Zaburi 130

Kuomba Msaada

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Kutoka katika vilindi ninakulilia, EeBwana,

2 EeBwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3 Kama wewe, EeBwana,

ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

EeBwana, ni nani

angeliweza kusimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5 NamngojeaBwana, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6 Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7 Ee Israeli, mtumainiBwana,

maana kwaBwanakuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka katika dhambi zao zote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/130-0fa0927afafceabcb36aa675010cc524.mp3?version_id=1627—

Zaburi 131

Maombi Ya Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi.)

1 Moyo wangu hauna kiburi, EeBwana,

macho yangu hayajivuni;

sijishughulishi na mambo makuu kunizidi

wala mambo ya ajabu mno kwangu.

2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.

3 Ee Israeli, mtumainiBwana

tangu sasa na hata milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/131-437d8757822eb8e3099c323a4841105e.mp3?version_id=1627—

Zaburi 132

Maskani Ya Mungu Ya Milele Katika Sayuni

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 EeBwana, mkumbuke Daudi

na taabu zote alizozistahimili.

2 Aliapa kiapo kwaBwana

na akaweka nadhiri kwa yeye

Mwenye Nguvu wa Yakobo:

3 “Sitaingia nyumbani mwangu

au kwenda kitandani mwangu:

4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu,

wala kope zangu kusinzia,

5 mpaka nitakapompatiaBwanamahali,

makao kwa ajili ya yeye

Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

6 Tulisikia habari hii huko Efrathi,

# tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara

7 “Twendeni kwenye makao yake,

na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;

8 inuka, EeBwana, uje mahali pako pa kupumzikia,

wewe na Sanduku la nguvu zako.

9 Makuhani wako na wavikwe haki,

watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”

10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,

usimkatae masiya wako.

11 Bwanaalimwapia Daudi kiapo,

kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua:

“Mmoja wa wazao wako mwenyewe

nitamweka katika kiti chako cha enzi,

12 kama wanao watashika Agano langu

na sheria ninazowafundisha,

ndipo wana wao watarithi

kiti chako cha enzi milele na milele.”

13 Kwa maanaBwanaameichagua Sayuni,

amepaonea shauku pawe maskani yake:

14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele;

hapa ndipo nitakapoketi nikitawala,

kwa sababu nimepaonea shauku:

15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele:

nitashibisha maskini wake kwa chakula.

16 Nitawavika makuhani wake wokovu,

nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.

17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe,

# na kuweka taa kwa ajili ya masiyawangu.

18 Adui zake nitawavika aibu,

bali taji kichwani pake itang’aa sana.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/132-f29cd9d9b7dc1d8d234191c8996384b2.mp3?version_id=1627—

Zaburi 133

Sifa Za Pendo La Undugu

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi)

1 Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza

wakati ndugu wanapoishi pamoja katika umoja!

2 Ni kama mafuta ya thamani yaliyomiminwa kichwani,

yakitiririka kwenye ndevu,

yakitiririka kwenye ndevu za Aroni,

mpaka kwenye upindo wa mavazi yake.

3 Ni kama vile umande wa Hermoni

unavyoanguka juu ya Mlima Sayuni.

Kwa maana huko ndikoBwana

alikoamuru baraka yake,

naam, hata uzima milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/133-38ef0c4a3e3a0da405966e0ae173ef01.mp3?version_id=1627—

Zaburi 134

Wito Wa Kumsifu Mungu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 MsifuniBwana, ninyi nyote

watumishi waBwana,

ninyi mnaotumika usiku

ndani ya nyumba yaBwana.

2 Inueni mikono yenu katika mahali patakatifu

na mumsifuBwana.

3 NayeBwana, Muumba wa mbingu na dunia,

awabariki kutoka Sayuni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/134-0ab0f077880d8b738f1866dcc6bb3977.mp3?version_id=1627—

Zaburi 135

Wimbo Wa Sifa Kwa Mungu

1 MsifuniBwana.

Lisifuni jina laBwana,

msifuni, enyi watumishi waBwana,

2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba yaBwana,

katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.

3 MsifuniBwana, kwa kuwaBwanani mwema,

liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.

4 Kwa maanaBwanaamemchagua Yakobo

kuwa wake mwenyewe,

Israeli kuwa mali yake ya thamani.

