Kumbukumbu La Torati 28

Baraka Kwa Ajili Ya Utii

1 Kama ukimtiiBwanaMungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii,BwanaMungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia.

2 Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtiiBwanaMungu wako:

3 Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ng’ombe, na wana-kondoo wa makundi yako.

5 Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.

6 Utabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.

7 Bwanaatasababisha adui wainukao dhidi yako kushindwa mbele yako. Watakujia kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

8 Bwanaataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako.BwanaMungu wako atakubariki katika nchi anayokupa.

9 Bwanaatakufanya kuwa taifa lake takatifu, kama alivyokuahidi kwa kiapo, kama ukishika maagizo yaBwanaMungu wako na kwenda katika njia zake.

10 Kisha mataifa yote ya dunia wataona kuwa unaitwa kwa jina laBwana, nao watakuogopa.

11 Bwanaatakupa kustawi kwa wingi, katika tunda la uzao wa tumbo lako, katika wanyama wachanga wa mifugo yako na katika mazao ya ardhi yako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwapa.

12 Bwanaatafungua mbingu, ghala zake za baraka, kukupa mvua kwa majira yake na kubariki kazi zako zote za mikono yako. Utakopesha mataifa mengi lakini hutakopa kwa ye yote.

13 Bwanaatakufanya kichwa, wala si mkia. Kama utazingatia maagizo yaBwanaMungu wako ninayokupa siku hii ya leo na kuyafuata kwa bidii, daima utakuwa juu, kamwe hutakuwa chini.

14 Usihalifu amri zangu zo zote ninazokupa leo, kwa kwenda kuume au kushoto, kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.

Laana Kwa Kutokutii

15 Hata hivyo, kama hutamtiiBwanaMungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata:

16 Utalaaniwa mjini na utalaaniwa mashambani.

17 Kapu lako na chombo chako cha kukandia kitalaaniwa.

18 Uzao wa tumbo lako utalaaniwa, mazao ya ardhi yako, ndama wa makundi yako ya ng’ombe na wana-kondoo wa makundi yako.

19 Utalaaniwa uingiapo na utokapo.

20 Bwanaataleta laana juu yako, fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu unachokigusa kwa mkono wako, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa ghafula kwa ajili ya maovu uliyoyafanya kwa kumwacha yeye.

21 Bwanaatakupiga kwa magonjwa mpaka akuangamize kutoka katika nchi unayoiingia kuimiliki.

22 Bwanaatakupiga kwa magonjwa ya kudhoofisha, kwa homa na kuwashwa, hari na kwa ukame, kutu na kuwa na uchungu ambavyo vitakupiga mpaka uangamie.

23 Anga juu yako itakuwa shaba, na ardhi chini yako itakuwa chuma.

24 Bwanaatafanya mvua ya nchi yako kuwa mavumbi na mchanga; vitakujia kutoka angani mpaka uangamie.

25 Bwanaatakufanya ushindwe mbele ya adui zako. Utawajia kwa njia moja lakini utawakimbia mbele yao kwa njia saba, nawe utakuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia.

26 Mizoga yenu itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo mtu ye yote wa kuwafukuza.

27 Bwanaatakupiga kwa majipu ya Misri na kwa vidonda vitokavyo usaha na kuwashwa, ambako huwezi kuponywa.

28 Bwanaatakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili.

29 Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huko na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lo lote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyang’anywa, wala hakuna ye yote atakayekuokoa.

30 Utaposa mke, lakini mtu mwingine atakutana naye kimwili. Utajenga nyumba, lakini hutaishi ndani yake. Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutakula matunda yake.

31 Ng’ombe wako atachinjwa mbele ya macho yako lakini hutakula nyama yake. Punda wako atachukuliwa kwa nguvu kutoka kwako wala hatarudishwa. Kondoo wako watapewa adui zako, wala hakuna mtu ye yote wa kuwaokoa.

32 Wanao na binti zako watatolewa kwa mataifa mengine, nawe utayachosha macho yako ukiwatazamia siku baada ya siku, hutakuwa na nguvu kuinua mkono.

33 Taifa usilolijua watakula mazao ya nchi yako na taabu ya kazi yako, hutakuwa na cho chote, bali kuonewa kikatili siku zako zote.

34 Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu.

35 Bwanaatayapiga magoti yako na miguu yako kwa majipu yenye maumivu makali yasiyoponyeka, yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini.

36 Bwanaatakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe.

37 Utakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote hukoBwanaatakakokupeleka.

38 Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila.

39 Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila.

40 Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika.

41 Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.

42 Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.

43 Mgeni anayeishi miongoni mwako atainuka juu zaidi na zaidi kuliko wewe, lakini wewe utashuka chini zaidi na zaidi.

44 Yeye atakukopesha, lakini wewe hutamkopesha. Yeye atakuwa kichwa, lakini wewe utakuwa mkia.

45 Laana hizi zote zitakuja juu yako. Zitakufuatia na kukupata mpaka uangamizwe, kwa sababu hukumtiiBwanaMungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake aliyokupa.

