2 Mambo ya nyakati 29

Hezekia Mfalme Wa Yuda

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala. Akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.

2 Akafanya yaliyo mema machoni paBwanasawasawa na alivyokuwa amefanya Daudi baba yake.

3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa kutawala kwake alifungua milango ya Hekalu laBwana, na kuikarabati.

4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki

5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba yaBwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka katika mahali patakatifu.

6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni paBwanaMungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani yaBwanawakamgeuzia visogo vyao.

7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yo yote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.

8 Kwa hiyo, hasira yaBwanaikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.

9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.

10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano naBwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.

11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwaBwanaamewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”

12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi:

Kutoka kwa Wakohathi,

Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria;

kutoka kwa Wamerari,

Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli;

kutoka kwa Wagerishoni,

Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;

13 kutoka kwa wana wa Elisafani,

Shimri na Yeieli;

kutoka kwa wana wa Asafu,

Zekaria na Matania;

14 kutoka kwa wana wa Hemani,

Yeieli na Shimei;

kutoka kwa wana wa Yeduthuni,

Shemaya na Uzieli.

15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu laBwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno laBwana.

16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu laBwanaili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu laBwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.

17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi waBwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe laBwanawakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.

18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote laBwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.

19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu yaBwana.”

Kuabudu Hekaluni Kwarudishwa

20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwaBwana.

21 Wakaleta mafahali saba, kondoo waume saba, wana-kondoo waume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu yaBwana.

22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo waume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo waume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.

23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.

24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.

25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu laBwanawakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamuriwa naBwanakupitia manabii wake.

26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.

27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbiaBwanapamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.

28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.

29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwapo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.

30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifuBwanakwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.

31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwaBwana. Njoni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwaBwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.

32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo waume 100 na wana-kondoo waume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwaBwana.

33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.

34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.

35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa.

Kwa hiyo huduma ya Hekalu laBwanaikarudishwa kwa upya.

36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2CH/29-17faaedf66f4b0ccef965f841978faa2.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

5 − four =