Yeremia 1

1 Maneno ya Yeremia mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani katika mji wa Anathothi katika nchi ya Benyamini. 2 Neno laBwanalilimjia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, 3 pia wakati wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, mpaka mwezi wa tano wa […]

Yeremia 2

Israeli Amwacha Mungu 1 Neno laBwanalilinijia kusema, 2 “Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu: “ ‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako, jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi na kunifuata katika jangwa lile lote, katika nchi isiyopandwa mbegu. 3 Israeli alikuwa mtakatifu kwaBwana, malimbuko ya kwanza ya mavuno yake; wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na […]

Yeremia 3

Israeli Asiye Mwaminifu 1 “Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asemaBwana. 2 “Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi […]

Yeremia 4

1 “Ikiwa utataka kurudi, Ee Israeli, nirudie mimi,” asemaBwana. “Ikiwa utataka kuachilia mbali na macho yangu sanamu zako za kuchukiza na usiendelee kutangatanga, 2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vileBwanaaishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.” 3 Hili ndilo asemaloBwanakwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: […]

Yeremia 5

Hakuna Hata Mmoja Aliye Mkamilifu 1 “Pandeni na kushuka katika mitaa ya Yerusalemu, tazameni pande zote na mkumbuke, tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja tu atendaye kwa uaminifu na kutafuta kweli, nitausamehe mji huu. 2 Ingawa wanasema, ‘Kwa hakika kamaBwanaaishivyo,’ bado wanaapa kwa uongo.” 3 EeBwana, je, macho yako hayaitafuti kweli? […]

Yeremia 6

Yerusalemu Imezingirwa Na Jeshi 1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini na uharibifu wa kutisha. 2 Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mororo. 3 Wachungaji pamoja na makundi yao ya kondoo na mbuzi watakuja […]

Yeremia 7

Dini Za Uongo Hazina Maana 1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwaBwana: 2 “Simama kwenye lango la nyumba yaBwanana huko upige mbiu ya ujumbe huu: “ ‘Sikieni neno laBwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabuduBwana. 3 Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo […]

Yeremia 8

1 “ ‘Wakati huo, asemaBwana, mifupa ya Wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, nayo mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka katika makaburi yao. 2 Itawekwa wazi juani na kwenye mwezi na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, […]

Yeremia 9

1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia mchana na usiku kwa kuuawa kwa watu wangu. 2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri katika jangwa, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wasio waaminifu. 3 “Huweka tayari ndimi […]

Yeremia 10

Mungu Na Sanamu 1 Sikieni lile ambaloBwana, anena nanyi Ee nyumba ya Israeli. 2 Hili ndilo asemaloBwana: “Usijifunze njia za mataifa wala usitishwe na ishara katika anga, ingawa mataifa yanatishwa nazo. 3 Kwa maana desturi za mataifa hazina maana, wanakata mti kutoka msituni na fundi anauchonga kwa patasi. 4 Wanaparemba kwa fedha na dhahabu, wanakikaza […]