Nehemiah 1

Maombi Ya Nehemia

1 Maneno ya Nehemia mwana wa Hakalia:

# Katika mwezi wa Kisleukatika mwaka wa ishirini, wakati nikiwa ngomeni katika jumba la kifalme la Shushani,

2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, alikuja kutoka Yuda akiwa na watu wengine, nami nikawauliza kuhusu mabaki ya Wayahudi walionusurika kwenda uhamishoni na pia kuhusu Yerusalemu.

3 Wakaniambia, “Wale walionusurika kwenda uhamishoni nao wamerudi kwenye lile jimbo wako katika taabu kubwa na aibu. Ukuta wa Yerusalemu umebomoka, na malango yake yamechomwa moto.”

4 Niliposikia mambo haya, niliketi na kulia. Kwa siku kadhaa niliomboleza na kufunga na kuomba mbele za Mungu wa mbinguni.

5 Kisha nikasema:

“EeBwana, Mungu wa mbinguni, mkuu na mwenye kuogofya, ambaye hulishika Agano lake la upendo na wale wampendao na kutii amri zake,

6 masikio yako na yawe masikivu na macho yako yafunguke ili usikie maombi ya mtumishi wako anayoomba mbele yako mchana na usiku kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli. Ninaungama dhambi zetu sisi Waisraeli, pamoja na zangu na za nyumba ya baba yangu, tulizotenda dhidi yako.

7 Tumetenda kwa uovu sana mbele zako. Hatukutii amri, maagizo wala sheria ulizompa Mose mtumishi wako.

8 “Kumbuka agizo ulilompa Mose mtumishi wako, ukisema, ‘Kama mkikosa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa,

9 lakini mkinirudia na kutii amri zangu, ndipo hata kama watu wenu walio uhamishoni wako mbali sana katika miisho ya dunia, nitawakusanya kutoka huko na kuwaleta mahali ambapo nimepachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina langu.’

10 “Hawa ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa nguvu zako kuu na mkono wako wenye nguvu.

11 Ee Bwana, tega sikio lako na usikie maombi ya huyu mtumishi wako na maombi ya watumishi wako wanaofurahia kuliheshimu Jina lako. Umpe leo mtumishi wako mafanikio kwa kumpa kibali mbele ya mtu huyu.”

Kwa maana nilikuwa mnyweshaji wa mfalme.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NEH/1-16ec27541f7ee4ac63cf57bd66e158bd.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

2 + 16 =