Kumbukumbu La Torati 33

Mose Anayabariki Makabila

1 Hii ndiyo baraka Mose mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake.

2 Alisema:

“Bwanaalikuja kutoka Mlima Sinai,

akachomoza kama jua juu yao

kutoka Mlima Seiri,

akaangaza kutoka Mlima Parani.

Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu

kutoka kusini,

kutoka matelemko ya mlima wake.

3 Hakika ni wewe ambaye huwapenda watu,

watakatifu wako wote wamo mkononi mwako.

Miguuni pako wote wanasujudu

na kutoka kwako wanapokea mafundisho,

4 sheria ile Mose aliyotupa sisi,

tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.

5 Alikuwa mfalme juu ya Yeshuruni

wakati viongozi wa watu walipokusanyika,

pamoja na makabila ya Israeli.

6 “Reubeni na aishi, asife,

wala watu wake wasiwe wachache.”

7 Akasema hili kuhusu Yuda:

“EeBwana, sikia kilio cha Yuda,

mlete kwa watu wake.

Kwa mikono yake mwenyewe hujitetea.

Naam, uwe msaada wake

dhidi ya adui zake!”

8 Kuhusu Lawi alisema:

# “Thumimu yako na Urimuyako ulimpa,

mtu yule aliyewaminifu kwako.

Ulimjaribu huko Masa

na kushindana naye

kwenye maji ya Meriba.

9 Alinena hivi kuhusu baba yake na mama yake,

‘Mimi siwahitaji kamwe.’

Akawasahau jamaa zake,

asiwatambue hata watoto wake,

lakini akaliangalia neno lako

na kulilinda Agano lako.

10 Humfundisha Yakobo mausia yako

na Israeli sheria yako.

Hufukiza uvumba mbele zako

na sadaka nzima za kuteketezwa

juu ya madhabahu yako.

11 EeBwana, bariki ustadi wake wote,

nawe upendezwe na kazi ya mikono yake.

Vipige viuno vya wale wainukao dhidi yake;

wapige adui zake hata wasiinuke tena.”

12 Kuhusu Benyamini akasema:

“Mwache mpenzi waBwana

apumzike salama kwake,

kwa maana humkinga mchana kutwa,

na yuleBwanaampendaye

hupumzika kati ya mabega yake.”

13 Kuhusu Yosefu akasema:

“Bwanana aibariki nchi yake

kwa umande wa thamani

kutoka mbinguni juu,

na vilindi vya maji

vilivyotulia chini;

14 pamoja na vitu vilivyo bora sana

viletwavyo na jua,

na vitu vizuri sana vinavyoweza

kutolewa na mwezi;

15 pamoja na zawadi bora sana

za milima ya zamani

na kwa wingi wa baraka

za vilima vya milele;

16 pamoja na baraka nzuri mno

za ardhi na ukamilifu wake,

na upendeleo wake yeye

aliyeishi kwenye kichaka

kilichokuwa kinawaka moto.

Hivi vyote na vikae juu ya kichwa cha Yosefu,

juu ya paji la uso la aliye mkuu

miongoni mwa ndugu zake.

17 Katika fahari yeye ni kama fahali mzaliwa wa kwanza;

pembe zake ni pembe za nyati,

na kwa pembe hizo atapiga mataifa,

hata yaliyo miisho ya dunia.

Hivyo ndivyo yalivyo makumi elfu ya Efraimu;

hivyo ndivyo yalivyo maelfu ya Manase.”

18 Kuhusu Zabuloni akasema:

“Shangilia, Zabuloni, wakati wa kutoka nje,

nawe Isakari, katika mahema yako.

19 Watawaita mataifa kwenye mlima,

na huko mtatoa dhabihu za haki;

watajifurahisha kwa wingi uliojaza bahari,

kwa hazina zilizofichwa mchangani.”

20 Kuhusu Gadi akasema:

“Atabarikiwa yeye aongezaye milki ya Gadi!

Gadi huishi huko kama simba,

akirarua kwenye mkono au kichwa.

21 Alijichagulia nchi nzuri kuliko zote

kwa ajili yake mwenyewe;

fungu la kiongozi lilikuwa limehifadhiwa

kwa ajili yake.

Viongozi wa watu walipokusanyika,

alitimiza haki ya mapenzi yaBwana,

na hukumu zake kuhusu Israeli.”

22 Kuhusu Dani akasema:

“Dani ni mwana simba,

akiruka kutoka Bashani.”

23 Kuhusu Naftali akasema:

“Naftali amejaa tele upendeleo waBwana,

naye amejaa baraka yake;

atarithi magharibi na kusini.”

24 Kuhusu Asheri akasema:

“Mbarikiwa zaidi sana katika wana ni Asheri;

yeye na apate upendeleo kwa ndugu zake,

yeye na anawe miguu yake kwenye mafuta.

25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba,

nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.

26 “Hakuna mwingine kama Mungu wa Yeshuruni,

ambaye hupanda juu ya mbingu ili akusaidie,

na juu ya mawingu katika utukufu wake.

27 Mungu wa milele ni kimbilio lako,

na chini kuna mikono ya milele.

Atamfukuza adui yako mbele yako,

akisema, ‘Mwangamize yeye!’

28 Hivyo Israeli ataishi salama peke yake.

Mzao wa Yakobo ni salama

katika nchi ya nafaka na divai mpya,

mahali ambapo mbingu

hudondosha umande.

29 Ee Israeli, wewe umebarikiwa!

Ni nani kama wewe,

taifa lililookolewa naBwana?

Yeye ni ngao yako na msaada wako,

na upanga wako uliotukuka.

Adui zako watatetemeka mbele yako,

nawe utapakanyaga

# mahali pao pa juu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/33-a6c4e364662300629ffa031e84f19aaf.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

4 + 14 =