Hosea 14

Toba Ya Kuleta Baraka

1 Rudi, Ee Israeli, kwaBwanaMungu wako.

Dhambi zako zimekuwa

ndilo anguko lako!

2 Chukueni maneno pamoja nanyi,

na mumrudieBwana.

Mwambieni:

“Samehe dhambi zetu zote

na utupokee kwa neema,

ili tuweze kutoa matunda yetu

kama sadaka za mafahali.

3 Ashuru hawezi kutuokoa,

hatutapanda farasi wa vita.

Kamwe hatutasema tena ‘Miungu yetu’

kwa kile ambacho mikono yetu wenyewe imetengeneza,

kwa kuwa kwako wewe yatima hupata huruma.”

4 “Nitaponya ukaidi wao

na kuwapenda kwa hiari yangu,

kwa kuwa hasira yangu imeondoka kwao.

5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli;

atachanua kama yungiyungi.

Kama mwerezi wa Lebanoni

atashusha mizizi yake chini;

6 matawi yake yatatanda.

Fahari yake itakuwa kama mti wa mzeituni,

harufu yake nzuri kama mwerezi wa Lebanoni.

7 Watu wataishi tena kwenye kivuli chake.

Atastawi kama nafaka.

Atachanua kama mzabibu,

nao umaarufu wake utakuwa

kama divai itokayo Lebanoni.

8 Ee Efraimu, utasema, ‘Mimi nina shughuli gani tena na sanamu?’

Nitamjibu na kumtunza.

Mimi ni kama msunobari wenye majani mabichi;

kuzaa kwako matunda kunatoka kwangu.”

9 Ni nani mwenye hekima? Atayatambua mambo haya.

Ni nani mwenye ufahamu? Huyu atayaelewa.

Njia zaBwanani adili;

wenye haki huenda katika njia hizo,

lakini waasi watajikwaa ndani yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/14-521fc4943468d9e6135356aa63b8d720.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

14 + 12 =