Kurudishwa kwa Israeli
1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwaBwana:
2 “Hili ndilo asemaloBwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
3 Siku zinakuja,’ asemaBwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asemaBwana.”
4 Haya ndiyo manenoBwanaaliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
5 “Hili ndilo asemaloBwana:
“ ‘Vilio vya woga vinasikika:
hofu kuu wala si amani.
6 Ulizeni na mkaone:
Je, mwanaume aweza kuzaa watoto?
Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu
ameweka mikono yake tumboni
kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa,
kila uso umegeuka rangi kabisa?
7 Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha!
Hakutakuwa na nyingine mfano wake.
Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo,
lakini ataokolewa kutoka katika hiyo.
8 “ ‘Katika siku ile,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote,
‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao
na kuvipasua vifungo vyao;
wageni hawatawafanya tena watumwa.
9 Badala yake, watamtumikiaBwana, Mungu wao
na Daudi mfalme wao,
nitakayemwinua kwa ajili yao.
10 “ ‘Hivyo usiogope, Ee Yakobo mtumishi wangu,
usifadhaike, Ee Israeli,’
asemaBwana.
‘Hakika, nitakuokoa wewe kutoka mahali pa mbali,
wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao,
Yakobo atakuwa tena na amani na usalama,
wala hakuna atakayemtia hofu.
11 Mimi niko pamoja nawe nami nitakuokoa,’
asemaBwana.
‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote
ambamo miongoni mwao nimewatawanya,
sitawaangamiza ninyi kabisa.
Nitawaadhibu, lakini kwa haki.
Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
12 “Hili ndilo asemaloBwana:
“ ‘Kidonda chako hakina dawa,
jeraha lako haliponyeki.
13 Hakuna ye yote wa kukutetea shauri lako,
hakuna dawa ya kidonda chako,
wewe hutapona.
14 Wale walioungana nawe wote wamekusahau,
hawajali cho chote kukuhusu wewe.
Nimekupiga kama vile ambavyo adui angelifanya
na kukuadhibu kama vile ambavyo
mtu mkatili angelifanya,
kwa sababu hatia yako ni kubwa mno
na dhambi zako ni nyingi sana.
15 Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako,
yale maumivu yako yasiyoponyeka?
Kwa sababu ya uovu wako mkubwa
na dhambi zako nyingi
nimekufanyia mambo haya.
16 “ ‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa;
adui zako wote watakwenda uhamishoni.
Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara;
wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
17 Lakini nitakurudishia afya yako
na kuyaponya majeraha yako,’
asemaBwana,
‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa,
Sayuni ambaye hakuna ye yote anayekujali.’
18 “Hili ndilo asemaloBwana:
“ ‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo
na kuhurumia maskani yake.
Mji utajengwa tena juu ya magofu yake,
nalo jumba la kifalme litasimama
mahali pake halisi.
19 Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao
na sauti ya furaha.
Nitaiongeza idadi yao
wala hawatapungua,
nitawapa heshima
na hawatadharauliwa.
20 Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa
siku za zamani,
nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu;
nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
21 Mmoja wao atakuwa kiongozi wao;
mtawala wao atainuka miongoni mwao.
Nitamleta karibu nami naye atanikaribia mimi,
kwa maana ni nani yule atakayejitolea
kuwa karibu nami?’
asemaBwana.
22 ‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu,
nami nitakuwa Mungu wenu.’ ”
23 Tazama, tufani yaBwana
italipuka kwa ghadhabu,
upepo wa kisulisuli uendao kasi
utashuka juu ya vichwa vya waovu.
24 Hasira kali yaBwanahaitarudi nyuma
mpaka atakapotimiza
makusudi yote ya moyo wake.
Siku zijazo
mtayaelewa haya.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/30-b858b21008b4995dad5e3ad2b0161b92.mp3?version_id=1627—