Zaburi 6

Sala Kwa Ajili Ya Msaada Wakati Wa Taabu

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Mtindo Wa Sheminithi

#

. Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, usinikemee katika hasira yako,

wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.

2 UnirehemuBwana,

kwa maana nimedhoofika;

EeBwana, uniponye,

kwa maana mifupa yangu

ina maumivu makali.

3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi.

Mpaka lini, EeBwana, mpaka lini?

4 Geuka EeBwana, unikomboe,

uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.

5 Hakuna mtu anayekukumbuka

akiwa amekufa.

Ni nani awezaye kukusifu

akiwa kuzimu?

6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;

usiku kucha nafurikisha

kitanda changu kwa machozi;

nimelowesha viti vyangu vya fahari

kwa machozi.

7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,

yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.

8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,

kwa maanaBwanaamesikia kulia kwangu.

9 Bwanaamesikia kilio changu kwa huruma,

Bwanaamekubali sala yangu.

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,

watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/6-a9a79421fa300ef0aa37e5024d36f37d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

twenty − six =