Waamuzi 1

Israeli Wapigana Na Wakanaani Waliobaki 1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamwulizaBwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?” 2 Bwanaakajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.” 3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. […]

Waamuzi 2

Malaika Wa Bwana Huko Bokimu 1 Malaika waBwanaakakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi. 2 Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu zao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili? 3 Sasa […]

Waamuzi 3

Mataifa Yaliyobaki Katika Ile Nchi 1 Haya ndiyo mataifaBwanaaliyoyaacha ili kuwajaribu Waisraeli wote ambao hawakujua vita yo yote ya Kanaani 2 (alifanya hivi ili tu kuwafundisha wazao wa Waisraeli ambao hawakuwa wamejua vita hapo awali): 3 wafalme watano wa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, Wahivi waishio katika milima ya Lebanoni kuanzia Mlima wa Baal-Hermoni hadi Lebo-Hamathi. […]

Waamuzi 4

Debora 1 Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena maovu machoni paBwana. 2 HivyoBwanaakawatia mikononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori. Jemadari wa jeshi lake alikuwa Sisera, aliyeishi huko Haroshethi-Hagoyimu. 3 Kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma yapatayo 900, naye alikuwa amewatesa Waisraeli kwa ukatili kwa muda wa miaka ishirini, Waisraeli […]

Waamuzi 5

Wimbo Wa Debora 1 Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu: 2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidiniBwana! 3 “Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! NitamwimbiaBwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidiBwana, Mungu wa Israeli. 4 “EeBwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, […]

Waamuzi 6

Gideoni 1 Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele zaBwana, naye kwa miaka sabaBwanaakawatia mikononi mwa Wamidiani. 2 Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome. 3 Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki […]

Waamuzi 7

Gideoni Awashinda Wamidiani 1 Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More. 2 Bwanaakamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. […]

Waamuzi 8

Ushindi Wa Gideoni Na Kulipiza Kisasi 1 Basi Waifraimu wakamwuliza Gideoni, “Mbona mmetutenda hivi? Kwa nini hukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakawalaumu kwa ukali sana. 2 Gideoni akawajibu, “Nilichofanya mimi ni nini kulinganisha na kile ninyi mlichofanya? Je, kuokoa masazo ya zabibu za Efraimu si bora kuliko mavuno kamili ya zabibu ya Abiezeri? 3 Mungu […]

Waamuzi 9

Abimeleki Ajaribu Kuanzisha Ufalme 1 Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu wa mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake, 2 “Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa […]

Waamuzi 10

Tola 1 Baada ya Abimeleki, Tola mwana wa Pua mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyeishi huko Shamiri, katika nchi ya vilima ya Efraimu, akainuka kuokoa Israeli. 2 Akaamua Israeli kwa miaka ishirini na mitatu. Ndipo akafa, naye akazikwa huko Shamiri. Yairi 3 Baada yake akafuatiwa na Yairi, Mgileadi, ambaye aliamua Israeli kwa miaka ishirini […]