiniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/104-e585def5ed27db73babc7cf5c5653b5a.mp3?version_id=1627—

Zaburi 105

Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli

1 MshukuruniBwana, liitieni jina lake,

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

2 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

3 Utukufu kwa jina lake takatifu,

mioyo ya wale wamtafutaoBwanana ifurahi.

4 MtafuteniBwanana nguvu zake,

utafuteni uso wake siku zote.

5 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka.

6 Enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake,

Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

7 Yeye ndiyeBwanaMungu wetu,

hukumu zake zimo duniani pote.

8 Hulikumbuka Agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

9 Agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

10 Alilithibitisha kwa Yakobo kama amri,

kwa Israeli kama Agano la milele:

11 “Wewe nitakupa nchi ya Kanaani

kama sehemu utakayoirithi.”

12 Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

13 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

14 Hakuruhusu mtu ye yote awaonee,

kwa ajili yao aliwakemea wafalme,

15 akisema, “Msiwaguse masiya wangu,

msiwadhuru manabii wangu.”

16 Akaiita njaa juu ya nchi

na kuharibu chakula chao chote,

17 naye akatuma mtu mbele yao,

Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.

18 Walichubua miguu yake kwa minyororo,

shingo yake ilifungwa kwa chuma,

19 mpaka yale aliyotangulia kusema yalipotimia,

mpaka neno laBwanalilipomjaribu

na kumthibitisha.

20 Mfalme alituma akamfungua,

mtawala wa watu alimwachia huru.

21 Alimfanya mkuu wa nyumba yake,

mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,

22 kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo

na kuwafundisha wazee wake hekima.

23 Kisha Israeli akaingia Misri,

Yakobo akaishi kama mgeni

katika nchi ya Hamu.

24 Bwanaaliwafanya watu wake kuzaana sana,

akawafanya kuwa wengi sana

kuliko adui zao,

25 ndiye aliyeigeuza mioyo yao iwachukie watu wake,

wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.

26 Akamtuma Mose mtumishi wake,

pamoja na Aroni,

ambaye alikuwa amemchagua.

27 Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao,

miujiza yake katika nchi ya Hamu.

28 Alituma giza na nchi ikawa giza,

kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?

29 Aligeuza maji yao kuwa damu,

ikasababisha samaki wao kufa.

30 Nchi yao ilijaa vyura tele,

ambao waliingia

hadi kwenye vyumba vya kulala

vya watawala wao.

31 Alisema, yakaja makundi ya mainzi,

na viroboto katika nchi yao yote.

32 Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe,

yenye umeme wa radi katika nchi yao yote,

33 akaharibu mizabibu yao na miti ya tini

na akaangamiza miti ya nchi yao.

34 Alisema, nzige wakaja,

tunutu wasio na idadi,

35 wakala kila kitu cha kijani kibichi katika nchi yao,

wakala mazao ya ardhi yao.

36 Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza

katika nchi yao,

matunda ya kwanza ya ujana wao wote.

37 Akawatoa Israeli katika nchi

wakiwa na fedha

na dhahabu nyingi,

wala hakuna hata mmoja

kutoka katika kabila zao aliyejikwaa.

38 Misri ilifurahi walipoondoka,

kwa sababu hofu ya Israeli

ilikuwa imewaangukia.

39 Alitandaza wingu kama kifuniko

na moto kuwamulikia usiku.

40 Waliomba, naye akawaletea kware,

akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.

41 Alipasua mwamba, maji yakabubujika,

yakatiririka jangwani kama mto.

42 Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu,

aliyompa Abrahamu mtumishi wake.

43 Aliwatoa watu wake kwa furaha,

wateule wake kwa kelele za shangwe,

44 akawapa nchi za mataifa,

wakawa warithi wa vitu

ambavyo wengine

walikuwa wamevitaabikia,

45 alifanya haya ili wayashike mausia yake

na kuzitii sheria zake.

# MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/105-11a17a0347b8487edfbd27bdbd14030f.mp3?version_id=1627—

Zaburi 106

Wema Wa Bwana Kwa Watu Wake

1 MsifuniBwana.

MshukuruniBwana, kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

2 Ni nani awezaye kusimulia

matendo makuu yaBwana

au kutangaza kikamilifu sifa zake?

3 Heri wale wanaodumisha haki,

ambao daima wanafanya yaliyo mema.

4 EeBwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako,

uwe msaada wangu unapowaokoa,

5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako,

niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako,

na kuungana na urithi wako katika kukusifu.

6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda,

tumekosa na tumetenda kwa uovu.

7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri,

hawakuzingatia maajabu yako,

wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako,

bali waliasi kando ya bahari,

Bahari ya Shamu.

8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake,

ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.

9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka,

akawaongoza katika vilindi vyake

kama vile jangwani.

10 Aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui;

kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.

11 Maji yaliwafunika adui zao,

hakunusurika hata mmoja.

12 Ndipo walipoamini ahadi zake,

nao wakaimba sifa zake.