5 Ninajua ya kuwaBwanani mkuu,

kwamba Bwana wetu ni mkuu zaidi

kuliko miungu yote.

6 Bwanahufanya lo lote apendalo,

mbinguni na duniani,

katika bahari na vilindi vyake vyote.

7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia;

hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua

na huleta upepo kutoka ghala zake.

8 Alimwua mzaliwa wa kwanza wa Misri,

mzaliwa wa kwanza

wa wanadamu na wanyama.

9 Alipeleka ishara zake na maajabu

katikati yako, Ee Misri,

dhidi ya Farao na watumishi wake wote.

10 Aliyapiga mataifa mengi,

na akaua wafalme wenye nguvu:

11 Mfalme Sihoni na Waamori,

Ogu mfalme wa Bashani

na wafalme wote wa Kanaani;

12 akatoa nchi yao kuwa urithi,

urithi kwa watu wake Israeli.

13 EeBwana, jina lako ladumu milele,

kumbukumbu za fahari zako,

EeBwana, kwa vizazi vyote.

14 MaanaBwanaatawathibitisha watu wake

kuwa wenye haki,

na kuwahurumia watumishi wake.

15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,

zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema,

zina macho, lakini haziwezi kuona,

17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia,

wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.

18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo,

vivyo hivyo wote wanaozitumainia.

19 Ee nyumba ya Israeli, msifuniBwana;

Ee nyumba ya Aroni, msifuniBwana;

20 Ee nyumba ya Lawi, msifuniBwana;

ninyi mnaomcha, msifuniBwana.

21 MsifuniBwanakutoka Sayuni,

msifuni yeye aishiye Yerusalemu.

MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/135-b3cc2ae163386368ef8435e6ed41db87.mp3?version_id=1627—

Zaburi 136

Wimbo Wa Kumshukuru Mungu

1 MshukuruniBwana, kwa kuwa ni mwema.

Fadhili zake zadumu milele.

2 Mshukuruni Mungu wa miungu.

Fadhili zake zadumu milele.

3 Mshukuruni Bwana wa mabwana:

Fadhili zake zadumu milele.

4 Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu,

Fadhili zake zadumu milele.

5 Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu,

Fadhili zake zadumu milele.

6 Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji,

Fadhili zake zadumu milele.

7 Ambaye aliumba mianga mikubwa,

Fadhili zake zadumu milele.

8 Jua litawale mchana,

Fadhili zake zadumu milele.

9 Mwezi na nyota vitawale usiku,

Fadhili zake zadumu milele.

10 Kwake yeye aliyemwua mzaliwa wa kwanza wa Misri,

Fadhili zake zadumu milele.

11 Na kuwatoa Israeli katikati yao,

Fadhili zake zadumu milele.

12 Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa,

Fadhili zake zadumu milele.

13 Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu,

Fadhili zake zadumu milele.

14 Na kuwapitisha Israeli katikati yake,

Fadhili zake zadumu milele.

15 Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu,

Fadhili zake zadumu milele.

16 Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa,

Fadhili zake zadumu milele.

17 Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu,

Fadhili zake zadumu milele.

18 Naye aliwaua wafalme wenye nguvu,

Fadhili zake zadumu milele.

19 Sihoni mfalme wa Waamori,

Fadhili zake zadumu milele.

20 Ogu mfalme wa Bashani,

Fadhili zake zadumu milele.

21 Akatoa nchi yao kuwa urithi,

Fadhili zake zadumu milele.

22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake,

Fadhili zake zadumu milele.

23 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu,

Fadhili zake zadumu milele.

24 Alituweka huru toka adui zetu,

Fadhili zake zadumu milele.

25 Ambaye humpa chakula kila kiumbe.

Fadhili zake zadumu milele.

26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni,

Fadhili zake zadumu milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/136-97e5e5a1599c147afab74fa8bd390b95.mp3?version_id=1627—

Zaburi 137

Maombolezo Ya Israeli Uhamishoni

1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza

tulipokumbuka Sayuni.

2 Kwenye miti ya huko

tulitundika vinubi vyetu,

3 kwa maana huko hao waliotuteka

walitaka tuwaimbie nyimbo,

watesi wetu walidai nyimbo za furaha;

walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja

kati ya nyimbo za Sayuni!”

