1 Samweli 1

Kuzaliwa Kwa Samweli 1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu. 2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto. […]

1 Samweli 2

Maombi Ya Hana 1 Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangiliaBwana, katikaBwanapembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako. 2 “Hakuna ye yote aliye mtakatifu kamaBwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu. 3 “Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena […]

1 Samweli 3

Bwana Amwita Samweli 1 Kijana Samweli alihudumu mbele zaBwanachini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi. 2 Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida. 3 Taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa […]

1 Samweli 4

1 Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote. Wafilisti Wateka Sanduku La Mungu Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki. 2 Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli […]

1 Samweli 5

Sanduku La Agano Huko Ashdodi Na Ekroni 1 Baada ya Wafilisti kuteka Sanduku la Mungu, walilichukua kutoka Ebenezeri mpaka Ashdodi. 2 Kisha wakaliingiza lile Sanduku ndani ya hekalu la Dagoni na kuliweka kando ya huyo Dagoni. 3 Watu wa Ashdodi walipoamka asubuhi na mapema kesho yake kumbe, wakamkuta Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya Sanduku […]

1 Samweli 6

Sanduku La Mungu Larudishwa Israeli 1 Wakati Sanduku laBwanalilipokuwa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba, 2 Wafilisti waliwaita makuhani wa Dagoni na waaguzi na kuwaambia, “Tutafanya nini na hili Sanduku laBwana? Tuambieni jinsi tutakavyolirudisha mahali pake.” 3 Wakajibu, “Kama mtalirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, msilirudishe mikono mitupu bali kwa vyo vyote mpelekeeni sadaka […]

1 Samweli 7

1 Kisha watu wa Kiriath-Yearimu wakaja na kulichukua Sanduku laBwana. Wakalipeleka katika nyumba ya Abinadabu juu kilimani na kumweka Eleazari mwanawe wakfu kulichunga Sanduku laBwana. Samweli Awatiisha Wafilisti Huko Mispa 2 Sanduku laBwanalilibakia huko Kiriath-Yearimu kwa muda mrefu, yaani jumla ya miaka ishirini, nao watu wa Israeli wakaomboleza na kumtafutaBwana. 3 Naye Samweli akawaambia nyumba […]

1 Samweli 8

Israeli Waomba Mfalme 1 Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli. 2 Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli na jina la wa pili alikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba. 3 Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki. 4 Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika […]

1 Samweli 9

Samweli Anamtia Sauli Mafuta 1 Kulikuweko Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini. 2 Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote. 3 Basi punda wa Kishi baba […]

1 Samweli 10

1 Ndipo Samweli akachukua chupa ndogo ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa cha Sauli, akambusu, akisema, “Je,Bwanahakukutia mafuta uwe kiongozi juu ya watu wake Israeli? 2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na watu wawili karibu na kaburi la Raheli, huko Selsa kwenye mpaka wa Benyamini. Watakuambia, ‘Punda wale uliotoka kwenda kuwatafuta, wamekwisha kupatikana. Sasa baba […]