Isaya 18

Unabii Dhidi Ya Kushi

1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa,

kwenye mito ya Kushi,

2 iwapelekayo wajumbe wake

kwa njia ya bahari

# kwa mashua za mafunjojuu ya maji.

Nendeni, wajumbe wepesi,

kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,

kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,

taifa gomvi lenye lugha ngeni,

ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.

3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu,

ninyi mnaoishi duniani

wakati bendera itakapoinuliwa milimani,

mtaiona,

nayo tarumbeta itakapolia,

mtaisikia.

4 Hili ndiloBwanaaliloniambia:

“Nitatulia kimya na kutazama

kutoka maskani yangu,

kama joto linalometameta katika mwanga wa jua,

kama wingu la umande

katika joto la wakati wa mavuno.”

5 Kwa maana, kabla ya mavuno,

wakati wa kuchanua ukishapita

na maua yakawa zabibu zinazoiva,

atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi,

naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.

6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani

na wanyama pori,

ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi,

nao wanyama pori wakati wote wa masika.

7 Wakati huo matoleo yataletwa kwaBwanaMwenye Nguvu Zote

kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,

kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,

kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni,

ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito,

matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina laBwanaMwenye Nguvu Zote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/18-57ad4b41e9dfa662f5ab0789c6356fd2.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eleven − 4 =