46 Zitakuwa ishara na ajabu kwako na kwa wazao wako milele.

47 Kwa sababu hukumtumikiaBwanaMungu wako kwa furaha na kwa moyo wakati wa kufanikiwa kwako,

48 kwa hiyo katika njaa na kiu, katika uchi na umaskini wa kutisha, utawatumikia adui ambaoBwanaatawatuma dhidi yako. Yeye ataweka nira ya chuma shingoni mwako hadi amekwisha kukuangamiza.

49 Bwanaataleta taifa dhidi yako kutoka mbali, kutoka miisho ya dunia, kama tai ashukiavyo mawindo chini, taifa ambalo hutaijua lugha yake,

50 taifa lenye uso mkali lisilojali wazee wala kuwahurumia vijana.

51 Watakula wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako mpaka umeangamia. Hawatakuachia nafaka, divai mpya au mafuta, wala ndama wo wote wa kundi lako au wana-kondoo wa kundi lako mpaka umekuwa magofu.

52 Nao wataizingira miji yote katika nchi yako mpaka kuta ndefu za ngome ambazo unazitegemea zimeanguka. Watazingira miji yote katika nchi ambayoBwanaMungu wako anakupa.

53 Utakula uzao wa tumbo lako, nyama ya wana wako na binti zako ambaoBwanaMungu wako amekupa, kwa sababu ya mateso yale adui zako watakayokuletea wakati wa kukuzingira.

54 Hata yule mtu mwungwana sana na makini miongoni mwako hatakuwa na huruma kwa ndugu yake mwenyewe au kwa mke ampendaye au watoto wake waliosalia,

55 naye hatampa hata mmoja wao nyama ya watoto wake ambao anawala. Kwa kuwa hakuna kitu kingine kilichosalia kwake katika mazingiwa makali ambayo adui yako watakuletea kwa miji yako yote.

56 Mwanamke ambaye ni muungwana sana na makini miongoni mwako, yaani ambaye ni makini sana na muungwana kiasi kwamba asingethubutu kugusa ardhi kwa wayo wa mguu wake, yeye atakuwa mchoyo kwa mume ampendaye na mwanawe mwenyewe au binti yake,

57 kondoo la nyuma kutoka kwenye tumbo lake na watoto anaowazaa. Kwa kuwa anakusudia kuwala kwa siri wakati wa kuzingirwa na katika taabu zile ambazo adui yako atazileta juu yako na miji yako.

58 Kama hutafuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii, ambayo yameandikwa katika kitabu hiki na kama hutalicha hili jina la fahari na la kutisha, yaani laBwanaMungu wako,

59 Bwanaataleta mapigo ya kutisha juu yako na kwa wazao wako, maafa makali na ya kudumu, magonjwa mazito na ya kudumu.

60 Atakuletea juu yako magonjwa yote ya Misri yale uliyoyaogopa, nayo yataambatana nawe.

61 PiaBwanaatakuletea kila aina ya ugonjwa na maafa ambayo hayakuandikwa humu katika kitabu hiki cha sheria, mpaka utakapokuwa umeangamizwa.

62 Ninyi ambao mlikuwa wengi kama nyota za angani mtaachwa wachache tu, kwa sababu hamkumtiiBwanaMungu wenu.

63 Kama ilivyompendezaBwanakuwafanya ninyi mstawi na kuongezeka kwa idadi, ndivyo itakavyompendeza kuwaharibu na kuwaangamiza ninyi. Mtang’olewa kutoka katika nchi mnayoiingia kuimiliki.

64 KishaBwanaatawatawanya miongoni mwa mataifa yote, kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi mwingine. Huko mtaabudu miungu mingine, miungu ya miti na ya mawe, ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua.

65 Miongoni mwa mataifa hayo hamtapata raha wala mahali pa kupumzisha wayo wa mguu wenu. HukoBwanaatawapa mahangaiko ya mawazo, macho yaliyochoka kwa kungojea na moyo uliokata tamaa.

66 Utaishi katika mahangaiko siku zote, ukiwa umejaa hofu usiku na mchana, wala hutakuwa kamwe na uhakika wa maisha yako.

67 Wakati wa asubuhi utasema hivi, “Laiti ingekuwa jioni!” Jioni utasema, “Laiti ingekuwa asubuhi,” kwa sababu ya hofu ile itakayojaza moyo wako na vitu vile macho yako yatakavyoviona.

68 Bwanaatawarudisha tena Misri kwa meli, safari niliyosema kamwe hamngeenda tena. Huko mtajiuza ninyi wenyewe kwa adui zenu kama watumwa wa kiume na wa kike, lakini hakuna ye yote atakayewanunua.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/28-6fbea6aabb2e7d221f9ac2e45f31a268.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eight + 18 =