1 Mambo ya Nyakati 26

Mabawabu

1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu:

Kutoka kwa Wakorahi alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.

2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao:

Zekaria mzaliwa wa kwanza,

Yadiaeli wa pili,

Zebadia wa tatu,

Yathnieli wa nne,

3 Elamu wa tano

Yehohanani wa sita

na Eliehoenai wa saba.

4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao:

Shemaya mzaliwa wa kwanza,

Yehozabadi wa pili,

Yoa wa tatu,

Sakari wa nne,

Nethaneli wa tano,

5 Amieli wa sita,

Isakari wa saba,

na Peulethai wa nane.

(Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)

6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.

7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.

8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.

9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo, jumla yao watu kumi na wanane.

10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),

11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.

12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwaBwanakama jamaa zao walivyokuwa nazo.

13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.

14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.

15 Kura ya Lango la Kusini ikamwungukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.

16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa.

Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:

17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.

18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.

19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.

Watunza Hazina Na Maafisa Wengine

20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.

21 Wazao wa Ladani, ambao walikuwa Wagerishoni kupitia Ladani na ambao walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgerishoni, walikuwa Yehieli,

22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu laBwana.

23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:

24 Shebueli, mzao wa Gershoni mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.

25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Oramu, Zikri na Shelomithi.

26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa aliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.

27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu laBwana.

28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.

29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenani na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.

30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote zaBwanana utumishi wa mfalme

31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.

32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1CH/26-be4a15950bc9bd7a041778b92a530266.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

5 × 2 =