Kutoka 30

Madhabahu Ya Kufukizia Uvumba

1 “Tengeneza madhabahu ya mti wa mshita kwa ajili ya kufukizia uvumba.

2 Madhabahu iwe mraba, urefu na upana wa dhiraa mojana kimo cha dhiraa mbili, pembe zake zitakuwa za kitu kimoja nayo.

3 Funika juu ya hiyo madhabahu, na pande zote na pembe zake kwa dhahabu safi, na ufanyize ukingo wa dhahabu kuizunguka.

4 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, nyingine mbili upande wa pili ili kushika hiyo mipiko itumikayo wakati wa kuibeba.

5 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita na uifunike kwa dhahabu.

6 Weka hiyo madhabahu mbele ya lile pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, lililo mbele ya kiti cha rehema kilicho juu ya Sanduku la Ushuhuda, mahali ambapo nitakutana nawe.

7 “Itampasa Aroni kufukiza uvumba wenye harufu nzuri juu ya madhabahu kila siku asubuhi wakati anapowasha zile taa.

8 Itampasa afukize uvumba tena wakati anapowasha taa wakati wa machweo ili uvumba ufukizwe daima mbele zaBwanakwa vizazi vijavyo.

9 Usifukize uvumba mwingine wo wote juu ya madhabahu hii au sadaka nyingine yo yote ya kuteketezwa wala sadaka ya nafaka, wala usimimine sadaka ya kinywaji juu yake.

10 Mara moja kwa mwaka Aroni atafanya upatanisho juu ya pembe za hiyo madhabahu. Upatanisho huu wa mwaka lazima ufanywe kwa damu ya sadaka ya upatanisho kwa ajili ya dhambi kwa vizazi vijavyo. Ni takatifu sana kwaBwana.”

Fedha Ya Upatanisho

11 NayeBwanaakamwambia Mose,

12 “Utakapowahesabu Waisraeli, kila mmoja lazima alipe kwaBwanafidia kwa ajili ya nafsi yake wakati wa kuhesabiwa kwake. Ndipo hakutakuwa na pigo juu yao unapowahesabu.

13 Kila mmoja anayekwenda upande wa wale waliokwisha hesabiwa atatoa nusu shekeli, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini. Hii nusu shekeli ni sadaka kwaBwana.

14 Wote wale wanaovuka, wenye umri wa miaka ishirini au zaidi, watatoa sadaka kwaBwana.

15 Matajiri hawatalipa zaidi ya nusu shekeli, nao maskini hawatatoa pungufu wakati mnatoa sadaka kwaBwanakwa kufanya upatanisho wa nafsi zenu.

16 Utapokea fedha ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli na uzitumie kwa ajili ya huduma ya Hema la Kukutania. Itakuwa ni ukumbusho kwa Waisraeli mbele zaBwanakufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.”

Sinia La Kunawia

17 KishaBwanaakamwambia Mose,

18 “Tengeneza sinia la shaba, lenye kishikilio cha shaba kwa ajili ya kunawia. Liweke kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, kisha weka maji ndani yake.

19 Aroni na wanawe watanawa mikono na miguu yao kwa maji yatokayo katika hilo sinia.

20 Wakati wo wote wanapoingia katika Hema la Kukutania, watanawa kwa maji ili kwamba wasije wakafa. Pia, wanapokaribia madhabahu ili kuhudumu kwa kuleta sadaka zilizotolewa kwaBwanakwa moto,

21 watanawa mikono na miguu yao ili kwamba wasije wakafa. Hii itakuwa ni amri ya kudumu kwa ajili ya Aroni na wazao wake kwa vizazi vijavyo.”

Mafuta Ya Upako

22 KishaBwanaakamwambia Mose,

23 “Chukua vikolezi bora vifuatavyo: shekeli 500za manemane ya maji, shekeli 250za mdalasini wenye harufu nzuri, shekeli 250 za miwa yenye harufu nzuri,

24 shekeli 500 za aina nyingine ya mdalasini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, pia hiniya mafuta ya zeituni.

25 Vikolezi hivi vitengeneze kuwa mafuta matakatifu ya upako yenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Yatakuwa mafuta matakatifu ya upako.

26 Kisha yatumie kupaka hilo Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda,

27 meza na vifaa vyake vyote, kinara cha taa na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba,

28 madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote na sinia pamoja na kitako chake.

29 Utaviweka wakfu ili viwe vitakatifu sana na kila kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.

30 “Mtie Aroni na wanawe mafuta na uwaweke wakfu ili waweze kunitumikia katika kazi ya ukuhani.

31 Waambie Waisraeli, ‘Haya yatakuwa mafuta matakatifu yangu ya upako kwa vizazi vijavyo.

32 Usiyamimine juu ya miili ya wanadamu wala usitengeneze mafuta ya aina nyingine kwa utaratibu huu. Ni mafuta matakatifu na ni lazima myaone kuwa ni matakatifu.

33 Mtu ye yote atakayetengeneza manukato kama hayo na ye yote atakayeyamimina juu ya mtu ye yote ambaye si kuhani atakatiliwa mbali na watu wake.’ ”

Uvumba

34 KishaBwanaakamwambia Mose, “Chukua vikolezi vyenye harufu nzuri vifuatavyo: natafi, shekelethi, kelbena na uvumba safi vyote vikiwa na vipimo sawa,

35 pia tengeneza mchanganyiko wa uvumba wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Utiwe chumvi ili upate kuwa safi na mtakatifu.

36 Saga baadhi yake kuwa unga na uweke mbele ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Hema la Kukutania, mahali ambapo nitakutana nawe. Itakuwa takatifu sana kwenu.

37 Msitengeneze uvumba mwingine wo wote wa namna hii kwa ajili yenu wenyewe; uoneni kuwa ni mtakatifu kwaBwana.

38 Ye yote atakayetengeneza uvumba kama huu ili kufurahia harufu yake nzuri lazima akatiliwe mbali na watu wake.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/EXO/30-f855ef22ca0022d537eab1870226f7ba.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

9 + 17 =