Yeremia 30

Kurudishwa kwa Israeli

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwaBwana:

2 “Hili ndilo asemaloBwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.

3 Siku zinakuja,’ asemaBwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asemaBwana.”

4 Haya ndiyo manenoBwanaaliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:

5 “Hili ndilo asemaloBwana:

“ ‘Vilio vya woga vinasikika:

hofu kuu wala si amani.

6 Ulizeni na mkaone:

Je, mwanaume aweza kuzaa watoto?

Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu

ameweka mikono yake tumboni

kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa,

kila uso umegeuka rangi kabisa?

7 Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha!

Hakutakuwa na nyingine mfano wake.

Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo,

lakini ataokolewa kutoka katika hiyo.

8 “ ‘Katika siku ile,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote,

‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao

na kuvipasua vifungo vyao;

wageni hawatawafanya tena watumwa.

9 Badala yake, watamtumikiaBwana, Mungu wao

na Daudi mfalme wao,

nitakayemwinua kwa ajili yao.

10 “ ‘Hivyo usiogope, Ee Yakobo mtumishi wangu,

usifadhaike, Ee Israeli,’

asemaBwana.

‘Hakika, nitakuokoa wewe kutoka mahali pa mbali,

wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao,

Yakobo atakuwa tena na amani na usalama,

wala hakuna atakayemtia hofu.

11 Mimi niko pamoja nawe nami nitakuokoa,’

asemaBwana.

‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote

ambamo miongoni mwao nimewatawanya,

sitawaangamiza ninyi kabisa.

Nitawaadhibu, lakini kwa haki.

Sitawaacha kabisa bila adhabu.’

12 “Hili ndilo asemaloBwana:

“ ‘Kidonda chako hakina dawa,

jeraha lako haliponyeki.

13 Hakuna ye yote wa kukutetea shauri lako,

hakuna dawa ya kidonda chako,

wewe hutapona.

14 Wale walioungana nawe wote wamekusahau,

hawajali cho chote kukuhusu wewe.

Nimekupiga kama vile ambavyo adui angelifanya

na kukuadhibu kama vile ambavyo

mtu mkatili angelifanya,

kwa sababu hatia yako ni kubwa mno

na dhambi zako ni nyingi sana.

15 Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako,

yale maumivu yako yasiyoponyeka?

Kwa sababu ya uovu wako mkubwa

na dhambi zako nyingi

nimekufanyia mambo haya.

16 “ ‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa;

adui zako wote watakwenda uhamishoni.

Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara;

wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.

17 Lakini nitakurudishia afya yako

na kuyaponya majeraha yako,’

asemaBwana,

‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa,

Sayuni ambaye hakuna ye yote anayekujali.’

18 “Hili ndilo asemaloBwana:

“ ‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo

na kuhurumia maskani yake.

Mji utajengwa tena juu ya magofu yake,

nalo jumba la kifalme litasimama

mahali pake halisi.

19 Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao

na sauti ya furaha.

Nitaiongeza idadi yao

wala hawatapungua,

nitawapa heshima

na hawatadharauliwa.

20 Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa

siku za zamani,

nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu;

nitawaadhibu wale wote wawaoneao.

21 Mmoja wao atakuwa kiongozi wao;

mtawala wao atainuka miongoni mwao.

Nitamleta karibu nami naye atanikaribia mimi,

kwa maana ni nani yule atakayejitolea

kuwa karibu nami?’

asemaBwana.

22 ‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu,

nami nitakuwa Mungu wenu.’ ”

23 Tazama, tufani yaBwana

italipuka kwa ghadhabu,

upepo wa kisulisuli uendao kasi

utashuka juu ya vichwa vya waovu.

24 Hasira kali yaBwanahaitarudi nyuma

mpaka atakapotimiza

makusudi yote ya moyo wake.

Siku zijazo

mtayaelewa haya.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/30-b858b21008b4995dad5e3ad2b0161b92.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

19 + fifteen =