Kumbukumbu La Torati 4

Waamriwa Utii

1 Sikia sasa, Ee Israeli, amri na sheria nitakazokufundisha wewe. Zifuate ili upate kuishi na uingie kuimiliki nchi ambayoBwana, Mungu wa baba zako anawapa.

2 Usiongeze wala usipunguze cho chote ninachowaamuru ninyi, ila myashike maagizo yaBwanaMungu wenu ambayo nawapa.

3 Mliona kwa macho yenu wenyewe kileBwanaalichokifanya kule Baal-Peori.BwanaMungu wenu aliwaangamiza kutoka miongoni mwenu kila mmoja aliyemfuata Baali wa Peori,

4 lakini ninyi nyote mlioshikamana naBwanakwa uthabiti, Mungu wenu, mko hai mpaka leo.

5 Tazama, nimewafundisha amri na sheria kamaBwanaMungu wangu alivyoniamuru mimi, ili mzifuate katika nchi mnayoiingia kuimiliki.

6 Zishikeni kwa uangalifu, kwa kuwa hii itaonyesha hekima na ufahamu wenu kwa mataifa, ambayo yatasikia kuhusu amri zote hizi, nao watasema, “Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na ufahamu.”

7 Ni taifa gani jingine lililo kubwa kiasi cha kuwa na miungu yao iliyo karibu nao kamaBwanaMungu wetu alivyo karibu nasi wakati wo wote tunapomwomba?

8 Nalo ni taifa gani jingine lililo kubwa hivi lenye kuwa na amri na sheria za haki kama hizi ninazoweka mbele yenu leo?

9 Mwe waangalifu, na makini ili msije mkasahau mambo ambayo mliyaona kwa macho yenu, wala kuyaacha yaondoke moyoni mwenu siku zote za uhai wenu. Mwafundishe hayo watoto wenu na watoto wao baada yao.

10 Kumbuka siku uliyosimama mbele zaBwanaMungu wako kule Horebu, wakati aliponiambia, “Wakutanishe watu mbele yangu wasikie maneno yangu ili kwamba waweze kujifunza kuniheshimu kwa muda wote watakaoishi katika nchi, nao waweze kuwafundisha watoto wao maneno hayo.”

11 Mlisogea karibu na mkasimama chini ya mlima wakati ulipowaka moto mpaka mbinguni juu, pamoja na mawingu meusi na giza nene.

12 NdipoBwanaalipozungumza nanyi kutoka katika moto. Mkasikia sauti ya maneno lakini hamkuona umbo, kulikuwa na sauti tu.

13 Aliwatangazia Agano lake na Amri Kumi, ambazo aliwaamuru mzifuate, kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe.

14 NayeBwanaalinielekeza wakati huo kuwafundisha ninyi sheria na amri ambazo mnapaswa kuzifuata katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.

Kuabudu Sanamu Kwakatazwa

15 Hamkuona umbo la aina yo yote siku ambayoBwanaalizungumza na ninyi kule Horebu kutoka kwenye moto. Kwa hiyo mjihadhari kwa uangalifu sana,

16 ili msije mkajichafua na kujitengenezea sanamu au kinyago chenye umbo lo lote kama la mwanaume au mwanamke,

17 au kama mnyama aliye juu ya nchi au ndege ye yote arukaye angani,

18 au kama kiumbe kitambaacho juu ya ardhi au samaki ye yote aliye ndani ya maji.

19 Na utazamapo juu angani na ukaliona jua, mwezi na nyota na vyote vinavyoipamba mbingu, usije ukashawishiwa kuviinamia na kuviabudu vile ambavyoBwanaMungu wenu alivyogawia mataifa yote chini ya mbingu.

20 Lakini kwenu ninyi,Bwanaamewatoa kutoka kwenye tanuru ya kuyeyushia chuma, katika Misri kuwa watu wa urithi wake kama mlivyo sasa.

21 Bwanaalinikasirikia kwa sababu yenu na akaapa kwamba sitavuka Yordani kuingia katika nchi nzuriBwanaMungu wenu anayowapa kuwa urithi wenu.

22 Nitakufa katika nchi hii; sitavuka Yordani, lakini ninyi ni karibu mvuke mkaimiliki ile nchi nzuri.

23 Jihadharini msilisahau Agano laBwanaMungu wenu lile alilofanya nanyi; msijitengenezee sanamu katika umbo la kitu cho chote ambachoBwanaMungu wenu amewakataza.

