Isaya 20

Unabii Dhidi Ya Misri Na Kushi

1 Katika mwaka ule ambao jemadari mkuu, alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja mpaka Ashdodi akaushambulia na kuuteka,

2 wakati uleBwanaalisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua nguo ya gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo akatembea huko na huko uchi na bila viatu.

3 KishaBwanaakasema, “Kama vile mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,

4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri na watu wa uhamisho wa Kushi uchi na bila viatu, vijana na wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.

5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.

6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa ajili ya msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/20-877f55b7e4e46243d495a2c18c32868d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eighteen − fifteen =