1 Mambo ya Nyakati 8

Ukoo Wa Sauli Mbenyamini

1 Benyamini akamzaa: Bela mzaliwa wake wa kwanza,

Ashbeli mwanawe wa pili, Ahara mwanawe wa tatu,

2 Noha mwanawe wa nne na Rafa mwanawe wa tano.

3 Wana wa Bela walikuwa:

Adari, Gera, Abihudi,

4 Abishua, Naamani, Ahoa,

5 Gera, Shefufani na Huramu.

6 Hawa ndio wazao wa Ehudi, waliokuwa viongozi wa jamaa za wale walioishi huko Geba na ambao walihamishiwa Manahathi:

7 Naamani, Ahiya na Gera. Gera alikuwa baba yao Uza na Ahihudi na ndiye aliyewaongoza kwenda uhamishoni.

8 Shaharaimu aliwazaa wana katika nchi ya Moabu baada ya kuwapa talaka wake zake wawili yaani, Hushimu na Baara.

9 Kwa mkewe Hodeshi, akawazaa wana saba: Yoabu, Sibia, Mesha, Malkamu,

10 Yeuzi, Sakia na Mirma. Hawa ndio waliokuwa wanawe, viongozi wa jamaa zao.

11 Hushimu alimzalia: Abitubu na Elpaali.

12 Wana wa Elpaali walikuwa:

Eberi, Mishamu, Shemedi (ambaye aliijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji vilivyoizunguka),

13 na Beria na Shema, ambao walikuwa viongozi wa zile jamaa zilizokuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na ambao waliwafukuza wenyeji wa Gathi.

14 Wana wa Beria walikuwa Ahio, Shashaki, Yerimothi,

15 Zebadia, Aradi, Ederi,

16 Mikaeli, Ishpa, na Yoha.

17 Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi,

18 Ishmerai, Izlia na Yobabu ndio waliokuwa wana wa Epaali.

19 Wana wa Shimei walikuwa Yakimu, Zikri, Zabdi,

20 Elienai, Zilethai, Elieli,

21 Adaya, Beraya na Shimrathi.

22 Wana wa Shashaki walikuwa Ishpani, Eberi, Elieli,

23 Abdoni, Zikri, Hanani,

24 Hanania, Elamu, Anthothiya,

25 Ifdeya na Penueli.

26 Wana wa Yerohamu walikuwa Shamsherai, Sheharia, Athalia,

27 Yaareshia, Eliya na Zikri.

28 Hawa wote walikuwa ni viongozi wa jamaa zao wakuu, kama ilivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.

29 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni.

Mke wake aliitwa Maaka.

30 Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Abdoni, wakafuatia Zuri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,

31 Gedori, Ahio, Zekeri,

32 na Miklothi ambaye alikuwa baba yake Shimea. Hawa pia waliishi karibu na jamaa zao katika Yerusalemu.

33 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli, Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.

34 Yonathani akamzaa:

# Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.

35 Wana wa Mika walikuwa:

Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi.

36 Ahazi akamzaa Yehoada. Naye Yehoada aliwazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.

37 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, Rafa akamzaa Eleasa na Aseli.

38 Aseli alikuwa na wana sita; haya ndiyo majina yao:

Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Aseli.

39 Wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa:

Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.

40 Wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kutumia upinde. Alikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla yao 150.

Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Benyamini.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1CH/8-8fac8885233ff6a0f615f14f44815b0d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

10 + six =