Ezekieli 6

Unabii Dhidi Ya Milima Ya Israeli

1 Neno laBwanalikanijia kusema,

2 “Mwanadamu, elekeza uso wako kukabili milima ya Israeli, utabiri dhidi yake

3 na useme: ‘Ee milima ya Israeli, sikia neno laBwanaMwenyezi. Hili ndiloBwanaMwenyezi aliambiayo milima na vilima, magenge na mabonde: Ninakaribia kuleta upanga dhidi yenu, nami nitapaharibu mahali penu pote pa juu pa kuabudia miungu.

4 Madhabahu zenu zitabomolewa na madhabahu zenu za kufukizia uvumba zitavunjwavunjwa, nami nitawachinja watu wenu mbele ya sanamu zenu.

5 Nitazilaza maiti za Waisraeli mbele ya sanamu zao, nami nitatawanya mifupa yenu kuzunguka madhabahu zenu.

6 Po pote mnapoishi, miji hiyo itafanywa ukiwa na mahali pa juu pa kuabudia miungu patabomolewa, ili madhabahu zenu zifanywe ukiwa na kuharibiwa, sanamu zenu zitavunjwavunjwa na kuharibiwa, madhabahu zenu za kufukizia uvumba zitabomolewa na kila mlichokifanya kitakatiliwa mbali.

7 Watu wenu watachinjwa katikati yenu, nanyi mtatambua Mimi ndimiBwana.

8 “ ‘Lakini nitawabakiza hai baadhi yenu, kwa kuwa baadhi yenu watanusurika kuuawa watakapokuwa wametawanyika katika nchi na mataifa.

9 Ndipo katika mataifa ambamo watakuwa wamechukuliwa mateka, wale ambao watanusurika watanikumbuka, jinsi ambavyo nimehuzunishwa na mioyo yao ya uzinzi, ambayo imegeukia mbali nami na macho yao ambayo yametamani sanamu zao. Watajichukia wenyewe kwa ajili ya uovu walioutenda na kwa ajili ya desturi zao za kuchukiza.

10 Nao watajua kuwa Mimi ndimiBwana, sikuwaonya bure kuwa nitaleta maafa hayo yote juu yao.

11 “ ‘Hili ndiloBwanaMwenyezi asemalo: Piga makofi, kanyaga chini kwa mguu na upige kelele, “Ole!” kwa sababu ya maovu yote na machukizo yote yanayofanywa na nyumba ya Israeli, kwa kuwa wataanguka kwa upanga, njaa na tauni.

12 Yeye aliye mbali sana atakufa kwa tauni, naye aliye karibu atauawa kwa upanga, naye yule atakayenusurika na kubaki atakufa kwa njaa. Hivyo ndivyo nitakavyotimiza ghadhabu yangu dhidi yao.

13 Nao watajua kwamba Mimi ndimiBwana, wakati maiti za watu wao zitakapokuwa zimelala katikati ya sanamu zao kuzunguka madhabahu zao, juu ya kila kilima kilichoinuka na juu ya vilele vyote vya milima, chini ya kila mti uliotanda na kila mwaloni wenye majani, yaani, sehemu walizofukizia uvumba kwa sanamu zao zote.

14 Nami nitanyosha mkono wangu dhidi yao na kuifanya nchi yao ukiwa, kuanzia jangwani hadi Dibla, kila mahali po pote wanapoishi. Ndipo watakapojua ya kwamba Mimi ndimiBwana.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/EZK/6-5bbfc8313a70f0bcacc143ef59f154f0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

two × five =