Kutoka 34

Vibao Vipya Vya Mawe

1 Bwanaakamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.

2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.

3 Mtu ye yote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu po pote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ng’ombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”

4 Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kamaBwanaalivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.

5 KishaBwanaakashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake,Bwana.

6 Bwanaakapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana,Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,

7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”

8 Mara Mose akasujudu na kuabudu.

9 Mose akasema, “EeBwana, kama nimepata kibali mbele zako, basiBwanauende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”

10 KishaBwanaakasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lo lote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimiBwanawenu.

11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.

13 Bomoa madhabahu zao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.

14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwaBwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.

15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.

16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.

17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.

18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamuriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.

19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ng’ombe au wa kondoo au mbuzi.

20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume.

“Mtu ye yote asije mbele zangu mikono mitupu.

21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.

22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka.

23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele zaBwanaMwenyezi, Mungu wa Israeli.

24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu ye yote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana naBwanaMungu wako.

25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu cho chote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yo yote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.

26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba yaBwanaMungu wako.

“Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”

27 KishaBwanaakamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”

28 Mose alikuwa huko pamoja naBwanakwa siku arobaini mchana na usiku bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.

Mng’ao Wa Uso Wa Mose

29 Mose alipotelemka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa uking’aa, kwa sababu alikuwa amezungumza naBwana.

30 Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unang’aa, waliogopa kumkaribia.

31 Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.

32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zoteBwanaalizompa katika Mlima wa Sinai.

33 Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.

34 Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele zaBwanakuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,

35 waliona kuwa uso wake unang’aa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza naBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/EXO/34-b3222e117fa8dbf0ba215956e619cab6.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

8 − six =