4 Tutaimbaje nyimbo zaBwana,

tukiwa katika nchi ya kigeni?

5 Nikikusahau wewe, Ee Yerusalemu,

basi mkono wangu wa kuume

na usahau ujuzi wake.

6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu

kama sitakukumbuka wewe,

kama nisipokufikiri Yerusalemu

kuwa furaha yangu kubwa.

7 Kumbuka, EeBwana,

walichokifanya Waedomu,

siku ile Yerusalemu ilipoanguka.

Walisema, “Bomoa, Bomoa

mpaka kwenye misingi yake!”

8 Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,

ana furaha yeye ambaye atakulipiza wewe

kwa yale uliyotutenda sisi:

9 yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga

na kuwaponda juu ya miamba.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/137-aa0e5e3e6f830102379a716d0b434f81.mp3?version_id=1627—

Zaburi 138

Maombi Ya Shukrani

(Zaburi Ya Daudi)

1 Nitakusifu wewe, EeBwana,

kwa moyo wangu wote,

mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.

2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,

nami nitalisifu jina lako

kwa ajili ya upendo wako

na uaminifu,

kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako

juu ya vitu vyote.

3 Nilipoita, ulinijibu;

ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4 Wafalme wote wa dunia,

na wakusifu wewe EeBwana,

wakati wanaposikia

maneno ya kinywa chako.

5 Wao na waimbe kuhusu njia zaBwana,

kwa maana utukufu waBwanani mkuu.

6 IngawaBwanayuko juu,

humwangalia mnyonge,

bali mwenye kiburi

yeye anamjua kutokea mbali.

7 Nijapopita katikati ya shida,

wewe unayahifadhi maisha yangu,

unanyosha mkono wako

dhidi ya hasira ya adui zangu,

kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

8 Bwanaatatimiza kusudi lake kwangu,

EeBwana, upendo wako wadumu milele:

usiziache kazi za mikono yako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/138-d40040723c8c708f47c1cf84d80d04cd.mp3?version_id=1627—

Zaburi 139

Mungu Asiyeweza Kukwepwa

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, umenichunguza

na kunijua.

2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka;

unatambua mawazo yangu tokea mbali.

3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;

unaelewa njia zangu zote.

4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu,

wewe walijua kikamilifu, EeBwana.

5 Umenizunguka nyuma na mbele;

umeweka mkono wako juu yangu.

6 Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu,

ni ya juu sana kwangu kuyafikia.

7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako?

Niende wapi niukimbie uso wako?

8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko;

# nikifanya vilindikuwa kitanda changu,

wewe uko huko.

9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko,

kama nikikaa pande za mbali za bahari,

10 hata huko mkono wako utaniongoza,

mkono wako wa kuume

utanishika kwa uthabiti.

11 Kama nikisema, “Hakika giza litanificha

na nuru inayonizunguka iwe usiku,”

12 hata giza halitakuwa giza kwako,

usiku utang’aa kama mchana,

kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.

13 Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba

utu wangu wa ndani;

uliniunga pamoja tumboni

mwa mama yangu.

14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa

kwa namna ya ajabu na ya kutisha;

kazi zako ni za ajabu,

ninajua hayo kikamilifu.

15 Umbile langu halikufichika kwako,

nilipoumbwa mahali pa siri.

Nilipoungwa pamoja kwa ustadi

katika vilindi vya nchi,

16 macho yako yaliniona

kabla mwili wangu haujakamilika.

Siku zangu zote ulizonipangia

ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwapo hata moja.

17 Tazama jinsi gani yalivyo ya thamani

mawazo yako kwangu, Ee Mungu!

Jinsi gani jumla yake ilivyo kubwa!

18 Kama ningezihesabu,

zingekuwa nyingi kuliko mchanga.

Niamkapo,

bado niko pamoja nawe.

19 Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu!

Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!

20 Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya,

adui zako wanatumia vibaya jina lako.

21 EeBwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia?

Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?

22 Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao,

ninawahesabu ni adui zangu.

23 Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu,

nijaribu na ujue mawazo yangu.

24 Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu,

uniongoze katika njia ya milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/139-a92dc228fd3bdfb24c069e45c20f4d67.mp3?version_id=1627—