13 Lakini mara walisahau aliyowatendea,

wala hawakungojea shauri lake.

14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao,

walimjaribu Mungu nyikani.

15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba,

lakini akatuma juu yao

ugonjwa wa kudhoofisha.

16 Kambini waliwaonea wivu Mose na Aroni,

ambaye alikuwa amewekwa wakfu kwaBwana.

17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani,

ikawazika Abiramu na kundi lake.

18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao,

mwali wa moto uliwateketeza waovu.

19 Huko Horebu walitengeneza ndama

na kuabudu sanamu ya kusubu

kutoka kwenye dhahabu.

20 Waliubadilisha Utukufu wa Mungu

na kuipa sanamu ya fahali,

ambaye hula majani.

21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa,

ambaye alikuwa ametenda

mambo makuu huko Misri,

22 miujiza katika nchi ya Hamu

na mambo ya kutisha

huko Bahari ya Shamu.

23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza:

kama Mose mteule wake,

asingesimama kati yao na Mungu

kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.

24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri,

hawakuiamini ahadi yake.

25 Walinung’unika ndani ya mahema yao,

wala hawakumtiiBwana.

26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa

kwamba atawafanya waanguke jangwani,

27 kuwatawanya wazao wao waanguke

miongoni mwa mataifa

na kuwatawanya katika nchi zote.

28 Walijifunga nira na Baali wa Peori,

wakala dhabihu zilizotolewa

kwa miungu isiyo na uhai,

29 waliichochea hasira yaBwana,

wakamkasirisha kwa matendo yao maovu,

tauni ikazuka katikati yao.

30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati,

nayo tauni ikazuiliwa.

31 Hili likahesabiwa kwake haki,

kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.

32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirishaBwana,

janga likampata Mose kwa sababu yao;

33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu

na maneno yakatoka midomoni kwa Mose bila kufikiri.

34 Hawakuyaangamiza yale mataifa

kamaBwanaalivyowaagiza,

35 bali walijichanganya na mataifa

na wakazikubali desturi zao.

36 Waliabudu sanamu zao,

zikawa mtego kwao.

37 Wakawatoa wana wao

na binti zao dhabihu kwa mashetani.

38 Walimwaga damu isiyo na hatia,

damu za wana wao na binti zao,

ambao waliwatoa dhabihu

kwa sanamu za Kanaani,

nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.

39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda;

kwa matendo yao wenyewe

wakajifanyia ukahaba.

40 Kwa hiyoBwanaakawakasirikia watu wake

na akauchukia sana urithi wake.

41 Akawakabidhi kwa mataifa

na adui zao wakawatawala.

42 Adui zao wakawaonea

na kuwatia chini ya mamlaka yao.

43 Mara nyingi aliwaokoa

lakini wao walikuwa wamezama kwenye uasi,

nao wakajiharibu katika dhambi zao.

44 Lakini akaangalia mateso yao

wakati aliposikia kilio chao;

45 kwa ajili yao akakumbuka Agano lake

na kutokana na upendo wake mkuu

akapooza hasira yake.

46 Akawafanya wahurumiwe

na wote waliowashikilia mateka.

47 EeBwanaMungu wetu, utuokoe,

utukusanye tena kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu

na kujisifu katika sifa zako.

48 AtukuzweBwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Watu wote na waseme, “Amen!”

MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/106-e75590dd685bd20a7f4923c70dfa3630.mp3?version_id=1627—

Zaburi 107

Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake

1 MshukuruniBwana, kwa kuwa yeye ni mwema,

upendo wake wadumu milele.

2 Waliokombolewa waBwanana waseme hivi,

wale aliowaokoa kutoka katika mkono wa adui,

3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali,

kutoka mashariki na magharibi,

kutoka kaskazini na kusini.

4 Baadhi yao walitangatanga jangwani,

hawakuona njia ya kuwafikisha katika mji

ambao wangeweza kuishi.

5 Walikuwa na njaa na kiu,

nafsi zao zikadhoofika.

6 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida zao,

naye akawaokoa kutoka katika taabu zao.

7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi kwenye mji

ambao wangeweza kuishi.

8 Basi na wamshukuruBwana

kwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu

kwa wanadamu,

9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu

na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.

10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu,

wafungwa wakiteseka katika minyororo,

11 kwa sababu walikuwa wameasi

dhidi ya maneno ya Mungu

na kudharau shauri

la Aliye Juu Sana.

12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu;

walijikwaa na hapakuwepo

na ye yote wa kuwasaidia.

13 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawaokoa kutoka kwenye taabu yao.

14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu

na akavunja minyororo yao.

15 Basi na wamshukuruBwana

kwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu

kwa wanadamu,

16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba

na kukata mapingo ya chuma.

17 Wengine wakawa wajinga kutokana na uasi wao,

wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.

18 Wakachukia kabisa vyakula vyote,

wakakaribia malango ya mauti.

