Solomoni Aomba Hekima 1 Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwaBwanaMungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno. 2 Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa. 3 Naye Solomoni na kusanyiko […]
Category Archives: 2 Mambo ya nyakati
2 Mambo ya nyakati 2
Maandalizi Ya Kujenga Hekalu 1 Solomoni akatoa amri kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina laBwanana jumba la kifalme kwa ajili yake mwenyewe. 2 Akaandika watu 70,000 kuwa wachukuzi wa mizigo, na watu 80,000 kuwa wachonga mawe vilimani, na watu 3,600 kuwa wasimamizi wao. 3 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Mfalme Hiramu wa Tiro: “Unitumie magogo […]
2 Mambo ya nyakati 3
Solomoni Ajenga Hekalu 1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu laBwanakatika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapoBwanaalikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi. 2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. 3 Msingi aliouweka Solomoni kwa […]
2 Mambo ya nyakati 4
Vifaa Vya Hekalu 1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi. 2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kina chake kilikuwa dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathiniingeweza kuizunguka. 3 Chini […]
2 Mambo ya nyakati 5
1 Hivyo kazi yote Solomoni aliyofanya kwa ajili ya Hekalu laBwanaikamalizika, Solomoni akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu, yaani, fedha, dhahabu na vyombo vingine vyote na kuviweka katika hazina za Hekalu la Mungu. Sanduku La Agano Laletwa Hekaluni 2 Kisha Mfalme Solomoni akawaita huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote […]
2 Mambo ya nyakati 6
Kuweka Hekalu Wakfu 1 Kisha Solomoni akasema, “Bwanaalisema ya kwamba angelikaa katika wingu jeusi. 2 Nimejenga Hekalu zuri kwa ajili yako, mahali pako pa kukaa milele.” 3 Wakati kusanyiko lote la Israeli likiwa limesimama huko, Mfalme Solomoni akageuka na kuwabariki. 4 Kisha akasema: “AhimidiweBwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi […]
2 Mambo ya nyakati 7
Hekalu Lawekwa Wakfu 1 Baada ya Solomoni kumaliza kuomba, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, nao utukufu waBwanaukalijaza Hekalu. 2 Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya Hekalu laBwanakwa sababu utukufu waBwanaulilijaza. 3 Waisraeli wote walipoona moto ukishuka na utukufu waBwanaukiwa juu ya Hekalu, wakapiga magoti sakafuni wakasujudu nyuso zao mpaka chini, […]
2 Mambo ya nyakati 8
Shughuli Nyingine Za Solomoni 1 Ikawa mwisho wa miaka ishirini, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu laBwanana jumba lake mwenyewe la kifalme, 2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo. 3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka. 4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote […]
2 Mambo ya nyakati 9
Malkia Wa Sheba Amtembelea Solomoni 1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina laBwana, huyo malkia akaja kumjaribu kwa maswali magumu. Alipofika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu […]
2 Mambo ya nyakati 10
Israeli Wanamwasi Rehoboamu 1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme. 2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri. 3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na […]