Zaburi 120

Kuomba Msaada

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Katika dhiki yangu namwitaBwana,

naye hunijibu.

2 EeBwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo

na ndimi za udanganyifu.

3 Atakufanyia nini,

au akufanyie nini zaidi,

Ewe ulimi mdanganyifu?

4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,

kwa makaa yanayowaka

ya mti wa mretemu.

5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,

kwamba naishi katikati

ya hema za Kedari!

6 Nimeishi muda mrefu mno

miongoni mwa wale

wanaochukia amani.

7 Mimi ni mtu wa amani;

lakini ninaposema,

wao wanataka vita.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/120-df46a67e829af36a3dad513361f137eb.mp3?version_id=1627—

Zaburi 121

Bwana Mlinzi Wetu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Nayainua macho yangu nitazame vilima,

msaada wangu utatoka wapi?

2 Msaada wangu hutoka kwaBwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

3 Hatauacha mguu wako uteleze,

yeye akulindaye hatasinzia,

4 hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.

5 Bwanaanakulinda,

Bwanani uvuli wako mkono wako wa kuume,

6 jua halitakudhuru mchana,

wala mwezi wakati wa usiku.

7 Bwanaatakukinga na madhara yote,

atayalinda maisha yako,

8 Bwanaatakulinda unapoingia na unapotoka,

tangu sasa na hata milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/121-8f6089c6e8e51612f7206e5112f479e0.mp3?version_id=1627—

Zaburi 122

Sifa Kwa Yerusalemu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Nilishangilia pamoja na wale walioniambia,

“Twende katika nyumba yaBwana.”

2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama

malangoni mwako.

3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji

ambao umeshikamanishwa pamoja.

4 Huko ndiko makabila hukwea,

makabila yaBwana,

kulisifu jina laBwanakulingana na maagizo

waliopewa Israeli.

5 Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa,

viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.

6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:

“Wote wakupendao na wawe salama.

7 Amani na iwepo ndani ya kuta zako

na usalama ndani ya ngome zako.”

8 Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki,

nitasema, “Amani iwe ndani yako.”

9 Kwa ajili ya nyumba yaBwanaMungu wetu,

nitatafuta mafanikio yako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/122-e9675173996f9bd2375b6b4776caf398.mp3?version_id=1627—

Zaburi 123

Kuomba Rehema

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Ninayainua macho yangu kwako,

kwako wewe ambaye

kiti cha enzi kiko mbinguni.

2 Kama vile macho ya watumwa

yatazamavyo mkono wa bwana wao,

kama vile macho ya mtumishi wa kike

yatazamavyo mkono wa bibi yake,

ndivyo macho yetu yamtazamavyoBwanaMungu wetu,

mpaka atakapotuhurumia.

3 Uturehemu, EeBwana, uturehemu,

kwa maana tumevumilia dharau nyingi.

4 Tumevumilia dhihaka nyingi

kutoka kwa wenye kiburi,

dharau nyingi

kutoka kwa wenye majivuno.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/123-731c2710bf4366fcd14b363a09c0ebe6.mp3?version_id=1627—

Zaburi 124

Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 KamaBwanaasingalikuwa upande wetu;

Israeli na aseme sasa:

2 kamaBwanaasingalikuwa upande wetu,

wakati watu walipotushambulia,

3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,

wangalitumeza tungali hai,

4 Mafuriko yangalitugharikisha,

maji mengi yangalitufunika,

5 maji yaendayo kasi

yangalituchukua.

6 Bwanaasifiwe,

yeye ambaye hakuruhusu

turaruliwe kwa meno yao.

7 Tumeponyoka kama ndege

kutoka katika mtego wa mwindaji;

mtego umevunjika,

nasi tukaokoka.

8 Msaada wetu ni katika jina laBwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/124-9ccb6bbd9ae29a84ffb8315500236917.mp3?version_id=1627—

Zaburi 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Wale wamtumainioBwanani kama mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika wadumu milele.

2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyoBwanaanavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliopewa wenye haki,

ili kwamba wenye haki wasije

wakatumia mikono yao

kutenda ubaya.

4 EeBwana, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Bwanaatawafukuza

pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/125-370cee1374973ac54166d030d902839e.mp3?version_id=1627—

Zaburi 126

Kurejeshwa Kutoka Utumwani

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Bwanaalipowarejeza mateka Sayuni,

tulikuwa kama watu walioota ndoto.

2 Vinywa vyetu vilijaa kicheko,

ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.

Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,

“Bwanaamewatendea mambo makuu.”

3 Bwanaametutendea mambo makuu,

nasi tumejaa furaha.

4 EeBwana, turejeshee watu wetu waliotekwa,

kama vijito katika Negebu.

5 Wapandao kwa machozi

watavuna kwa nyimbo za shangwe.

6 Yeye azichukuaye mbegu zake

kwenda kupanda,

huku akilia,

atarudi kwa nyimbo za shangwe,

akiwa ameyachukua

matita ya mavuno yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/126-911e1a86f635da446023b7d1d66d0b5f.mp3?version_id=1627—

Zaburi 127

Bila Mungu, Kazi Ya Mwanadamu Haifai

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Solomoni)

1 Bwanaasipoijenga nyumba,

wajengao hufanya kazi bure.

Bwanaasipoulinda mji,

walinzi wakesha bure.

2 Mnajisumbua bure kuamka mapema

na kuchelewa kulala,

mkitaabikia chakula:

kwa maana yeye huwapa usingizi

wapenzi wake.

3 Wana ni urithi utokao kwaBwana,

watoto ni zawadi kutoka kwake.

4 Kama mishale mikononi mwa shujaa

ndivyo walivyo wana

awazaao mtu katika ujana wake.

5 Heri mtu ambaye podo lake

limejazwa nao.

Hawataaibishwa wanaposhindana

na adui zao langoni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/127-3d0950ea8f485d2b1b38b93607d112ef.mp3?version_id=1627—

Zaburi 128

Thawabu Ya Kumtii Bwana

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Heri ni wale wote wamchaoBwana,

waendao katika njia zake.

2 Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

katika nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchayeBwana.

5 Bwanana akubariki kutoka Sayuni

siku zote za maisha yako,

na uone mafanikio ya Yerusalemu,

6 nawe ujaliwe kuishi

uone watoto wa watoto wako.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/128-42322bf991cd46273a32779b87cfd157.mp3?version_id=1627—

Zaburi 129

Maombi Dhidi Ya Adui Wa Israeli

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Wamenionea mno tangu ujana wangu;

Israeli na aseme sasa:

2 wamenionea mno tangu ujana wangu,

lakini bado hawajanishinda.

3 Wakulima wamelima mgongo wangu,

na kufanya mifereji yao mirefu.

4 LakiniBwanani mwenye haki;

amenifungua toka kamba za waovu.

5 Wale wote waichukiao Sayuni

na warudishwe nyuma kwa aibu.

6 Wawe kama majani juu ya paa,

ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,

wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8 Wale wapitao karibu na wasiseme,

“Baraka yaBwanaiwe juu yako;

tunakubariki katika jina laBwana.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/129-9ffa949f38b7f78e6764c6dbb56706d0.mp3?version_id=1627—