19 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawaokoa kutoka kwenye taabu yao.

20 Akalituma neno lake na kuwaponya,

akawaokoa kutoka maangamizo.

21 Basi na wamshukuruBwana

kwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu

kwa wanadamu,

22 Na watoe dhabihu za kushukuru,

na wasimulie matendo yake

kwa nyimbo za furaha.

23 Wengine walisafiri baharini kwa meli,

walikuwa wafanya biashara kwenye maji makuu.

24 Waliziona kazi zaBwana,

matendo yake ya ajabu katika kilindi.

25 Kwa maana alisema

na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.

26 Yakainuka juu mbinguni yakashuka chini hadi vilindini,

katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.

27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi,

ujanja wao ukafikia ukomo.

28 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawatoa kutoka kwenye taabu yao.

29 Akatuliza dhoruba kwa mnong’ono,

mawimbi ya bahari yakatulia.

30 Walifurahi ilipokuwa shwari,

naye akawaongoza hadi kwenye bandari waliyoitamani.

31 Basi na wamshukuruBwana

kwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu

kwa wanadamu,

32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu,

na wamsifu katika baraza la wazee.

33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa,

chemchemi za maji zitiririkazo

kuwa ardhi yenye kiu,

34 nchi izaayo ikawa ya chumvi na isiyofaa,

kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.

35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji,

nayo ardhi kame

kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;

36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo,

nao wakajenga mji wakaishi humo.

37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu,

nayo ikazaa matunda mengi,

38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana,

wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.

39 Kisha hesabu yao ilipungua,

walinyenyekeshwa kwa kuonewa,

maafa na huzuni,

40 yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu,

aliwafanya watangetange

kwenye nyika isiyo na njia.

41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao,

na kuongeza jamaa zao

kama makundi ya kondoo.

42 Wanyofu wataona na kufurahi,

lakini waovu wote

watafunga vinywa vyao.

43 Ye yote aliye na hekima, ayasikie mambo haya

na atafakari upendo mkuu waBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/107-26377a1b5677ac9f51893a4d49503e03.mp3?version_id=1627—

Zaburi 108

Kuomba Msaada Dhidi Ya Adui

(Zaburi Ya Daudi. Wimbo)

1 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti,

nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.

2 Amka, kinubi na zeze!

Nitayaamsha mapambazuko.

3 EeBwana, nitakusifu katikati ya mataifa,

nitaimba sifa zako katikati ya mataifa.

4 Kwa maana upendo wako ni mkuu,

juu kuliko mbingu,

uaminifu wako hufika mpaka angani.

5 Ee Mungu, utukuzwe, juu ya mbingu,

utukufu wako na uwe duniani pote.

6 Utuokoe na kutusaidia kwa mkono wako wa kuume,

ili wale uwapendao wapate kuokolewa.

7 Mungu amesema kutoka patakatifu pake:

“Kwa furaha na ushindi nitaigawa Shekemu

na kulipima Bonde la Sukothi.

8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu,

Efraimu ni kofia yangu ya chuma,

Yuda ni fimbo yangu ya utawala.

9 Moabu ni sinia langu la kunawia,

juu ya Edomu natupa kiatu changu;

juu ya Ufilisti napiga kelele

ya furaha ya ushindi.”

10 Ni nani atakayenileta hadi kwenye mji wenye ngome?

Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?

11 Si wewe, Ee Mungu, wewe ambaye umetukataa

nawe huendi tena na majeshi yetu?

12 Utusaidie kukabiliana na adui,

kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.

13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi,

naye atawaponda adui zetu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/108-39932af83d283fa9eb8ec3980fb18537.mp3?version_id=1627—

Zaburi 109

Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5 Wananilipiza baya kwa jema,

chuki badala ya urafiki wangu.

6 Agiza mtu mwovu ampinge,

# mshtakina asimame mkono wake wa kuume.

7 Anapohukumiwa na apatikane na hatia,

nayo maombi yake na yamhukumu.

8 Siku zake za kuishi na ziwe chache,

uongozi wake na apewe mtu mwingine.

9 Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10 Watoto wake na watangetange wakiomba-omba,

na wafukuzwe kwenye magofu

ya nyumba zao zilizobomoka.

11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake

na yatekwe nyara na wageni.

12 Asiwepo mtu ye yote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13 Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele zaBwana,

dhambi ya mama yake

na isifutwe kamwe.

15 Dhambi zao na zibaki daima mbele zaBwana,

ili apate kukatilia mbali

kumbukumbu lao duniani.

16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17 Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18 Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19 Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20 Haya na yawe malipo yaBwana

kwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.

21 Lakini wewe, EeBwanaMwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wako.

22 Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23 Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa

kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.

26 EeBwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, EeBwana,

umetenda hili.

28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29 Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.

30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sanaBwana

katika umati mkubwa nitamsifu.

31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake

kutoka kwa wale wanaomhukumu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/109-fd72b023db33f14ecb3b7e5a63785879.mp3?version_id=1627—