Maombi ya Yona Katika Tumbo la Nyangumi
1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwombaBwanaMungu wake.
2 Akasema:
“Katika shida yangu nalimwitaBwana,
naye akanijibu.
# Kutoka kina cha kaburiniliomba msaada,
nawe ukasikiliza kilio changu.
3 Ulinitupa kwenye kilindi,
ndani kabisa ya moyo wa bahari,
mikondo ya maji ilinizunguka,
mawimbi yako yote na viwimbi
vilipita juu yangu.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa
mbali na uso wako,
hata hivyo nitatazama tena
kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha,
kilindi kilinizunguka;
# mwaniulijisokota kichwani pangu.
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima,
makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele.
Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni,
EeBwanaMungu wangu.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka,
nilikukumbuka wewe,Bwana,
nayo maombi yangu yalikufikia wewe,
katika Hekalu lako takatifu.
8 “Wale watu wanaong’ang’ana na sanamu zisizofaa
hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,
nitakutolea dhabihu.
Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza.
Wokovu watoka kwaBwana.”
10 BasiBwanaakamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JON/2-1ef80839c1ff5f108dbc49b6c823801f.mp3?version_id=1627—