Mhubiri 1

Kila Kitu Ni Ubatili Mtupu 1 Maneno ya Mhubiri, mwana wa Daudi, mfalme huko Yerusalemu: 2 “Ubatili mtupu! Ubatili mtupu!” Mhubiri anasema. “Ubatili mtupu! Kila kitu ni ubatili.” 3 Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote anayotaabikia chini ya jua? 4 Vizazi huja na vizazi hupita, lakini dunia inadumu milele. 5 Jua huchomoza na […]

Mhubiri 2

Anasa Ni Ubatili 1 Nikafikiri moyoni mwangu, “Haya basi, nitakujaribu kwa anasa nione ni lipi lililo jema.” Lakini hilo nalo likaonekana ni ubatili. 2 Nikasema, “Kicheko nacho ni upumbavu. Nayo matokeo ya anasa ni nini?” 3 Nikajaribu kujifurahisha kwa mvinyo na kukumbatia upumbavu, huku bado akili yangu inaniongoza kwa hekima. Nilitaka kuona ni lipi bora […]

Mhubiri 3

Kila Jambo Lina Wakati Wake 1 Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu: 2 wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa yaliyopandwa, 3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga, 4 wakati wa […]

Mhubiri 4

Uonevu, Taabu, Uadui 1 Nikatazama tena nikaona uonevu wote uliokuwa unafanyika chini ya jua: Nikaona machozi ya walioonewa, wala hawana wa kuwafariji; uwezo ulikuwa upande wa wale wanaowaonea, wala hawana wa kuwafariji. 2 Nami nikasema kwamba wafu, waliokwisha kufa, wana furaha kuliko watu walio hai, ambao bado wanaishi. 3 Lakini aliye bora kuliko hao wawili […]

Mhubiri 5

Simama Katika Kicho Cha Mungu 1 Linda hatua zako uendapo katika nyumba ya Mungu. Karibia usikilize kuliko kutoa dhabihu ya wapumbavu, ambao hawajui kuwa wanafanya kosa. 2 Usiwe mwepesi kuzungumza, usiwe na haraka katika moyo wako kuzungumza lo lote mbele za Mungu. Mungu yuko mbinguni nawe uko duniani, kwa hiyo maneno yako na yawe machache. […]

Mhubiri 6

1 Nimeona ubaya mwingine chini ya jua, nao unalemea sana wanadamu: 2 Mungu humpa mwanadamu utajiri, mali na heshima, hivyo hakukosa cho chote moyo wake unachokitamani. Lakini Mungu hamwezeshi kuvifurahia, badala yake mgeni ndiye anayevifurahia. Hili ni ubatili, ni ubaya unaosikitisha. 3 Mtu anaweza kuwa na watoto mia moja naye akaishi miaka mingi, lakini haidhuru […]

Mhubiri 7

Hekima 1 Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa. 2 Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao. 3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa […]

Mhubiri 8

1 Ni nani aliye kama mtu mwenye hekima? Ni nani ajuaye maelezo ya mambo? Hekima hung’arisha uso wa mtu na kubadili ugumu wa uso wake. Mtii Mfalme 2 Nawaambia, Tii amri ya mfalme, kwa sababu uliapa mbele za Mungu. 3 Usiharakishe kuondoka mbele ya mfalme. Usiendelee kutenda lililo baya, kwa maana mfalme atafanya lo lote […]

Mhubiri 9

Hatima Ya Wote 1 Kwa hiyo niliyatafakari yote haya nikafikia uamuzi kwamba waadilifu na wenye hekima na yale wanayoyafanya yako mikononi mwa Mungu, lakini hakuna mtu ajuaye kama anangojewa na upendo au chuki. 2 Wote wanayo hatima inayofanana, mwadilifu na mwovu, mwema na mbaya, aliye safi na aliye najisi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa. […]

Mhubiri 10

1 Kama vile mainzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima. 2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto. 3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu. 4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache […]