1 Petro 5

Kulichunga Kundi La Mungu

1 Kwa wazee waliomo miongoni mwenu, nawasihi mimi nikiwa mzee mwenzenu, shahidi wa mateso ya Kristo na mshiriki katika utukufu utakaofunuliwa,

2 lichungeni kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mkitumika kama waangalizi, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari, kama Mungu anavyowataka mwe, si kwa tamaa ya fedha, bali mlio na bidii katika kutumika.

3 Msijifanye mabwana juu ya wale walio chini ya uangalizi wenu, bali iweni vielelezo kwa hilo kundi.

4 Naye Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa mtapokea taji ya utukufu isiyoharibika.

5 Vivyo hivyo ninyi mlio vijana hamna budi kuwatii wazee. Nanyi nyote imewapasa kujivika unyenyekevu katika kuhudumiana, kila mtu na mwenzake, kwa kuwa,

“Mungu huwapinga wenye kiburi

bali huwapa wanyenyekevu neema.”

6 Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake.

7 Mtwikeni yeye fadhaa zenu zote kwa maana hujishughulisha sana na mambo yenu.

8 Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu ibilisi, kama simba angurumaye huzungukazunguka akitafuta mtu ili apate kummeza.

9 Mpingeni huyo mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kwamba mateso yayo hayo yanawapata ndugu zenu pote duniani.

10 Nanyi mkiisha kuteswa kwa kitambo kidogo, Mungu wa neema yote aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atawatengeneza upya, atawasaidia, atawatia nguvu na kuwathibitisha.

11 Uweza una yeye milele na milele. Amen.

Salamu Za Mwisho

12 Kwa msaada wa Silvano, yeye ambaye ninamhesabu kuwa ndugu mwaminifu, nimewaandikia waraka huu mfupi ili kuwatia moyo na kushuhudia kwamba hii ni neema halisi ya Mungu. Simameni imara katika neema hiyo.

13 Kanisa lililoko Babeli, lililochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu; vivyo hivyo mwanangu Marko anawasalimu.

14 Salimianeni kwa busu la upendo.

Amani iwe nanyi nyote mlio katika Kristo. Amen.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1PE/5-b774f816aa939fce279531236a4db09f.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

thirteen − 11 =