1 Wafalme 1

Adonia Ajitangaza Mwenyewe Kuwa Mfalme 1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee umri ukiwa umesogea, hakuweza kupata joto hata walipomfunika kwa nguo. 2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Turuhusu tumtafute kijana mwanamwali bikira amhudumie mfalme na kumtunza. Anaweza kulala pembeni mwake ili bwana wetu mfalme apate joto.” 3 Kisha wakatafuta katika Israeli yote ili kumpata msichana mzuri […]

1 Wafalme 2

Maagizo Ya Daudi Kwa Solomoni 1 Siku zilipokaribia za Daudi kufa, akampa mwanawe Solomoni agizo. 2 Akasema, “Mimi ninakaribia kwenda njia ya dunia yote. Hivyo uwe hodari, jionyeshe kuwa mwanaume, 3 shika lileBwanaMungu wako analokuagiza: Enenda katika njia zake, ushike maagizo na amri zake, sheria zake na kanuni zake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, […]

1 Wafalme 3

Solomoni Anaomba Hekima 1 Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu laBwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu. 2 Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa […]

1 Wafalme 4

Maafisa Wa Solomoni Na Watawala 1 Basi Mfalme Solomoni akatawala Israeli yote. 2 Hawa ndio waliokuwa maafisa wake wakuu: Kuhani: Azaria mwana wa Sadoki; 3 Elihorefu na Ahiya, wana wa Shisha: waandishi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi: karani; 4 Benaya mwana wa Yehoyada: jemadari mkuu wa jeshi; Sadoki na Abiathari: makuhani; 5 Azaria mwana wa Nathani: […]

1 Wafalme 5

Maandalio Ya Ujenzi Wa Hekalu 1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi. 2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu: 3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi […]

1 Wafalme 6

Solomoni Ajenga Hekalu 1 Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa kutawala kwa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu laBwana. 2 Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili yaBwanalilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa […]

1 Wafalme 7

Solomoni Ajenga Jumba Lake La Kifalme 1 Ilimchukua Solomoni miaka kumi na mitatu kukamilisha ujenzi wa Jumba lake la kifalme. 2 Alijenga Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni, urefu wake ulikuwa dhiraa 100, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini, likiwa na safu nne za nguzo za mierezi zikishikilia boriti za mierezi […]

1 Wafalme 8

Sanduku La Agano Laletwa Hekaluni 1 Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano laBwanakutoka Sayuni, Mji wa Daudi. 2 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi […]

1 Wafalme 9

Bwana Anamtokea Solomoni 1 Solomoni alipomaliza kujenga Hekalu laBwanapamoja na jumba la kifalme, alipokwisha kufanya yote aliyotaka kufanya, 2 Bwanaakamtokea mara ya pili, kama alivyokuwa amemtokea huko Gibeoni. 3 Bwanaakamwambia: “Nimesikia dua na maombi uliyofanya mbele zangu, nimeliweka wakfu Hekalu hili ambalo umelijenga, kwa kuweka Jina langu humo milele. Macho yangu na moyo wangu utakuwa […]

1 Wafalme 10

Malkia Wa Sheba Amtembelea Solomoni 1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina laBwana, malkia alikuja kumjaribu kwa maswali magumu. 2 Alipofika Yerusalemu pamoja na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu […]