Sala Kwa Ajili Ya Msaada Wakati Wa Taabu
(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Mtindo Wa Sheminithi
#
. Zaburi Ya Daudi)
1 EeBwana, usinikemee katika hasira yako,
wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 UnirehemuBwana,
kwa maana nimedhoofika;
EeBwana, uniponye,
kwa maana mifupa yangu
ina maumivu makali.
3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi.
Mpaka lini, EeBwana, mpaka lini?
4 Geuka EeBwana, unikomboe,
uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 Hakuna mtu anayekukumbuka
akiwa amekufa.
Ni nani awezaye kukusifu
akiwa kuzimu?
6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;
usiku kucha nafurikisha
kitanda changu kwa machozi;
nimelowesha viti vyangu vya fahari
kwa machozi.
7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,
yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,
kwa maanaBwanaamesikia kulia kwangu.
9 Bwanaamesikia kilio changu kwa huruma,
Bwanaamekubali sala yangu.
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,
watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/6-a9a79421fa300ef0aa37e5024d36f37d.mp3?version_id=1627—