24 Kwa kuwaBwanaMungu wenu ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.

25 Baada ya kuwa na watoto na wajukuu na kuishi katika nchi hiyo siku nyingi, tena kama mkijichafua na kutengeneza sanamu ya aina yo yote, mkifanya maovu machoni paBwanaMungu wenu na kumfanya awe na hasira,

26 ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yenu siku hii kwamba mtaangamia mara moja kutoka katika nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki. Hamtaishi kule kwa muda mrefu bali kwa hakika mtaangamizwa.

27 Bwanaatawatawanya miongoni mwa mataifa, na ni wachache wenu tu watakaosalia miongoni mwa mataifa hayo ambayoBwanaatawafukuzia.

28 Huko mtaabudu miungu ya miti na mawe iliyotengenezwa na watu, ambayo haiwezi kuona au kusikia wala kula au kunusa.

29 Lakini kama mtamtafutaBwanaMungu wenu, mtampata; kama mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yote.

30 Wakati mnapokuwa katika dhiki, nayo mambo haya yote yamewatokea siku hizo, ndipo mtamrudiaBwanaMungu wenu na kumtii.

31 Kwa maanaBwanaMungu wenu ni Mungu mwenye huruma, hatawaacha au kuwaangamiza wala kusahau Agano alilofanya na baba zenu, alilowathibitishia kwa kiapo.

Bwana Ndiye Mungu

32 Sasa uliza kuhusu siku za zamani, zamani kabla ya wakati wako, tangu siku ile Mungu alipomwumba mtu juu ya nchi, uliza kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kumepata kutokea jambo jingine lililo kubwa kama hili, au kuna jambo jingine kama hilo limepata kusikiwa?

33 Je, kuna watu wengine wo wote waliosikia sauti ya Mungu ikizungumza kwenye moto, kama mlivyosikia, nao wakaishi?

34 Je, kuna mungu ye yote amepata kujaribu mwenyewe kuchukua taifa moja kutoka taifa lingine, kwa mapigo, kwa ishara za miujiza na maajabu, kwa vita, kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa au kwa matendo makuu yakutisha, kama yale ambayoBwanaMungu wenu aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu?

35 Mlionyeshwa mambo haya ili mpate kujua kuwaBwanandiye Mungu; hakuna mwingine ila yeye.

36 Kutoka mbinguni amewasikizisha sauti yake ili kuwaadilisha. Hapa duniani aliwaonyesha moto wake mkubwa, nanyi mlisikia maneno yake kutoka kwenye ule moto.

37 Kwa sababu aliwapenda baba zenu na alichagua wazao wao baada yao, aliwatoa katika nchi ya Misri kwa Uwepo wake na kwa uwezo wake mkuu,

38 aliwafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi na kuwaleta ninyi katika nchi yao na akawapa ninyi kuwa urithi wenu, kama ilivyo leo.

39 Kubalini na mweke moyoni leo kuwaBwanandiye Mungu mbinguni juu na duniani chini. Hakuna mwingine.

40 Mshike amri na maagizo yake ninayowapa leo, ili mpate kufanikiwa ninyi na watoto wenu baada yenu, na mpate kuishi maisha marefu katika nchi awapayoBwanaMungu wenu siku zote.

Miji Ya Makimbilio

41 Kisha Mose akatenga miji mitatu mashariki ya Yordani,

42 ambayo mtu ye yote aliyemwua mtu angeweza kukimbilia ikiwa amemwua jirani yake bila kukusudia na bila kuwa na chuki naye siku zilizopita. Angeweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake.

43 Miji hiyo ilikuwa: Beseri katika tambarare ya jangwa kwa ajili ya Wareubeni; Ramoth katika nchi ya Gileadi kwa ajili ya Wagadi; nao mji wa Golani katika nchi ya Bashani kwa ajili ya Wamanase.

Utangulizi Wa Sheria

44 Hii ndiyo sheria Mose aliyoweka mbele ya Waisraeli.

45 Haya ndiyo masharti, amri na sheria Mose aliyowapa wakati walipotoka Misri,

46 nao walikuwa katika bonde karibu na Beth-Peori mashariki ya Yordani, katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, naye alishindwa na Mose na Waisraeli walipokuja toka Misri.

47 Waliimiliki nchi yake na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, wafalme hao wawili waliotawala mashariki ya Yordani.

48 Nchi hii ilienea kutoka Aroeri ukingoni mwa Bonde la Arnoni mpaka Mlima Sioni (yaani Hermoni),

49 pamoja na eneo lote la Araba mashariki ya Yordani, na kuenea mpaka Bahari ya Araba kwenye mitelemko ya Pisga.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/4-e54feee2029e3988abaff35b8a4b587e.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

19 − four =