1 Wimbo ulio Bora wa Solomoni. Shairi La Kwanza 2 Unibusu kwa busu la kinywa chako, kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai. 3 Manukato yako yananukia vizuri, jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa. Ndiyo sababu wanawali wanakupenda! 4 Nichukue twende nawe, na tufanye haraka! Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake. Tunakushangilia na kukufurahia, […]
Category Archives: Wimbo Ulio Bora
Wimbo Ulio Bora 2
1 Mimi ni ua la waridi la Sharoni, yungiyungi ya bondeni. Mpenzi 2 Kama yungiyungi katikati ya miiba ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali. 3 Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msituni ndivyo alivyo mpenzi wangu miongoni mwa wanaume vijana. Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu, na tunda lake ni tamu kwangu. […]
Wimbo Ulio Bora 3
1 Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta huyo mwanaume lakini sikumpata. 2 Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, kupitia katika barabara zake na viwanjani; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata huyo mwanaume. 3 Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?” 4 Kitambo […]
Wimbo Ulio Bora 4
1 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! O, jinsi ulivyo mzuri! Macho yako nyuma ya shela yako ni kama ya hua. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi zikishuka kutoka Mlima Gileadi. 2 Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi, watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye […]
Wimbo Ulio Bora 5
1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, Ee wapenzi. 2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi […]
Wimbo Ulio Bora 6
1 Mpenzi wako amekwenda wapi, yule mzuri kupita wanawake wote? Mpenzi wako amegeukia njia ipi, tupate kumtafuta pamoja nawe? 2 Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake, kwenye vitalu vya vikolezo, kujilisha bustanini na kukusanya yungiyungi. 3 Mimi ni wake mpenzi wangu, na mpenzi wangu ni wangu mimi; huyu mwanaume hulisha katikati ya yungiyungi. 4 Wewe ni […]
Wimbo Ulio Bora 7
1 Ee binti wa mwana wa mfalme, tazama jinsi inavyopendeza miguu yako katika viatu! Miguu yako yenye madaha ni kama vito vya thamani, kazi ya mikono ya fundi stadi. 2 Kitovu chako ni kama bilauri ya mviringo ambayo kamwe haikosi divai iliyochanganywa. Kiuno chako ni kichuguu cha ngano kilichozungukwa kwa yungiyungi. 3 Matiti yako ni […]
Wimbo Ulio Bora 8
1 Laiti ungelikuwa kwangu kama ndugu wa kiume, ambaye aliyanyonya matiti ya mama yangu! Kisha, kama ningekukuta huko nje, ningelikubusu, wala hakuna mtu ye yote angelinidharau. 2 Ningelikuongoza na kukuleta katika nyumba ya mama yangu, yeye ambaye amenifundisha. Ningelikupa divai iliyokolezwa unywe, asali ya maua ya mikomamanga yangu. 3 Mkono wa kushoto wa huyo mwanaume […]