Hesabu 11

Moto Kutoka Kwa Bwana

1 Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwaBwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwaBwanaukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.

2 Watu walipomlilia Mose, akamwombaBwana, nao moto ukazimika.

3 Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwaBwanauliwaka miongoni mwao.

Kware Kutoka Kwa Bwana

4 Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!

5 Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.

6 Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine cho chote isipokuwa hii mana!”

7 Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.

8 Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.

9 Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.

10 Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake.Bwanaakakasirika mno, naye Mose akafadhaika.

11 AkamwulizaBwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?

12 Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?

13 Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’

14 Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.

15 Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”

16 Bwanaakamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.

17 Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho ile iliyo juu yako na kuiweka hiyo Roho juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.

18 “Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama.Bwanaaliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” SasaBwanaatawapa nyama, nanyi mtaila.

19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,

20 bali kwa mwezi mzima mpaka ziwatokee puani nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataaBwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?” ’ ”

21 Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama za kula kwa mwezi mzima!’

22 Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ng’ombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”

23 Bwanaakamjibu Mose, “Je, mkono waBwanani mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema halitatimizwa kwa ajili yako au la.”

24 Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambaloBwanaalikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.

25 KishaBwanaakashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka hiyo Roho juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.

26 Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.

27 Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”

28 Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”

29 Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote waBwanawangekuwa manabii na kwambaBwanaangeweka Roho yake juu yao!”

30 Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.

31 Kisha ukatokea upepo kutoka kwaBwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.

32 Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu ye yote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.

33 Lakini wakati walipokuwa wakila nyama ingali bado kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira yaBwanaikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.

34 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.

35 Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haaserothi na kukaa huko.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NUM/11-58a1d45624f44c87cc2c9f6eeef0d02d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

15 − four =