Kutoka 16

Mana Na Kware

1 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka Elimu, wakafika Jangwa la Sini, lililokuwa kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka Misri.

2 Huko jangwani hiyo jumuiya yote ikamnung’unikia Mose na Aroni.

3 Waisraeli wakawaambia, “Laiti tungelikufa kwa mkono waBwanahuko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa.”

4 KishaBwanaakamwambia Mose, “Nitanyesha mikate kutoka mbinguni kwa ajili yenu. Watu watatoka kila siku na kukusanya kitakachowatosha kwa siku ile, kwa njia hii, nitawajaribu nione kama watafuata maelekezo yangu.

5 Siku ya sita watatayarisha kile waletacho ndani, nacho kitakuwa mara mbili kuliko ya kile walichokusanya kila siku.”

6 Kwa hiyo Mose na Aroni wakawaambia Waisraeli wote, “Jioni mtajua kwambaBwanandiye aliyewatoa katika Misri,

7 kisha asubuhi mtauona utukufu waBwana, kwa sababu amesikia manung’uniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani hata mtunung’unikie?”

8 Pia Mose akasema, “Mtajua kuwa alikuwaBwanawakati atakapowapa nyama mle ifikapo jioni na mikate yote mtakayohitaji asubuhi kwa sababu amesikia manung’uniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani? Hamnung’uniki dhidi yetu, bali dhidi yaBwana.”

9 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli kwamba, ‘Mje mbele zakeBwana, kwa maana amesikia manung’uniko yenu.’ ”

10 Aroni alipokuwa akizungumza na jumuiya yote ya Waisraeli, wakatazama kuelekea jangwani, na huko wakaona utukufu waBwanaukitokeza katika wingu.

11 Bwanaakamwambia Mose,

12 “Nimesikia manung’uniko ya Waisraeli. Waambie, ‘Jioni mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate. Ndipo mtajua ya kwamba Mimi ndimiBwanaMungu wenu.’ ”

13 Jioni ile kware wakaja wakaifunika kambi na asubuhi kulikuwa na tabaka la umande kuzunguka kambi.

14 Wakati umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya uso wa jangwa.

15 Waisraeli walipoona, wakaambiana, “Hiki ni nini?” Kwa kuwa hawakujua kilikuwa kitu gani.

Mose akawaambia, “Huu ndio mkate ambaoBwanaamewapa mle.

16 Hivi ndivyoBwanaalivyoamuru: ‘Kila mmoja akusanye kiasi anachohitaji. Chukueni pishimoja kwa kila mtu mliye naye katika hema yenu.’ ”

17 Waisraeli wakafanya kama walivyoambiwa, baadhi yao wakakusanya zaidi, wengine pungufu.

18 Nao walipopima katika pishi, yule aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, pia yule aliyekusanya kidogo hakuwa na upungufu. Kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji.

19 Kisha Mose akawaambia, “Mtu ye yote asibakize cho chote mpaka asubuhi.”

20 Hata hivyo, wengine hawakuzingatia aliyosema Mose, wakahifadhi kiasi fulani mpaka asubuhi, lakini kile alichohifadhi kikajaa mabuu na kuanza kunuka. Kwa hiyo Mose akawakasirikia.

21 Kila asubuhi, kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji na jua lilipokuwa kali, iliyeyuka.

22 Siku ya sita, wakakusanya mara mbili, kiasi cha pishi mbili kwa kila mtu, nao viongozi wa jumuiya wakaja kumwuarifu Mose.

23 Mose akawaambia, “Hivi ndivyo alivyoagizaBwana: ‘Kesho itakuwa siku ya mapumziko, Sabato takatifu kwaBwana. Kwa hiyo okeni kile mnachotaka kuoka na mchemshe kile mnachotaka kuchemsha. Hifadhini cho chote kinachobaki na mkiweke mpaka asubuhi.’ ”

24 Kwa hiyo wakavihifadhi mpaka asubuhi, kama Mose alivyoagiza, na havikunuka wala kuwa na mabuu.

25 Mose akawaambia, “Kuleni leo, kwa sababu leo ni Sabato kwaBwana. Hamtapata cho chote juu ya nchi leo.

26 Kwa siku sita mtakusanya, lakini siku ya saba, yaani Sabato, hakutakuwepo cho chote.”

27 Hata hivyo, baadhi ya watu wakatoka kwenda kukusanya siku ya saba, lakini hawakupata cho chote.

28 NdipoBwanaakamwambia Mose, “Je, mtaacha kushika maagizo na maelekezo yangu mpaka lini?

29 Fahamuni kuwaBwanaamewapa ninyi Sabato, ndiyo sababu katika siku ya sita amewapa mikate ya siku mbili. Kila mmoja inampasa kukaa pale alipo katika siku ya saba. Hata mmoja haruhusiwi kutoka.”

30 Kwa hiyo watu wakapumzika siku ya saba.

31 Watu wa Israeli wakaita ile mikate mana. Ilikuwa myeupe kama mbegu za mtama na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotengenezwa kwa asali.

32 Mose akasema, “Hivi ndivyo alivyoagizaBwana: ‘Chukueni pishi ya mana na kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo ili vione mikate niliyowapa mle jangwani nilipowatoa katika nchi ya Misri.’ ”

33 Kwa hiyo Mose akamwambia Aroni, “Chukua gudulia na uweke pishi moja ya mana ndani yake. Kisha uweke mbele zaBwanaili kihifadhiwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.”

34 KamaBwanaalivyomwagiza Mose, hatimaye Aroni alikuja kuihifadhi ndani ya Sanduku la Ushuhuda.

35 Waisraeli wakala mana kwa miaka arobaini, mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu; walikula mana mpaka walipofika mpakani mwa Kanaani.

36 (Pishi moja ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.)

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/EXO/16-021c3b6793586c4779042bb2798f880c.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

two × one =